Maswali ya Sensa 8 tu? why



Ni busara tu inatumika hapa hata mimi nina matusi ya kutukana sema sijalelewa mazingira kama yako.

USIKURUPUKE TU NA KUANZA KUMLALAMIKIA KARANI

1. Utamuulizaje mtu kama ni Albino wakati unamwona si albino

2. Utamuulizaje Mwanafunzi wa Chuo aliyepanga hostel kama Anamifugo mahali alipopanga wakati unamwona kabisa hana. Maana unahesabu kitu alichonacho kwenye kaya

3. Utamuulizaje mtu kama ni kilema wa kutembea wakati ulipoingia ulimwona anatembea

4. Utamuulizaje mtu kama anakichwa kikubwa wakati unamwona hana

5. Utamuulizaje Mwanafunzi aliyepanga hostel kama anafuga kuku,ng'ombe au mbuzi.

6. Utamuulizaje mtu kama anajua kusoma na kuandika wakati amekuambia hajawahi kwenda shule

Hebu wanaJF na Makarani wenzangu amueni wenyewe nani anaHANG OVER kati yangu na Mleta Mada
 
Last edited by a moderator:
Mi wameniuliza we mbona mweupe sana alafu akabonyea kwenye karatasi na kuandika Sijui aliandika nin?
 
Si tumekubali kuesabiwa jamani kizalendo! Sasa hata wakiuliza swali moja nyie waacheni jaman
 
Sina imani na sensa hii maana wanachakachua majibu! Hapa kama kile kipengele cha ustaadh ndevu za Usama kingewekwa kulikuwa na hatari ya kujaziwa tofauti! Umesema nina dini ya kijadi jamaa anajipinda kushade kwenye ukristo au uislam! Kazi tunayo!
 
Mie niliuzwa mengi sana hata sikumbuki idadi nadhani yalifika hiyo namba waliyosema.
 

Sio kila Topic lazima Uchangie.. Mimi Nimeandika kilichonitokea kwani Sensa nayo ni kama Siasa? Ukiwataarifu watu kuwa Sensa ina umuhimu na kama kuna maswali yameandaliwa basi yaulizwe yote.

sio sababu umetauliwa kuwa Karani basi ndio ujifanye mjuaji kuliko huyo aliyetunga maneno kwenye Dodoso la Sensa na kama Karani uliyepitia Semina basi utamuweka wazi huyo unayemuhesabu.

mimi nimesema nimeulizwa maswali manane! wewe unaniambia nalalamika JF si ningelalamika Kwa karani wa Sensa!
niambie Umejiunga JF kusumbua na kukera watu? Ushauri wangu Bora uachane na Topic usizozipenda Waacha Mods wa deal na Thread kama wanaona zinafaa au hazifai watazitoa au Wataziacha ziendelee kuyoyoma...

Hii thread itawasaidia hata Sensa zijazo wakiona haya yanayofanyika kwa Makarani Wao...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…