Nafikiri kipengele kidogo cha 7 cha kipengele cha 33 katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, 2004 kinajibu swali lako kuhusu jambo hili. Ukisoma kipengele chote cha 33 ukifika kipengele kidogo cha 7 kinasema hivi kwa Kiingereza:
"(7) Notwithstanding the provisions subsection (6)(a), an employee is
entitled to an additional 84 days paid maternity leave within the leave
cycle if the child dies within a year of birth."
Ingawa inasemwa within a year of birth, nafikiri wasomi wenzangu wanaweza wakafafanua zaidi kama hiyo phrase inahusu pia kifo cha mtoto wakati wa kuzaliwa. I submit.
naomba muongozo, hivi hawa house girls wanalindwa kisheria hapa Tanzania? na ikitokea akapata ujauzito akiwa kazini sheria inasemaje?
Housegirl/houseboy or mfanyakazi yoyote wa nyumbani anatambulika na analindwa na sheria reje vifungu vifuatavyo kwa ufafanuzi zaidi , section 4 ot the Employment and Labour Relations Act No.6 of 2004 na section 61 of the Labour Institutions Act.No.7 of 2004.
Kwa maana hiyo kama housegirl akipata mimba kazini inabidi umpe likizo yake ya uzazi siku 84 kama sheria inavyosema. Sio lazima umwambie aende kwao au huko kwa aliyempa mimba kutegemea na circumstances anaweza kuendelea kuwa hapo nyumbani but discharge her from her duties and let her take care of the baby wakati naye akiendelea kurecover kiafya baada ya kujifungua.
Kwa mujibu wa sheria, mfanyakazi akipata ujauzito anaenda likizo ya uzazi (maternity leave) kwa siku 84, je ikitokea bahati mbaya baada au wakati wa kujifungua mtoto akafariki bado ataendelea na likizo yake ya uzazi?