Mbona mlishafanya huo mpango angalia hapa kwenye link (Kigamboni New City) au mnataka kupiga hela nyingine za ili mtutengenezee video nyingine?
Mkuu Anna Tibaijuka nasapoti hoja yako ila kwa mawazo tofauti!
Suala la masterplan ni suala la serikali inajenga ama property developer? Ukiangalia picha hapo chini ni mji wa mwanza, watu wanakimbilia milimani na matokeo yake miundombinu inakuwa shida kuwafikia na kuongeza makazi holela.
Ninachoomba suala la upimaji wa ardhi ipewe sekta binafsi na serikali ibaki kuwa wasimamizi wa zoning. Sababu kubwa ni urasimu uliopo serikalini..viwanja vikipimwa mwaka huu mnaweza kukaa hadi miaka 3 hamjui nini hatma yenu nami ni mmoja wa wahusika coz toka mwaka 2010 kuna viwanja vilipimwa mpaka leo jiji wapo kimya.
Mimi nashauri hiyo kazi wapewe property developers
Mbona mlishafanya huo mpango angalia hapa kwenye link (Kigamboni New City) au mnataka kupiga hela nyingine za ili mtutengenezee video nyingine?
Mimi nashauri Mjenge makao makuu ya Tanzania inakuwaje nchi haina mji mkuu Mnazidi kujibana Dar??Jengeni Dodoma fumueni miundo mbinu ya CDA anzisheni miundombinu mipya!!Kigamboni nisawa kwa swala la ustawi wa nchi lakini kwa heshima ya nchi Makao makuu yanahitaji kujengwa pia!!
Hata sielewi kilichowavutia ktk master plan ya Singapore kwasababu kwenye dunia ya kwanza hicho ni kitu cha kawaida yaani safari zote mnazochoma pesa za walala hoi kwa kutembea kundi kubwa mmejifunza master plan! Hivi hatuna architecture engineer tanzania? Nafikiri tatizo ni serikali isiyokuwa na mipango, ufisadi na uvivu wa kujituma, nchi inazalisha wasomi kibao kwenye kilimo Lakini watu wanakufa njaa hili nalo tunataka watu waje kutufundisha kulima! Ni kitu gani tunachoweza Kama watanzania? Gossip na ngonjera, tanzania itajengwa na sisi watanzania, Hakuna nchi duniani iliyojengwa na wageni.
WanaJF
Nilikuwa mmojawapo wa viongozi tulioandamana na Mhe Rais katika ziara yake ya majuzi nchini Singapore. Ninawaletea sehemu ya Master Plan ya mji wao mpya unaojengwa kutokana na kuokoa ardhi baharini (reclamation). Unaona kila kipande cha ardhi mpya kimeshapangiwa matumizi yake na kuwekewa malengo ya majengo yanayotakiwa.
Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu.
Anayedai vinginevyo si msema kweli. WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.
Mama Tibaijuka
Labda swali la Msingi, tunahitaji kufanya Land reclamation Tanzania?
Kwa nini wameenda kujifunza reclamation kama hatuihitaji?
Lakini mh. Kwanini mumeshindwa kuboresha huu mji tulionao sasa hivi na munaanza kutafuta mpya wakati bado hamjachelewa? Tunahitaji tuone mabadiliko hapa tulipo sasa, Hizi sheria ndogondogo za miji zinafanya kazi?
Mtu kuweka maeneo ya mjini vibanda, parking ziko ndani ya barabara ukipita maeneo yote ya mjini sehemu za kupita watu na magari zimepakiwa gari na barabara inakua finyu. Majumba mjini yamekua kama magovu je hakuna sheria ya kuwaagiza wamiliki kuyarekebisha kila kipindi inapofika?