Matokeo kidato cha 4 yaua tena!

Matokeo kidato cha 4 yaua tena!

Eyoma

Senior Member
Joined
Sep 9, 2011
Posts
166
Reaction score
40
Kwa taarifa nilizozipata kwa jamaa alieko monduli Arusha kwamba mwanafumzi wa kike aliemaliza shule moja hapo minduli na kufeli kidato cha 4 ajinyonga na kufariki kisa matokeo mabaya ya mwaka huu.

Huyu nadhani atakuwa wa 3 au wa 4 sasa kujiua kutokana na matokeo mabaya,mmh nini hatima yake?

Naiomba na jamii na wananchi tuache kuwakejeli au kuwasemasema vijana waliofeli,kufeli sio kufeli maisha.

Poleni wafiwa.
 
kwa taarifa nilizozipata kwa jamaa alieko monduli Arusha kwamba mwanafumzi wa kike aliemaliza shule moja hapo minduli na kufeli kidato cha 4 ajinyonga na kufariki kisa matokeo mabaya ya mwaka huu.huyu nadhani atakuwa wa 3 au wa 4 sasa kujiua kutokana na matokeo mabaya.mmh nini hatima yake.naiomba na jamii na wananchi tuache kuwakejeli au kuwasemasema vijana waliofeli.kufeli sio kufeli maisha.sijui watajiua wangapi mwaka huu.duuh.poleni wafiwa
tatizo siyo kukejeliwa bali ni hasira kwa serikali kumpotezea miaka yake minne bure kwenye shule za kata ambazo hazina maabara na waalimu wenye sifa!!!!
 
ina maana kizazi hiki ndicho chenye machungu sana!au wana mengine?hata miaka ya nyuma kuna wanafunzi walikuwa wana pata matokeo mabaya tofauti na matarajio yao,na kweli unakuta mpaka walimu wanashangaa imekuwaje!lakini walikuwa hawajiui sembuse hawa wa cku hizi kusoma hawasomi,wana kalia ku bet mipira tu ya ulaya.
 
Nimesikia kifo cha huyo msichana.
 
Tanzania ni nchi ya ajabu sana ambayo watu wake hawaujali uhai wala kuishi na kuhisi maumivu na matatizo ya wenzi wao.,TUNISIA ALIJICHOMA RAIA MMOJA KWA KUKATAA UNYANYASAJI WATU WOTE WAKAJIHISI UCHUNGU,HAPA KWETU WANAJIUA WATOTO WETU 3-4 KWA UZEMBE WA SERIKALI KUSHINDWA KUWEKA MIPANGO DHABITI NA SAHIHI KUNAKO NYANJA YA ELIMU KUNAKOSABABISHA (WATOTO)WATU WENYE MOYO NA NIA DHABITI YA KUSOMA NA KUSONGA MBELE WANAIKOSA KWA KUNYIMWA AU UZEMBE WA WAZI LAKINI HAMNA ANAYEJALI NA HATA VYOMBO VYA HABARI HAVIONI YA KWAMBA NI HABARI KILA MTU NA LWAKE,Duh!~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~Tujali nini kwani hata wasipojiua si tutawapiga kiberiti kesho watakapokwapua T-shirt na jeans kwa njaa ya kukosa mlo???KUUA,kUJIUA INAKUWA KAWAIDA KWA MTANZANIA HII NI HATARI KUBWA NA TUIKATAE SASA.
 
TUNISIA ALIJICHOMA RAIA MMOJA KWA KUKATAA UNYANYASAJI WATU WOTE WAKAJIHISI UCHUNGU

Acha kupotosha watu wewe! Akili zenu hizi za kukariri mambo ndiyo maana mnapachikwa ukamanda usiyokuwa na kichwa wala miguu.

Yule raia wa Tunisia aliyejichoma moto alikuwa ni msomi ila hakupata kazi, akaamua kujiajiri lakini bado serikali yake ikamzingua ndiyo maana wananchi waliungana naye.

Unataka kumfananisha na hawa ambao hata "ordinary level" imewashinda?

Usikariri maisha.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
This is sad....hivi Mpaka sasa Kawambwa ajajiuzulu?
 
duh!Hawa wadogo zetu ni hatari!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Acha kupotosha watu wewe! Akili zenu hizi za kukariri mambo ndiyo maana mnapachikwa ukamanda usiyokuwa na kichwa wala miguu. Yule raia wa Tunisia aliyejichoma moto alikuwa ni msomi ila hakupata kazi, akaamua kujiajiri lakini bado serikali yake ikamzingua ndiyo maana wananchi waliungana naye. Unataka kumfananisha na hawa ambao hata "ordinary level" imewashinda? Usikariri maisha. ACHA UGIZA,UHAI NI UHAI HAUJALISHI WA MBUMBUMBU WALA WA MSOMI.,KAMA MTU HAJAFANYA MTIHANI NA AMEFAULU WAONA AJABU GANI KWA ALIYEFANYA VIZURI AKAFELISHWA?*?HIYO ORDINARY LEVEL UNAYOWADHARAU NAYO WANGEFANIKIWA VIPI BILA MIPANGO MADHUBUTI YA SERIKALI?ULIVYO GIZANI NA KUJISKIA KWAKO WAONA WAO NDIO WALIOFAIL,AMKA NDUGU ILIYOFAIL NI SERIKALI SIO WATOTO WETU.
 
ina maana kizazi hiki ndicho chenye machungu sana!au wana mengine?hata miaka ya nyuma kuna wanafunzi walikuwa wana pata matokeo mabaya tofauti na matarajio yao,na kweli unakuta mpaka walimu wanashangaa imekuwaje!lakini walikuwa hawajiui sembuse hawa wa cku hizi kusoma hawasomi,wana kalia ku bet mipira tu ya ulaya.

Ni ishara tosha ya kumtaka waziri Kawambwa ajiuzuru.
 
Alitaka afaulu bila kusoma?

Ndugu zangu hususani wakubwa wenzangu. Nadhani mnajua hakuna kazi ngumu kama kusoma. Ukiwa mwanafunzi inahitaji sana commitment na kusoma vitu vingine vyote unaviweka pembeni na kupiga shule kama tulivyokuwa tunafanya.

Sasa hawa watoto wetu wa siku hizi hawasomi,kila mtoto msanii (wavulana wanavaa mibato na kunyoa viduku darasani wengine wanasuka nywele),hawajitumi,wanaendekeza mapenzi,kila saa wapo twitter na facebook.
Sasa hapo wanajiua baada ya kufeli. Wasalimie wote huko uendako.
 
Tanzania ni nchi ya ajabu sana ambayo watu wake hawaujali uhai wala kuishi na kuhisi maumivu na matatizo ya wenzi wao.,TUNISIA ALIJICHOMA RAIA MMOJA KWA KUKATAA UNYANYASAJI WATU WOTE WAKAJIHISI UCHUNGU,HAPA KWETU WANAJIUA WATOTO WETU 3-4 KWA UZEMBE WA SERIKALI KUSHINDWA KUWEKA MIPANGO DHABITI NA SAHIHI KUNAKO NYANJA YA ELIMU KUNAKOSABABISHA (WATOTO)WATU WENYE MOYO NA NIA DHABITI YA KUSOMA NA KUSONGA MBELE WANAIKOSA KWA KUNYIMWA AU UZEMBE WA WAZI LAKINI HAMNA ANAYEJALI NA HATA VYOMBO VYA HABARI HAVIONI YA KWAMBA NI HABARI KILA MTU NA LWAKE,Duh!~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~Tujali nini kwani hata wasipojiua si tutawapiga kiberiti kesho watakapokwapua T-shirt na jeans kwa njaa ya kukosa mlo???KUUA,kUJIUA INAKUWA KAWAIDA KWA MTANZANIA HII NI HATARI KUBWA NA TUIKATAE SASA.

Acha kuchukulia kila kitu siasa unakuta mwanafunzi yeye mwenyewe elimu hajaipa kipaombele hajisomei nyumbani unategemea apasi vipi hata kama kawezeshwa vipi.kama kufeli hawakuanza wao wanalao tu.
 
Acha kupotosha watu wewe! Akili zenu hizi za kukariri mambo ndiyo maana mnapachikwa ukamanda usiyokuwa na kichwa wala miguu.

Yule raia wa Tunisia aliyejichoma moto alikuwa ni msomi ila hakupata kazi, akaamua kujiajiri lakini bado serikali yake ikamzingua ndiyo maana wananchi waliungana naye.

Unataka kumfananisha na hawa ambao hata "ordinary level" imewashinda?

Usikariri maisha.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

we ndo mjinga kabisa umekurupuka utadhani umeshindiliwa jiti......ovyo..
 
hii siyo tetesi bali ni habari ya kweli kabisa,na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya wilaya monduli kwa uchunguzi zaidi,lakini taarifa za awali zinasema kuwa marehemu huyo alijaribu kunywa sumu lakini mauti hayakumkuta,mpaka alipo amua kujinyonga usiku wa kuamkia jana na ndipo mauti yalivyo mkuta.
 
Na bado.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mungu wawape ujasili na imani ya maisha mazuri wale wote waliofeli kidato cha nne. Jamani mungu yupo watanzania tusikate tamaa ya maisha, tuzidi kumuomba Mungu atufungulie milango mingine ya mafanikio, atupatie nulu katika giza la matokeo haya, atushike mkono na kutuinua. By Mwl Mwakajila k.
 
Back
Top Bottom