Matokeo Kidato cha Nne 2012 ni FEKI (yamepikwa) - GREEN ACRES

Hivi kweli inakuja akilini kwamba matokeo ndo yenyewe? Hapo nazidi kuzidi kuamini kwamba kunakitu kimetokea huko. Kwanza inakuaje matokeo yanatangazwa na waziri wakati tumezoea Dr. Ndalichako ndoutangazaga? Kama huyo mama haligoma kutangaza kwann asijiuzulu hili tumuenzi kwani elimu yake inamwezesha kufanya kazi sehemu yeyote dunia.
Hivi mbona viongozi watz baadhi yao hawana uchungu na wanachi wa nchi hii? Tatizo kubwa hapa tz ni ubinafsi sana umetawala leo hii zunguka shule za kata, shule za msingi za wananchi angalia kama kuna watoto waviongozi kama wapo? Watoto wenu wote wapo Saint school kweli mtapata uchungu wakukaa chini bila madawati, hakuna vitabu au kutokuwa na walimu wa masomo miaka mi4 kweli?

Mungu ibariki Tanzania.
 
makubwa haya jamani,hivi wanaokusanya data za maajabu ya dunia wanachukua vigezo gani?hivi havitoshi kutuingiza kweli???
 
"Alimtaja mwanafunzi mwingine, Martin Rushaigwa, namba 01197/0173, ambaye alifanya masomo ya ‘Arts’.
Alisema matokeo ya mwanafunzi huyo yanaonesha kuwa ameongezewa alama za masomo ya biashara ya Bookeeping na Commerce, ambayo hakuyafanya kabisa".

S1197/0173
M
34
FLD
CIV-F HIST-F GEO-F KISW-D ENGL-F LIT ENG-F BIO-F B/MATH-F

Sina uhakika na kinachosemwa na huyo Mwl. Bujugo na matokeo yaliyoandikwa kwenye Mtandao!
 
Ni kweli haya matokeo yamechakachuliwa and this report confirms my suspicions even further kwasababu mimi mdogo wangu hakuchukua lilterature english lakin kwenye matokeo wamemuandikia kama alichukua hyo literature english na wamempa grade "B"...how can this possibly happen...majibu wadau
 
Ukistaajabu ya musa utayaona ya firauni
kumbe mbatia niliona anapiga porojo za siasa sasa nimeamini ukweli shukuru kawambwa
anaitaj kujiuzulu na kutuwekea mtaala mahususi wa elimu yetu

ndugu zanguni kwa mliosikia redio clouds masaa mawili yaliyopita walikuwa wakimhoji
mwalimu mkuu wa shule moja aliesema wazi matokeo ya form four ni feki
wakati anahojiwa kwa nini anasema hivyo nahisi kama mtanzania ulimsikia ulipata
hamu ya haja kubwa gafla .......

Mwalimu mkuu huyo aliekuwa akihojiwa anasema amekuwa wa kwanza kulalamika matokeo yale
na kusema kumekuwa na matatizo mengi pale kwenye baraza na bado awataki kuyakubali

1..usahihishaji
anasema kumekuwa na matatizo makubwa kwenye usahihishaji na kusema kama waislamu wangekaa
kimya kipindi kile kwa kukubali matokeo yale basi upumbavu huu ungeendelea na anashangaa
mpaka leo bado unaendeleea.....

2..hili ndilo la kustaajabisha akataja na majina kabisa akasema ana wanafunzi wake kwenye shule
walishindwa kufanya mtihani kutokaa na na sababu mbali mbali lakiiiiiiiiniiiiiiiiiiiiiiiii
ameshikwa na butwaaaa kukuta wanafunzi zaidi ya watano katika hao wasiofanya mtihani majina
yao yako kwenye ubao wa matokeo na tena wana div ii na wengine iii

akasema kwa hili yuko radhi kutoa ushirikiano na serikali kuwadhihirishia hawa watoto awakufanya mtihani kabisa kabisa

sasa ndugu zangu watanzania hivi unajua hata wewe ulishindwa kufaulu la saba yawezekana ulifaulu matokeo yako akapewa asha ama mwakatobe ,ama mwafilimbi ,,ama mwaigomole??sisemi kufeli maana naamini akuna kufeli la saba bali kushindwa kufaulu

mh waziri natamani kusikia lafudh i yako kwenye hili nini kinaendelea.....
Ni wangapi jamani wako vyuoni kwa style hii wapendwa katika bwana nashindwa kuendeleaaaa nimepatwa na uwoga kwenye mikono namini waziri atarudi tena kutusaidia hili

mama yetu yule anaekuwaga wa kwanza kuroppoka matokeo nae atusaidie kwa hili
 
Kwanini asitaje majina ya hao watoto na wanapoishi ili kila mtu aweze kufanya uhakiki mwenyewe?
 
Headmaster wa Green acress international ametoa tuhuma kwa baraza la mtihani akisema kuwa matokeo ya shule yake yamechakachuliwa,
anadai kuna mwanafunzi ambaye alifukuzwa na akufanya mtihani lakini amejaziwa matokeo kama amefanya mtihani na amefaulu,

mwingine aliyekuwa anasoma arts amejaziwa masomo ya biashara,

kuna wengine walifanya lakini wameandikiwa absent,

pia kuna wengine wamechanganya marks na majina, bahati kapewa ben, ben kapewa bahati.

kama ni kweli huu ni upuuzi kabisa.
Source: clouds now kwenye xxl
 
"No data, No right to speak" Tunaomba uwazi na ukweli wa jambo hili!!!!!! Hakuna mtu anaweza kubeba lawama za kufeli au kufaulu kwa watoto, kwa kuwa matokeo ya mtoto, huchangiwa na factors chungu nzima, zikiwemo:-
  • Serikali
  • Wazazi
  • Mtoto mwenyewe
  • Mazingira
Kila kimoja kati ya hayo hapo juu kina mchango, Changanua kuonesha wewe ulitimiza wajibu gani, na factor zingine ilishindwa kutimiza wajibu upi, hadi watoto kufeli.
  • Tusihukumu factor moja, kabla ya kutafakari michango ya factor zingine. That is not fair!!!!!!! Let we be serious on such issue!!!!!!!!!
 
Taifa la walevi tatizo watu wanafanya kazi huku wanakunywa pombe what do u expect
 
hawa Clouds walihoji mkuu wa shule au muhuni anaejiita mkuu wa shule?km Clouds mko makini tuleteeni NDALICHAKO ajibu hzo hoja kwa sababu ni hoja nzito na ni kashfa kwa BARAZA LA MITIHANI.
 
Hatareeeeeee!! Weka mbali na watoto!!!! Hiii kitu hatareee! Keep away from direct sunlight!!
 
kwanini wasiende lalamika NECTA? wanaenda clouds yaani hawa watu mbulula kweli
 
huyu mtoto ni jirani yangu kule bunju, ni kweli hakufanya mtihani, na yuko shule moja mbeya, nimemuulizia mama yake mzazi kasema naye anasikia kwenye redio anashangaa.
 
Yawekwe wazi hayo majina ya watoto watanzania tujiridhishe na anachosema"isijekuwa
mbinu ya kumnusuru waziri"
 
Back
Top Bottom