Sikiliza ndugu yangu mwenye uwezo mdogo wa kufikiri na ukadhani wote tunapaswa kufanana na wewe.
Hapo kwenye RED kunaonesha ukomo wako wa fikra. Tanzania ina ardhi kubwa kiasi gani isiyotumika mpaka useme tatizo la ajira halitatuliki? Au MADESA yanakufanya ufikiri Buguruni tu unapoishi?
Jiji la Dar es Salaam peke yake, lina watu walio kwenye ajira isiyo rasmi si chini ya 1,800,000. Watu hawa wote hawalipi kodi, au hata wale wanaolipa ushuru huishia kwenye posho za vikao vya Halmashauri. Nakupa tu changamoto, tafuata calculator unihakiki.
Watu 1,800,000 walipe just 1000 kwa wiki kutoka kwenye biashara zao za Mama Ntilie, Boda Boda, Mitumba, Mihogo, Samaki n.k = 1,800,000,000. (1.8bn)
Hiyo Bilioni moja nukta 8, izidishe kwa wiki 4, yaani iwe mwezi. Hapa utapata 7.2bn, sasa assume 1.2bn ziishie kwenye gharama za makusanyo, kwamba tumebaki na 6bn. Kama una uwezo wa kukusanya 6bn kwa mwezi na ukazirudisha pale pale zilipokusanywa kwa mandeleo ya waliozichanga (zingatia kwamba kodi ikiwa ndogo huwa rafiki) basi kuna kitu kinaweza kufanyika.
Kwa mwezi mmoja, tunaweza kununua nyumba 10 zilizo karibu na vituo vikuu vya daladala, kuzibomoa na kujnga soko la kutosha wafanyabishara 300. Kama leo tukijenga Temeke, mwezi ujao itakuwa zamu ya Keko, by the way, hata masoko mawili yanaweza kujengwa kwa mwezi mmoja. Ukiweza kuwawekea paa watu uliokuwa unawachaji 1000 kwa wiki, unayo basi sababu ya kuwachaji 2000 kwa wiki.
Nikukumbushe pia, ni nchi hii ndio kinara wa kugombania mazao na wakulima ilhali serikali haina mashamba yake. Huko ndio kwenye ajira hasa, lkn MADESA yanawafanya muamini kwamba kamwe haiwezekani.
Kuhusu kwa nini fulani anang'ang'ania madaraka, hili ni swali la kuwauliza CCM pia. Kama kwa miaka yote serikali ya chama kile kile ipo madarakani, mbinu zake ni zile zile za kuongeza kodi kwenye BIA na SIGARA na kukamua P.A.Y.E bila huruma, kwa nini wasifikirie kukaa pembeni?
'Chama kilichomlea'......how pathetic? Yaani wewe unaishi kwa fatherhood sympathy? Amsha kichwa ndugu yangu. Hii nchi haikupaswa watu kuuana sababu ya ardhi.