kalipeni
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 1,533
- 1,242
Maisja ya shule bwana we acha tu!
Nilipokuwa shule ya Msingi enzi hizoo kuanzia Darasa la Nne hadi la Saba maksi zangu za somo la Hisabati (Hesabu) zilikuwa zinacheza kwenye 03% - 08% na kwa bahati mbaya matokeo yalikuwa yanatangazwa mbele ya Darasa.
Yanapotangazwa mwalimu anaanza kuwaita Wanafunzi kuanzia maksi ndogo kwenda kubwa kwahiyo darasa lote lilikuwa linajua Karatasi zikiletwa lazima niitwe Mwanzoni kama si wa kwanza Basi wapili toka chini.
Siku moja mwalimu akaanza kuita majina mpaka akafika maksi 50%,60%,70% Bado tu hajaniita,basi watu wakaanza kuniangalia na kuniambia 'Ee umepasua leo' Basi mimi nilianza kuvimba kichwa huku mwalimu anaendelea kugawa tu karatasi kwa wahusika.
Hatimaye yakabaki makaratasi machache 80%, 90% bado mimi sijapata tu. Mara akabaki na Moja mkononi. Hahaha! Yaani Darasa lote macho kwangu hawaamini maana bado mimi tu ndo sijapata.
Mwishoni mwalimu akaangalia juu kama Muda wa Sekunde 30 kisha akashusha Pumzi kwa nguvu akasema "Kuna NGUCHIRO mmoja hajaandika jina lake kwenye karatasi kapata 00% Aje achukue Karatasi yake".
🤣🤣🤣
Nilipokuwa shule ya Msingi enzi hizoo kuanzia Darasa la Nne hadi la Saba maksi zangu za somo la Hisabati (Hesabu) zilikuwa zinacheza kwenye 03% - 08% na kwa bahati mbaya matokeo yalikuwa yanatangazwa mbele ya Darasa.
Yanapotangazwa mwalimu anaanza kuwaita Wanafunzi kuanzia maksi ndogo kwenda kubwa kwahiyo darasa lote lilikuwa linajua Karatasi zikiletwa lazima niitwe Mwanzoni kama si wa kwanza Basi wapili toka chini.
Siku moja mwalimu akaanza kuita majina mpaka akafika maksi 50%,60%,70% Bado tu hajaniita,basi watu wakaanza kuniangalia na kuniambia 'Ee umepasua leo' Basi mimi nilianza kuvimba kichwa huku mwalimu anaendelea kugawa tu karatasi kwa wahusika.
Hatimaye yakabaki makaratasi machache 80%, 90% bado mimi sijapata tu. Mara akabaki na Moja mkononi. Hahaha! Yaani Darasa lote macho kwangu hawaamini maana bado mimi tu ndo sijapata.
Mwishoni mwalimu akaangalia juu kama Muda wa Sekunde 30 kisha akashusha Pumzi kwa nguvu akasema "Kuna NGUCHIRO mmoja hajaandika jina lake kwenye karatasi kapata 00% Aje achukue Karatasi yake".
🤣🤣🤣