Operation ya M4C imeanza kitambo na imezunguka sehemu nyingi sana hasa ngombe za CUF na CCM mikoa ya kusini, iweje hapo kwa Mwigulu ndo zitokee vurugu? Inaonyesha huyu jamaa ni zero brain ndo maana akaandaa vijana wake wafanye fujo. Kuna watu wenye nguvu ya pesa na kisiasa km Lowassa, Rostam, Chenge, etc na wanakashfa kibao ila hawakuandaa vijana wa kupambana na wapinzani bali walikaa kimya na kuyapokea maneno ambayo yamepita na maisha yao yanaendelea vizuri kwa sasa mpk wanataka kugombea Urais na wanaongoza kamati za Bunge. Kwa wale wanaoneza chuki na propaganda chafu kuhusu kilichotokea Singida, mwambieni Mwigulu ajifunze siasa, kuandaa na kuwalipa vijana ili wafanye vurugu kuonyesha wanakupenda sana na wana uchungu na wewe ni utoto na uchanga kisiasa. Naomba kuwasilisha!