MASWALI 11 KUHUSU 'UJAMBAZI' WA BABA ASKOFU DALLU
Kupitia
gazeti la Kiongozi, ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Songea, Mhashamu Damian Dallu, amesema kuwa anaunga mkono hatua ya Rais John Magufuli kutoruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo.
"Hayo mambo siyo sehemu ya utamaduni wetu wa Afrika, ni mambo ya kigeni yanayotaka kutuchafulia utamaduni wetu."
Ameelezwa kushangazwa na watu wanaoongelea "haki ya tendo la ndoa" miongoni mwa wanafunzi walio shuleni. "Nawashangaa eti wanapigania haki ya tendo la ndoa, haki ya wapi hiyo?" Alihoji.
Hata hivyo, hakuna mwanaharakati anayeongelea "haki ya tendo la ndoa" miongoni mwa wanafunzi, kama Askofu Dallu anavyodai.
Kinachoongelewa na baadhi ya wanaharakati ni "haki ya kufanya tendo la ngono" waliyo nayo vijana ambao wamekwisha balehe, lakini bado ni matineja--vijana walio chini ya miaka 18.
Kwa hiyo, Askofu Dallu hapa ametengeneza "hoja-mwanasesere" (straw man), kuishambulia, na kujiona amefanya uenjilishaji wa uhakika, kwa kutumia mbinu halali.
Askofu Dallu anaendelea kuhoji tena, " Tutakuwa na shule za namna gani zinazoruhusu mwanafunzi kwenda kulea mtoto kisha arudi tena [shuleni] na akipata mimba nyingine aende tena nyumbani?'”
Hapa, Askofu Dullu ameuliza maswali mawili kwa mpigo. Hebu tuyatenganishe maswali ya Askofu Dallu ili yaweze kujibika vizuri, baada ya kuonyesha ulaghai wa kifalsafa anaoutumia.
Askofu Dallu, hapa ameuliza maswali mawili yafuatayo:
- Je, mwanafunzi akibeba mimba mara ya kwanza aruhusiwe tena kurudi shuleni baada ya kujifungua?
- Je, mwanafunzi akibeba mimba mara ya pili aruhusiwe tena kurudi shuleni baada ya kujifungua?
Katika namna yake ya kuuliza maswali haya mawili kwa mpigo, ametumia silaha za ujambazi wa kifalsafa kuwaburuza wasikilizaji wake. Yaani, anatumia silaha mbili za kutekeleza ujambazi wa kifalsafa--"the fallacy of loaded question" na "the fallacy of slippery slope."
Kwanza anatumia mbinu iitwayo "the fallacy of loaded question." Kwa ufupi, the fallacy of loaded question assumes a particular answer to another unasked question. Mfano wake ni huu, “Umekwisha acha kumpiga mkeo?” Swali hili linaulizwa kwa kuzingatia dhahania kwamba, tayari umekwisha jibu “ndiyo” kwa swali, “Je, huwa unampiga mkeo?”, swali ambalo, kwa kweli halijaulizwa kabisa.
Anafikiri kuwa, kwa vile wanaharakati wanatoa jawabu la "ndiyo" kwa swali la kwanza, basi wamekwishatoa jawabu la "ndiyo" kwa swali la pili. Sio kweli. Hilo ni swali ambalo bado halijajibiwa na yeyote. Njadala bado unaendelea.
Na pili anatumia mbinu iitwayo "the fallacy of slippery slope."
Kwa ufupi, according to the slippery-slope fallacy, if we permit a certain action, then all actions of this type, even the most extreme ones, will soon be permissible. In other words, once we start down the slope or (to vary the metaphor) get a foot in the door, there is no holding back. We commit the slippery-slope fallacy when evidence does not support this predicted outcome.
Kwa kutumia ulaghai huu, Askofu Dallu anasema bila ushahidi usiokanushika, kwamba, kama mwanafunzi aliyezaa mara moja ataruhusiwa kurudi shuleni, basi atapata sababu ya kuzaa mtoto wa pili, automatically! Kweli?
Hayo yote tisa. Kumi ni hoja ya Askofu Dallu ifuatayo, na inayopaswa kutufikirisha sana kuhusu namna baadhi ya Maaskofu wanavyotekeleza majukumu yao:
Askofu Dallu amejenga hoja ifuatayo:
- Kama "hayo mambo [ya kuruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo] yangekuwa sehemu ya utamaduni wetu wa Afrika," basi yangekuwa halali.
- Lakini, "hayo mambo [ya kuruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo] sio sehemu ya utamaduni wetu wa Afrika," badala yake, "ni mambo ya kigeni yanayotaka kutuchafulia utamaduni wetu."
- Kwa hiyo, "hayo mambo [ya kuruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo]" ni haramu.
- Hivyo, "hatua ya Rais John Magufuli kutoruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo" ni halali.
Kimuundo, hoja hii iko sawa. Lakini kimaudhui ni hoja mbaya. Yaani, baadhi ya madokezo yake sio ya kweli hata kidogo.
Kwa sababu ya ubovu wa kimaudhui katika hoja hii, ninayo maswali kadhaa kwa Baba Askofu Dallu.
Hapa Afrika, kabla ya ujio wa wageni, tulikuwa na mfumo wa elimu isiyo rasmi, familia zikiwa ni kitovu cha utekelezaji wake. Kabla ya kuja kwa wageni, mabinti walikuwa wanabeba mimba, kama ambavyo misamiati ya kimila kuhusu uwepo wa mimba kabla ya ndoa inavyoonyesha. Kule kwetu, tunaziita "ensinjo."
- Kama hivyo ndivyo, kabla ya ujio wa wageni, hawa mabinti zetu walikuwa wanatupwa jalalani baada ya kupata "mimba ya utotoni" tena kabla ya ndoa?
- Je, sheria asilia ya maadili kuhusu elimu inayosimamiwa na kanisa inasema nini kuhusu jukumu la serikali kukuza na kuhami maslahi ya kielimu?
- Je, sheria asilia ya maadili kuhusu ujinsia inayosimamiwa na kanisa inasema nini kuhusu jukumu la serikali kukuza na kuhami maslahi ya kijinsia?
- Je, sheria asilia ya maadili inasema kuwa maslahi ya kijinsia yana kipaumbele kikubwa zaidi ya maslahi ya kielimu?
- Je, sheria asilia ya maadili inasema nini kuhusu uchumi, afya, mazingira, siasa, na sekta nyingine za maisha ya binadamu?
- Mbona baadhi ya Maaskofu, nawe ukiwemo, hamsikiki kuongelea maadili katika sekta hizi baki?
- Neno maadili linamaanisha "maadili ya ngono" pekee?
- Ni halali kwa Askofu kufanya uenjilishaji kwa kutumia silaha ya ujambazi wa kifalsafa iitwayo "the fallacy of loaded question?"
- Ni halali kwa Askofu kufanya uenjilishaji kwa kutumia silaha ya ujambazi wa kifalsafa iitwayo "the fallacy of slippery slope?"
- Na je, kwa mujibu wa sheria asilia ya maadili, ni katika umri gani binadamu anakuwa na haki ya kufanya tendo la ngono?
- Na je, kwa mujibu wa sheria asilia ya maadili, ni katika umri gani binadamu anakuwa na haki ya kufanya tendo la ndoa?
Mwisho, niseme tu kwamba, baadhi ya waumini makini tungependa kuwasikia Maaskofu wetu mkijadili uhusiano uliopo kati ya sheria asilia ya maadili, kwa upande mmoja, na mdororo wa uchumi, uharibifu wa mazingira, wananchi kuwekwa rumande kwa siku 7 bila kupelekwa mahakamani, kwa upande mwingine. Hatuwasikii.
Ni kama vile ajenda kuu ya Kanisa ni kusimamia maadili ya gono.
Why?
Napendekeza kuwa Maaskofu Katoliki wajitafakari juu ya utume wao, wakiongozwa na Askofu Dallu.
Najua wanafanya kazi nzuri, lakini wakati mwingine wanaangukia pua...
RtbKazoba--Retired Bishop Kazoba