Maswali magumu kwa Edward Ngoyai Lowassa

Maswali magumu kwa Edward Ngoyai Lowassa

Kolimba Jr

Member
Joined
Nov 24, 2014
Posts
83
Reaction score
68
MASWALI MAGUMU KWA MH. EDWARD NGOYAI LOWASA
Kwako mh. Edward Lowassa,
Ni matumaini yetu kuwa u mzima wa afya. Kuelekea mchakato wa Urais mwaka huu tumesikia kuwa nawe baba utatangaza nia. Sisi wananchi wa mtaani tunayo maswali machache tunaomba utusaidie tupate kujua wakati utakapotangaza nia yako rasmi uwanja wa Sheikh Abeid Karume huko Arusha. Maswali yetu ni machache tu mh. mpendwa:-

1.Tangu umejiuzulu nafasi yako ya uwaziri mkuu kufuatia kashfa ya ufisadi wa Richmond, imekuchukua miaka 7 kujitetea mbele ya umma.Ulikua wapi muda wote huo?

2.Umelieleza taifa na dunia kuwa hukufanya kazi sehemu yoyote zaidi ya CCM tangu mwaka 1977, Je utajiri ulionao umeutoa wapi? Huko CCM kuna biashara gani ulifanya?

3.Kwanini hujawahi na inaonekana huwezi kukemea wala kuzungumzia Rushwa na ufisadi? Unatofautiana vipi na kauli ya mwenyekiti mwenza wa UKAWA mh Freeman Mbowe kuwa wewe ni "dhaifu, usiyeweza kukemea rushwa, ufisadi na ubadhirifu?"

4.Kwanini sehemu kubwa ya wanaokuunga mkono ni wale ambao walifeli au kukataliwa na wananchi au kufukuzwa kazi katika nafasi mbalimbali za chama na serikali kwa kashfa? Mfano Rostam Azizi, Nazir Karamagi, Andrew Chenge, Lawrence Masha, Juma Kapuya, Cyril Chami n.k?

5.Ulizipataje hisa zako unazomiliki VODACOM? Ulizinunua lini na kwa kiasi gani?

6.Wakati unaajiriwa na CCM kama katibu msaidizi miaka ya 70, inasemekana ulimuibia baba yako mzazi ng'ombe ukawauza na kununua gari, kisha mzee wako akaenda kukushitaki kwa viongozi wa Chama kuwa hufai na ufukuzwe kazi. Je, hii ni kweli?

7.Wewe ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa, kikao kinachojadili na kuamua mambo makubwa ya kusimamia serikali inayotawala. Je,umewahi kujenga hoja zipi za kutetea wananchi? Kusimamia serikali? Mara ngapi? Lini?

8.Tangu umekua mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje miaka mitano sasa, wewe ni mwenyekiti pekee ambae hujawahi kusimama hata mara moja kusoma taarifa ya kamati bungeni. Je, ni kwanini? Tatizo ni afya yako inakufanya usiweze kusimama kuongea kwa muda mrefu au nini?

9.Kwanini unatumia pesa nyingi sana kutafuta urais wa nchi? Pesa hizo utazirudishaje kwa hao unaowaita marafiki zako? Ikulu kuna biashara gani? Je, ikiwa Urais unanunuliwa, sisi watoto wa masikini watoto wetu wajifunze nini? Kuwa wataendelea kubaki katika tabaka la watawaliwa hadi watakapokuwa na mabilioni ya kutosha?

10.Kumbukumbu zinaonesha kuwa hayati mwalimu Julius Nyerere aliwahi kukukataa kutokana na kuonekana ukiwa na ukwasi usio na maelezo,Je, uliwahi kumjibu mwalimu kabla ya umauti wake kuwa ulipataje mali zako? Ili arekebishe kauli yake?
NAKUOMBA UTUSAIDIE SISI WANYONGE TUJUE KAMA TUNAWEZA KUKUAMINI KWA HILO UNALOOMBA.MAANA TUNA MASHAKA.
WAANDISHI MLIOZUNGUMZA NA LOWASA MLIPASWA KUMUULIZA MASWALI HAYA.
Tunatanguliza shukrani,
Ni sisi wananchi wa kawaida mtaani.
 
MASWALI MAGUMU KWA MH. EDWARD NGOYAI LOWASA
1.Tangu umejiuzulu nafasi yako ya uwaziri mkuu kufuatia kashfa ya ufisadi wa Richmond, imekuchukua miaka 7 kujitetea mbele ya umma.Ulikua wapi muda wote huo?

2.Umelieleza taifa na dunia kuwa hukufanya kazi sehemu yoyote zaidi ya CCM tangu mwaka 1977, Je utajiri ulionao umeutoa wapi? Huko CCM kuna biashara gani ulifanya?

3.Kwanini hajawahi na inaonekana huwezi kukemea wala kuzungumzia Rushwa na ufisadi? Unatofautiana vipi na kauli ya mwenyekiti mwenza wa UKAWA mh Freeman Mbowe kuwa wewe ni "dhaifu, usiyeweza kukemea rushwa, ufisadi na ubadhirifu?"

4.Kwanini sehemu kubwa ya wanaokuunga mkono ni wale ambao walifeli au kukataliwa na wananchi au kufukuzwa kazi katika nafasi mbalimbali za chama na serikali kwa kashfa? Mfano Rostam Azizi, Nazir Karamagi, Andrew Chenge, Lawrence Masha, Juma Kapuya, Cyril Chami n.k?

5.Ulizipataje hisa zako unazomiliki VODACOM? Ulizinunua lini na kwa kiasi gani?

6.Wakati unaajiriwa na CCM kama katibu msaidizi miaka ya 70, inasemekana ulimuibia baba yako mzazi ng'ombe ukawauza na kununua gari, kisha mzee wako akaenda kukushitaki kwa viongozi wa Chama kuwa hufai na ufukuzwe kazi. Je, hii ni kweli?

7.Wewe ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa, kikao kinachojadili na kuamua mambo makubwa ya kusimamia serikali inayotawala. Je,umewahi kujenga hoja zipi za kutetea wananchi? Kusimamia serikali? Mara ngapi? Lini?

8.Tangu umekua mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje miaka mitano sasa, wewe ni mwenyekiti pekee ambae hujawahi kusimama hata mara moja kusoma taarifa ya kamati bungeni. Je, ni kwanini? Tatizo ni afya yako inakufanya usiweze kusimama kuongea kwa muda mrefu au nini?

9.Kwanini unatumia pesa nyingi sana kutafuta urais wa nchi? Pesa hizo utazirudishaje kwa hao unaowaita marafiki zako? Ikulu kuna biashara gani? Je, ikiwa Urais unanunuliwa, sisi watoto wa masikini watoto wetu wajifunze nini? Kuwa wataendelea kubaki katika tabaka la watawaliwa hadi watakapokuwa na mabilioni ya kutosha?

10.Kumbukumbu zinaonesha kuwa hayati mwalimu Julius Nyerere aliwahi kukukataa kutokana na kuonekana ukiwa na ukwasi usio na maelezo,Je, uliwahi kumjibu mwalimu kabla ya umauti wake kuwa ulipataje mali zako? Ili arekebishe kauli yake?
NAKUOMBA UTUSAIDIE SISI WANYONGE TUJUE KAMA TUNAWEZA KUKUAMINI KWA HILO UNALOOMBA.MAANA TUNA MASHAKA.
 
Hilo swali la utajiri alishalijibu baada ya kuulizwa na nyerere hayo mengine yatajibiwa may 30 kwa sasa tupo busy na maandalizi ya rais wa mioyo ya watanzania
 
Team lowasa na marafiki tunaomba majibu....... yaani kweli nikijibiwa hata mm hayo maswali ninaweza kugikiria kuweka tick kwake October 😉
 

Attachments

  • 1432746835444.jpg
    1432746835444.jpg
    52 KB · Views: 1,917
...Mhh yaani haya maswali nikijaribu kubadili jina na kupachika la JK, sijui kama majibu yatakuwa yale yale au ? Kusimama kusoma taarifa ndiyo nn, bora hata mtu anaye-delegate hasa ukichukulia taarifa zenyewe ni ndiyoooo hata wale wanaokuwa wameuchapa usingizi !! Kama una makamu, delegation ni sifa ya uongozi bora !! Kwa bunge ili la kusifia bange, au kutukana matusi na urongo km akina kibajaji si bora kukaa kimya... !!
 
Mi binafsi sijawai muona lowassa akichangia bugeni au kuuliza swali kuwatetea wafugaji wenzake ambao kila kukicha wanatwangana na wakulikulima. Je akipewa nchi ataweza kweli ata kuandaa hotuba ya kila mwisho wa mwezi kama wenzake au kujenga hoja ya kuwatetea watz au ndo atakuwa anafikiria namna ya kurudisha pesa atakazo kuwa ametumia kipindi cha kutangaza nia!
 
Haya maswali ndio yalipaswa kuulizwa na waandishi wa habari.chaa ajabu sijuwi ndio nani yule wa clouds tv anamuuliza kwanini unaitwa edward.
 
MASWALI MAGUMU KWA MH. EDWARD NGOYAI LOWASA
1.Tangu umejiuzulu nafasi yako ya uwaziri mkuu kufuatia kashfa ya ufisadi wa Richmond, imekuchukua miaka 7 kujitetea mbele ya umma.Ulikua wapi muda wote huo?

2.Umelieleza taifa na dunia kuwa hukufanya kazi sehemu yoyote zaidi ya CCM tangu mwaka 1977, Je utajiri ulionao umeutoa wapi? Huko CCM kuna biashara gani ulifanya?

3.Kwanini hajawahi na inaonekana huwezi kukemea wala kuzungumzia Rushwa na ufisadi? Unatofautiana vipi na kauli ya mwenyekiti mwenza wa UKAWA mh Freeman Mbowe kuwa wewe ni "dhaifu, usiyeweza kukemea rushwa, ufisadi na ubadhirifu?"

4.Kwanini sehemu kubwa ya wanaokuunga mkono ni wale ambao walifeli au kukataliwa na wananchi au kufukuzwa kazi katika nafasi mbalimbali za chama na serikali kwa kashfa? Mfano Rostam Azizi, Nazir Karamagi, Andrew Chenge, Lawrence Masha, Juma Kapuya, Cyril Chami n.k?

5.Ulizipataje hisa zako unazomiliki VODACOM? Ulizinunua lini na kwa kiasi gani?

6.Wakati unaajiriwa na CCM kama katibu msaidizi miaka ya 70, inasemekana ulimuibia baba yako mzazi ng'ombe ukawauza na kununua gari, kisha mzee wako akaenda kukushitaki kwa viongozi wa Chama kuwa hufai na ufukuzwe kazi. Je, hii ni kweli?

7.Wewe ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa, kikao kinachojadili na kuamua mambo makubwa ya kusimamia serikali inayotawala. Je,umewahi kujenga hoja zipi za kutetea wananchi? Kusimamia serikali? Mara ngapi? Lini?

8.Tangu umekua mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje miaka mitano sasa, wewe ni mwenyekiti pekee ambae hujawahi kusimama hata mara moja kusoma taarifa ya kamati bungeni. Je, ni kwanini? Tatizo ni afya yako inakufanya usiweze kusimama kuongea kwa muda mrefu au nini?

9.Kwanini unatumia pesa nyingi sana kutafuta urais wa nchi? Pesa hizo utazirudishaje kwa hao unaowaita marafiki zako? Ikulu kuna biashara gani? Je, ikiwa Urais unanunuliwa, sisi watoto wa masikini watoto wetu wajifunze nini? Kuwa wataendelea kubaki katika tabaka la watawaliwa hadi watakapokuwa na mabilioni ya kutosha?

10.Kumbukumbu zinaonesha kuwa hayati mwalimu Julius Nyerere aliwahi kukukataa kutokana na kuonekana ukiwa na ukwasi usio na maelezo,Je, uliwahi kumjibu mwalimu kabla ya umauti wake kuwa ulipataje mali zako? Ili arekebishe kauli yake?
NAKUOMBA UTUSAIDIE SISI WANYONGE TUJUE KAMA TUNAWEZA KUKUAMINI KWA HILO UNALOOMBA.MAANA TUNA MASHAKA.

aswali muhimu kabisa.
 
Maswali yote kumi kwa huyu fisadi hana hata swali moja lenye kuweza kulitolea majibu sahihi! Bonge la Jambazi.
 
Back
Top Bottom