Mauaji ya kutisha yatikisa JIJINI ARUSHA tena!

Mauaji ya kutisha yatikisa JIJINI ARUSHA tena!

LiverpoolFC

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2011
Posts
11,498
Reaction score
3,390
Ni usiku mwingine tena katika kitongoji cha Ilkiurei wilaya Arusha kijana mmoja kuuawa kinyama na watu wasiojulikana na hata hivyo kusababisha mkusanyiko mkubwa wa raia mtaani hapa baada ya kijana huyu aliyeuawa kujulikana hapa mtaani!
Hapa mpaka muda huu hakuna polisi waliofika na ingali taarifa kupewa kitambo na mwenyekiti wa mtaa ndg Hussen Abdul Leja!
Kwa walio karibu kabisa na marehemu alipouawa wanasema malumbano yaliendelea usiku wa manane baina ya marehemu na wale waliomwua na hata hivyo walishindwa kuamka wakiohofia usalama wao.

Picha ninazo na baada ya hapa nitafanya iwekanavyo nibandike!

Na marehemu kwa mawili matatu ninayopata hapa ni pacha na anafanya kazi katika kampuni ya usafirishaji ya abiria Hood Bussines Class ya hapa Arusha Mbeya!

Marehemu ni maarufu kwa jina pacha na nimebahatika kupata jina lake la pili na anaitwa HUSSEN na ni mzaliwa wa Mkoa wa Tanga!
 
Ma-Pai hawawezi fika on time hapo, si hakuna wa kumnyanganya rushwa?

Plus saa hii gari za Patrol ndio zinarudi kutoka kusindikiza Deals.
 
Wanasubiri Chadema wafanye maandamano na Mikutano na hapo utawaona kwa wingiii.....

Hawa dawa ni kuwa Mtwara tu na office zao za CCM.
 
Wananchi nao! Wahamasishane kupata namba za polisi wa doria na kupeana filimbi. Wangepiga filimbi mtaa mzima mbona kingeeleweka? Very sad!
 
Ni njia ya kupandisha hapa Whiterose bar na baada ya kuiacha Whiterose bar kidogo unaingia mkono wa kushoto ama kama unaijua kanisa la Moravian ilipo kabla ya TRIPPLE A na ndipo unaingia ndani kidogo na unakuta haya yote live bila chenga.

Na gari pickup ya police imeshawasili na wanapakia mwili wa marehemu tangu muda ule mpaka sasa na hapa naona ndg wa marehemu wamefika na wakilia kwa uchungu bila ya majibu!


njia ya kuelekea wapi?
 
King'asti; Yani nakwambia hakika marehemu amekosa ushirikiano kwani yaelekea amepambana kweli kweli bila ya kupata masaada wowote na majamaa waliomwua wakamponda ponda na majabali mpaka mauti yanamkuta Ndg yetu Pacha.


Wananchi nao! Wahamasishane kupata namba za polisi wa doria na kupeana filimbi. Wangepiga filimbi mtaa mzima mbona kingeeleweka? Very sad!
 
Last edited by a moderator:
Wananchi nao! Wahamasishane kupata namba za polisi wa doria na kupeana filimbi. Wangepiga filimbi mtaa mzima mbona kingeeleweka? Very sad!

Kwani vijana wa siku hizi wanaelewa maana ya filimbi hata ikipulizwa? Na wazee ndo hivyo waoga sana.
Utaratibu wa filimbi tunaujua mimi na wewe wa enzi za mwalimu bana!
 
Siku hizi ukitoa taarifa polisi kuhusu mambo ya uhalifu wanakuambia gari la polisi halina mafuta...utoe kamchango kidogo.....
 
saragossa; Kha ha ha ha ha ha ha ha haaaa! Kweli Mkubwa! Loh! Hasara tupu!


Kwani vijana wa siku hizi wanaelewa maana ya filimbi hata ikipulizwa? Na wazee ndo hivyo waoga sana.
Utaratibu wa filimbi tunaujua mimi na wewe wa enzi za mwalimu bana!
 
Last edited by a moderator:
Tumeambiwa tuwe na ulinzi shirikishi. Hata hivyo pamoja na polisi kuchelewa, majirani wamesaidia! Jamani tusaidiane.
 
Dah..Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi! mkuu hakuna fununu juu ya sababu ya kuuawa kwake?
 
Poleni sana!hao majirani walikuwa wemeusikia mzozo huo kwa muda mrefu kilichowanda kupiga simu polisi ni kipi? Hivi ungekuta ni ndugu yako si nafsi ingekusuta! R .i .p, pacha
 
wanasema malumbano yaliendelea usiku wa manane baina ya marehemu na wale waliomwua na hata hivyo walishindwa kuamka wakiohofia usalama wao.
Sijawahi kusikia wananchi wapuuzi kama hawa...
 
Pole kwa wafiwa, RIP Pacha Hussein, ahsante kwa taarifa mkuu LiverpoolFC.
 
Last edited by a moderator:
Ama kwel kila msiba unawenyewe,
na roho za wanadam hazna utash yan majran nalshndwa kusidia? je angekua ndug yao?
 
HB.DOCTOR; Yani best wewe acha tu hutamani kusikia haya yametokea mazingira yenye makazi ya watu!

So sad!

Ama kwel kila msiba unawenyewe,
na roho za wanadam hazna utash yan majran nalshndwa kusidia? je angekua ndug yao?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom