ShyaRuwa
JF-Expert Member
- May 30, 2015
- 8,248
- 14,770
1.Mungu kama ulimwumba kila mtu kwa mfano wako, je wewe ni mwamaume au mwanamke?
2.Mtu akiugua, aende hospitalini kupewa tiba au akafanyiwe maombi? Na akifanya vyote, kipi kitasaidia zaidi?
3.Mungu wakati unamwumba mwanaume uliweka govi, hukujua ni najisi? mbona unasema likwatwe? huko siyo kuediti uumbaji wako?
4.Watakaoingia mbinguni, watafurahi vipi kama ndugu zao wawapendao watakuwa jehanamu?
5.Baada ya gharika ya Nuhu, maji ya mafuriko yalielekea wapi??? Kwa sababu kila mahali palijaa maji.
6.Kwanini ulichelewa kumwumba mwanamke ilihali ulimuumba mwanaume na uhitaji wa mwanamke? Nadhani hapo ndo chanzo cha kujichua.
7.Mungu kwanini uliumba bangi? ni ya kazi gani? Mbona watu wako wanaipinga sana?
8.Mungu kama wewe ni mpangaji wa maisha yetu, kwanini tukusumbue kwa sala?
9.Mbona watu wema wanapatwa na mabaya? Si uliahidi mema ya nchi kwa watenda mema?
10.Kama watu wote ni uzao wa Adam na Eva, mbona tunatofautiana sana...nini chanzo cha kuwepo kwa watu weupe na weusi?
11.Mungu mbona kwenye maandiko yako umechochea sana utumwa(slavery)? kwani tukiishi kwa usawa haikupendezi?
12.Mungu una urafiki na shetani? mbona mnakutana mara kwa mara na kupiga stori( Ayubu 1:6-12)
14.Kwanini ulimtese Ayubu kwa lengo la kuridhisha matakwa shetani?
15.Mungu mbona ulimpa Musa amri ya usiue lakini ukampa maagizo ya kuua...Mungu hadi leo pale middle east wanauana.
16.Mungu kwa kuwa ulisema tupumzike siku ya 7, mbona watu wanatembea umbali mrefu kutafuata majumba ya ibada na wengine wanatumia hiyo siku ya 7 kupata pesa kwa njia ya sadaka? kwanini tusibaki nyumbani tupumzike?
17.Baada ya Kaini kumua Abeli ulimuuliza Kaini ndugu yako yupo wapi, hivi ni kweli hukujua alipokua Abeli?
18.Mungu kama unalounganisha hakuna awezae kulitenganisha, mbona ndoa zinavunjika?
19.Mungu hivi Suleiman ndiye aliyekuwa na hekima kuliko wote? mbona alifanya mambo kuntu sana? Wanawake 1000 siyo mchezo...au polygamism ndio hekima yenyewe?
20.Mungu kwanini ulimpa Hitler roho mabaya kiasi kile? yaani alichokifanya humu duniani we acha tu.
Naamini kuna watumishi wa Mungu huku jf, kwahiyo ningepende wanisaidie majibu ya haya maswali...nimeuliza siyo ayajibu Mungu bali watu wenye uelewa na haya mambo...Kama mtu huna jibu kuwa mvumilivu maana wapo wenye ufahamu wa kutosha na siyo kulaani, kuhukumu na kuniona kana kwamba nimepotea...Muhimu zaidi jibu la uongo halitakiwi...pia kama jibu lina utata nitauliza.Karibuni kwa majadiliano yenye nia ya kueleweshana
2.Mtu akiugua, aende hospitalini kupewa tiba au akafanyiwe maombi? Na akifanya vyote, kipi kitasaidia zaidi?
3.Mungu wakati unamwumba mwanaume uliweka govi, hukujua ni najisi? mbona unasema likwatwe? huko siyo kuediti uumbaji wako?
4.Watakaoingia mbinguni, watafurahi vipi kama ndugu zao wawapendao watakuwa jehanamu?
5.Baada ya gharika ya Nuhu, maji ya mafuriko yalielekea wapi??? Kwa sababu kila mahali palijaa maji.
6.Kwanini ulichelewa kumwumba mwanamke ilihali ulimuumba mwanaume na uhitaji wa mwanamke? Nadhani hapo ndo chanzo cha kujichua.
7.Mungu kwanini uliumba bangi? ni ya kazi gani? Mbona watu wako wanaipinga sana?
8.Mungu kama wewe ni mpangaji wa maisha yetu, kwanini tukusumbue kwa sala?
9.Mbona watu wema wanapatwa na mabaya? Si uliahidi mema ya nchi kwa watenda mema?
10.Kama watu wote ni uzao wa Adam na Eva, mbona tunatofautiana sana...nini chanzo cha kuwepo kwa watu weupe na weusi?
11.Mungu mbona kwenye maandiko yako umechochea sana utumwa(slavery)? kwani tukiishi kwa usawa haikupendezi?
12.Mungu una urafiki na shetani? mbona mnakutana mara kwa mara na kupiga stori( Ayubu 1:6-12)
14.Kwanini ulimtese Ayubu kwa lengo la kuridhisha matakwa shetani?
15.Mungu mbona ulimpa Musa amri ya usiue lakini ukampa maagizo ya kuua...Mungu hadi leo pale middle east wanauana.
16.Mungu kwa kuwa ulisema tupumzike siku ya 7, mbona watu wanatembea umbali mrefu kutafuata majumba ya ibada na wengine wanatumia hiyo siku ya 7 kupata pesa kwa njia ya sadaka? kwanini tusibaki nyumbani tupumzike?
17.Baada ya Kaini kumua Abeli ulimuuliza Kaini ndugu yako yupo wapi, hivi ni kweli hukujua alipokua Abeli?
18.Mungu kama unalounganisha hakuna awezae kulitenganisha, mbona ndoa zinavunjika?
19.Mungu hivi Suleiman ndiye aliyekuwa na hekima kuliko wote? mbona alifanya mambo kuntu sana? Wanawake 1000 siyo mchezo...au polygamism ndio hekima yenyewe?
20.Mungu kwanini ulimpa Hitler roho mabaya kiasi kile? yaani alichokifanya humu duniani we acha tu.
Naamini kuna watumishi wa Mungu huku jf, kwahiyo ningepende wanisaidie majibu ya haya maswali...nimeuliza siyo ayajibu Mungu bali watu wenye uelewa na haya mambo...Kama mtu huna jibu kuwa mvumilivu maana wapo wenye ufahamu wa kutosha na siyo kulaani, kuhukumu na kuniona kana kwamba nimepotea...Muhimu zaidi jibu la uongo halitakiwi...pia kama jibu lina utata nitauliza.Karibuni kwa majadiliano yenye nia ya kueleweshana