Dereva Suka
Senior Member
- Sep 25, 2014
- 176
- 289
- Thread starter
- #41
Namba moja sijakupata...ila kwa namba 2 kama kuna mistari miwili katikati ya barabara na wa kushoto ni wa dash dash maana yake wew dereva unae kwenda mbele unaruhusiwa kulipita gari la mbele yako kama ni salama kufanya hivyo...lakini yule ambae anaelekea ulipotoka au unaepishana nae haruhusiwi kulipita gari lililopo mbele yake kwa sababu mstari wake ni wa moja kwa moja hauna dash. Hii yote imetokana na utaratibu kuwa kama mstari wa katikati ya barabara ni wa moja kwa moja yaani hauna dash dash ina maanisha hakuna dereva wa upande wowote anaeruhusiwa kulipita gari lililopo mbele yake....lakini kama mstari ni wa dash dash basi dereva anaruhisiwa kulipita gari la mbele KAMA ni salama kufanya hivyo.Nitakuwa nje kidogo ya mada lakini ni katika masuala mazima ya barabarani.
Naulizia mistari ya barabarani ya katikati.
1)Kuna sehemu za barabara ukipita unakuta mstari umepigwa mmoja lakini ukienda mbele inakuta ipo miwili. Hapo inaashiria nini?
2)Pia,katikati ya barabara kuna sehemu mistari yake ni dash-line style upande mmoja mf.kulia na kushoto ni mstari wa moja kwa moja then kwa mbele unakuta ule uliokuwa dash-line kulia umewekwa kushoto tena na mstari wa moja kwa moja upo kulia. Hii maana yake nini?
3)Sehemu mistari yake ni dash-line tu inamaanisha nini? Ukiwa mmoja au miwili.