Matabaka yanavyoitafuna CHADEMA na kuvuruga Ustawi wa chama chetu

Matabaka yanavyoitafuna CHADEMA na kuvuruga Ustawi wa chama chetu

Albert Einstein

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2017
Posts
394
Reaction score
583
CHADEMA haipo salama hata kidogo kutokana na kuwepo kwa matabaka ndani ya chama hicho yana wakatisha tamaa wanachama wa chini wenye mapenzi ya dhati na chama hicho. Ni ajabu sana kuona ndani ya chama kimoja kunakua na matabaka zaidi ya saba.

Tabaka la viongozi wakuu akiwamo Mwenyekiti Mbowe wao kazi yao ni kuzunguka na ndege kwenda kula raha kwenye mataifa mbalimbali bila ya kueleza lengo la ziara, matumizi na faida ya safari kwa chama.

Makundi mengine ni viongozi wa Kanda, Mabaraza, Mameya na Wabunge, Wajumbe wa kuchaguliwa, Sekretarieti, na wale wenye kazi isiyojulikana. Kwaujumla, makundi haya yote niliyoyataja ni miongoni mwa wapiga dili ndani ya CHADEMA wasiozoeleka kirahisi.

Kundi la mwisho ni la wale kajamba nani, yaani pangu pakavu tia mchuzi. Kundi hili ndio kubwa sana ukilinganisha na mengine. Hawa ndio wanaolipa michango ya uanachama na fedha hizo ndizo hutumiwa na wavimba matumbo.

Kundi hili la daraja la mwisho, ndio lina kazi ya kuyavusha makundi mengine. Pia hujulikana kama bendera fuata upepo yaani wakiambiwa waandamane huandamana, hukanyagana na kuuana wenyewe kwa wenyewe huku waliowaambia waandamane wakiwa na familia zao nyumbani wakila kuku.


Morely John,
Mwanachama, Chadema,
Moshi.
 
Kundi la mwisho ni la wale kajamba nani, yaani pangu pakavu tia mchuzi. Kundi hili ndio kubwa sana ukilinganisha na mengine. Hawa ndio wanaolipa michango ya uanachama na fedha hizo ndizo hutumiwa na wavimba matumbo.

Kundi hili la daraja la mwisho, ndio lina kazi ya kuyavusha makundi mengine.
Niwataje wachache Hili kundi wamo Akina Malisa,Salary slip,Mdude na Goliath Mfalamagoha.
 
Kwani kabla ya Chadema hakukuwa na maisha? Kuna watu wanafikiri wakiiharibu Chadema ni kama vile wamemharibia maisha mtu fulani. Hayo ni mawazo finyu.

Wewe ukiona unatamani kuwa mwanachama wa CCM hakuna haja ya kuleta chokochoko kwenye chama kama Selasini, bali ni kuondoka tu basi. Maisha yataendelea hata kama wewe hutakuwa mwanachama wa Chadema.

Mtu una uhuru wa kuwa katika chama ukipendacho, sasa kila wakati ni kumwandama tu Mbowe na Chadema. Shida ni nini? Kwani ni nani kawakataza msiende huko mkaunge mkono juhudi za Jiwe?
 
Albert Einstein,

Unaona huu unafiki?

Unaona Mwenyekiti wa Taifa ni sawa na Katibu Wa Chama wa Kata?

Yaani Magufuli akisafiri kwa Ndege kwenda Zanzibar kutangaza chama chake unataka na wewe Mwenyekiti wa Chama wa Wilaya upakie ndege?

Una hoja za kimaandazi sana

Unajaribu ku-propagate hateful claims ambapo ni normal practice across the political divide in the country!

Mwenyekiti wa Chama Taifa akipakia ndege ng’ombe kama wewe unalalamika?

Really?
 
Zamani kulikuwaga na post kama hizi zilikuwa zinaletwana kina Tuntemeke, baadae mgao ulipokata kwa kina Mwigulu na yeye akaacha kupost.
 
Wewe mwanaFisiem pambana huko lumumba,makundi zaidi ya saba halafu umetaja matatu tu,unafiki umeanzia hapo!
Mwenyekiti wa CDM taifa unataka awe kama mwenyekiti wa kijiji?Mbona Magufuli anachukua ndege ya ATCL Airbus kwa safari zake kwenda kupumzika Chato?Sisi wananchi tunazipanda?
 
Hakuna matabaka yoyote ndani ya chama.Kutofautiana mawazi sio matabaka hayo.Hata ndani ya familia moja kuna matabaka.Huwezi kumtendea kaka mkubwa kama unavyomfanyia kifunga-mimba.Uwepo wa matabaka ndio unafanya chama kisonge mbele kwa sababu hayo ni matabaka ambayo hayana uhasi.Na uzuri wa CDM mwenyewe anaehitaji kuondoka magufuli anasajili masalia na makapi ya CDM kwa hiyo akina selasini na akina Mwambe wakienda CCM hawakosi vyeo.Kama Waitara anavyeo ccm selasini na Mwambe wanaweza pewa hata uPM.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CHADEMA hii sasa imegeuka kuwa chama cha wajaza matumbo yao tu. Maana ni kama hawana hoja ambayo itawafanya kuikabiri au kuisumbua CCM chama kinachotawala. Wakati wa Dk slaa kilikuwa chama kweli ambacho kilipigania maslahi ya wanyonge.

CCM iliyokuwa imechafuka kwa kukumbatia ufisadi iliwapa mwanya wa kuonekana kuwa chama kinachotakiwa kukabidhiwa dola ili kulinda mali za Watanzania zilizokuwa zinaibiwa. Lakini hoja ya ufisadi haipo tena sababu kuna watu wamedhibiti. Sasa kilichobaki chadema ni kuuza sura na kudili na ishu ambazo hata hazina mashiko.

Kwani ufisadi tu ndio mnadhani ndio kick katika siasa? Hamuwezi kuwa creative? Chama kimekuwa mufu. Au sababu jamaa waliopo madarakani wanafukia kila shimo!
 
Back
Top Bottom