Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,331
KWANINI serikali inahangaika kupandikiza hisia za udini na ugaidi katika siasa? Mwaka 2005 ilikitangaza Chama cha Wananchi (CUF) kuwa cha kidini na kigaidi. Sasa hivi inasema vitu viwili.
Kwanza, inasema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kidini, kikabila na kigaidi. Pili, inawatumia makada wake kutamka kwamba chama hicho kitakufa.
Tunajua kuwa inafanya hivyo kunusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM). Lakini kwa tabia hii, tutaiita serikali au genge la wapika propaganda za kigaidi?
Hebu tuulizane. Watawala wanaotumia na kupandikiza hisia za udini na ukabila kama mbinu ya kuwashinda wapinzani wao wanastahili kuaminiwa tena? Wanaweza kuzungumzia amani na utulivu?
Watawala wanaoingiza Jeshi la Polisi katika misukosuko ya kiitikadi, wanadhani wanapanda mbegu ya amani na ustahamilivu? Chama cha siasa kinachotegemea nguvu za dola kama njia ya kupata ushindi kina haki ya kuendelea kuaminiwa?
Tukumbushane. Mwaka 2005, katikati ya joto kali la Uchaguzi Mkuu, baada ya kubanwa na CUF, serikali ilimtumia Mkuu wa Jeshi la Polisi wa wakati ule, Inspekta Jenerali Omar Mahita, kutisha wapiga kura.
Mahita akajidhalilisha, akaibukia kwenye TV akiwa na visu vilivyopakwa rangi za bendera ya CUF, akisema jeshi lake limekamata kontena la visu ambavyo chama hicho kilikuwa kinakusudia kufanyia ugaidi.
Hadi leo hawajatueleza visu hivyo vilipelekwa wapi. Hatujaambiwa kontena hilo liliishia wapi. Hatujasikia mtu yeyote au kiongozi wa CUF amekamatwa kwa ugaidi. Wala hakuna kesi yoyote mahakamani dhidi ya viongozi au wanachama wa CUF kutokana na tukio hilo.
Ni dhahiri lilikuwa tukio la kupika na kuidhalilisha CUF mbele ya umma. Ilikuwa mbinu ya ushindi mchafu. Na kwa kuwa iliwasaidia kuipiku CUF na kuidhoofisha, sasa wamedhani mbinu ile ile itakuwa msaada kwao kuimaliza CHADEMA.
Ndiyo maana na tambo zao eti CHADEMA kitakufa kabla ya 2015. Ndiyo sababu ya kauli za kidini, kikabila ka kigaidi dhidi ya CHADEMA. Wanapanda mbegu chafu katika siasa za Tanzania, kwa hofu tu ya kuondoka madarakani!
Halafu wanathubutu kusimama majukwaani kutamka kwamba wapinzani wana uchu wa madaraka. Yapi? Nani anangangania madaraka kati ya wale waliokaa madarakani kwa miaka 50 na wale wanaotaka kuingia madarakani kwa mara ya kwanza?
Mbinu chafu za kutumia vyombo vya dola, udini, ukabila na ugaidi hazioneshi uzoefu, weledi, wala umakini katika kutawala. Kwa maana nyingine, tunaweza kusema miaka 50 ya kukaa madarakani haijawasaidia watawala wetu. Bado wanabahatisha!
Zaidi ya hayo, wanatujengea Jeshi la Polisi lisilo adilifu, lililo tayari kuingizwa kwenye michezo michafu ya kihuni na kihalifu kwa ajili ya kutukuza watawala.
Kama leo tungeulizana, upo wapi uadilifu wa Mahita? Tunakuwa na uhakika gani na uadilifu wa viongozi wa Jeshi la Polisi baada ya Mahita?
Kwanini serikali inataka kulifikisha Jeshi la Polisi mahali ambapo halitaheshimika wala kuaminika? Kwanini inatumia vyombo vya dola kukandamiza haki na kulinda uovu?
Na baada ya yote yaliyotokea katika nchi za wenzetu Syria, Tunisia, Misri, Libya, Kenya, Zimbabwe na kwingineko, kwanini watawala hawajifunzi kwamba matumizi ya Jeshi la Polisi hayawezi kuzuia wimbi la mabadiliko?
Jambo moja ambalo watawala hawajaelewa ni kwamba walifanikiwa kuidhoofisha CUF kwa sababu kilishitukizwa. CHADEMA kimeandaliwa, na kimejiandaa kisaikolojia na kimkakati kushinda propaganda hizi.
Tatizo si CHADEMA. Hoja si CHADEMA. Hoja ni mabadiliko. Yatakuja tu. Kama si kwa kupitia mlangoni, yatapitia dirishani. Nguvu ya mabadiliko ni baraka. Hata ukifunga milango, itapenya!
Bahati mbaya, watawala hawajasoma alama za nyakati. Wananchi wa sasa wameshaelewa mbinu zao. Maoni ya kizazi cha leo cha Watanzania ni kuondoa mfumo wa utawala uliodumu kwa miaka 50.
Elimu ya uraia iliyotolewa kwa wananchi wa sasa ikichangiwa na harakati za vyama vya siasa, asasi za kiraia na udhaifu wa serikali yenyewe katika kuhudumia wananchi imesaidia kuamsha wananchi kuamka. Wanajua haki zao, na wapo tayari kupambana na dhalimu yeyote.
Kwa muda sasa, kutokana na mwenendo wa serikali, wananchi wamejenga hasira dhidi ya watawala, kiasi kwamba anapopatikana hata mtu mmoja wa kupambana na watawala hao anaonekana shujaa mbele ya umma.
Na jitihada zozote za watawala kumdhulumu mtu yeyote anayekosoa au kusumbua watawala huzaa chuki kutoka kwa umma.
Ndiyo maana wananchi wanaelewa fika kwamba ugaidi wa CHADEMA unaozungumzwa sasa ni siasa za mchoko wa CCM na serikali yake. Ni propaganda na hujuma zile zile walizofanyiwa CUF miaka ile.
Ni hatua za mwisho za kutapatapa kwao baada ya kushindwa siasa za hoja majukwaani na katika nyanja nyingine rasmi. Ni teke zito la ngamia anayekata roho!
Kizazi cha leo kinachotafuta ukombozi wa pili wa Tanzania hakiwezi kuogopa kuitwa magaidi. Kinajua kuwa hata ikibidi, CUF na CHADEMA si wa kwanza kuitwa hivyo.
Mifano ni mingi, lakini nitatoa michache kukazia hoja hii. Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, aliitwa gaidi baada ya kutishia masilahi ya watawala.
Alitafutwa kunyongwa. Alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Kumbukumbu zinaonesha yeye mwenyewe aliwahi kukiri makosa yapatayo 156 ya kigaidi dhidi ya serikali ya Kaburu!
Mara kadhaa, utawala wa kikaburu, chini ya Rais P. W. Botha uliwahi kumtaka Mandela akanushe kuhusika na ugaidi ili rais amsamehe, amwondolee kifungo.
Mandela alikataa! Aliona ni bora aendelee kuitwa gaidi iwapo ugaidi huo ni harakati za kuwakomboa wananchi wa Afrika Kusini.
Lakini watawala wa Afrika Kusini, hawakuanza na Mandela. Walianza na Chama chake, African National Congress (ANC), kilichoasisiwa mwaka 1912. Kati ya 1961 na 1990, watawala na maswahiba wao wa ndani na nje walitangaza na kutuhumu ANC kuwa ni chama cha kigaidi.
Historia imekitetea. Mwaka 1994 gaidi akawa rais; na chama cha kigaidi kikawa chama tawala!
Hoja yangu hapa ni kwamba Serikali ya Tanzania inajua kuwa CHADEMA si chama cha kigaidi. Inajua ni chama cha siasa kinachowapa watawala wakati mgumu sasa. Inaona kinaungwa mkono na wananchi wengi, hasa vijana.
Inaona kimebeba dhima ya mabadiliko. Inajaribu kujenga mazingira ya kutengeneza hofu miongoni mwa Watanzania. Inadhani kwamba itakapotangaza CHADEMA kuwa chama cha kigaidi kitakosa mashabiki, kitapwaya na kitakufa!
Bahati mbaya, serikali haijasoma hata saikolojia ya umma inaoulazimisha ukubali suala hili. Hadi sasa viongozi wa serikali na CCM hawajajua kwamba wanafanya kazi nzuri ya kisiasa kwa manufaa ya CHADEMA.
Hawajajua kwamba kwa kelele hizi wanakipigia debe. Hawajajua kwamba kwa tuhuma hizi wanakifanyia kampeni. Hawajajua kwamba kwa kukisingizia ugaidi wanakifanya kionewe huruma hata na wale waliokuwa hawajakiunga mkono. Hawajajua kwamba kwa kukisakama namna hii wanaonesha kwamba wanakiogopa.
Kimsingi, wanataka kuilazimisha CHADEMA ifanye ugaidi kama wa kina Mandela. Inavyoonekana, wameshindwa kujifunza kutokana na historia.
Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya, Raila Odinga, hakufika hapo kirahisi. Miongoni mwa misukosuko ya kisiasa iliyompata ni pamoja na kuitwa gaidi, mhaini na kufungwa zaidi ya mara tisa. Haikuzuia harakati za kuleta mabadiliko Kenya. Leo wana katiba mpya, sisi bado tunangangania mambo yale yale!
Mwaka 1995 viongozi wa CCM walitumia mikanda ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda kutisha wananchi, eti wakichagua upinzani wataleta vita kama ya Rwanda. Mbinu na hofu hiyo haviwezi kufanya kazi leo.
Watawala wetu wa sasa wasipopata mwanga mpya, iwapo wataendelea kupanda mbegu ya udini, ukabila na ugaidi wa kisiasa, wananchi wapenda mabadiliko watatumia udini, ukabila na ugaidi huo huo kuwaondoa madarakani. Lakini nchi itakuwa imegawanyika, na imechafuka. Badala ya kuwa tishio, ugaidi unaweza kugeuka silaha ya mabadiliko.
Watawala wasipotaka kutumia hoja kukabiliana na nguvu ya kisiasa ya CHADEMA, wakawekeza kwenye hila na dhana ya ugaidi; kama watafunga milango ya hoja na kutumia mabavu ya vyombo vya dola, wasidhani hawatavuna zao la mbegu wanayopanda.
CHADEMA wako katika kipindi kigumu. Lakini ni kipindi kizuri, chenye rutuba kisiasa, kwa sababu wanasaidiwa na CCM na serikali. Ni kipindi pekee katika historia ya mageuzi nchini ambapo chama tawala kinafanya siasa za kujiua na kukuza wapinzani. Tulalamike? Tushangilie?
Imeandikwa na Ansebert Ngurumo.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Kwanza, inasema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kidini, kikabila na kigaidi. Pili, inawatumia makada wake kutamka kwamba chama hicho kitakufa.
Tunajua kuwa inafanya hivyo kunusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM). Lakini kwa tabia hii, tutaiita serikali au genge la wapika propaganda za kigaidi?
Hebu tuulizane. Watawala wanaotumia na kupandikiza hisia za udini na ukabila kama mbinu ya kuwashinda wapinzani wao wanastahili kuaminiwa tena? Wanaweza kuzungumzia amani na utulivu?
Watawala wanaoingiza Jeshi la Polisi katika misukosuko ya kiitikadi, wanadhani wanapanda mbegu ya amani na ustahamilivu? Chama cha siasa kinachotegemea nguvu za dola kama njia ya kupata ushindi kina haki ya kuendelea kuaminiwa?
Tukumbushane. Mwaka 2005, katikati ya joto kali la Uchaguzi Mkuu, baada ya kubanwa na CUF, serikali ilimtumia Mkuu wa Jeshi la Polisi wa wakati ule, Inspekta Jenerali Omar Mahita, kutisha wapiga kura.
Mahita akajidhalilisha, akaibukia kwenye TV akiwa na visu vilivyopakwa rangi za bendera ya CUF, akisema jeshi lake limekamata kontena la visu ambavyo chama hicho kilikuwa kinakusudia kufanyia ugaidi.
Hadi leo hawajatueleza visu hivyo vilipelekwa wapi. Hatujaambiwa kontena hilo liliishia wapi. Hatujasikia mtu yeyote au kiongozi wa CUF amekamatwa kwa ugaidi. Wala hakuna kesi yoyote mahakamani dhidi ya viongozi au wanachama wa CUF kutokana na tukio hilo.
Ni dhahiri lilikuwa tukio la kupika na kuidhalilisha CUF mbele ya umma. Ilikuwa mbinu ya ushindi mchafu. Na kwa kuwa iliwasaidia kuipiku CUF na kuidhoofisha, sasa wamedhani mbinu ile ile itakuwa msaada kwao kuimaliza CHADEMA.
Ndiyo maana na tambo zao eti CHADEMA kitakufa kabla ya 2015. Ndiyo sababu ya kauli za kidini, kikabila ka kigaidi dhidi ya CHADEMA. Wanapanda mbegu chafu katika siasa za Tanzania, kwa hofu tu ya kuondoka madarakani!
Halafu wanathubutu kusimama majukwaani kutamka kwamba wapinzani wana uchu wa madaraka. Yapi? Nani anangangania madaraka kati ya wale waliokaa madarakani kwa miaka 50 na wale wanaotaka kuingia madarakani kwa mara ya kwanza?
Mbinu chafu za kutumia vyombo vya dola, udini, ukabila na ugaidi hazioneshi uzoefu, weledi, wala umakini katika kutawala. Kwa maana nyingine, tunaweza kusema miaka 50 ya kukaa madarakani haijawasaidia watawala wetu. Bado wanabahatisha!
Zaidi ya hayo, wanatujengea Jeshi la Polisi lisilo adilifu, lililo tayari kuingizwa kwenye michezo michafu ya kihuni na kihalifu kwa ajili ya kutukuza watawala.
Kama leo tungeulizana, upo wapi uadilifu wa Mahita? Tunakuwa na uhakika gani na uadilifu wa viongozi wa Jeshi la Polisi baada ya Mahita?
Kwanini serikali inataka kulifikisha Jeshi la Polisi mahali ambapo halitaheshimika wala kuaminika? Kwanini inatumia vyombo vya dola kukandamiza haki na kulinda uovu?
Na baada ya yote yaliyotokea katika nchi za wenzetu Syria, Tunisia, Misri, Libya, Kenya, Zimbabwe na kwingineko, kwanini watawala hawajifunzi kwamba matumizi ya Jeshi la Polisi hayawezi kuzuia wimbi la mabadiliko?
Jambo moja ambalo watawala hawajaelewa ni kwamba walifanikiwa kuidhoofisha CUF kwa sababu kilishitukizwa. CHADEMA kimeandaliwa, na kimejiandaa kisaikolojia na kimkakati kushinda propaganda hizi.
Tatizo si CHADEMA. Hoja si CHADEMA. Hoja ni mabadiliko. Yatakuja tu. Kama si kwa kupitia mlangoni, yatapitia dirishani. Nguvu ya mabadiliko ni baraka. Hata ukifunga milango, itapenya!
Bahati mbaya, watawala hawajasoma alama za nyakati. Wananchi wa sasa wameshaelewa mbinu zao. Maoni ya kizazi cha leo cha Watanzania ni kuondoa mfumo wa utawala uliodumu kwa miaka 50.
Elimu ya uraia iliyotolewa kwa wananchi wa sasa ikichangiwa na harakati za vyama vya siasa, asasi za kiraia na udhaifu wa serikali yenyewe katika kuhudumia wananchi imesaidia kuamsha wananchi kuamka. Wanajua haki zao, na wapo tayari kupambana na dhalimu yeyote.
Kwa muda sasa, kutokana na mwenendo wa serikali, wananchi wamejenga hasira dhidi ya watawala, kiasi kwamba anapopatikana hata mtu mmoja wa kupambana na watawala hao anaonekana shujaa mbele ya umma.
Na jitihada zozote za watawala kumdhulumu mtu yeyote anayekosoa au kusumbua watawala huzaa chuki kutoka kwa umma.
Ndiyo maana wananchi wanaelewa fika kwamba ugaidi wa CHADEMA unaozungumzwa sasa ni siasa za mchoko wa CCM na serikali yake. Ni propaganda na hujuma zile zile walizofanyiwa CUF miaka ile.
Ni hatua za mwisho za kutapatapa kwao baada ya kushindwa siasa za hoja majukwaani na katika nyanja nyingine rasmi. Ni teke zito la ngamia anayekata roho!
Kizazi cha leo kinachotafuta ukombozi wa pili wa Tanzania hakiwezi kuogopa kuitwa magaidi. Kinajua kuwa hata ikibidi, CUF na CHADEMA si wa kwanza kuitwa hivyo.
Mifano ni mingi, lakini nitatoa michache kukazia hoja hii. Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, aliitwa gaidi baada ya kutishia masilahi ya watawala.
Alitafutwa kunyongwa. Alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Kumbukumbu zinaonesha yeye mwenyewe aliwahi kukiri makosa yapatayo 156 ya kigaidi dhidi ya serikali ya Kaburu!
Mara kadhaa, utawala wa kikaburu, chini ya Rais P. W. Botha uliwahi kumtaka Mandela akanushe kuhusika na ugaidi ili rais amsamehe, amwondolee kifungo.
Mandela alikataa! Aliona ni bora aendelee kuitwa gaidi iwapo ugaidi huo ni harakati za kuwakomboa wananchi wa Afrika Kusini.
Lakini watawala wa Afrika Kusini, hawakuanza na Mandela. Walianza na Chama chake, African National Congress (ANC), kilichoasisiwa mwaka 1912. Kati ya 1961 na 1990, watawala na maswahiba wao wa ndani na nje walitangaza na kutuhumu ANC kuwa ni chama cha kigaidi.
Historia imekitetea. Mwaka 1994 gaidi akawa rais; na chama cha kigaidi kikawa chama tawala!
Hoja yangu hapa ni kwamba Serikali ya Tanzania inajua kuwa CHADEMA si chama cha kigaidi. Inajua ni chama cha siasa kinachowapa watawala wakati mgumu sasa. Inaona kinaungwa mkono na wananchi wengi, hasa vijana.
Inaona kimebeba dhima ya mabadiliko. Inajaribu kujenga mazingira ya kutengeneza hofu miongoni mwa Watanzania. Inadhani kwamba itakapotangaza CHADEMA kuwa chama cha kigaidi kitakosa mashabiki, kitapwaya na kitakufa!
Bahati mbaya, serikali haijasoma hata saikolojia ya umma inaoulazimisha ukubali suala hili. Hadi sasa viongozi wa serikali na CCM hawajajua kwamba wanafanya kazi nzuri ya kisiasa kwa manufaa ya CHADEMA.
Hawajajua kwamba kwa kelele hizi wanakipigia debe. Hawajajua kwamba kwa tuhuma hizi wanakifanyia kampeni. Hawajajua kwamba kwa kukisingizia ugaidi wanakifanya kionewe huruma hata na wale waliokuwa hawajakiunga mkono. Hawajajua kwamba kwa kukisakama namna hii wanaonesha kwamba wanakiogopa.
Kimsingi, wanataka kuilazimisha CHADEMA ifanye ugaidi kama wa kina Mandela. Inavyoonekana, wameshindwa kujifunza kutokana na historia.
Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya, Raila Odinga, hakufika hapo kirahisi. Miongoni mwa misukosuko ya kisiasa iliyompata ni pamoja na kuitwa gaidi, mhaini na kufungwa zaidi ya mara tisa. Haikuzuia harakati za kuleta mabadiliko Kenya. Leo wana katiba mpya, sisi bado tunangangania mambo yale yale!
Mwaka 1995 viongozi wa CCM walitumia mikanda ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda kutisha wananchi, eti wakichagua upinzani wataleta vita kama ya Rwanda. Mbinu na hofu hiyo haviwezi kufanya kazi leo.
Watawala wetu wa sasa wasipopata mwanga mpya, iwapo wataendelea kupanda mbegu ya udini, ukabila na ugaidi wa kisiasa, wananchi wapenda mabadiliko watatumia udini, ukabila na ugaidi huo huo kuwaondoa madarakani. Lakini nchi itakuwa imegawanyika, na imechafuka. Badala ya kuwa tishio, ugaidi unaweza kugeuka silaha ya mabadiliko.
Watawala wasipotaka kutumia hoja kukabiliana na nguvu ya kisiasa ya CHADEMA, wakawekeza kwenye hila na dhana ya ugaidi; kama watafunga milango ya hoja na kutumia mabavu ya vyombo vya dola, wasidhani hawatavuna zao la mbegu wanayopanda.
CHADEMA wako katika kipindi kigumu. Lakini ni kipindi kizuri, chenye rutuba kisiasa, kwa sababu wanasaidiwa na CCM na serikali. Ni kipindi pekee katika historia ya mageuzi nchini ambapo chama tawala kinafanya siasa za kujiua na kukuza wapinzani. Tulalamike? Tushangilie?
Imeandikwa na Ansebert Ngurumo.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums