Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Ha ha ha tumekula sana mizizi ile tukiamin machine inakaa sawa

Busy kuoga mto Rau kipindi kama hichi

Sa hiv maji hata kisigino hayafiki

Mamaeeh! Nishakudaka hahahaaaaa!! ukiitumia sana inakuwa mitamu kinoma. Nadhani ni addiction ile, tulikuwa tunachimba mingi tunakula sana! Sikuona changes zozote zaidi ya kuipenda tuu
 
Ha ha ha tumekula sana mizizi ile tukiamin machine inakaa sawa

Busy kuoga mto Rau kipindi kama hichi

Sa hiv maji hata kisigino hayafiki

Rau sikuogelea sana sababu ya wizi wa watoto wa Kwamtei!! Kuna madogo walikuwa maarufu enzi hizo kwa utundu na wizi!! Wenzao wanaogelea wao wanaficha nguo zao!!

Lakini pia nilikuwa muoga sana wa maji kuna dogo alisombwa na maji pale kwenye boda la kutoka kwaMtei kwenda Msaranga ingawa aliokolewa lakini kwangu ilikuwa shule tosha.
 
Rau sikuogelea sana sababu ya wizi wa watoto wa Kwamtei!! Kuna madogo walikuwa maarufu enzi hizo kwa utundu na wizi!! Wenzao wanaogelea wao wanaficha nguo zao!!

Lakini pia nilikuwa muoga sana wa maji kuna dogo alisombwa na maji pale kwenye boda la kutoka kwaMtei kwenda Msaranga ingawa aliokolewa lakini kwangu ilikuwa shule tosha.
Ni wapi huko maana nimesoma Majengo sekondari iko upande upi huo
 
Kinu...!!!!!! kocha simbaa!!! tupo wengi aise au ilikua inakaukweli maana nmetafuna sana labda ndio sababu bado sijakubwa na Janga la taifa...
Ata mimi nilikuwa natafuna na big G na Bubble gum ila sijawahi ona ila kuna jamaa angu mmoja alikuwa anaitwaga Salim alikuwa na bonge la boloo kipindi hicho tuko msingi na mimi nikataka niwe nalo ila sasa siri yangu
 
Naskia mkongoraa unarefusha naniliu kuna ukweli hapo

Si kweli! Tumekula sana hiyo mizizi toka darasa la tatu mpaka la sita nikajiondoa kwenye hilo kundi nikaanza kupambana na maisha ya shule!!

Hakuna hata mmoja anaweza kukupa ushahidi wa kuongeza nguvu za kiume wala kukuza uume!

Nilichogundua ni kwamba unakuwa addicted nayo, mnajikuta tu mnaenda porini kuchimba kwa wingi kwa ajili ya kula tu!!
 
Ni wapi huko maana nimesoma Majengo sekondari iko upande upi huo

Kukuelekeza ni ngumu lakini kuna njia ya shortcut inayotoka Majengo Kwamtei inakwenda Msaranga. Wakati huo soko la mitumba lipo Kiborloni ilikuwa ndiyo njia kuu ya watembea kwa miguu!!

Kuna sehemu unaukuta mto Rau ila hapo hakuna daraja, kama maji ni machache mnakanyaga mawe mnavuka ila kama ni mengi mnatumbukia kwenye maji!!

Kwa juu kidogo palikuwa na pool humo humo mtoni na nahisi lilitokana na wachimba mchanga! Ndipo ilikuwa sehemu maarufu kuogelea ukiacha pale Kingston darajani walipokuwa wanaosha na magari!!

Kwenye kuvuka sasa! Maji yanapokuwa mengi ukileta usambwina yanakuondoa vizuri tuu
 
jmushi1 historia ya Moshi yote iko kichwani mwako,
Hivi nani alikuwa anamiliki Changbay ?

Hebu tukumbushe kuna basi lilikuwa linaenda Arusha likatumbukia mto Karanga

Nikiwa mdogo nakumbuka KCMC kulikuwa na mgonjwa alikuwa amepooza alikuwa mshabiki wa Yanga aliitwa Mrema wikiendi watu wengi walikuwa wanaenda kumtembelea alilazwa pale zaidi ya miaka 10

Kulikuwa na Mzee Athuman Mwariko alikuwa na kikundi cha sanaa kuna kipindi aligombea ubunge Moshi Mjini
Mangi mwenye Changbai ni Mama Changbai mwenyewe jina lake ndio hilo hilo tangu miaka ya nyuma anajulikana kwa mishe za misosi Moshi na uuzaji wa Maua.
 
Changbay inamilikiwa na mama mmoja hivi ambaye alianza kuwa maarufu kwa jina la “mama kuku”.

Basi lilotumbukia mto Karanga, lilikuwa likiitwa Safina! Kuna watu walitajirikia pale, maana wafanyabiashara enzi hizo walisafiri na kiasi kikubwa cha pesa kwenda kununua bidhaa kutoka Dar to Nairobi, Arusha na Moshi.

Mzee Mwariko sina uhakika kuhusu alipo kwa sasa, ila alikuwa na gallery maeneo ya Dar St kama sikosei ilikuwa ikiitwa Mwariko’s Art Gallery. Enzi hizo mzee Makassy akiwepo kama sikosei.
Mangi kuhusu mama kuku sio huyo mwenye changbai na hilo jina la kuku ni nickname yake yeye anaitwa "MAMA FEI" alikuwa pia na mchongo KCMC huyu alijulikana kwa kuuza sana makuku ya broiler kipindi hicho hayajajulikana sana ana ofisi Moshi na Arusha kama sijasahau maeneo ya Usa River.
 
Mangi kuhusu mama kuku sio huyo mwenye changbai na hilo jina la kuku ni nickname yake yeye anaitwa "MAMA FEI" alikuwa pia na mchongo KCMC huyu alijulikana kwa kuuza sana makuku ya broiler kipindi hicho hayajajulikana sana ana ofisi Moshi na Arusha kama sijasahau maeneo ya Usa River.
Mama fei kabibi flani hivi kakizungu
 
Back
Top Bottom