Nashindwa kumuelewa Nape! Saizi ndio kakutwa na uchungu mwingi zaidi na wananchi! Au ndo ameshushwa saizi Tanzania kutoka kusikojulikana?
Kutumika na wenye pesa ni shida sana, utauza utu wako na hata kuonekana huna maana tena katika jamii. Ajitafakari upya, siasa anazozifanya sasa ni za chuki na kutoheshimu sera ambazo yeye mwenyewe alihusika katika namna moja ama nyingine katika kuzitengeneza.
Tuamini lipi kutoka kwake? Amekua kigeugeu eti serikali haitendi haki kwa wananchi wake, mara ooh! maisha ya wananchi yamekuwa magumu!
Turejee nyuma kauli za viongozi wa vyama vya sasa hapo siku za nyuma na kuona wanachokiongea sasa ndipo utagundua mtu huyu anafanana na nani na anafanya hayo yote kwa maslahi ya nani?
[HASHTAG]#Katika[/HASHTAG] Awamu ya nne: Rais Kikwete ameshindwa kuwashughulikia Watendaji wazembe, Mafisadi na Wala rushwa,,,,Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa Raisi Kikwete, Atakaye Muunga mkono Lowassa katika uchaguzi ndani ya CCM anastahili kwenda kupimwa akiri yake Milembe Hospital,Rais wetu Kikwete anasafiri sana kuliko Rais yeyote Duniani, Tunataka Rais ajaye awe ni mwenye Maamuzi makini na sahihi ya papo kwa papo nasio mpaka tume iundwe. Tunataka Rais ajaye awe ni Dikteta ndio nchi Itakwenda.Mafisadi kwetu ni Mwiko, Serikali ya CCM inawafunga wezi wa kuku halafu inawaacha Mafisadi papa kama Lowassa yanatembea mtaani tu.. Hizi ni Miongoni mwa kauli kutoka kwa viongozi wa Upinzani katika Awamu ya nne.