Masuala Yenye Utata - 1: Je; Kutoa Mimba Kuhalalishwe?

Masuala Yenye Utata - 1: Je; Kutoa Mimba Kuhalalishwe?

WAZO BINAFSI:
Kwa ufupi hili ni suala gumu kulijadili kwa sababu kuna pande mbili zinapingana: Kidini/Maadili, na Haki za binadamu.

Kidini, kama tungelikuwa tunafuata maamrisho ya dini zetu, wala kusingelikuwepo na tatizo hili. Lakini kwa kukiuka dini na maadili, ndio maana utoaji mimba upo na unazidi kila uchao.

Kwa kuwa tumewacha mafundisho na maadili, kwa sabau ya usasa wetu wa "haki za binadamu", tunafuata matakwa yetu kuliko maadili hayo, matokeo yake ni mimba zisizo tarajiwa na watoto wasiotakiwa.

Kwa tulipofika njia ni mbili tu: Ama turudi katika maadili yetu au tukubali ukweli. Ukweli uliopo sasa ni kuwa utoaji mimba upo. Tukiuharamisha mimba zitatolewa, tukiuhalalisha mimba zitatolewa. Madhara ya kuuharamisha ni kutolewa mimba kisirisiri, pengine na watu wasio wataalamu na waganga wa kienyeji. Inasikitisha kuwa baadhi ya wanaotoa mimba hufariki, wanaopona hubakiwa na madhara ya kudumu, kimwili na kisaikolojia.

Pengine ni bora kuuhalalisha huku kukiwa na sheria za kudhibiti hii hali, kwa mfano, mwisho wa umri wa ujauzito kutolewa, na sababu za kutolewa. Pia hii itapunguza machinjio bila ya utaalamu.

Mimi ninabakia na wazo la mchangiaji mmoja: Kinga ni bora kuliko tiba.
 
WAZO BINAFSI:
Kwa ufupi hili ni suala gumu kulijadili kwa sababu kuna pande mbili zinapingana: Kidini/Maadili, na Haki za binadamu.

Kidini, kama tungelikuwa tunafuata maamrisho ya dini zetu, wala kusingelikuwepo na tatizo hili. Lakini kwa kukiuka dini na maadili, ndio maana utoaji mimba upo na unazidi kila uchao.

Kwa kuwa tumewacha mafundisho na maadili, kwa sabau ya usasa wetu wa "haki za binadamu", tunafuata matakwa yetu kuliko maadili hayo, matokeo yake ni mimba zisizo tarajiwa na watoto wasiotakiwa.

Kwa tulipofika njia ni mbili tu: Ama turudi katika maadili yetu au tukubali ukweli. Ukweli uliopo sasa ni kuwa utoaji mimba upo. Tukiuharamisha mimba zitatolewa, tukiuhalalisha mimba zitatolewa. Madhara ya kuuharamisha ni kutolewa mimba kisirisiri, pengine na watu wasio wataalamu na waganga wa kienyeji. Inasikitisha kuwa baadhi ya wanaotoa mimba hufariki, wanaopona hubakiwa na madhara ya kudumu, kimwili na kisaikolojia.

Pengine ni bora kuuhalalisha huku kukiwa na sheria za kudhibiti hii hali, kwa mfano, mwisho wa umri wa ujauzito kutolewa, na sababu za kutolewa. Pia hii itapunguza machinjio bila ya utaalamu.

Mimi ninabakia na wazo la mchangiaji mmoja: Kinga ni bora kuliko tiba.

Well written.

Respect.
 
Kuna kitu najiuliza ni kwa nini mwanadamu amekuwa na maarifa kupita kiasi?? Yani mwanadamu anafanya juhudi aishi kama anavyotaka yeye, kwamba nafanya dhambi mfano hiyo uzinzi mimba ikipatikana na mimi siitaki hata kwa mti shamba itatolewa.

Ni nini kinasababisha tunakosa ustaarabu kuliko hata wanyama wa kufugwa na wa mwituni? Ni kwa sababu sisi tumepewa ujuzi, akili, maarifa na utashi sasa tunavitumia vibaya?

Manake mambo ya kubakwa,kupewa mimba ktk umri mdogo yanafanywa na mwanadamu mwenye akili, ambaye anatumia nguvu na ushawishi kwa huyo asiyeweza kuamua then anamuangusha.

Nikirudi kwenye Mada, Mimba iliyotungwa katika mazingira ya afya mbaya, inaweza ikatolewa kwa usalama wa maisha ya mama.

Lakini hizi zinazotokana na starehe zetu wenyewe nashauri isiruhusiwe hata kidogo, acha anayetoa awajibike kwa hiyo damu aliyomwaga peke yake. Manake hapo unaua na unamwaga damu ya mtu ambayo itakulilia maisha yako yote.

Sidhani kama kuna mtu ambaye amewahi kutoa mimba halafu akawa na AMANI moyoni. Siku zote utakuwa unajuta ukizaa mtoto unajua kabisa huyu ni mtoto wa tano ingawa dunia inaona ni mtoto wa 1!!
 
ukipata mimba nje ya ndoa, tubu umlee. Akikushinda tugawoe tukusaidie kulea! Hata kama kuna hatari ya kiafya haitakiwi kuua! Kuua ni kuua tu!:A S 20:
 
Back
Top Bottom