Maswali ya Watanzania kwa Mzee Lowassa

Maswali ya Watanzania kwa Mzee Lowassa

mzugaji tuh huyo mzee, anaendelea kutuonesha maigizo hana lolote.katika hotuba zote mbili kama anajua matatizo ya wananchi kiukweli angekua ameshayajibu hayo maswali
 
YAANI CCM MNAHANGAIKA NA LOWASSA NA UKAWA HADI MNAMSAHAU MAGUFULI WENU,hahaha...Lowassa anawanyima usingizi,poleni sana

Mimi nadhani kuna haja ya kuzipima akili zetu, maana tunaona lakini hatufahamu. Tunaacha kuyafikiria mambo ya msingi na kupata majibu ya maswali haya, tunaleta ushabiki. Kama ushabiki basi CCM itashinda maana ndiyo ina mashabiki wengi, UKAWA ina vyama vinne, CCm kipo peke yake lakini jaribu kupima mafuriko uone,

20150830001525 (1).jpg
 
Umenena kiongozi, wakipata maswali ya majibu haya, basi IKULU wataingia, kura tutawapa
 
YAANI CCM MNAHANGAIKA NA LOWASSA NA UKAWA HADI MNAMSAHAU MAGUFULI WENU,hahaha...Lowassa anawanyima usingizi,poleni sana

Lowassa Amegeuka Kua "Kituko" Cha Mjini.Ngoja Tumzungumzie Ili Tuongezea Siku Za Kuishi.Vituko Usanii Maigizo Ya Lowassa Vinatupa Afya
 
Baada ya kufuatilia hotuba yako ya ufunguzi wa kampeni za UKAWA jangwani kwa umakini mkubwa, naomba Mzee Edward Ngoyai Lowassa unisaidie mimi na wananchi wenzangu wa TANZANIA kujibu maswali haya;



  1. WANAMABADILIKO;
Watanzania wamechoshwa na Rushwa, wanachukia UFISADI, Mzee unamkakati gani dhidiya wala rushwa na mafisadi..?



  1. MAMA NTILIE;
Kilio chetu ni juu ya mgambo kutusumbua na mazingira mabovu ya biashara,tukakulalamikia bei kubwa ya vyakula na mazao, jibu letu liko wapi..?au atakuja kutujibu Babu Seya ukishamtoa jela..?



  1. MADALADALA;
Mzee tulikubeba kutoka Masaki mpaka Gongo la mboto, njia nzima tukikueleza kero zetu, Hatujakusikia ukisema kitu kuhusu usumbufu wa Traffic na kutunyang'anya leseni zetu..?



  1. WAKAZI WA DAR;
Mzee tumekupa mapokezi ya kufa mtu, lakini unajua kuwa tumeamka saa kumina moja alfajir ili kuwahi mkutano wako wa saa tisa Jangwani, Tatizo la foleni na shida ya Usafiri haujazungumzia kabisa...Mzee umetusahau..?



  1. WANAFUNZI;
Elimu bure kutoka shule ya msingi mpaka chuo kikuu, sawa ila Mzee kwa mapato gani..? Au ndio muendelezo wa maigizo..?



  1. WACHUMI;
Sarafu yetu imeendelea kushuka kwa kasi ya ajabu, imetoka kuwa hela ya madafu imekuwa hela ya pipi, Mzee na hili nalo umelisahau..?



  1. WANASHERIA:
Nini maana ya utawala wa sheria unaouzungumzia..? ipi haki ya watoto waliolawitiwa kinyume na maumbile na Babu Seya na Wanawe, au Mzee unaujua Ukweli ambao hautaki kutuambia..?





  1. WAZANZIBARI;
Ni upi msimamo wako na maoni yako juu ya Katiba inayopendekezwa..kuwa Muwazi..?
MZEE hauoni tofauti ya maisha ya Wazanzibari kabla na baada ya kufungwa kwa Farid na Kundi lake..? Mzee amani imerudi Zanzibar au tuambie mahusiano yako na UAMSHO..?



  1. WAGONJWA;
MZEE watanzania wenzako tunaumwa Mzee..,Nini Hatma ya Afya za Watanzaniaau WEWE mwenzetu sio mgonjwa..?



  1. WANAMABADILIKO;
MZEE tuliahidiwa SLAA atahudhuria jangwani na kuipa nguvu mpya kasi ya mabadiliko, Mzee mlimsahau au ilikuwa ni Changa la macho..?



  1. VIJANA;
MZEE ulisema tatizo la ajira ni bomu, ila hatujakuelewa, ina maana umetuacha tulipuke au mkakati wetu uko kwa Balal..?



  1. WANAKIJIJI;
MZEE umetukomoa au umefanya kwa bahati mbaya kutuwekea hotuba yako kwenye Intaneti, haujui zaidi ya watanzania asilimi 80 hawajui kitu kinaitwa Intaneti..?



  1. WATUMISHI;
MZEE, mishahara yetu haikidhi mahitaji, gharama za maisha ni ghali mno..mbona hatujakusikia ukitutaja, au sisi ni mpango wa kando..?



  1. WACHUMI;
MZEE, nini hatma ya mchumi mwenzetu Prof Lipumba katika genge la wanamabadiliko, au umemchukua TAMBWE Hizza Mhitimu wa darasa la saba kuwa mbadala..?

Nilifikiri maswali ya maana.... lakini Jibu moja tu linatosha. Kuiondoa CCM na vijibwa vyake madarakani. Matatizo yote hayo yasingekuwepo kama tungekuwa tunaongozwa na chama makini kama CHADEMA. Unatumisi eh?
 
Hakuna mtu anaehangaika na lowasa_fisadi ila shauku yetu ni kutaka watanzania watambue lowasa_feki ni kidudu mtu anaetaka kujifanya kondoo msafi wakati ni mkaaa mweusi
ata maandiko ya vitabu vya dini vinasema ukimwona mtu anapotea na ukamwacha usimwambie iliyo kweli basi hata wewe umetenda dhambi


HahAhahaaaaaa mpaka nahisi raha ccm... Nyang'anyang'a, ndembendembe, kifo cha mende, chaliiiii.....(kwa sauti ya Babu Duni)
 
Unapoongelea Lowassa unaongelea UKAWA. Unapomuongelea mgonjwa wa kubadilisha damu Ulaya kutokana na kuugua ugonjwa ule mkubwa, ina maana unaongelea chama ambacho kimechoka na kuchokwa baada ya kukaa madarakani kwa muda mrefu. We dogo nakufahamu sana, hamna kitu kichwani. Ulishaharibikiwa muda mrefu. Mimi nikupe ushauri wa bure, jikiteni kumnadi zaidi mgombea wenu Dr.Magufuli lakini kwa Lowassa kumsema vibaya or whatever haitawasaidia sana. Mwaka huu Wtz wengi tumejipanga vizuri. Zaidi mnampa promo zisizo na sbb

Wengi kiasi gani au UKAWA mnaochangia hapa ndiyo watanzania mtakaye mpa ushindi FISADI?
 
Nilifikiri maswali ya maana.... lakini Jibu moja tu linatosha. Kuiondoa CCM na vijibwa vyake madarakani. Matatizo yote hayo yasingekuwepo kama tungekuwa tunaongozwa na chama makini kama CHADEMA. Unatumisi eh?

Chama makini hakiwezi kuogopa kutamka neno FISADI
 
Baada ya kufuatilia hotuba yako ya ufunguzi wa kampeni za UKAWA jangwani kwa umakini mkubwa, naomba Mzee Edward Ngoyai Lowassa unisaidie mimi na wananchi wenzangu wa TANZANIA kujibu maswali haya;



  1. WANAMABADILIKO;
Watanzania wamechoshwa na Rushwa, wanachukia UFISADI, Mzee unamkakati gani dhidiya wala rushwa na mafisadi..?



  1. MAMA NTILIE;
Kilio chetu ni juu ya mgambo kutusumbua na mazingira mabovu ya biashara,tukakulalamikia bei kubwa ya vyakula na mazao, jibu letu liko wapi..?au atakuja kutujibu Babu Seya ukishamtoa jela..?



  1. MADALADALA;
Mzee tulikubeba kutoka Masaki mpaka Gongo la mboto, njia nzima tukikueleza kero zetu, Hatujakusikia ukisema kitu kuhusu usumbufu wa Traffic na kutunyang'anya leseni zetu..?



  1. WAKAZI WA DAR;
Mzee tumekupa mapokezi ya kufa mtu, lakini unajua kuwa tumeamka saa kumina moja alfajir ili kuwahi mkutano wako wa saa tisa Jangwani, Tatizo la foleni na shida ya Usafiri haujazungumzia kabisa...Mzee umetusahau..?



  1. WANAFUNZI;
Elimu bure kutoka shule ya msingi mpaka chuo kikuu, sawa ila Mzee kwa mapato gani..? Au ndio muendelezo wa maigizo..?



  1. WACHUMI;
Sarafu yetu imeendelea kushuka kwa kasi ya ajabu, imetoka kuwa hela ya madafu imekuwa hela ya pipi, Mzee na hili nalo umelisahau..?



  1. WANASHERIA:
Nini maana ya utawala wa sheria unaouzungumzia..? ipi haki ya watoto waliolawitiwa kinyume na maumbile na Babu Seya na Wanawe, au Mzee unaujua Ukweli ambao hautaki kutuambia..?





  1. WAZANZIBARI;
Ni upi msimamo wako na maoni yako juu ya Katiba inayopendekezwa..kuwa Muwazi..?
MZEE hauoni tofauti ya maisha ya Wazanzibari kabla na baada ya kufungwa kwa Farid na Kundi lake..? Mzee amani imerudi Zanzibar au tuambie mahusiano yako na UAMSHO..?



  1. WAGONJWA;
MZEE watanzania wenzako tunaumwa Mzee..,Nini Hatma ya Afya za Watanzaniaau WEWE mwenzetu sio mgonjwa..?



  1. WANAMABADILIKO;
MZEE tuliahidiwa SLAA atahudhuria jangwani na kuipa nguvu mpya kasi ya mabadiliko, Mzee mlimsahau au ilikuwa ni Changa la macho..?



  1. VIJANA;
MZEE ulisema tatizo la ajira ni bomu, ila hatujakuelewa, ina maana umetuacha tulipuke au mkakati wetu uko kwa Balal..?



  1. WANAKIJIJI;
MZEE umetukomoa au umefanya kwa bahati mbaya kutuwekea hotuba yako kwenye Intaneti, haujui zaidi ya watanzania asilimi 80 hawajui kitu kinaitwa Intaneti..?



  1. WATUMISHI;
MZEE, mishahara yetu haikidhi mahitaji, gharama za maisha ni ghali mno..mbona hatujakusikia ukitutaja, au sisi ni mpango wa kando..?



  1. WACHUMI;
MZEE, nini hatma ya mchumi mwenzetu Prof Lipumba katika genge la wanamabadiliko, au umemchukua TAMBWE Hizza Mhitimu wa darasa la saba kuwa mbadala..?

Muulize mwigulu akikupakua huku akijua wazi una mume
 
Mitanzania mingine bhana yaani hela trillions zinaliwa na bado kuna mtu anawasiwasi eti elimu bure haiwezekani
 
Baada ya kufuatilia hotuba yako ya ufunguzi wa kampeni za UKAWA jangwani kwa umakini mkubwa, naomba Mzee Edward Ngoyai Lowassa unisaidie mimi na wananchi wenzangu wa TANZANIA kujibu maswali haya;



  1. WANAMABADILIKO;
Watanzania wamechoshwa na Rushwa, wanachukia UFISADI, Mzee unamkakati gani dhidiya wala rushwa na mafisadi..?



  1. MAMA NTILIE;
Kilio chetu ni juu ya mgambo kutusumbua na mazingira mabovu ya biashara,tukakulalamikia bei kubwa ya vyakula na mazao, jibu letu liko wapi..?au atakuja kutujibu Babu Seya ukishamtoa jela..?



  1. MADALADALA;
Mzee tulikubeba kutoka Masaki mpaka Gongo la mboto, njia nzima tukikueleza kero zetu, Hatujakusikia ukisema kitu kuhusu usumbufu wa Traffic na kutunyang'anya leseni zetu..?



  1. WAKAZI WA DAR;
Mzee tumekupa mapokezi ya kufa mtu, lakini unajua kuwa tumeamka saa kumina moja alfajir ili kuwahi mkutano wako wa saa tisa Jangwani, Tatizo la foleni na shida ya Usafiri haujazungumzia kabisa...Mzee umetusahau..?



  1. WANAFUNZI;
Elimu bure kutoka shule ya msingi mpaka chuo kikuu, sawa ila Mzee kwa mapato gani..? Au ndio muendelezo wa maigizo..?



  1. WACHUMI;
Sarafu yetu imeendelea kushuka kwa kasi ya ajabu, imetoka kuwa hela ya madafu imekuwa hela ya pipi, Mzee na hili nalo umelisahau..?



  1. WANASHERIA:
Nini maana ya utawala wa sheria unaouzungumzia..? ipi haki ya watoto waliolawitiwa kinyume na maumbile na Babu Seya na Wanawe, au Mzee unaujua Ukweli ambao hautaki kutuambia..?





  1. WAZANZIBARI;
Ni upi msimamo wako na maoni yako juu ya Katiba inayopendekezwa..kuwa Muwazi..?
MZEE hauoni tofauti ya maisha ya Wazanzibari kabla na baada ya kufungwa kwa Farid na Kundi lake..? Mzee amani imerudi Zanzibar au tuambie mahusiano yako na UAMSHO..?



  1. WAGONJWA;
MZEE watanzania wenzako tunaumwa Mzee..,Nini Hatma ya Afya za Watanzaniaau WEWE mwenzetu sio mgonjwa..?



  1. WANAMABADILIKO;
MZEE tuliahidiwa SLAA atahudhuria jangwani na kuipa nguvu mpya kasi ya mabadiliko, Mzee mlimsahau au ilikuwa ni Changa la macho..?



  1. VIJANA;
MZEE ulisema tatizo la ajira ni bomu, ila hatujakuelewa, ina maana umetuacha tulipuke au mkakati wetu uko kwa Balal..?



  1. WANAKIJIJI;
MZEE umetukomoa au umefanya kwa bahati mbaya kutuwekea hotuba yako kwenye Intaneti, haujui zaidi ya watanzania asilimi 80 hawajui kitu kinaitwa Intaneti..?



  1. WATUMISHI;
MZEE, mishahara yetu haikidhi mahitaji, gharama za maisha ni ghali mno..mbona hatujakusikia ukitutaja, au sisi ni mpango wa kando..?



  1. WACHUMI;
MZEE, nini hatma ya mchumi mwenzetu Prof Lipumba katika genge la wanamabadiliko, au umemchukua TAMBWE Hizza Mhitimu wa darasa la saba kuwa mbadala..?

Watanzania gani wakutumie wewe kumuuliza maswali mh rais mtarajiwa?au unataka kuchangamsha watu na week end hii....
 
Nianze kama ulivyomaliza..kwa kujibu salamu yako iliyotukuka ya Chama kitakatifu cha CCM, Kidumu Chama Tawala.
hebu ondoa ushetani wenu hapa ilo li chama lina utakatifu gani na muuaji wenu huyo hawala yako Mwigulu???ngoja siku ufumaniwe na mama Mwigulu ndo utaideku
 
[29/08 9:29 PM] ‪+255 716 305 006‬: HOTUBA YA MGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA CHADEMA NA UKAWA MH. EDWARD NGOYAI LOWASSA YA KUZINDUA ILANI NA KAMPENI YA UCHAGUZI MKUU
Jangwani-Dar-es-Salaam, 29 AGOSTI 2015
Ndugu Wana Dar es salaam na Watanzania wenzangu
1. Leo ni siku ya kihistoria. Baada ya miaka ishirini na tano tangu mfumo wa vyama vingi urejeshwe, vyama vya upinzani wa CHADEMA, CUF, NCCR na NLD umeungana chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi kupigania uchaguzi mkuu wa mwaka huu na kuwa na mgombea mmoja katika ngazi zote.
2. Miaka zaidi ya hamsini ya utawala wa serikali za CCM na waasisi wake, umekuwa utawala wa wachache walio hodhi madaraka na mali za nchi.
3. Leo tunaanza safari ya uhakika ya kuleta mabadiliko ya kweli nchini.
a. Mabadiliko yaletayo neema na kujenga upya mfumo wa uchumi, haki na sheria nchini.
b. Mabadiliko ya kuimarisha huduma za jamii kama elimu, afya, maji na makazi.
c. Mabadiliko ya kuondoa umaskini.
d. Mabadiliko tunayatoahidi ni mabadiliko ya kurejesha matumaini kwa Watanzania kwa kubadili hali zao za maisha.
4. Kila mwaka hali na ubora wa maisha ya Watanzania imeshuka wakati tunaambiwa kuwa pato laTaifa linakuwa.
5. Lakini Watanzania wanachotaka siyo takwimu bali kuona kipato chao kinakua, shule, hospitali na barabara bora zinajengwa.
6. Wanataka kupata maji safi na salama ya kunywa. Wanataka makazi bora.
7. CHADEMA na UKAWA, tuna dhamira ya kuleta mabadiliko ya kweli ili kuona azma ya Watanzania tangu uhuru ya kuondoa umaskini, maradhi,na ujinga inahitimishwa.
8. Ili tufanye hivyo tuahitaji tufanye mabadiliko ya fikra, uongozi, sera na utendaji.
9. Leo Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi za ki-uchumi, kisiasa na kijamii. Changamoto hizi ni matokeo ya sera za utawala wa Chama kimoja wa miaka hamsini. Sote ni wahanga wa siasa na sera hizi.
10. Miaka Hamsini ya CCM imetosha. Tunataka mabadiliko na siyo ahadi zile zile kila mwaka
11. Tusidanganyike, CCM hawana jipya
12. Chagueni UKAWA wenye dira ya kubadili maisha ya wananchi.
13. Mimi ninauchukia umaskini na mimesimamia maendeleo kwa vitendo. Nilipokuwa Waziri Mkuu nilijaribu kubadili hali hii. Nilisimamia ujenzi wa shule za kata, Chuo Kikuu cha Dodoma. Nilihakikisha mikataba mibovu ya maji inavunjwa na sasa wananchi wa kanda ya ziwa wanapata maji safi.
Ndugu watanzania
14. CCM wanauliza tuna mpango gani wa kumaliza umaskini. Sisi hatuahidi tu. Tutatenda.
15. Ilani yetu ni dira ya kuondoa umaskini kwa mikakati sahihi na siyo nadharia.
16. Mkakati wa kuondoa umaskini si wa sekta kwa sekta bali wa sekta zote kwa pamoja. Ni ujumla wa utendaji na utekelezaji wa sera za kila sekta utakao leta maendeleo.
17. Mkakati wangu na UKAWA wa kuondoa umaskini utakuwa na nguzo tano:-
a. Kupunguza matumizi ya serikali na mashirika yake na kuimarisha utendaji na uwajibikaji.
b. Kukuza pato la serikali kwa kudhibiti ukwepaji na misamaha ya kodi holela na kuhakikisha nchi inawekeza katika sekta muhimu na inapata gawio halisia kutoka wawekezaji
c. Kukuza uchumi kwa sera na sheria endelevu ikiwa ni pamoja na kukuza biashara na uwekezaji hasa katika sekta za madini, kilimo, viwanda, ufugaji na uvuvi na kuondoa kodi kwa wanyonge.
d. Kuimarisha huduma za umma kama elimu, afya, maji na makazi, na mazingira
e. Kuimarisha utawala bora na mfumo wa haki na sheria chini ya Katiba ya Wananchi.
18. Chini ya misingi hii na ili kufanikisha mkakati wa kuondoa umaskini, serikali yangu itafanya yafuatayo:-
ELIMU BORA KWA KILA MTANZANIA
Nimelisema hili huko nyuma. Nalisema tena leo. Elimu kwanza, Elimu kwanza, Elimu kwanza.
Kwa hiyo mkakati wetu wa msingi utakuwa kutoa Elimu itatayogharamiwa na serikali kwa kila Mtanzania kutoka elimu ya msingi hadi Chuo Kikuu na pia:-
1. Kuimarisha elimu ya teknolojia, ustadi na ufundi inayojenga uwezo wa kujiajiri na ushindani katika soko la ajira.
2. Ujenzi na uimarishaji wa miundombinu ya elimu ikiwa ni pamoja na shule za Kata.
3. Kusimamia ubora wa viwango vya elimu kote nchini.
4. Kuimarisha taaluma na mitaala katika mashule.
5. Kuondoa utoro darasani, na kuboresha afya za wanafunzi.
6. Kuboresha maslahi na vitendea kazi kwa walimu ikiwa ni pamoja na nyumba, posho ya kufundishia, usafiri na zana za teknolojia.
7. Kufuta michango ya maabara ya shule za kata

AFYA
1. Afya na tiba ya kila Mtanzania itagharamiwa kupitia bima za gharama nafuu na mifuko ya hifadhi ya jamii
2. Tutaimarisha afya ya msingi pamoja na kinga kupunguza gharama za tiba.
3. Serikali itahakikisha kuna uwiano na upatikanaji wa watumishi wa afya katika kada mbalimbali ili kuleta tija na huduma stahiki.
4. Itaimarisha miundombinu ya afya pamoja na kujenga hospitali za kisasa ili kusogeza huduma za afya karibu na jamii na pia kuepukana na tiba za nje ya nchi.
5. Tutarejea kwa lengo la kuboresha maslahi na vitendea kazi katika sekta ya Afya ikiwa ni pamoja na nyumba na usafiri.
6. Tutathibiti ongezeko la gharama za huduma za afya bila kuathiri uendeshaji wa watoaji huduma za afya kama vile serikali na hospitali za sekta binafsi.

ARDHI, MAJI NA KILIMO

1. Tutaimarisha mfumo wa umiliki wa ardhi kwa Watanzania na kudhibiti migogoro ya ardhi hasa kati ya wakulima na wafugaji.
2. Tutapima ardhi yote ya Tanzania na kumilikisha vijiji na wakulima kwa hati za serikali ili kuipa thamani.
3. Tutaleta mapinduzi ya kilimo kwa kuimarisha elimu, ufundi na teknolojia ya kisasa na kumkomboa mkulima kutoka jembe la mkono.
4. Tutasimamia kilimo, ufugaji na uvuvi wa kisasa na kuunganisha sekta hizo na ya viwanda.
5. Kuhakikisha kuwa wananchi wanatunza na kulinda vyanzo vya maji.
6. Tutakuza kilimo cha umwagiliaji kwa kuwapa wakulima elimu na mikopo ya riba nafuu ya kuvuna maji na kujenga miundombinu husika.
7. Tutaweka mazingira rafiki yatakayomhakikishia kwa kila Mtanzania kupata maji safi na salama. Kumaliza kero za maji nchini kutamkomboa mwanamke kutokana na adha ya kuchota maji kwa kichwa
8. Nitafuta kodi zote za mazao na mifugo kwa wakulima na wafugaji.
9. Tutasimamia kilimo cha biashara kinachozingatia maslahi ya nchi na ya Watanzania.
10. Tutaanzisha programu maalum ya kufufua mazao asilia ya Tanzania hususan mkonge.
11. Tutaanzisha Benki ya Maendelo ya Ufugaji na Uvuvi.

MIUNDOMBINU
1. Tutaboresha bandari zilizopo na kujenga mpya kama vitega uchumi vya Taifa ili kurejesha biashara tulizopoteza kwa bandari za nchi jirani.
2. Tutajenga barabara nchini kwa kuzingatia ubora hasa zile za vijijini.
3. Tutajenga reli ya kati kwa viwango vya kisasa
4. Tutajenga shirika la Ndege la Taifa linalojiendesha kwa misingi ya faida.
5. Tutajenga miundombinu ya kisasa na kuondosha misongamano ya magari hasa katika majiji ya Dar es salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha
6. Tutaimarisha uzalishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kufikia zaidi ya asili mia sabini na tano ya Watanzania
VIWANDA
1. Tutaimarisha sekta ya viwanda kuwa mhimili wa uchumi kwa uzalishaji wa bidhaa na ajira endelevu
2. Tutajenga viwanda vipya vya kusindika mazao ya kilimo, uvuvi na ufugaji.
3. Tutahakikisha kuwa ndani ya miaka mitano mali ghafi zote za Tanzania zinasindikwa kabla ya kusafirishwa nje ili kuongeza mapato na ajira ya mamilioni ya vijana.
4. Tutaanzisha Benki ya Ukuzaji wa Viwanda

UCHUMI
1. Tutabadili mfumo wa Uchumi wa nchi ili kuhakikisha kuwa mfumo wa uchumi wa Tanzania unakuwa ni wa soko-kijamii ambapo nguvu za soko zitatumikia jamii kwa serikali kuweka uwiano wa mapato unaohakikisha huduma za kijamii zinapatikana kwa ufanisi.
2. Tutalinda sekta binafsi na bidhaa za ndani kwa kuwapa Watanzania upendeleo wa maksudi kwa kipindi cha mpito ili waimarike na waweze kuhimili ushindani. Tutawapa wafanyabiashara wetu upendeleo katika manunuzi ya serikali na kuwajengea mazingira mazuri ya biashara na kodi endelevu.
3. Tutawawezesha Watanzania kupata mitaji ya biashara kwa masharti nafuu kabisa.
4. Tutavutia uwekezaji na wawekezaji wenye tija. Kuweka udhibiti wa wahamiaji wasioleta tija wala maslahi kwa Taifa.
5. Tutaimarisha sera ya ubia baina ya Serikali na Sekta binafsi kwenye maeneo muhimu ya kiuchumi na kibiashara. Pia, kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na wawekezaji wenye mitaji mikubwa bila kujali wanapotoka.
6. Tutaimarisha usimamizi kwa kubadilisha mfumo wa Vyama vya Ushirika nchini ili utokane na uendeshwe na wakulima wenyewe ikiwa na pa
[29/08 9:29 PM] ‪+255 716 305 006‬: wa mabadiliko ni sasa.
Mungu ibariki Tanzania. Asanteni sana
[29/08 9:29 PM] ‪+255 716 305 006‬: moja na kuwawezesha kuboresha makazi kwa mpango wa kushirikiana kujenga nyumba bora
7. Tutaanzisha na kuwezesha uanzishaji wa viwanda vidogovidogo vinavyotoa ajira kwa wingi kwa kuvihusisha na vyuo vya ufundi na benki maalum kwa lengo hilo.
AJIRA
1. Tutasimamia swala la ajira hasa kwa vijana kwa kukuza elimu ya ufundi ili waweze kujiajiri
2. Tutazipa kipaumbele sekta zinazozalisha ajira kwa wingi hasa za viwanda, kilimo, ufugaji, uvuvi na utalii na kuzipa unafuu wa kodi ili zikue kwa haraka.
3. Tutawapa wawekezaji wakubwa katika sekta hizi upendeleo maalum na viwango vya kodi nafuu.
NISHATI NA MADINI
1. Serikali itashiriki kikamilifu katika uzalishaji wa nishati
2. Itatengeneza mazingara mazuri ya kisera yatakayovutia na kuwezesha ushiriki wa Watanzania na ubia kati yao na wageni.
3. Serikali yangu itaupa uzalishaji mkubwa wa umeme wa maji kipaumbele namba moja, umeme wa makaa ya mawe kipaumbele namba mbili, umeme wa gesi asilia kipaumbele namba tatu na umeme wa urana kipaumbele namba nne.
4. Serikali itatoa vipaumbele muhimu kwenye usambazaji wa huduma kubwa ya umeme sehemu za uzalishaji uliyolenga masoko ya ndani, ya nchi jirani na ya nchi za kigeni.
5. Itapitia upya mikataba yote mikubwa ya nishati na madini ili kubaini iliyo mibovu na kuifanyia maboresho.
6. Serikali yangu itatumia sehemu ya hisa zake kwenye raslimali kubwa ya gesi asilia iliyopatikana hapa nchini kama rehani kwenye kujichukulia mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya mabomba ya gesi.
7. Serikali itatoza kodi na ada ndogo zaidi kwa wazawa wenye ubia kati yao na wageni kuliko zitakazotozwa kwa wageni wasiowekeza kwa kushirikisha wazawa.

8. Serikali itasitisha utoaji wa misamaha ya kodi isiyo lazima kwenye sekta ya madini, na badala yake itawekeza kwenye kuongeza thamani ya raslimali zake za madini.
9. Tutakuza nishati mbadala kutamkomboa mwanamke kutokana na adha ya kukata kuni

MALIASILI NA UTALII
1. Tutasimamia uvunaji na matumizi ya rasilimali za Taifa kwa manufaa ya kila Mtanzania wa kizazi hiki na kijacho
2. Tutapiga vita ujangiri na kuimarisha utunzanji wa hifadhi za taifa na mazingira
3. Tutachochea ujenzi wa miundombinu ya utalii nchini ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mahoteli na kuimarisha mafunzo
4. Tutaongeza idadi ya watalii kufikia milion mbili ifikapo 2020.


UTAWALA BORA, ULINZI WA NCHI NA USALAMA WA RAIA
1. Tutasimamia Katiba mpya inayolinda haki za msingi za wananchi na kuweka bayana mipaka ya madaraka ya serikali na viongozi, Bunge na Mahakama.
2. Tutaboresha miundobinu ya sheria na kuimarisha utendaji wa Mahakama na maslahi ya wafanyakazi
3. Tutasimamia haki za raia na kuangalia upya sheria kandamizi ili wananchi kama Masheik wa Zanzibar hawasoti jela kwa sababu za kisiasa.
4. Tutaimarisha mafunzo ya vyombo ya Polisi hasa wapelelezi na waongoza mashtaka ili wapate uwezo wa kusimamia utoaji wa haki.
5. Tutavipa vyombo vyote vya ulinzi na usalama nyenzo na kuboresha mazingira yao ya kazi na maslahi
UZALENDO, UTENDAJI NA UWAJIBIKAJI
1. Tutajenga uzalendo ili kila Mtanzania aweze kutathmini mchango wake kwa taifa kila siku
2. Tutaimarisha nidhamu, utendaji na uwajibikaji katika Sekta ya Umma
3. Tutaimarisha mchango wa Wataalam wetu, wanawake na vijana katika kusimamia uchumi na kuwajengea mazingira stahiki ya kazi pamoja na mafao.
4. Tutapiga vita rushwa na ubadhirifu katika sekta ya Umma na binafsi
5. Tutadhibiti na kupunguza matumizi ya serikali ikiwa ni pamoja na kufuta safari za watumishi serikalini zisizokuwa muhimu pamoja na zile za Rais na kupiga marufuku matumizi ya mashangingi serikalini.
6. Tutadhibiti deni la Taifa kwa kuanza na ukaguzi wa madeni ya serikali ili kuhakiki jinsi yalivyotumika
7. Tutaimarisha uwazi na kuondoa usiri katika shughuli za serikali na kuweka bayana mikataba yote ya nchi ikiwa ni pamoja na ile ya mafuta, madini na gesi asilia
KUKUZA PATO LA SERIKALI
1. Tutadhibiti mapato kutokana na raslimali kwa kupitia upya viwango vya mirabaha kutokana na madini na gesi asilia ili kuhakikisha kuwa Tanzania inapata gawio stahiki.
2. Serikali itaanzisha Wizara maalum itakayosimamia nishati ya gesi na mafuta.
3. Tutaimarisha ofisi ya Msajili wa Hazina ili kusimamia vema uwekezaji wa Serikali katika mashirika na mapato yake.
4. Tutahakikisha kuwa mashirika ya umma yanaendeshwa kwa misingi ya faida na uadilifu.
5. Tutadhibiti ukwepaji kodi za ushuru wa forodha na kupiga marufuku misamaha ya kodi holela ili kuokoa mabilioni ya fedha yanayopotea kila wiki.
6. Sambamba na hilo tutarahisisha utaratibu wa kulipa kodi ili kuondoa kero na mazingira ya rushwa. Kwa kudhibiti makusanyo ya kodi tutakusanya fedha za kugharimia huduma za msingi kama afya na elimu kikamilifu.
KUIMARISHA MUUNGANO
1. Tutaimarisha umoja, usalama na udugu wa Watanzania na Muungano kwa misingi ya haki na usawa
WANAWAKE, WATOTO NA WAZEE
1. Wanawake watapewa fursa na haki sawa katika elimu na uchumi ili waweze bila kuwezeshwa.
2. Tutahakikisha wazazi wanapata fursa ya kuwa walezi na wafanyakazi kwa kuongeza urefu wa likizo ya uzazi
3. Tutaimarisha elimu ya watoto hasa wasichana na kukuza fursa zao na kukomesha ndoa za watoto wadogo.
4. Tutaongeza uwakilishi wa akina mama katika ngazi zote serikalini na mashirika yake kufikia asili mia hamsini ifikapo 2020.
5. Wazee na wasiojiweza watapewa posho ya kujikimu inayokidhi mahitaji ya msingi itakayowawezesha kuishi kwa heshima na kulinda utu wao ndani ya familia na jamii zao.
SANAA, UTAMADUNI NA MICHEZO
1. Tutaendeleza na kuwezesha vipaji vya sanaa na michezo
2. Tutarudisha viwanja vya michezo vilivyovamiwa
3. Tutafuta kodi zote za vifaa vya michezo.
4. Tutadhibiti viwango na maadili ya bidhaa za nje zinazoingizwa nchini na kuzitoza kodi halisia
5. Tutajenga taasisi na vyuo vya kukuza michezo ili kuhakikisha kuwa ndani ya miaka mitano Tanzania inashiriki kwa ushindi katika mashindano ya kimataifa ya soka na riadha
6. Tutalinda Hakimiliki za sanaa nchini
7. Tutafuta kodi za sanaa kwa wasanii chipukizi ili kuwapa muda kwa kujijenga.
SERA YA MAMBO YA NJE YENYE TIJA KWA TAIFA
1. Tutakuza ushirikiano wa Kimataifa wenye tija na Ujirani mwema.
2. Tutatetea haki za binadamu, usawa wa nchi na kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika diplomasia ya kimataifa.
3. Tutakuza umoja na ushirikiano wa Umoja wa Afrika, Jumuia ya Afrika Mashariki, SADC na Umoja wa Mataifa.
4. Tutaimarisha Umoja wa Mataifa ikiwa ni pamoja na kudai mabadiliko ya mfumo ili kuleta usawa wa nchi shiriki.
Ndugu Watanzania
Naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo
1. Natambua kuwa uongozi ni dhamana. Mkinichagua nitaienzi dhamana hiyo kwa utendaji uliotukuka.
2. Nawaahidi Watanzania kuwa kwa uwezo, akili, uzoefu na nguvu zangu zote nitawatumikia. Nawaomba nanyi mniahidi jasho lenu na uwezo wenu wote ili kwa pamoja tuvuke. Tutajikomboa toka utawala wa CCM unaodumaza uchumi na maendeleo. Tutaanza safari ya uhakika kuondoa umaskini.
3. Mabadiliko pia ni kuthamini utu na kukataa hadaa ya hongo ili kuuza haki yako ya kuchagua. Msikubali rubuni za uchaguzi kwa kupewa pesa au vitu. Rushwa ya uchaguzi ndiyo sera ya CCM. Ukikubali basi umeuza pia haki na sauti yako ya kuwalalamikia walio madarakani. Imetosha. Tukatae. Tulinde utu na haki zetu. Tuchague mabadiliko.
4. Mabadiliko ni fikra. Ni kufikiri na kutenda tofauti. Hatuwezi kuendelea kufikiri na kutenda kama kwamba hatuna dharura ya maendeleo. Kwanza tuanze kwa kufanya mabadiliko na tujiamini kuwa sisi kama Taifa tunaweza. Tunaweza kujitegemea na kuleta maendeleo yetu wenyewe bila kutegemea wafadhili. Hii si ndoto. Nchi nyingi zimefanikiwa kuondoa umaskini katika kizazi kimoja. Tujifunze kutoka kwao.
5. Tuwe taifa linalotumia raslimali zake kujiendeleza na siyo kuwanufaisha wageni na kuwafanya Watanzania watwana katika nchi yao. Inabidi tuache kuwa taifa ombaomba. Tuache kuukubali na kuvaa umaskini kama joho la fahari.
6. Mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na CCM. Tusitegemee kuwa leo wana jipya. Ndiyo maana ahadi walizotoa miaka thelathini iliyopita ndizo wametoa juzi. Tukatae hadaa. Miaka hamsini ya CCM imetosha.
7. Tunaamani kwamba tutashinda kwa sababu Watanzania mpo nyuma yetu. Watanzania mmeamua kuleta mabadiliko. Kura yako ndiyo itakayokuwa mkombozi wako. Hakikisha unapiga na kuilinda kura yako. Wakati
[29/08 9:31 PM] ‪+255 716 305 006‬: MALIASILI NA UTALII
1. Tutasimamia uvunaji na matumizi ya rasilimali za Taifa kwa manufaa ya kila Mtanzania wa kizazi hiki na kijacho
2. Tutapiga vita ujangiri na kuimarisha utunzanji wa hifadhi za taifa na mazingira
3. Tutachochea ujenzi wa miundombinu ya utalii nchini ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mahoteli na kuimarisha mafunzo
4. Tutaongeza idadi ya watalii kufikia milion mbili ifikapo 2020.


UTAWALA BORA, ULINZI WA NCHI NA USALAMA WA RAIA
1. Tutasimamia Katiba mpya inayolinda haki za msingi za wananchi na kuweka bayana mipaka ya madaraka ya serikali na viongozi, Bunge na Mahakama.
2. Tutaboresha miundobinu ya sheria na kuimarisha utendaji wa Mahakama na maslahi ya wafanyakazi
3. Tutasimamia haki za raia na kuangalia upya sheria kandamizi ili wananchi kama Masheik wa Zanzibar hawasoti jela kwa sababu za kisiasa.
4. Tutaimarisha mafunzo ya vyombo ya Polisi hasa wapelelezi na waongoza mashtaka ili wapate uwezo wa kusimamia utoaji wa haki.
5. Tutavipa vyombo vyote vya ulinzi na usalama nyenzo na kuboresha mazingira yao ya kazi na maslahi
UZALENDO, UTENDAJI NA UWAJIBIKAJI
1. Tutajenga uzalendo ili kila Mtanzania aweze kutathmini mchango wake kwa taifa kila siku
2. Tutaimarisha nidhamu, utendaji na uwajibikaji katika Sekta ya Umma
3. Tutaimarisha mchango wa Wataalam wetu, wanawake na vijana katika kusimamia uchumi na kuwajengea mazingira stahiki ya kazi pamoja na mafao.
4. Tutapiga vita rushwa na ubadhirifu katika sekta ya Umma na binafsi
5. Tutadhibiti na kupunguza matumizi ya serikali ikiwa ni pamoja na kufuta safari za watumishi serikalini zisizokuwa muhimu pamoja na zile za Rais na kupiga marufuku matumizi ya mashangingi serikalini.
6. Tutadhibiti deni la Taifa kwa kuanza na ukaguzi wa madeni ya serikali ili kuhakiki jinsi yalivyotumika
7. Tutaimarisha uwazi na kuondoa usiri katika shughuli za serikali na kuweka bayana mikataba yote ya nchi ikiwa ni pamoja na ile ya mafuta, madini na gesi asilia
KUKUZA PATO LA SERIKALI
1. Tutadhibiti mapato kutokana na raslimali kwa kupitia upya viwango vya mirabaha kutokana na madini na gesi asilia ili kuhakikisha kuwa Tanzania inapata gawio stahiki.
2. Serikali itaanzisha Wizara maalum itakayosimamia nishati ya gesi na mafuta.
3. Tutaimarisha ofisi ya Msajili wa Hazina ili kusimamia vema uwekezaji wa Serikali katika mashirika na mapato yake.
4. Tutahakikisha kuwa mashirika ya umma yanaendeshwa kwa misingi ya faida na uadilifu.
5. Tutadhibiti ukwepaji kodi za ushuru wa forodha na kupiga marufuku misamaha ya kodi holela ili kuokoa mabilioni ya fedha yanayopotea kila wiki.
6. Sambamba na hilo tutarahisisha utaratibu wa kulipa kodi ili kuondoa kero na mazingira ya rushwa. Kwa kudhibiti makusanyo ya kodi tutakusanya fedha za kugharimia huduma za msingi kama afya na elimu kikamilifu.
KUIMARISHA MUUNGANO
1. Tutaimarisha umoja, usalama na udugu wa Watanzania na Muungano kwa misingi ya haki na usawa
WANAWAKE, WATOTO NA WAZEE
1. Wanawake watapewa fursa na haki sawa katika elimu na uchumi ili waweze bila kuwezeshwa.
2. Tutahakikisha wazazi wanapata fursa ya kuwa walezi na wafanyakazi kwa kuongeza urefu wa likizo ya uzazi
3. Tutaimarisha elimu ya watoto hasa wasichana na kukuza fursa zao na kukomesha ndoa za watoto wadogo.
4. Tutaongeza uwakilishi wa akina mama katika ngazi zote serikalini na mashirika yake kufikia asili mia hamsini ifikapo 2020.
5. Wazee na wasiojiweza watapewa posho ya kujikimu inayokidhi mahitaji ya msingi itakayowawezesha kuishi kwa heshima na kulinda utu wao ndani ya familia na jamii zao.
SANAA, UTAMADUNI NA MICHEZO
1. Tutaendeleza na kuwezesha vipaji vya sanaa na michezo
2. Tutarudisha viwanja vya michezo vilivyovamiwa
3. Tutafuta kodi zote za vifaa vya michezo.
4. Tutadhibiti viwango na maadili ya bidhaa za nje zinazoingizwa nchini na kuzitoza kodi halisia
5. Tutajenga taasisi na vyuo vya kukuza michezo ili kuhakikisha kuwa ndani ya miaka mitano Tanzania inashiriki kwa ushindi katika mashindano ya kimataifa ya soka na riadha
6. Tutalinda Hakimiliki za sanaa nchini
7. Tutafuta kodi za sanaa kwa wasanii chipukizi ili kuwapa muda kwa kujijenga.
SERA YA MAMBO YA NJE YENYE TIJA KWA TAIFA
1. Tutakuza ushirikiano wa Kimataifa wenye tija na Ujirani mwema.
2. Tutatetea haki za binadamu, usawa wa nchi na kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika diplomasia ya kimataifa.
3. Tutakuza umoja na ushirikiano wa Umoja wa Afrika, Jumuia ya Afrika Mashariki, SADC na Umoja wa Mataifa.
4. Tutaimarisha Umoja wa Mataifa ikiwa ni pamoja na kudai mabadiliko ya mfumo ili kuleta usawa wa nchi shiriki.
Ndugu Watanzania
Naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo
1. Natambua kuwa uongozi ni dhamana. Mkinichagua nitaienzi dhamana hiyo kwa utendaji uliotukuka.
2. Nawaahidi Watanzania kuwa kwa uwezo, akili, uzoefu na nguvu zangu zote nitawatumikia. Nawaomba nanyi mniahidi jasho lenu na uwezo wenu wote ili kwa pamoja tuvuke. Tutajikomboa toka utawala wa CCM unaodumaza uchumi na maendeleo. Tutaanza safari ya uhakika kuondoa umaskini.
3. Mabadiliko pia ni kuthamini utu na kukataa hadaa ya hongo ili kuuza haki yako ya kuchagua. Msikubali rubuni za uchaguzi kwa kupewa pesa au vitu. Rushwa ya uchaguzi ndiyo sera ya CCM. Ukikubali basi umeuza pia haki na sauti yako ya kuwalalamikia walio madarakani. Imetosha. Tukatae. Tulinde utu na haki zetu. Tuchague mabadiliko.
4. Mabadiliko ni fikra. Ni kufikiri na kutenda tofauti. Hatuwezi kuendelea kufikiri na kutenda kama kwamba hatuna dharura ya maendeleo. Kwanza tuanze kwa kufanya mabadiliko na tujiamini kuwa sisi kama Taifa tunaweza. Tunaweza kujitegemea na kuleta maendeleo yetu wenyewe bila kutegemea wafadhili. Hii si ndoto. Nchi nyingi zimefanikiwa kuondoa umaskini katika kizazi kimoja. Tujifunze kutoka kwao.
5. Tuwe taifa linalotumia raslimali zake kujiendeleza na siyo kuwanufaisha wageni na kuwafanya Watanzania watwana katika nchi yao. Inabidi tuache kuwa taifa ombaomba. Tuache kuukubali na kuvaa umaskini kama joho la fahari.
6. Mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na CCM. Tusitegemee kuwa leo wana jipya. Ndiyo maana ahadi walizotoa miaka thelathini iliyopita ndizo wametoa juzi. Tukatae hadaa. Miaka hamsini ya CCM imetosha.
7. Tunaamani kwamba tutashinda kwa sababu Watanzania mpo nyuma yetu. Watanzania mmeamua kuleta mabadiliko. Kura yako ndiyo itakayokuwa mkombozi wako. Hakikisha unapiga na kuilinda kura yako. Wakati wa mabadiliko ni sasa.
Mungu ibariki Tanzania. Asanteni sana
 
Wa kukubeza wakubeze tu mleta mada, ila umeuliza maswali ya msingi ambayo yalihitaji maelezo!
Pamoja!
 
Juzi nimekuchora umepanda bajaji mnazi mmoja ukageuzia sura upande wa pili. Sema wanaosema unatumia mkorogo wanakusingizia shosti. Upo vizuri sema watu wenye vitambi watakupwerepweta achana nao.
 
Nianze kama ulivyomaliza..kwa kujibu salamu yako iliyotukuka ya Chama kitakatifu cha CCM, Kidumu Chama Tawala.

Kwanza nikukumbushe jambo, hakuna sehemu imetajwa wala kuzungumziwa UKAWA kwenye thread yangu, labda haujaisoma ama haujaielewa, lakini thread hii imemtaja na kumzungumzia MZEE LOWASSA na ni Mzee LOWASSA pekee..

USHAURI:
Kabla ya kuandika comment yeyote, hakikisha umesoma na kuelewa kile unachotaka kukichangia.

wew umerogwa si bure na tena hujitambui.unatumika tu kwa maccm hata ubunge wa vt maalum huna sjui unashanikia nn??chadema walikulaaani
 
FULL TEXT; HOTUBA ya
Mgombea Urais wa CHADEMA,
Edward Lowassa, live ITV.

HOTUBA YA MGOMBEA URAIS
KUPITIA CHAMA CHA CHADEMA
NA UKAWA MH. EDWARD
NGOYAI LOWASSA
YA KUZINDUA ILANI NA
KAMPENI YA UCHAGUZI MKUU
Jangwani-Dar-es-Salaam, 29
AGOSTI 2015
Ndugu Wana Dar es salaam na
Watanzania wenzangu
1. Leo ni siku ya kihistoria.
Baada ya miaka ishirini na tano
tangu mfumo wa vyama vingi
urejeshwe, vyama vya upinzani
wa CHADEMA, CUF, NCCR na
NLD umeungana chini ya Umoja
wa Katiba ya Wananchi
kupigania uchaguzi mkuu wa
mwaka huu na kuwa na
mgombea mmoja katika ngazi
zote.
2. Miaka zaidi ya hamsini ya
utawala wa serikali za CCM na
waasisi wake, umekuwa utawala
wa wachache walio hodhi
madaraka na mali za nchi.
3. Leo tunaanza safari ya
uhakika ya kuleta mabadiliko
ya kweli nchini.
a. Mabadiliko yaletayo neema
na kujenga upya mfumo wa
uchumi, haki na sheria nchini.
b. Mabadiliko ya kuimarisha
huduma za jamii kama elimu,
afya, maji na makazi.
c. Mabadiliko ya kuondoa
umaskini.
d. Mabadiliko tunayatoahidi ni
mabadiliko ya kurejesha
matumaini kwa Watanzania kwa
kubadili hali zao za maisha.
4. Kila mwaka hali na ubora wa
maisha ya Watanzania imeshuka
wakati tunaambiwa kuwa pato
laTaifa linakuwa.
5. Lakini Watanzania
wanachotaka siyo takwimu bali
kuona kipato chao kinakua,
shule, hospitali na barabara
bora zinajengwa.
6. Wanataka kupata maji safi
na salama ya kunywa.
Wanataka makazi bora.
7. CHADEMA na UKAWA, tuna
dhamira ya kuleta mabadiliko
ya kweli ili kuona azma ya
Watanzania tangu uhuru ya
kuondoa umaskini, maradhi,na
ujinga inahitimishwa.
8. Ili tufanye hivyo tuahitaji
tufanye mabadiliko ya fikra,
uongozi, sera na utendaji.
9. Leo Tanzania inakabiliwa na
changamoto nyingi za ki-
uchumi, kisiasa na kijamii.
Changamoto hizi ni matokeo ya
sera za utawala wa Chama
kimoja wa miaka hamsini. Sote
ni wahanga wa siasa na sera
hizi.
10. Miaka Hamsini ya CCM
imetosha. Tunataka mabadiliko
na siyo ahadi zile zile kila
mwaka
11. Tusidanganyike, CCM
hawana jipya
12. Chagueni UKAWA wenye
dira ya kubadili maisha ya
wananchi.
13. Mimi ninauchukia umaskini
na mimesimamia maendeleo
kwa vitendo. Nilipokuwa Waziri
Mkuu nilijaribu kubadili hali hii.
Nilisimamia ujenzi wa shule za
kata, Chuo Kikuu cha Dodoma.
Nilihakikisha mikataba mibovu
ya maji inavunjwa na sasa
wananchi wa kanda ya ziwa
wanapata maji safi.
Ndugu watanzania
14. CCM wanauliza tuna
mpango gani wa kumaliza
umaskini. Sisi hatuahidi tu.
Tutatenda.
15. Ilani yetu ni dira ya
kuondoa umaskini kwa mikakati
sahihi na siyo nadharia.
16. Mkakati wa kuondoa
umaskini si wa sekta kwa sekta
bali wa sekta zote kwa pamoja.
Ni ujumla wa utendaji na
utekelezaji wa sera za kila sekta
utakao leta maendeleo.
17. Mkakati wangu na UKAWA
wa kuondoa umaskini utakuwa
na nguzo tano:-
a. Kupunguza matumizi ya
serikali na mashirika yake na
kuimarisha utendaji na
uwajibikaji.
b. Kukuza pato la serikali kwa
kudhibiti ukwepaji na misamaha
ya kodi holela na kuhakikisha
nchi inawekeza katika sekta
muhimu na inapata gawio
halisia kutoka wawekezaji
c. Kukuza uchumi kwa sera na
sheria endelevu ikiwa ni pamoja
na kukuza biashara na
uwekezaji hasa katika sekta za
madini, kilimo, viwanda, ufugaji
na uvuvi na kuondoa kodi kwa
wanyonge.
d. Kuimarisha huduma za
umma kama elimu, afya, maji
na makazi, na mazingira
e. Kuimarisha utawala bora na
mfumo wa haki na sheria chini
ya Katiba ya Wananchi.
18. Chini ya misingi hii na ili
kufanikisha mkakati wa
kuondoa umaskini, serikali
yangu itafanya yafuatayo:-
ELIMU BORA KWA KILA
MTANZANIA
Nimelisema hili huko nyuma.
Nalisema tena leo. Elimu
kwanza, Elimu kwanza, Elimu
kwanza.
Kwa hiyo mkakati wetu wa
msingi utakuwa kutoa Elimu
itatayogharamiwa na serikali
kwa kila Mtanzania kutoka
elimu ya msingi hadi Chuo
Kikuu na pia:-
1. Kuimarisha elimu ya
teknolojia, ustadi na ufundi
inayojenga uwezo wa kujiajiri na
ushindani katika soko la ajira.
2. Ujenzi na uimarishaji wa
miundombinu ya elimu ikiwa ni
pamoja na shule za Kata.
3. Kusimamia ubora wa viwango
vya elimu kote nchini.
4. Kuimarisha taaluma na
mitaala katika mashule.
5. Kuondoa utoro darasani, na
kuboresha afya za wanafunzi.
6. Kuboresha maslahi na
vitendea kazi kwa walimu ikiwa
ni pamoja na nyumba, posho
ya kufundishia, usafiri na zana
za teknolojia.
7. Kufuta michango ya maabara
ya shule za kata
AFYA
1. Afya na tiba ya kila
Mtanzania itagharamiwa kupitia
bima za gharama nafuu na
mifuko ya hifadhi ya jamii
2. Tutaimarisha afya ya msingi
pamoja na kinga kupunguza
gharama za tiba.
3. Serikali itahakikisha kuna
uwiano na upatikanaji wa
watumishi wa afya katika kada
mbalimbali ili kuleta tija na
huduma stahiki.
4. Itaimarisha miundombinu ya
afya pamoja na kujenga
hospitali za kisasa ili kusogeza
huduma za afya karibu na jamii
na pia kuepukana na tiba za
nje ya nchi.
5. Tutarejea kwa lengo la
kuboresha maslahi na vitendea
kazi katika sekta ya Afya ikiwa
ni pamoja na nyumba na
usafiri.
6. Tutathibiti ongezeko la
gharama za huduma za afya
bila kuathiri uendeshaji wa
watoaji huduma za afya kama
vile serikali na hospitali za
sekta binafsi.
ARDHI, MAJI NA KILIMO
1. Tutaimarisha mfumo wa
umiliki wa ardhi kwa
Watanzania na kudhibiti
migogoro ya ardhi hasa kati ya
wakulima na wafugaji.
2. Tutapima ardhi yote ya
Tanzania na kumilikisha vijiji na
wakulima kwa hati za serikali ili
kuipa thamani.
3. Tutaleta mapinduzi ya kilimo
kwa kuimarisha elimu, ufundi
na teknolojia ya kisasa na
kumkomboa mkulima kutoka
jembe la mkono.
4. Tutasimamia kilimo, ufugaji
na uvuvi wa kisasa na
kuunganisha sekta hizo na ya
viwanda.
5. Kuhakikisha kuwa wananchi
wanatunza na kulinda vyanzo
vya maji.
6. Tutakuza kilimo cha
umwagiliaji kwa kuwapa
wakulima elimu na mikopo ya
riba nafuu ya kuvuna maji na
kujenga miundombinu husika.
7. Tutaweka mazingira rafiki
yatakayomhakikishia kwa kila
Mtanzania kupata maji safi na
salama. Kumaliza kero za maji
nchini kutamkomboa
mwanamke kutokana na adha
ya kuchota maji kwa kichwa
8. Nitafuta kodi zote za mazao
na mifugo kwa wakulima na
wafugaji.
9. Tutasimamia kilimo cha
biashara kinachozingatia
maslahi ya nchi na ya
Watanzania.
10. Tutaanzisha programu
maalum ya kufufua mazao asilia
ya Tanzania hususan mkonge.
11. Tutaanzisha Benki ya
Maendelo ya Ufugaji na Uvuvi.
MIUNDOMBINU
1. Tutaboresha bandari zilizopo
na kujenga mpya kama vitega
uchumi vya Taifa ili kurejesha
biashara tulizopoteza kwa
bandari za nchi jirani.
2. Tutajenga barabara nchini
kwa kuzingatia ubora hasa zile
za vijijini.
3. Tutajenga reli ya kati kwa
viwango vya kisasa
4. Tutajenga shirika la Ndege la
Taifa linalojiendesha kwa
misingi ya faida.
5. Tutajenga miundombinu ya
kisasa na kuondosha
misongamano ya magari hasa
katika majiji ya Dar es salaam,
Mwanza, Mbeya na Arusha
6. Tutaimarisha uzalishaji na
usambazaji wa umeme vijijini ili
kufikia zaidi ya asili mia sabini
na tano ya Watanzania
VIWANDA
1. Tutaimarisha sekta ya
viwanda kuwa mhimili wa
uchumi kwa uzalishaji wa
bidhaa na ajira endelevu
2. Tutajenga viwanda vipya vya
kusindika mazao ya kilimo,
uvuvi na ufugaji.
3. Tutahakikisha kuwa ndani ya
miaka mitano mali ghafi zote za
Tanzania zinasindikwa kabla ya
kusafirishwa nje ili kuongeza
mapato na ajira ya mamilioni
ya vijana.
4. Tutaanzisha Benki ya Ukuzaji
wa Viwanda
UCHUMI
1. Tutabadili mfumo wa Uchumi
wa nchi ili kuhakikisha kuwa
mfumo wa uchumi wa Tanzania
unakuwa ni wa soko-kijamii
ambapo nguvu za soko
zitatumikia jamii kwa serikali
kuweka uwiano wa mapato
unaohakikisha huduma za
kijamii zinapatikana kwa ufanisi.
2. Tutalinda sekta binafsi na
bidhaa za ndani kwa kuwapa
Watanzania upendeleo wa
maksudi kwa kipindi cha mpito
ili waimarike na waweze
kuhimili ushindani. Tutawapa
wafanyabiashara wetu
upendeleo katika manunuzi ya
serikali na kuwajengea
mazingira mazuri ya biashara
na kodi endelevu.
3. Tutawawezesha Watanzania
kupata mitaji ya biashara kwa
masharti nafuu kabisa.
4. Tutavutia uwekezaji na
wawekezaji wenye tija. Kuweka
udhibiti wa wahamiaji wasioleta
tija wala maslahi kwa Taifa.
5. Tutaimarisha sera ya ubia
baina ya Serikali na Sekta
binafsi kwenye maeneo muhimu
ya kiuchumi na kibiashara. Pia,
kuwawezesha Watanzania
kuwekeza kwa njia ya ubia na
wawekezaji wenye mitaji
mikubwa bila kujali
wanapotoka.
6. Tutaimarisha usimamizi kwa
kubadilisha mfumo wa Vyama
vya Ushirika nchini ili utokane
na uendeshwe na wakulima
wenyewe ikiwa na pamoja na
kuwawezesha kuboresha makazi
kwa mpango wa kushirikiana
kujenga nyumba bora
7. Tutaanzisha na kuwezesha
uanzishaji wa viwanda
vidogovidogo vinavyotoa ajira
kwa wingi kwa kuvihusisha na
vyuo vya ufundi na benki
maalum kwa lengo hilo.
AJIRA
1. Tutasimamia swala la ajira
hasa kwa vijana kwa kukuza
elimu ya ufundi ili waweze
kujiajiri
2. Tutazipa kipaumbele sekta
zinazozalisha ajira kwa wingi
hasa za viwanda, kilimo,
ufugaji, uvuvi na utalii na
kuzipa unafuu wa kodi ili zikue
kwa haraka.
3. Tutawapa wawekezaji
wakubwa katika sekta hizi
upendeleo maalum na viwango
vya kodi nafuu.
NISHATI NA MADINI
1. Serikali itashiriki kikamilifu
katika uzalishaji wa nishati
2. Itatengeneza mazingara
mazuri ya kisera yatakayovutia
na kuwezesha ushiriki wa
Watanzania na ubia kati yao na
wageni.
3. Serikali yangu itaupa
uzalishaji mkubwa wa umeme
wa maji kipaumbele namba
moja, umeme wa makaa ya
mawe kipaumbele namba mbili,
umeme wa gesi asilia
kipaumbele namba tatu na
umeme wa urana kipaumbele
namba nne.
4. Serikali itatoa vipaumbele
muhimu kwenye usambazaji wa
huduma kubwa ya umeme
sehemu za uzalishaji uliyolenga
masoko ya ndani, ya nchi jirani
na ya nchi za kigeni.
5. Itapitia upya mikataba yote
mikubwa ya nishati na madini
ili kubaini iliyo mibovu na
kuifanyia maboresho.
6. Serikali yangu itatumia
sehemu ya hisa zake kwenye
raslimali kubwa ya gesi asilia
iliyopatikana hapa nchini kama
rehani kwenye kujichukulia
mikopo kwa ajili ya ujenzi wa
miundo mbinu ya mabomba ya
gesi.
7. Serikali itatoza kodi na ada
ndogo zaidi kwa wazawa wenye
ubia kati yao na wageni kuliko
zitakazotozwa kwa wageni
wasiowekeza kwa kushirikisha
wazawa.
8. Serikali itasitisha utoaji wa
misamaha ya kodi isiyo lazima
kwenye sekta ya madini, na
badala yake itawekeza kwenye
kuongeza thamani ya raslimali
zake za madini.
9. Tutakuza nishati mbadala
kutamkomboa mwanamke
kutokana na adha ya kukata
kuni
MALIASILI NA UTALII
1. Tutasimamia uvunaji na
matumizi ya rasilimali za Taifa
kwa manufaa ya kila Mtanzania
wa kizazi hiki na kijacho
2. Tutapiga vita ujangiri na
kuimarisha utunzanji wa hifadhi
za taifa na mazingira
3. Tutachochea ujenzi wa
miundombinu ya utalii nchini
ikiwa ni pamoja na ujenzi wa
mahoteli na kuimarisha
mafunzo
4. Tutaongeza idadi ya watalii
kufikia milion mbili ifikapo
2020.
UTAWALA BORA, ULINZI WA
NCHI NA USALAMA WA RAIA
1. Tutasimamia Katiba mpya
inayolinda haki za msingi za
wananchi na kuweka bayana
mipaka ya madaraka ya serikali
na viongozi, Bunge na
Mahakama.
2. Tutaboresha miundobinu ya
sheria na kuimarisha utendaji
wa Mahakama na maslahi ya
wafanyakazi
3. Tutasimamia haki za raia na
kuangalia upya sheria
kandamizi ili wananchi kama
Masheik wa Zanzibar hawasoti
jela kwa sababu za kisiasa.
4. Tutaimarisha mafunzo ya
vyombo ya Polisi hasa
wapelelezi na waongoza
mashtaka ili wapate uwezo wa
kusimamia utoaji wa haki.
5. Tutavipa vyombo vyote vya
ulinzi na usalama nyenzo na
kuboresha mazingira yao ya kazi
na maslahi
UZALENDO, UTENDAJI NA
UWAJIBIKAJI
1. Tutajenga uzalendo ili kila
Mtanzania aweze kutathmini
mchango wake kwa taifa kila
siku
2. Tutaimarisha nidhamu,
utendaji na uwajibikaji katika
Sekta ya Umma
3. Tutaimarisha mchango wa
Wataalam wetu, wanawake na
vijana katika kusimamia uchumi
na kuwajengea mazingira
stahiki ya kazi pamoja na
mafao.
4. Tutapiga vita rushwa na
ubadhirifu katika sekta ya
Umma na binafsi
5. Tutadhibiti na kupunguza
matumizi ya serikali ikiwa ni
pamoja na kufuta safari za
watumishi serikalini zisizokuwa
muhimu pamoja na zile za Rais
na kupiga marufuku matumizi
ya mashangingi serikalini.
6. Tutadhibiti deni la Taifa kwa
kuanza na ukaguzi wa madeni
ya serikali ili kuhakiki jinsi
yalivyotumika
7. Tutaimarisha uwazi na
kuondoa usiri katika shughuli
za serikali na kuweka bayana
mikataba yote ya nchi ikiwa ni
pamoja na ile ya mafuta,
madini na gesi asilia
KUKUZA PATO LA SERIKALI
1. Tutadhibiti mapato kutokana
na raslimali kwa kupitia upya
viwango vya mirabaha kutokana
na madini na gesi asilia ili
kuhakikisha kuwa Tanzania
inapata gawio stahiki.
2. Serikali itaanzisha Wizara
maalum itakayosimamia nishati
ya gesi na mafuta.
3. Tutaimarisha ofisi ya Msajili
wa Hazina ili kusimamia vema
uwekezaji wa Serikali katika
mashirika na mapato yake.
4. Tutahakikisha kuwa
mashirika ya umma
yanaendeshwa kwa misingi ya
faida na uadilifu.
5. Tutadhibiti ukwepaji kodi za
ushuru wa forodha na kupiga
marufuku misamaha ya kodi
holela ili kuokoa mabilioni ya
fedha yanayopotea kila wiki.
6. Sambamba na hilo
tutarahisisha utaratibu wa
kulipa kodi ili kuondoa kero na
mazingira ya rushwa. Kwa
kudhibiti makusanyo ya kodi
tutakusanya fedha za
kugharimia huduma za msingi
kama afya na elimu kikamilifu.
KUIMARISHA MUUNGANO
1. Tutaimarisha umoja, usalama
na udugu wa Watanzania na
Muungano kwa misingi ya haki
na usawa
WANAWAKE, WATOTO NA
WAZEE
1. Wanawake watapewa fursa
na haki sawa katika elimu na
uchumi ili waweze bila
kuwezeshwa.
2. Tutahakikisha wazazi
wanapata fursa ya kuwa walezi
na wafanyakazi kwa kuongeza
urefu wa likizo ya uzazi
3. Tutaimarisha elimu ya
watoto hasa wasichana na
kukuza fursa zao na kukomesha
ndoa za watoto wadogo.
4. Tutaongeza uwakilishi wa
akina mama katika ngazi zote
serikalini na mashirika yake
kufikia asili mia hamsini ifikapo
2020.
5. Wazee na wasiojiweza
watapewa posho ya kujikimu
inayokidhi mahitaji ya msingi
itakayowawezesha kuishi kwa
heshima na kulinda utu wao
ndani ya familia na jamii zao.
SANAA, UTAMADUNI NA
MICHEZO
1. Tutaendeleza na kuwezesha
vipaji vya sanaa na michezo
2. Tutarudisha viwanja vya
michezo vilivyovamiwa
3. Tutafuta kodi zote za vifaa
vya michezo.
4. Tutadhibiti viwango na
maadili ya bidhaa za nje
zinazoingizwa nchini na kuzitoza
kodi halisia
5. Tutajenga taasisi na vyuo
vya kukuza michezo ili
kuhakikisha kuwa ndani ya
miaka mitano Tanzania
inashiriki kwa ushindi katika
mashindano ya kimataifa ya
soka na riadha
6. Tutalinda Hakimiliki za sanaa
nchini
7. Tutafuta kodi za sanaa kwa
wasanii chipukizi ili kuwapa
muda kwa kujijenga.
SERA YA MAMBO YA NJE YENYE
TIJA KWA TAIFA
1. Tutakuza ushirikiano wa
Kimataifa wenye tija na Ujirani
mwema.
2. Tutatetea haki za binadamu,
usawa wa nchi na kuimarisha
ushiriki wa Tanzania katika
diplomasia ya kimataifa.
3. Tutakuza umoja na
ushirikiano wa Umoja wa Afrika,
Jumuia ya Afrika Mashariki,
SADC na Umoja wa Mataifa.
4. Tutaimarisha Umoja wa
Mataifa ikiwa ni pamoja na
kudai mabadiliko ya mfumo ili
kuleta usawa wa nchi shiriki.
Ndugu Watanzania
Naomba nimalizie kwa kusema
yafuatayo
1. Natambua kuwa uongozi ni
dhamana. Mkinichagua nitaienzi
dhamana hiyo kwa utendaji
uliotukuka.
2. Nawaahidi Watanzania kuwa
kwa uwezo, akili, uzoefu na
nguvu zangu zote
nitawatumikia. Nawaomba
nanyi mniahidi jasho lenu na
uwezo wenu wote ili kwa
pamoja tuvuke. Tutajikomboa
toka utawala wa CCM
unaodumaza uchumi na
maendeleo. Tutaanza safari ya
uhakika kuondoa umaskini.
3. Mabadiliko pia ni kuthamini
utu na kukataa hadaa ya hongo
ili kuuza haki yako ya
kuchagua. Msikubali rubuni za
uchaguzi kwa kupewa pesa au
vitu. Rushwa ya uchaguzi ndiyo
sera ya CCM. Ukikubali basi
umeuza pia haki na sauti yako
ya kuwalalamikia walio
madarakani. Imetosha.
Tukatae. Tulinde utu na haki
zetu. Tuchague mabadiliko.
4. Mabadiliko ni fikra. Ni
kufikiri na kutenda tofauti.
Hatuwezi kuendelea kufikiri na
kutenda kama kwamba hatuna
dharura ya maendeleo. Kwanza
tuanze kwa kufanya mabadiliko
na tujiamini kuwa sisi kama
Taifa tunaweza. Tunaweza
kujitegemea na kuleta
maendeleo yetu wenyewe bila
kutegemea wafadhili. Hii si
ndoto. Nchi nyingi zimefanikiwa
kuondoa umaskini katika kizazi
kimoja. Tujifunze kutoka kwao.
5. Tuwe taifa linalotumia
raslimali zake kujiendeleza na
siyo kuwanufaisha wageni na
kuwafanya Watanzania watwana
katika nchi yao. Inabidi tuache
kuwa taifa ombaomba. Tuache
kuukubali na kuvaa umaskini
kama joho la fahari.
6. Mabadiliko ya kweli hayawezi
kuletwa na CCM. Tusitegemee
kuwa leo wana jipya. Ndiyo
maana ahadi walizotoa miaka
thelathini iliyopita ndizo
wametoa juzi. Tukatae hadaa.
Miaka hamsini ya CCM
imetosha.
7. Tunaamani kwamba
tutashinda kwa sababu
Watanzania mpo nyuma yetu.
Watanzania mmeamua kuleta
mabadiliko. Kura yako ndiyo
itakayokuwa mkombozi wako.
Hakikisha unapiga na kuilinda
kura yako. Wakati wa
mabadiliko ni sasa.
Mungu ibariki Tanzania.
Asanteni sana
 
Baada ya kufuatilia hotuba yako ya ufunguzi wa kampeni za UKAWA jangwani kwa umakini mkubwa, naomba Mzee Edward Ngoyai Lowassa unisaidie mimi na wananchi wenzangu wa TANZANIA kujibu maswali haya;



  1. WANAMABADILIKO;
Watanzania wamechoshwa na Rushwa, wanachukia UFISADI, Mzee unamkakati gani dhidiya wala rushwa na mafisadi..?



  1. MAMA NTILIE;
Kilio chetu ni juu ya mgambo kutusumbua na mazingira mabovu ya biashara,tukakulalamikia bei kubwa ya vyakula na mazao, jibu letu liko wapi..?au atakuja kutujibu Babu Seya ukishamtoa jela..?



  1. MADALADALA;
Mzee tulikubeba kutoka Masaki mpaka Gongo la mboto, njia nzima tukikueleza kero zetu, Hatujakusikia ukisema kitu kuhusu usumbufu wa Traffic na kutunyang'anya leseni zetu..?



  1. WAKAZI WA DAR;
Mzee tumekupa mapokezi ya kufa mtu, lakini unajua kuwa tumeamka saa kumina moja alfajir ili kuwahi mkutano wako wa saa tisa Jangwani, Tatizo la foleni na shida ya Usafiri haujazungumzia kabisa...Mzee umetusahau..?



  1. WANAFUNZI;
Elimu bure kutoka shule ya msingi mpaka chuo kikuu, sawa ila Mzee kwa mapato gani..? Au ndio muendelezo wa maigizo..?



  1. WACHUMI;
Sarafu yetu imeendelea kushuka kwa kasi ya ajabu, imetoka kuwa hela ya madafu imekuwa hela ya pipi, Mzee na hili nalo umelisahau..?



  1. WANASHERIA:
Nini maana ya utawala wa sheria unaouzungumzia..? ipi haki ya watoto waliolawitiwa kinyume na maumbile na Babu Seya na Wanawe, au Mzee unaujua Ukweli ambao hautaki kutuambia..?





  1. WAZANZIBARI;
Ni upi msimamo wako na maoni yako juu ya Katiba inayopendekezwa..kuwa Muwazi..?
MZEE hauoni tofauti ya maisha ya Wazanzibari kabla na baada ya kufungwa kwa Farid na Kundi lake..? Mzee amani imerudi Zanzibar au tuambie mahusiano yako na UAMSHO..?



  1. WAGONJWA;
MZEE watanzania wenzako tunaumwa Mzee..,Nini Hatma ya Afya za Watanzaniaau WEWE mwenzetu sio mgonjwa..?



  1. WANAMABADILIKO;
MZEE tuliahidiwa SLAA atahudhuria jangwani na kuipa nguvu mpya kasi ya mabadiliko, Mzee mlimsahau au ilikuwa ni Changa la macho..?



  1. VIJANA;
MZEE ulisema tatizo la ajira ni bomu, ila hatujakuelewa, ina maana umetuacha tulipuke au mkakati wetu uko kwa Balal..?



  1. WANAKIJIJI;
MZEE umetukomoa au umefanya kwa bahati mbaya kutuwekea hotuba yako kwenye Intaneti, haujui zaidi ya watanzania asilimi 80 hawajui kitu kinaitwa Intaneti..?



  1. WATUMISHI;
MZEE, mishahara yetu haikidhi mahitaji, gharama za maisha ni ghali mno..mbona hatujakusikia ukitutaja, au sisi ni mpango wa kando..?



  1. WACHUMI;
MZEE, nini hatma ya mchumi mwenzetu Prof Lipumba katika genge la wanamabadiliko, au umemchukua TAMBWE Hizza Mhitimu wa darasa la saba kuwa mbadala..?

umejitoa ufahamu wewe,maswali yako unataka ayajibu vipi huku jf,mpelekee nyumbani kwake
 
Hawezi kujibu hayo maswali, Unataka kumuua tuh huyo mzee wa watu, yaani amenivuruga kwa hotuba ya kipimbi aliyotoa jana
 
Back
Top Bottom