Matiko Matare ni mzima

Matiko Matare ni mzima

Status
Not open for further replies.

kistwangara

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
656
Reaction score
94
Taarifa kwa wanajf,

MATIKO MATARE aliyewahi kuongoza maandamano makubwa chuo kikuu cha dar (UDSM) miaka ya 1990 na kusumbua serikali ya rais Mwinyi pamoja na jaji Warioba, ni mzima wa afya na yupo mkoa wa Ruvuma,tena ni katibu wa kanda ya kusini wa CHADEMA kupitia uchaguzi uliofanyika tar. 17 july 2013 siku ya uzinduzi wa kanda chini ya m/kiti wa CHADEMA taifa MH. Mbowe.

Hivyo kwa wale wanaojua kuwa alifariki si kweli.
 
Ahsante kwa taarifa hii manake tayari kulikuwa na sintofahamu kufuatia uzushi uliokuwa unasambazwa kuwa ametangulia mbele ya haki.
 
Mchawi utamjua tu. We chapa lapa tu unataka ushahidi wa nini na ili iweje? Au wewe ndiye ulimroga na kisha kuanza kueneza habari za uzushi dhidi yake.
[MENTION][JFMP3][/JFMP3][/MENTION]

Anataka kumjua kwa sura inawezekana alikosea mahesabu
 
Kwa vile yuko cdm usalama wake hauna mashaka , walinzi wapo .
 
Shukrani kwa taarifa! Mara nyingi nilikuwa nikiuliza huyu shujaa wa enzi zile pale Mlimani alikuja kupotelea wapi! Na Je vipi kuna mwenye kujua habari za Bazigiza?
 
Taarifa kwa wanajf, MATIKO MATARE aliyewahi kuongoza maandamano makubwa chuo kikuu cha dar (UDSM) miaka ya 1990 na kusumbua serikali ya rais mwinyi pamoja na jaji warioba, ni mzima wa afya na yupo mkoa wa ruvuma Tena ni katibu wa kanda ya kusini wa CHADEMA kupitia uchaguzi uliofanyika tar. 17 july 2013 siku ya uzinduzi wa kanda chini ya m/kiti wa CDM taifa MH. Mbowe. Hivyo kwa wale wanaojua kuwa alifariki si kweli.

Huyo anafaa kuwa chadema kwa sababu chadema wamespecialize kwenye maandamano ya kugomea shughuli za maendeleo...
 
Taarifa kwa wanajf, MATIKO MATARE aliyewahi kuongoza maandamano makubwa chuo kikuu cha dar (UDSM) miaka ya 1990 na kusumbua serikali ya rais mwinyi pamoja na jaji warioba,....

Huyu jamaa alibadirisha "mihula" ya masomo UDSM...!
 
Huyo anafaa kuwa chadema kwa sababu chadema wamespecialize kwenye maandamano ya kugomea shughuli za maendeleo...
Kama hujui kitu ni bora ukauliza kuliko kuanika umbumbumbu! Huyo bwana ndie aliyesababisha chuo kikuu kiwe kwenye status hii ya sasa! Hujui kuwa kabla ya uongozi wake wanafunzi tulikuwa tumejengewa vyoo vya mabati vya nje kujisaidia hall moja na matundu idadi ndogo ya kutisha! Maji chuo yalikuwa historia, chuo kikuu kilikuwa choo kukuuu! hujui ni bora uliza usichangie usicho kijua!
 
Huyu jamaa alibadirisha "mihula" ya masomo UDSM...!

Siyo mihula bali alifanya kuwe na Backlog ya kujiunga na UDSM.

Mkuu Mwita Maranya ni vyema kwa kweli tukapata habari kamili za huyu jamaa pamoja na hata picha ikiwezekana. Mtu kama huyu ambaye alikuwa maarufu wakati ule na kisha kukawa na habari kwamba alikuwa kichaa kisha aktangulia mbele za haki, basi maneno tu yanakuwa hayatoshi. Tupate ushahidi zaidi.

Mkuu Kashishi habari za Bazigiza nazo zimekuwa kama za Matiku Matare. Kuna tetesi zilizagaa kuwa alionekana huko Ngara kisha akatangulia mbele za haki. Kama hawa jamaa wapo ni vyema wakajitokeza na kutuambia kama kweli bado wapo. Pia wanaweza hata kuandika kitabu kuhusu ule mgomo na jinsi walivyouendesha kwa ajili ya historia tu ya UDSM pamoja na nchi kwa ujumla. Ule ulikuwa mgomo mama wa migomo yote tangia UDSM ianzishwe na siamini kwa hali ya sasa kama mgomo kama ule unaweza kutokea tena. Miaka zaidi ya 30 sasa kila kitu kinaweza wekwa wazi na wanaoweza kuweka wazi kila kitu ni pamoja na Matiku, Bazigiza, jamaa mmoja akiitwa Sarungi na wengine kadhaa. Imani yangu ni kwamba mgomo ule ulikuwa ni mikono mingi na si ajabu hata wanasiasa walikuwemo.
 
Kama hujui kitu ni bora ukauliza kuliko kuanika umbumbumbu! Huyo bwana ndie aliyesababisha chuo kikuu kiwe kwenye status hii ya sasa! Hujui kuwa kabla ya uongozi wake wanafunzi tulikuwa tumejengewa vyoo vya mabati vya nje kujisaidia hall moja na matundu idadi ndogo ya kutisha! Maji chuo yalikuwa historia, chuo kikuu kilikuwa choo kukuuu! hujui ni bora uliza usichangie usicho kijua!
Hapo tatizo ni upeo wa maprofesa wenu sio ushujaa wa msababisha migomo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom