Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Matokeo ya Jimbo la Bumbuli yana Utata

Status
Not open for further replies.

Delegate

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2012
Posts
331
Reaction score
203
Jimbo la Bumbuli matokeo ya Ubunge yanaonesha kuwa waliopiga kura ni watu 20,512 ambapo January Makamba amepata kura 17,805. Lakini cha ajabu kwenye matokeo ya Urais jimbo hilohilo la Bumbuli waliopiga kura ni watu 44,011 ambapo Magufuli anadaiwa kupata kura 35,801.

Sasa jiulize imekuaje waliopiga kura za mbunge wawe watu 20,512 halafu kura za Rais wawe 44,011. Yani kuna watu 24,000 walienda vituoni kupiga kura za Rais tu lakini hawakupiga za Mbunge.

Haya ni maajabu ya dunia. Haihitaji degree kujua kwamba Tume imeongeza wapiga kura hewa 24,000 na kura zote hizo wakampa Magufuli.

CSP98ZFUcAAsPtG.png
 
Hadi hapo sie tunawaamini tume!!!!!! ndio tuliowapa dhamana.......huna ushaidi mzushi tu wewe
 
Mbona wameondoa kitufe cha LIKE? Pokea LIKE yangu Mkuu. Wanadhani wanadanganya watu, lakini mwisho wa siku serikali ya ccm itakosa uhalali wa kutawala kwa sababu hawakuingia madarakani kwa njia sahihi. Matokeo yangu ni serikali kudhoofika na mwisho wa siku kushindwa kuendelea kufanya kazi. Historia haidanganyi!
 
Lubuva anajitia uchizi yani anapokea matokeo kutoka CCM ndiyo anatangaza.
hizi figisu ziko well observed very soon kitaumana.
 
Duh......haya sasa ngoja wafia chama waje hapa na mapovu mdomoni kutetea matatizo.
 
Sasa ukawa tukisema wizi kama huu watu wanasema eti sisi waongo. Hata hao waangalizi wa uchaguzi wamejifungia kwenye mahoteli Dar na mijini kula posho, hawana msaada, yatapasa kukomaa wenyewe. Siku ya kupiga kura, nimetoka kupiga kura nikapitia bar fulani nikakuta watu wanne na manguo yao ya election observer wapo wanapombeka ile mbaya, sasa sijui ni waangalizi wa pombe!?
 
hawa chichiem sikuzote ni wezi wa kura, hawajawahi kushinda kiuhalisia, cheki hata huko zanzibar kinachoendelea, na je matokeo ya 2010!

ukizoea kula nyama ya binadamu huwezi kuicha daima.
 
Kila sehemu walikua wameandaa kura za Magufuli ili apite.Watanzania wamemchagua Lowassa lakini wao wanalazimsha.
 
wewe ndio yule mmtaalam wa IT mkorea uliyeletwa na cdm?
 
Tanzania yangu inaangamia kwa upole wetu

Kabisa mkuu. Historia duniani kote ipo wazi kuwa kuwaondoa watawala dhalimu ni lazima kinuke. Lakini kwa hizi keyboard, sidhani! Yaani kutokana na upole wetu, ccm sasa wala hawaiibi tena bali inapora ushindi kweupe huku tunaona, nasi tunasema, hewala baba ccm!?
 
Mmmmh aisee hao wataalam wa IT nina mashaka nao, ni aina gani ya uchakachuaji wanayoitumia mbona inagundulika kiurahisi? Sifa ya kufoji ni kushindwa kutambua kiurahisi
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom