Maswali 11 kwa Baba Askofu Dallu

Huyu mkuu bado yuko mbali kweli...hivi bado tuna hoja za rais muislam na mkristu..?

germve himself
 
akitoa ufafamuzi kuhusu wake mapandre na maaakofu wanaowalawiti watoto wakiumee mnitag na mimi.
 
Umeandika vizuri,ila huwezi kuwa unahangaika kutafuta pesa ,kisha unasomesha mwanao au nduguyo wa kike kumbe yeye tamaa za mapenzi ndo ziko mbele kuliko elimu ,hakika hili jambo halikubaliki. Sisi tunaosomesha tunajua maumivu yake ,ndo maana tunawaasa sana. Ukiruhusu MTU kuzaa na kuja shule ,uneruhusu uzinifu.
Tendo la ndoa hufanywa na wanandoa,, ndo maana hakuna maadili siku hizi. Mabinti wanapewa mimba na wauza viepe (chips) na Bodaboda kisha wanawatelekeza,kisha kazi inakuwa kwako kulea mtoto wa mwanaume mwenzio,kibaya zaidi hawa mabinti wanawakinngia kifua hao waliowapa ujauzito "wakisema wanawapenda sana" tena hutishia kujiua unapomwuliza maswali mengi.

Kiufupi mambo mawili hayachanganyikani .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mavazi yake tu yanaonesha si utamaduni wake zaidi ya kuendeleza utamaduni wa wayahudi

tamaduni wetu ni kaniki na kusalia panapo miti mikubwa, vichuguu na makaburini

baba askofu anajua wazi kwamba tumeacha kuwa kumbuka mababu zetu tumebaki kuwa kumbuka na kuwaombea mababu wa kiyahudi, eti wao ndio wanafaa kukumbukwa na kuombewa

kwa ufupi amepotoka arudi kwenye misingi yetu
 

Hiki ni kipindi ambacho Kanisa kwa ujumla wake limekuwa na kigugumizi tangu Tanzania kupata uhuru.
Dhana ya utamaduni wa mwafrika nadhani ni ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia, nasema hivo kwa sababu hata hili kanisa analo liongoza yeye halikuwa utamaduni wa kiafrika. Kama kweli Askofu anaamini katika utamaduni wa kiafrika kwanza yeye atoe rozari alovaa shingoni, kwani siyo utamaduni wetu. Zama za mababu zetu kihistoria walivaa shanga, pembe, manyoa ya wanyama nk.

Ikiwa baba askofu anataka tufuate utamaduni kanisa analongooza liliruhusu mapadri kuoa kwani kutokuoa haukuwa utamaduni wa kiafrika, waafrika waliruhusiwa kuoa tena zaidi ya mke mmoja, Utamaduni wa mwafrika ni upi anaongelea askofu?

Utamaduni wa afrika ni kina dada kutokuolewa na kuruhusiwa kuzaa kwa misingi ya usista? Utamaduni wa mwafrika ni upi?

Anasema kanisa litakuwa na masisita wa aina gani? Je anataka kutuaminisha kuwa wote waliosoma hizo shule anazoongelea ni masisita leo? Hapana askofu huu siyo utamaduni wa kiafrika unaohubiri yeye. Ingekuwa vizuri kama ungeongelea maadili zaidi, Umejiuliza hawa wanaopata mimba mashuleni ni watoto wa familia za uwezo gani wa kipato zaidi?

Baba askofu asingetaja utamaduni ningemwelewa. Kama kanisa mungejaribu kutafuta changamoto kwa nini watoto wanapata mimba mashuleni na jinsi ya kusaidia.

Baba askofu mbona kanisa lako ndo linaongoza kwa kwesi za kudharirisha watoto kote duniani? au unataka tuwafungie ndani kama ilivokuwa utamaduni wa kanisa kuwafungia wasichana wote wanaopata ujauzito na hatimaye wakaishiakuolewa na walinzi na madereva wenu maaskofu.

Askofu rudi katika magoti tafakari na Mungu wako kuhusu hili tamko lako. Yesu asingekufa msalabani kama kusingekuwa na msamaha wa dhambi, lakini pia biblia ama maandiko yanatuzuia tusihukumu tusijehukumiwa.
 

Unadhani njia sahihi ya kudhibiti tamaa ni kumzuia kwenda shule? Unatoka kusema wewe hukuwahi kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa? Hii sheria ilikuwepo toka zamani je imeshazuia mimba kwa kiasi gani? hebu lete takwimu. Ni rahisi sana kuongea hapa mtandaoni na kujinasibu eti wewe unasomesha, hebu sasa fikiria tayari amezaa na ametelekezwa hapo kwako asipomrudisha shule ina maana yeye ataendeelea kuwa jobless na mtoto wake pia ni jobless, maanake utaendelea kulea binti yako na mjukuu. Ni vema ukamsaidia huyo binti ili baadae aweze kusimama. Tofauti na hapo ni mzigo wako mpaka siku unaenda kaburini.
 
Ukweli in za ghali yaani wanasoma wenye nazo tuu...ila uache uongo seminary nyingi zimejengwa na wafadhili sio waamini

germve himself
Kwa mtazamo wako shule za Kanisa ni seminary tu, si ndiyo eeh?
 
Awamu ya mkatoliki mwenzao, ingekuwa awamu ya muislam Kikwete wangepishana kutoa matamko.
 
Nimekuelewa sana, yah man[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji377] [emoji377] [emoji377]

Jamii Forums mobile app
 
Wanatamani dunia ingekuwa yao peke yao

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni kweli. Wanaipupia sana dunia kiasi kwamba wapo tayari kuua au kuwaharibia wenzao maisha ili mradi tu dunia yao ipatikane utadhani wataishi milele! Hawana budi kutanabahi kuwa duniani tunapita tu na watakutana na Mola wao watake wasitake.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…