Matumizi sahihi ya taa za gari.

Nitakuwa nje kidogo ya mada lakini ni katika masuala mazima ya barabarani.

Naulizia mistari ya barabarani ya katikati.

1)Kuna sehemu za barabara ukipita unakuta mstari umepigwa mmoja lakini ukienda mbele inakuta ipo miwili. Hapo inaashiria nini?

2)Pia,katikati ya barabara kuna sehemu mistari yake ni dash-line style upande mmoja mf.kulia na kushoto ni mstari wa moja kwa moja then kwa mbele unakuta ule uliokuwa dash-line kulia umewekwa kushoto tena na mstari wa moja kwa moja upo kulia. Hii maana yake nini?

3)Sehemu mistari yake ni dash-line tu inamaanisha nini? Ukiwa mmoja au miwili.
Namba moja sijakupata...ila kwa namba 2 kama kuna mistari miwili katikati ya barabara na wa kushoto ni wa dash dash maana yake wew dereva unae kwenda mbele unaruhusiwa kulipita gari la mbele yako kama ni salama kufanya hivyo...lakini yule ambae anaelekea ulipotoka au unaepishana nae haruhusiwi kulipita gari lililopo mbele yake kwa sababu mstari wake ni wa moja kwa moja hauna dash. Hii yote imetokana na utaratibu kuwa kama mstari wa katikati ya barabara ni wa moja kwa moja yaani hauna dash dash ina maanisha hakuna dereva wa upande wowote anaeruhusiwa kulipita gari lililopo mbele yake....lakini kama mstari ni wa dash dash basi dereva anaruhisiwa kulipita gari la mbele KAMA ni salama kufanya hivyo.
 
Achana na mambo ya kucopy na ku paste bana me naongea kutokana na halisi ya mambo maana hiyo pdf ni tofauti na sheria za bongo umeona mataa ya bongo yanavyofanya kazi umeona ni sawa na UK??so ongea vitu ambavyo unajuwa na sio kukurupuka....

Nicheke mie, Watanzania tuache uvivu, hiyo document hata hujasoma unakurupuka tu, unatakiwa utafuniwe kila kitu, haya, Road Markings kuanzia ukurasa 162 nk, warning signs kuanzia ukurasa 47 na chochote kuhusiana na matumizi ya barabara, ulitegemea nikutafunie hata uji, Grow up! Hiki ndicho kinarudisha maendeleo ya nchi hii, hamtaki kusoma mnataka mambo rahisi mkifanyiwa mnakurupuka. Nilikwambia Wacha uongo kwa sababu ulisema full beam inatumika UK kukiwa na fog etc huo ni uongo, kuna fog lights kwenye magari siku hizi sio uongo wa kusema full beam ndio inatumika. Achana na mambo ya chupi kaka/dada weka hoja.

upload_2016-12-24_10-55-5.png


Fog lights kama hizi .... ..
BTW sheria za barabarani za Tanzania tumerithi kutoka kwa Uingereza. Tuna ajali nyingi kwa sababu wengi wa madereva hawana vigezo vya kuendesha magari na hawafuati sheria za barabarani. Watu wanakunywa pombe then wanaendesha magari, what stupidity is that?
 
Ningependa Traffic wawe wanawakamata Madereva Vilaza ambao hawajaui matumizi ya Taa,Utamkuta mpo kwenye foleni gari zimesimama jamaa wa nyuma kawasha full hadi balaa,utakuta mtu anapita sehemu ambayo ina mwanga mzuri kabisa lakini kawasha taa full,Ni kero sana,Dawa ya watu kama hao akiwa nyuma mgeuzie kioo cha juu kwenye roof kimmulike yeye,na njia ya pili kama akiwasha full na wewe mpige full tu basi.
 
Namba moja sijakupata...ila kwa namba 2 kama kuna mistari miwili katikati ya barabara na wa kushoto ni wa dash dash maana yake wew dereva unae kwenda mbele unaruhusiwa kulipita gari la mbele yako kama ni salama kufanya hivyo...lakini yule ambae anaelekea ulipotoka au unaepishana nae haruhusiwi kulipita gari lililopo mbele yake kwa sababu mstari wake ni wa moja kwa moja hauna dash. Hii yote imetokana na utaratibu kuwa kama mstari wa katikati ya barabara ni wa moja kwa moja yaani hauna dash dash ina maanisha hakuna dereva wa upande wowote anaeruhusiwa kulipita gari lililopo mbele yake....lakini kama mstari ni wa dash dash basi dereva anaruhisiwa kulipita gari la mbele KAMA ni salama kufanya hivyo.
Ok, nashukuru kwa majibu yako. Hata hiyo namba moja nimejiongeza nimeelewa itakuwa na maana gani.
 
Ningependa Traffic wawe wanawakamata Madereva Vilaza ambao hawajaui matumizi ya Taa,Utamkuta mpo kwenye foleni gari zimesimama jamaa wa nyuma kawasha full hadi balaa,utakuta mtu anapita sehemu ambayo ina mwanga mzuri kabisa lakini kawasha taa full,Ni kero sana,Dawa ya watu kama hao akiwa nyuma mgeuzie kioo cha juu kwenye roof kimmulike yeye,na njia ya pili kama akiwasha full na wewe mpige full tu basi.
Sio matumizi ya taa peke yake mkuu. Hata alama za barabarani ni tatizo kubwa sana na tatizo linakuwa kubwa kwenye maungio ya barabara.
 
Habari zenu wana jamvi...Mi napenda sana usalama barabarani....huwa naumia sana nikisikia ajali ambayo imetokana na uzembe au kutofuata sheria za barabarani....Haya ni matumizi ya taa za gari yakiyowekwa kisheria.

Tuanze na taa za mbele ya gari ambazo kimsingi zinatakiwa ziwepo taa za aina tatu....
1..>>>>>Taa kubwa za mbele ambazo hutumika kuanzia giza linapoanza kuingia mpaka giza linapoisha asubuhi pamoja na sehemu zenye tunnel na nyakati za ukungu au mvua..Taa mbili hizi kwa haraka unaweza ukasema zina matumizi sawa lakini kila taa ina kazi yake...yaani taa ya kulia ina kazi yake na ya kushoto pia....Taa ya kulia ambapo ndio upande wa dereva kazi yake ni kumulika kuanzia mstari mweupe wa katikati ya barabara kuelekea kushoto ili kumrahisishia dereva unaepishana nae asipate shida sana wakati mnapishana....na taa ya kushoto kazi yake ni kumulika kuanzia mstari wa njano kuelekea kushoto ili iwe rahisi kuwaona waendesha vyombo vya baridi na watembea kwa miguu......taa kubwa zina low beam(mwanga usiomulika mbali) na high beam ( mwanga unaomulika mbali)....matumiz ya low beam kisheria ni pale .....
@unapopita katika barabara yenye taa (taa za barabarani hasa mjini) .....
@unapopishana na gari nyingine ni lazima na sio ombi kutumia low beam.....
@unapotaka kulipita gari la mbele yako (over take) ni lazima kutumia low beam kabla hujaanza kulipita gari hilo....endapo utatumia high beam wakati wa kuover take basi mwanga wa taa zako utapiga moja kwa moja katika kioo cha cha gar ya mbele ( side mirror) then mwanga ule utakuwa reflected kwa dereva unaetaka kumpita na kumsababishia kuanza kuyumba na hatimaye unaweza ukakosa njia nzuri ya kumpita.

2. Kuna taa za kuegeshea gari ( parking light) ambazo hutumika ukiwa umepaka gari lako pembeni ya barabara nyakati za usiku ili liweze kuoneka kirahisi. Ni muhimu sana taa hizi.

3. Taa za kuonesha uelekeo yaani indicators lights...hiz ni taa ambazo kisheria zinatakiwa ziwe mbili mbele ya gari yako..yaani kulia na kushoto....utawasha ya kulia kuonesha unaingia kulia na kushoto kuonesha unaingia kushoto angalau mita 30 kabla ya kufanya kitendo hicho..... Taa hiz zinaweza kutumika pia wakati ukivunja sheria kwa kuziwasha zote mbili kwa wakati mmoja yaani HAZARD ukionesha kuwa gari yako inaweza kusababisha maafa au ajali hivyo basi watumiaji wengine kuwa makini au na tahadhari dhidi ya gari yako...kuna aina tatu ya uvunjaji wa sheria kwa kutumia HAZARD.....
Moja..kama gari yako ipo kwenye mwendo wa kasi kuliko mwendo ulioainishwa katika eneo husika( labda ni eneo la mjini mwisho 50 kmh lakin wew una dharula ya mgonjwa unamuwaisha itabidi utumie HAZARD.....
pili...kama unaenda kwa mwendo wa polepole sana kiasi ambacho unaweza kusababisha ajali...mfano njia za nje ya mji magari huwa yakienda kwa mwendo wa kasi...hivyo basi kama gari ina tatizo labda imeshindwa kuingiza gia zaid ya namba moja na kukulazimu kutembea mwendo wa gia moja ni lazima uwashe HAZARD.
Tatu...kama gari yako imeharibika barabarani na sehemu hiyo huruhusiwi kuegesha gari...mfano barabara zote ambazo zina mstari wa njano pembeni huruhisi kusimama bali unatakiwa uendelee mbele tu. Ukipata tatizo katika maeneo haya basi utavunja sheria ya kutokusimama kwa kuwasha HAZARD pamoja na kuweka vibao vya tahadhari.(triangles)

Uzi huu ni kwa ajili ya taa za mbele tu....nitaandaa uzi mwingine kwa ajili ya taa za nyuma ambazo jumla yake zipo sita...ni vyema ukajua matumizi yake kuepuka/kuepusha ajali na mambo mengine. Aksante kwa kusoma.
Na pia naomba niongezee katika suala la uwashaji wa indicator za magari....kuna namna flani hivi madereva wengi tumekuwa tukiitumia hususani katika uwashaji wa indicator.
INDICATOR YA KULIA: Kipindi gari la nyuma yako inataka kukuovertake na dereva wa hilo gari akikupa ishara kuwa anataka kukuovertake, na wewe uliye mbele yake unaona kabisa eneo hilo sio zuri kwa kuovertake hususan kama kuna gari linakuja huko mbele au kama kuna tatizo huko mbele, wewe kama dereva wa gari la mbele yake unabidi uwashe hiyo indicator kama tahadhari na kumuonya.
INDICATOR YA KUSHOTO: Dereva wa gari ambayo inapitwa na gari lingine huwasha hii taa ya indicator ili kumweleza dereva wa gari linalotaka kumuovertake kuwa huko mbele kupo salama kwa hiyo anamruhusu aovertake.
 
Asante sana mkuu kwa somo hili. Umenifundisha vitu ambavyo nilikua sijui
 
ni ishara ya kuwa hukati kulia wala kushoto bali unanyoosha tu
Ni kosa kuwasha hazard( indicator zote )kwenye makutano ya barabara kama hukati kulia au kushoto huna haja ya kuwasha indicator yoyete wewe nyoosha tu.
 
Watumiaji wa full lights usiku unawazungumziaje..ama matumizi sahihj ya full lights yakoje,baadhi ya magari akikuwashia full unaweza pata ajali kabisaa
 
Mkuu naomba kuuliza na zile taa za full zinawashwa na madereva wakati wa mchana mkiwa mnapishana hasa kwenye highway tunapokwenda mikoani? Wengine wanazitumia kuuliza hali ya barabara huko unakotoka (anakokwenda) kama kuna traffic police au la? Sasa swali langu ni je namjibuje? Nawasha full muda mrefu mpaka tupishane au nawasha na kuzima haraka haraka? Hapo atatakiwa kuelewa nimemwambia nini sasa incase imeamua kutumia aina mojawapo (full muda mrefu mpaka tupishane au nawasha na kuzima haraka haraka)?
 
Mi nisaidieni kama kuna fundi au mtumiaji mdadisi wa pikipiki aina ya Boxer BM150 kuna pipe moja nimesikia wakiita bliza pikipiki ikiwa mpya ile pipe inakiplastic cheupe kimeziba je? Ndio inavyopaswa kuwa? Na kama sivyo nin nikifanye??
 
Back
Top Bottom