Matiko Matare ni mzima

Matiko Matare ni mzima

Status
Not open for further replies.
Kama hujui kitu ni bora ukauliza kuliko kuanika umbumbumbu! Huyo bwana ndie aliyesababisha chuo kikuu kiwe kwenye status hii ya sasa! Hujui kuwa kabla ya uongozi wake wanafunzi tulikuwa tumejengewa vyoo vya mabati vya nje kujisaidia hall moja na matundu idadi ndogo ya kutisha! Maji chuo yalikuwa historia, chuo kikuu kilikuwa choo kukuuu! hujui ni bora uliza usichangie usicho kijua!

Mkuu mahall hayakuwa na vyoo?
 
Weka hata kapicha kake mkuu,wengne hatumjui.

0757282151 ndiyo namba yake.Huyu Bwana tulikuwa naye katika mapambano UDSM kilipofungwa tar 12 Mei 1990 na kufunguliwa tar 1 Januari 1991.Wadogo zangu mambo yalikuwa makubwa. Hapa yupo Ludovick Kashaju Bazigiza, pembeni yupo Ally Salehe, kushoto yupo Sarungi, kulia yupo Harun Kimaro, mie nikiwa kiungo, James Mbatia akiwa winga, golini yupo Adolph Mkenda, Mosena Nyambabe centre half, benchi la ufundi yuko Lugemeleza Nshala na Asha Mzava, Kangi Ligola anaokota mipira,....
Nakumbuka mbali.
 
Taarifa kwa wanajf, MATIKO MATARE aliyewahi kuongoza maandamano makubwa chuo kikuu cha dar (UDSM) miaka ya 1990 na kusumbua serikali ya rais mwinyi pamoja na jaji warioba, ni mzima wa afya na yupo mkoa wa ruvuma Tena ni katibu wa kanda ya kusini wa CHADEMA kupitia uchaguzi uliofanyika tar. 17 july 2013 siku ya uzinduzi wa kanda chini ya m/kiti wa CDM taifa MH. Mbowe. Hivyo kwa wale wanaojua kuwa alifariki si kweli.

Angalizo: Usalama wa Taifa wakati ule walikamata wasumbufu (au niseme walioonekana kuwa wasumbufu), waliwafunga vitambaa machoni wasione wanaenda wapi, walifichwa mahali kwa muda wakifanya mahojiano kutumia mbinu za kisaikolojia BILA KUTHURU MWILI vibaya. Hawakuwavuta pumbu, hawakuwang'owa meno, hawakuwatobowa macho. Kama yupo atatoa ushahidi huu naamini.
 
0757282151 ndiyo namba yake.Huyu Bwana tulikuwa naye katika mapambano UDSM kilipofungwa tar 12 Mei 1990 na kufunguliwa tar 1 Januari 1991.Wadogo zangu mambo yalikuwa makubwa. Hapa yupo Ludovick Kashaju Bazigiza, pembeni yupo Ally Salehe, kushoto yupo Sarungi, kulia yupo Harun Kimaro, mie nikiwa kiungo, James Mbatia akiwa winga, golini yupo Adolph Mkenda, Mosena Nyambabe centre half, benchi la ufundi yuko Lugemeleza Nshala na Asha Mzava, Kangi Ligola anaokota mipira,....
Nakumbuka mbali.

Nilikuwa form one hapa mkuu na nakumbuka mgomo huu mlirudishwa nyumbani alafu wananchi tukaandamana kulaani mgomo wa UDSM, au nimekosea?
 
Angalizo: Usalama wa Taifa wakati ule walikamata wasumbufu (au niseme walioonekana kuwa wasumbufu), waliwafunga vitambaa machoni wasione wanaenda wapi, walifichwa mahali kwa muda wakifanya mahojiano kutumia mbinu za kisaikolojia BILA KUTHURU MWILI vibaya. Hawakuwavuta pumbu, hawakuwang'owa meno, hawakuwatobowa macho. Kama yupo atatoa ushahidi huu naamini.

Enzi hizo serikali ilikuwa inafanya kazi kwa ueledi na iliheshimika sana, sasa hivi unaminywa korodani sijui wapi lakini watu bado wanakomaa
 
Wakati huo tuna RTD(Radio Tanzania Dar-es-salaam),nakumbuka hilo jina.MATIKO MATARE ndiyo lilikuwa la kwanza kutajwa kwenye taarifa ya habari kwamba ni kati ya wanafunzi waliofukuzwa UDSM.Kuna uzi humu unaelezea hao mashujaa wa Elimu.
 
0757282151 ndiyo namba yake.Huyu Bwana tulikuwa naye katika mapambano UDSM kilipofungwa tar 12 Mei 1990 na kufunguliwa tar 1 Januari 1991.Wadogo zangu mambo yalikuwa makubwa. Hapa yupo Ludovick Kashaju Bazigiza, pembeni yupo Ally Salehe, kushoto yupo Sarungi, kulia yupo Harun Kimaro, mie nikiwa kiungo, James Mbatia akiwa winga, golini yupo Adolph Mkenda, Mosena Nyambabe centre half, benchi la ufundi yuko Lugemeleza Nshala na Asha Mzava, Kangi Ligola anaokota mipira,....
Nakumbuka mbali.

Asante sana.
 
Hapo tatizo ni upeo wa maprofesa wenu sio ushujaa wa msababisha migomo.
Unajua unaongea nini? Maprofessor ndio wanaojenga vyoo au ndio mamonitor? umeshawahi kuwa chuokikuu? manaake unaonyesha hujui system inavyofanya kavi! Maprof sio kama walimu wa primary au secondary nadhani ndio ideal yako!
 
Unajua unaongea nini? Maprofessor ndio wanaojenga vyoo au ndio mamonitor? umeshawahi kuwa chuokikuu? manaake unaonyesha hujui system inavyofanya kavi! Maprof sio kama walimu wa primary au secondary nadhani ndio ideal yako!
Kwahiyo maprofesa nao walikuwa wanajisaidia kwenye vyoo vya shimo? Mkuu wa chuo naye alikuwa anakuja kazini kwa miguu?
 
Nilikuwa form one hapa mkuu na nakumbuka mgomo huu mlirudishwa nyumbani alafu wananchi tukaandamana kulaani mgomo wa UDSM, au nimekosea?

Siku hiyo mabehewa yote ya TRC ya daraja la pili kulala tuliyachukua yote Kanda ya Ziwa. Alafu nyie madogo mkaandamana kutuzomea. Lipi kipindi cha mazungumzo baada ya habari cha Mzee Sozigwa wakasema LY alijiona msomi akavaa kaptula kichwani. Tumeanza ukombozi kwa suluba.
 
Siyo mihula bali alifanya kuwe na Backlog ya kujiunga na UDSM.

Mkuu Mwita Maranya ni vyema kwa kweli tukapata habari kamili za huyu jamaa pamoja na hata picha ikiwezekana. Mtu kama huyu ambaye alikuwa maarufu wakati ule na kisha kukawa na habari kwamba alikuwa kichaa kisha aktangulia mbele za haki, basi maneno tu yanakuwa hayatoshi. Tupate ushahidi zaidi.

Mkuu Kashishi habari za Bazigiza nazo zimekuwa kama za Matiku Matare. Kuna tetesi zilizagaa kuwa alionekana huko Ngara kisha akatangulia mbele za haki. Kama hawa jamaa wapo ni vyema wakajitokeza na kutuambia kama kweli bado wapo. Pia wanaweza hata kuandika kitabu kuhusu ule mgomo na jinsi walivyouendesha kwa ajili ya historia tu ya UDSM pamoja na nchi kwa ujumla. Ule ulikuwa mgomo mama wa migomo yote tangia UDSM ianzishwe na siamini kwa hali ya sasa kama mgomo kama ule unaweza kutokea tena. Miaka zaidi ya 30 sasa kila kitu kinaweza wekwa wazi na wanaoweza kuweka wazi kila kitu ni pamoja na Matiku, Bazigiza, jamaa mmoja akiitwa Sarungi na wengine kadhaa. Imani yangu ni kwamba mgomo ule ulikuwa ni mikono mingi na si ajabu hata wanasiasa walikuwemo.

Pia kulikuwa na Dr. Kimaro pale Muhimbili
 
Siku hiyo mabehewa yote ya TRC ya daraja la pili kulala tuliyachukua yote Kanda ya Ziwa. Alafu nyie madogo mkaandamana kutuzomea. Lipi kipindi cha mazungumzo baada ya habari cha Mzee Sozigwa wakasema LY alijiona msomi akavaa kaptula kichwani. Tumeanza ukombozi kwa suluba.

Mkuu ulikuwa ukiripoti kwa mkuu wa Wilaya kila mwezi?
 
Huyo anafaa kuwa chadema kwa sababu chadema wamespecialize kwenye maandamano ya kugomea shughuli za maendeleo...
Na hao wasioandamana wala kugomea shughuli za maendeleo wanafanya hizo shughuli za maendeleo maana maendeleo yenyewe hatuyaoni zaidi ya Propaganda uchwala.
 
Mchawi utamjua tu. We chapa lapa tu unataka ushahidi wa nini na ili iweje? Au wewe ndiye ulimroga na kisha kuanza kueneza habari za uzushi dhidi yake.

Kwa nini hutaki aweke picha? Yawezekana akawa matiko feki au mtu anatumia vyeti vya marehemu.
 
Taarifa kwa wanajf, MATIKO MATARE aliyewahi kuongoza maandamano makubwa chuo kikuu cha dar (UDSM) miaka ya 1990 na kusumbua serikali ya rais mwinyi pamoja na jaji warioba, ni mzima wa afya na yupo mkoa wa ruvuma Tena ni katibu wa kanda ya kusini wa CHADEMA kupitia uchaguzi uliofanyika tar. 17 july 2013 siku ya uzinduzi wa kanda chini ya m/kiti wa CDM taifa MH. Mbowe. Hivyo kwa wale wanaojua kuwa alifariki si kweli.


Nimefarijika sana kusikia ili jembe bado liko hai. Anafanya nini huko Ruvuma?

Tiba
 
Huyu Bwana Matiko Matare mara ya mwisho katufundisha Musoma Tech High School 2003-2004 then usalama wakamuondoa akahamia Mwembeni Sec, after that alinambia personally 2007 tukiwa Musoma na baadaye pale UDSM kuwa anasoma Masters Open na alikuwa mbioni ku-secure Scholarship MISRI. Ni mpambanaji na hakika alitufundisha kujua na kutetea haki zetu; sishangai kusikia yupo CHADEMA!!! Nice to get his Mobile number, tutamtafuta.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom