Matatizo ya afya ya akili (kwa wanafunzi na walimu) mashuleni, wanasaikolojia (Educational Psychologists) waajiriwe kupunguza matatizo.

April26

JF-Expert Member
Jul 14, 2020
1,403
2,118
Habari ya weekend wakuu.

Kuna kozi mbalimbali za saikolojia (afya ya akili) zinazotolewa na vyuo vyetu hapa Tanzania kwa ngazi mbalimbali.

Kuna wahitimu wengi ambao wanafaa sana kuwa kwenye shule na vyuo vyetu kama wanasihi/washauri (school counselors) lakini wapo mtaani au wanatumika sehemu nyinginezo.

Mfano: waliosoma Bachelor of Education in Psychology, huu ni mfano mmoja tu lakini zipo kozi nyingine,,,,hawa ni special kwa kuwa wanasihi mashuleni kuhakikisha wadau wa elimu kuanzia wanafunzi, walimu, wazazi na viongozi wanakuwa fit psychologically kimaadili na kimaamuzi ili kulinda na kutoathiri lengo la elimu Tanzania.

Nafahamu kuwa kila mwalimu anagusa baadhi ya kozi za saikolojia ya watoto, lakini sio kama wale wataalamu waliosoma programme nzima. Kuna upungufu kiutendaji kwa baadhi ya walimu na means of counseling service aproaches inakuwa sio effective kiasi kinachotakiwa.

Kumekuwa na matukio mengi sana mashuleni ambayo kwa % kubwa chanzo chake ni matatizo ya kisaikolojia yanayopelekea tabia, maamuzi na matokeo mabaya.

Hawa wataalamu waajiriwe mashuleni kunusuru majanga kwa wanafunzi na walimu. Wizara husika inafahamu na vyuo wamewafunza hawa wataalamu kwa lengo hilohilo.

Sidhani kama chuo kinaweza kujipangia kozi za kufundisha bila kuwasiliana na gvt na bila kuangalia uhitaji.

Kama zamani palikuwa hapajaonekana uhitaji kwa sasa hata kama huna macho wala masikio ukipapasa utaona uhitaji ni mkubwa sana.

Bila shaka nimeeleweka lengo langu la kufikisha ujumbe kwa wadau ambao naamini wamo humu.

Ahsante!
 
Majanga Kama mwalimu kupiga mwanafunzi hadi kuuwa au kumpga mwanafunzi hadi kumsababishia ulemavu? Au mwanafunzi kuichukia Shule na kuanza kuwadharau walimu? Nadhani mleta hoja umejikita huko eeh? Nikweli baadhi ya walimu na wanafunzi wanamatatizo ya kisaukolojia hivyo pawepo watu kama hao ili kunusuru majanga.
 
Majanga Kama mwalimu kupiga mwanafunzi hadi kuuwa au kumpga mwanafunzi hadi kumsababishia ulemavu? Au mwanafunzi kuichukia Shule na kuanza kuwadharau walimu? Nadhani mleta hoja umejikita huko eeh? Nikweli baadhi ya walimu na wanafunzi wanamatatizo ya kisaukolojia hivyo pawepo watu kama hao ili kunusuru majanga.
Kabisa kabisa mkuu hayo tajwa ni machache kati ya mengi. Hali si shwari mashuleni.
 
Nadhani shida ni kubwa sana kila kona kwa hii nchi. Kuna mindset ya kuwa mtoto kumtia adabu ni kumcharaza sana.

Kiufupi ukipita huko mitaani usiposikia mama anacharaza mtoto wake analia mpaka mtaa wapili basi ujue ni mchana wa weekday watoto wapo shuleni.

Pia huko huko mitaani usiku nyumba moja ukisikia milio ya starehe za wenye mji nyumba ya pili unasikia baba flani unaniuaaaa.

So what's wrong:- my opinion:-
Nchi ina hali ngumu ya kimaisha. Watu wengi wanaopitia misongo ya mawazo na matatizo ya afya ya akili ni wale ambao hali ya kimaisha ni duni.

Nchi hii imefikia watu wakiwa duni kuonekana wazembe. Nchi yenye ardhi iliyojaa rutuba kuwa na unga wa mahindi unaouzwa zaidi ya 2000 ni ajabu sana, ile 1000 per kg tu ilikuwa too much kwa average person. Ilifaa kuwa below 500 per kg.

Tanzania isipoweza kuwahakikishia wananchi wake milo mitatu, maendeleo yake yatakuwa temporary sana. Nchi haiwezi kuendelezwa na watu waliojaa msongo. Zaidi ya 50% ya watoto hufundishwa na walimu wenye uduni wa kipato. Watoto hao hao ndio waje waendeleze nchi.
 
Nadhani shida ni kubwa sana kila kona kwa hii nchi. Kuna mindset ya kuwa mtoto kumtia adabu ni kumcharaza sana.

Kiufupi ukipita huko mitaani usiposikia mama anacharaza mtoto wake analia mpaka mtaa wapili basi ujue ni mchana wa weekday watoto wapo shuleni.

Pia huko huko mitaani usiku nyumba moja ukisikia milio ya starehe za wenye mji nyumba ya pili unasikia baba flani unaniuaaaa.

So what's wrong:- my opinion:-
Nchi ina hali ngumu ya kimaisha. Watu wengi wanaopitia misongo ya mawazo na matatizo ya afya ya akili ni wale ambao hali ya kimaisha ni duni.

Nchi hii imefikia watu wakiwa duni kuonekana wazembe. Nchi yenye ardhi iliyojaa rutuba kuwa na unga wa mahindi unaouzwa zaidi ya 2000 ni ajabu sana, ile 1000 per kg tu ilikuwa too much kwa average person. Ilifaa kuwa below 500 per kg.

Tanzania isipoweza kuwahakikishia wananchi wake milo mitatu, maendeleo yake yatakuwa temporary sana. Nchi haiwezi kuendelezwa na watu waliojaa msongo. Zaidi ya 50% ya watoto hufundishwa na walimu wenye uduni wa kipato. Watoto hao hao ndio waje waendeleze nchi.
Umeongea kwa uchungu sana mkuu. Ukweli ni huo kuwa msongo wa mawazo umejaa hata kwa wale tu aotegemea waje wasaidie nchi ndiyo hao walioharibikiwa.

Hatua za makusudi zichukuliwe !!
 
Umeongea kwa uchungu sana mkuu. Ukweli ni huo kuwa msongo wa mawazo umejaa hata kwa wale tu aotegemea waje wasaidie nchi ndiyo hao walioharibikiwa.

Hatua za makusudi zichukuliwe !!
Nikiiangalia Tanzania huwa naumia sana mana haina muelekeo unaoeleweka. Hivi seriously tunashindwa kuwapa chakula watoto wetu wanapojifunza?

Mtoto anashinda shuleni anakula chama, ubuyu, etc. Mwanafunzi wa chuo kikuu anapiga pasi ndefu? Seriously kwa karne hii? Sijui nani kairoga hii nchi.

Kila taifa litavuna linachokipanda. Mtu anakuwa UDSM anapiga pasi ndefu anatembea chuo to hostel. Vyuo vingi vina shida wanafunzi wana ukata wa kipato.

Yet hao hao ndio watakabiziwa maofisi na baadae uongozi waeneleze nchi, seriously? Watakapoamua kusema dah acha nifidie mateso nilopitia, kitachotokea ni nchi kuvurugika mana kila mtu atajiangalie yeye binafsi.

It's really painful for sure.
 
Tuanze kutengeneza watoto tokea chini na tuwezeshe wale wanao wafundisha ili kuleta tija kwenye elimu.

School Counselors ni mhimu sana kuliko fikra fupi zisizofikia maono halisi yanayo ona athari.
 
Emotional intelligence is far more of Paramount importance than high iq.
Huyu jamaa akaongea ishu za Mana mno. Hata huko nje Hakuna taasisi isiyo na mtalaaamu wa Mambo ya saikolojia. Huku watu wanachukuliana poa. Emotions shit is more big and toughest than you. They control you and they have you and you don't have them.
 
Tuanze kutengeneza watoto tokea chini na tuwezeshe wale wanao wafundisha ili kuleta tija kwenye elimu.

School Counselors ni mhimu sana kuliko fikra fupi zisizofikia maono halisi yanayo ona athari.
Kwa maoni yangu kwanza Afrika itatue shida ya njaa. Nusu ya magonjwa ya Afrika hutokana na lishe duni. 70% ya wagonjwa wa akili wana stress za uduni wa maisha na 10% wanapitia wakati mgumu kwenye mapenzi na wanavumili mana ni tegemezi kiuchumi.

Mwanamke anaishi na mwanaume mkatili kwa kuhofia maisha kwamba akitoka ataenda wapi. Mchana mtu akimkwaza kidogo tu anafunga mtaa kutukanana na kusutana na jirani.

Watoto wanashuhudia wazazi wakipigana, wakitukanana, wakisutana, etc. Ukipita uswahilini kila siku mchana kuna japo mtaa mmoja watu wanatukanana hadharani, wanasutana, wanagombana na watoto wanaotoka shule wakikutana na issue kama hizi wanasimama kushangaa kwanza. So saikolojia yao hujengeka anzia udogo kuwa ukimkwaza solution ni kukutukana ama kupigana.

Unam counsel mwenye njaa anawaza home akirudi jiko limenuna. Unajua usipofanya tafiti huwezi liona tatizo la njaa.

Ila waliopita sensa wanajua mengi na hili la kushindwa kumudu milo mitatu limetokea kwenye fomu nyingi sana za familia za kawaida na za chini.
 
Walimu wote wanasoma educational psychology hila hayo yote matatizo yanasababishwa na pressure kutoka kwa viongozi wao wa juu
Educational paychology ni Programe kabisa mkuu hao walimu wanasoma course tu sijui ndo modules.

Hawachimbi ndani kama mtu anaesoma Educational psychology as a degree programe.

Mfano mwalimu anaechukua degree ya history anasoma vi module kidogo kidogo kuhusu saikolojia ya watoto.

So hawezi kuwa master wa saikolojia.

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Educational paychology ni Programe kabisa mkuu hao walimu wanasoma course tu sijui ndo modules.

Hawachimbi ndani kama mtu anaesoma Educational psychology as a degree programe.

Mfano mwalimu anaechukua degree ya history anasoma vi module kidogo kidogo kuhusu saikolojia ya watoto.

So hawezi kuwa master wa saikolojia.

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForumsmo

Educational paychology ni Programe kabisa mkuu hao walimu wanasoma course tu sijui ndo modules.

Hawachimbi ndani kama mtu anaesoma Educational psychology as a degree programe.

Mfano mwalimu anaechukua degree ya history anasoma vi module kidogo kidogo kuhusu saikolojia ya watoto.

So hawezi kuwa master wa saikolojia.

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Najua cpo mbali na wew hla usiangalie jina la coz ukajua basi ndio ukajua ni wabobevu wa hcho kitu c kweli mimi nilikimbiaga chuo miaka hiyo hila kwa kiasi fulani niliona mambo yanavyoenda hvi unajua kuna degree program inaitwa bachelor of education in early childhood education Hawa wanasoma coz nyingi za psychology kuliko bachelor of education in psychology ?.
 
Back
Top Bottom