Naomba tujadili hili la matumizi ya dola wakati watanzania wengi mishahara yao inalipwa kwa madafu. Mimi ni mmoja wa wateja wa Dstv tanzania inasikitisha monthly subscription fee ni USD 78. Ni kweli sheria iliyopo inakataza mtoa huduma kutokataa pesa ya kitanzania kama mtoa huduma gharama zake zipo kwa USD. Hii haimsaidii kitu mtanzania hata kidogo kwani kushuka kwa thamani ya Tshilingi haimuadhiri hata kidogo mwekezaji kama Dstv. Na sina uhakika kama wafanyakazi wa Dstv wa hapa tanzania kama wanalipwa kwa dola mishahara yao. Kwa mtazamo wangu huu ni aina ya ufisadi kwa watanzania na Dstv anafanya hivi kwa sababu ya monopoly ya huduma anayoitoa. Tujadili...