Mjasiriamali1
JF-Expert Member
- Jun 8, 2009
- 891
- 240
- Thread starter
- #61
Yaani vijana wa Tanzania bwana utasema wamerogwa.....kila jitu mawazo yake ni kuajiriwa.......
Jitu linakuuliza eti nikisoma kozi hii nitaajiriwa kweli.........
Yaani kuna mijitu ipo radhi hata kuuza nyumba ili isome na baadaye ije kuajiriwa na kuna mijitu ipo tayari hata kukaa miaka ishirini inasubiria ajira tu......yaani yenyewe inawaza kuajiriwa tu.......katika vichwa vyao.......
Alafu eti ikikaa pamoja inajiita misomi na kazi kutwa nzima ni kusoma magazeti ya kiingereza na kuangalia BBC.......Msomi gani unashindwa hata kubuni kamradi ka kukuingizia kipato mpaka unangoja uajiriwe.......
Halifikirii kuwa kwenye hayo mashirika binafsi anayoyangoja yampe ajira yalianzishwa na watu......
Pamba.vuu zao kabisaaaaa.....
Kutokana na upeo wako ni haki yako kuropoka na kutukana, naomba nikueleweshe kitu, mtoto wa familia ya kitanzania kasomeshwa na kwa taabu amemaliza degree yake, wale waliokuwa wakimsupport baada ya kumaliza degree yake, hawamsupport tena anaingia soko la ajira anatafuta kazi kwa mda mrefu hata mwaka mmoja, anakuja na miradi ya kujiajiri , anaangalia fursa zilizopo mtaani kwake mpango biashara unakaa vizuri kabisa, anakuja na idea ya kuzoa takataka, anakuja na idea ya kilimo, ni sawa tatizo atapata wap mtaji, kama hana mtu wa kumshika mkono, anenda seminar, anajifunza kwenye kwa matendo ishu inabakia atapata wap mtaji, anakuja na idea ya kupull capital anakusanya watu. Wanaanza ila sababu mtaji wao ni mdogo changamoto zinapokuja zinakula mtaji au kutingisha mtaji maana bado si mzoefu, wale waliomsomesha hawamuelewi wanampa pressure kuwa kasoma alafu anafanya kazi ambazo za wasiosoma, mwisho wa siku anatakiwa apate kazi ahudumie familia yake, ni mda wa kurudisha fadhila kwa waliokusomesha, ni mda na yeye asomeshe ndugu zake kama yeye alivyosaidiwa, kwa sababu ya mtaji mdogo hawezi kuajiri watu mambo yote anafanya yeye, mwisho wa siku unajiuliza uyu kasoma ili iweje tofauti ya kazi anazofanya na wasio soma hakuna, na bado hata izo ela hazimtoshi kuiishi, kwa iyo watu wanaonyooshea watu vidole eti hawajiajiri, eti hawatumii akili zao je umewashika mkono? Umewatafutia wafadhili wa kuwasaidia mipango biashara yao? Mfumo uliopo si rafiki kwa vijana wasomi kujiajiri, kumejaa rushwa, kumejaa urasimu, kila mahali serikali inangilia kati, kila mtu anataka pesa toka kwako wanaosurvive ni wale wenye mtaji mkubwa. Lakini huku chini unapoteza mda tuu, watu ajira