Matokeo yangu ya hesabu

Matokeo yangu ya hesabu

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,419
Reaction score
18,341
Nilipokuwa shule ya msingi kuanzia la 4 hadi la 7 maksi zangu za hesabu kwenye mitihani zilikuwa zinacheza kwenye 03% hadi 08%.

Matokeo yalikuwa yanatangazwa mbele ya darasa!yanapotangazwa mwalimu anaanza kuwaita wanafunzi kwakuanzia maksi za chini kwenda juu (0-100),kwahiyo darasa lote linajua makaratasi yakiletwa lazima niitwe kama si wa kwanza basi wa pili.

Siku moja mwalimu akaanza kuita majina,mpaka akafikia kwenye maksi 30%,40%,50%,60%,70% bado tu mi hajaniita.
Watu wakaanza kuniangalia waliokuwa karibu wakaanza kuniuliza....""eeeh umepasua hujaitwa,ilikwaje??"
Nilianza kuvimba kichwa,huku mwalimu anaendelea kugawa tu makaratasi.

Yakabaki makaratasi ya waliopata 80%-90% bado mi sijaitwa tu.
Mara akabaki na karatasi moja mkononi,darasa lote macho kwangu hawaamini kinachotokea maana bado sijapata karatasi.

Mwishoni mwalimu akaangalia juu,kisha akasema "kuna ng'omba hajaandika jina kapata 0% aje achukue karatasi yake"
Nilienda kuchukua nikiwa mpole.
 
Mkuu nmejikuta naangua kicheko cha hatari aisee..kwi kwi kwi kwi ila pole sn!!
 
Last edited by a moderator:
Kuna jamaa yangu sana alikuwa zuzu sana class miaka ile..aliwahi kupata zero mock ya standard seven. Iliniuma saaana!
 
Kuna jamaa yangu sana alikuwa zuzu sana class miaka ile..aliwahi kupata zero mock ya standard seven. Iliniuma saaana!
heri hata hizo level za chini,kuna mshikaji wangu form six necta aliambulia ziro tena ya arts HGK,inauma sana aisee
 
Sasa kwanini ulienda kuchukua karatasi yako si ungesema siyo ya kwako.
 
Sifa ni sifa tu hata kama za muda mfupi unapaswa kukifurahia kipindi kile kifupi AMBacho watu waliojua umepasua kumbe sio.
 
Back
Top Bottom