Massage Parlour...

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,801
Reaction score
43,177
SAA MOJA NDANI YA CHUMBA CHA KUSINGA


Habari za usiku mnene mabibi na mabwana, leo nina tukio limetokea le oleo hivi bado ni la moto wala halijapoa.

Niko sehemu flani hivi mahsusi kwa ajili ya mishe flani hivi, baada ya kupiga kazi kutwa nzima nikapata mlo wa mchana kwa kuchelewa kidogo kutokana na umuhimu wa kazi iliyokuwa inasubiriwa na viongozi tayari kwa kujadiliwa kesho kwenye kikao asubuhi na mapema.

Sasa baada ya kula nikawa nasikia uchovu maana leo nilidamka tangu saa 11 alfajiri ndo nikaanza kuifanya hiyo kazi na jana nilichelewa kulala. Nikajikokota moja kwa moja hadi mahala pangu nilikopangiwa kulala, nikaoga maji ya uvuguvugu kasha nikaweka mvinyo nusu glasi, kabla hata sijapiga fundo moja nikajisikia hovyo. Nikawapigia watu wa mapokezi kuwa nahitaji mhudumu mmoja aje nione ananisaidiaje. Alipofika nikamueleza nnavojisikia akanishauri niende kusingwa kwa saa moja kisha niingie kwenye chumba cha mvuke wa moto (steam room) sijui ndo wanaita sauna and spa…. Halafu ndo ninywe wine ntajisikia vizuri huo ni uchovu tuu wa mwili.

Mhudumu Yule akaniambia huduma yote hiyo itagharimu dola 50, nikasema sawa pesa makaratasi na inatafutwa uzima kwanza. Akaniacha mule chumbani nikaingia tena bafuni kujimwagia maji ya moto tayari kuelekea chumba cha kusingwa (massage room)

Nikafika eneo la tukio (chumba cha kusingwa) kulikuwa na mapokezi yake, mhudumu wa pale akanitaka nijaze fomu kabla na kunielezea aina ya kusingwa ntakayofanyiwa. Akanishauri nisingwe aina ya kuondoa uchovu wenyewe wanaita (whole body relaxtation massage). Nikajaza fomu na kupewa maelekezo nikawa tayari kuelekea chumba cha kusingwa. Kabla sijaenda huyo mdada wa mapokezi akaniuliza, ungependa kusingwa na mwanaume au mwanamke?? Kwakuwa nilikuwa nimechoka nikamjibu kwa haraka mwanaume huku nikielekea chumba cha kusingwa. Yule dada wa mapokezi akanipeleka hadi kwenye chumba na kuniambia ataniacha kwenye chumba hicho kwa dakika 10 nibadili nguo zangu kisha akanielekeza mahali pa kuziweka. Akaniambia nina uamuzi wa kuvua cupi au kuiacha nikiwa nimeivaa wakati wa kusingwa. Kisha kuna kitanda kirefu chembamba akielekeza nikimaliza kuvua nguo nijifunge taulo kubwa tuu kutoka kifuani hadi miguuni chini, nikishajifunga taulo nilale kifudifudi au nilalie tumbo kisha mkaka atayenisinga ataingia na kuanza kazi yake.

Ndani ya Chumba cha Kusinga!!!

Yule mdada mhudumu aliniacha pale chumbani, mwanga wa chumba akaucha ukiwa hafifu alizima taa kali na kubakisha taa hafifu. Kulikuwa na mziki maliniiii au mziki wa taratibu wa ala. Yaani ni vyombo vya mziki tuu ndo vilikuwa vikiimba huku chumba kikiwa na joto la wastani kwa makadirio nyuzi 24.

Basi nikachojoa nguo zangu zote nikaziweka nilipoelekezwa na uchukua taulo nikajifunga na kujilaza hapo kitandani huku nikiwa nimelalia tumbo. Usawa wa kichwani kitanda kina tundu ambapo uso unakuwa unaangalia chini sakafuni ikiwa utafumbua macho au utaacha macho wazi. (mfano wa picha hapo chini)



Basi mpenda starehe mie nikajilegeza mwili wote tayari kuubwaga uchovu kwa kusingwa, nikafumba macho huku nikisikilizia ala za mziki na utulivu wa kile chumba.

Kuja kuhamaki nasikia taulo linavutwa lile nililolilalia na kuwekwa kwa mtindo kama vile nimejifunika shuka bila kuchomekewa. Akanisalimia mkaka mweeh sauti nzito sikutaka hata kugeuka kumuangalia, nikaitikia salamu kisha akaniuliza napendelea mafuta yenye harufu ipi, nikachagua Rosiena kisha huduma ikaanza. Alichukua mikono yangu akaining’iniza chini kwa utaratibu kama vile isije ikanyofoka, kisha akafunua lile taulo hadi usawa wa matako yaani kiuno chote kikawa wazi. (mfano wa picha hapo chini)




Akaniambia ukiona tofauti au hujisikii sawa uniambie nipunguze mkandamizo au pia waweza sema niongeze, nikamuitikia sawa.


Akaanza kunisinga mgongo kisha shingo kisha kiuno na tumbo la pembeni pande zote mbili kisha akashuka kwenye matako usawa wa kiuno mikono inaingia ndani ya taulo kidogoo kama anataka kuyatomasa matako… hapo ndo nikagundua kumbe naweza kufika orgasm / mshindo kwa kusingwa tuu.



Niianza kusikia damu inachemka, kusisimka hasa alipokuwa akishika maeneo kwa maeneo, kumbuka taulo limekunjwa hadi usawa wa matako ila yamefunikwa, mie nikawa nasikilizia jinsi uchovu unavotoka mwilini.




Akamaliza akanifunika na taulo hadi shingoni kisha akaniachama miguu ili kuwe na uwazi katikati bado nikiwa nimelalia tumbo, akafunua taulo upande wa mguu wa kushoto na kuliweka katikati ya miguu. Mguu wote ukawa wazi kuanzia kwenye paja hadi chini, tako tuu ndo lilikuwa limefunikwa. Akachukua mafuta na kuanza kunisinga oohh la laah… hapo ndo nikakumbuka nimekosea kuchagua msingaji wa kiume daah. Niseme ukweli tuu alinipandisha nyege maana alikuwa ananisinga kuanzia miguu chini anapanda kwenye mapaja kisha anaingiza mikono yake hadi chini ya matako na kurudi hadi miguuni chini. Daaah nikamwambia naomba breki kidogo akasema akisimama sitamaliza mwili wote na muda wangu ukiisha ntatakiwa kutoka ama laah nilipie tena.



Nikatamani kusema nibadilishiwe msingaji aje wa kike, ila nikasema haya endelea hela yangu iende kihalali ila punguza makali kidogo maana chumbani niko mwenyewe. Basi nikamwambia apunguze mkandamizo ili usiniletee mhemko bali uchovu ndo utoke. Akamaliza na mguu wa kulia kisha akafunua taulo kujiziba uso na kuniamia nigeuke kulala kichali chali au nilalie mgongo ili anisinge na upande wa juu.

Nikafanya hivyo na hapa alinisinga usoni, kuanzia mapajani na kushuka chini hadi kwenye unyayo na mikono yote miwili.



Wakati ananisinga kwa upande wa juu mapajani alichukua kitaulo kidogo akakilowesha maji ya moto na kuniwekea shingoni kwa chini nikalalia kile kitaulo uuuh kikanipa tulizo zuri hadi nikawa nasikia damu inavochemka ndani. Kifuani na tumboni hakupasinga na hapo akawa amemaliza.



Saa ilipoisha akaniambia ananiacha kwa dakika 10 nijifunge taulo kisha anipeleke chumba cha mvuke wa moto. Basi nikaamka pale kitandani mwepesii nikajifunga taulo kubwa na kuvaa housecoat kuelekea chumba cha mvuke.

Huko aliniwekea nyuzi joto 42 nikakaa kwa dakika 10 kisha nikatoka kupoa kidogo. Nikiwa kwenye chumba cha mvuke, nilitoka majacho na kujisikia kama naondolewa dhambi zangu maana nilijiona uchovu wote kwisha. Basi nikaingia kuoga bafuni kisa nikavaa na kutoka mapokezi ya hiyo health club. Nika saini bili na kuelekea chumbani kwangu.

Nikafika bafuni nikaoga tena maji ya moto kwa kujisugua vizuri maana kule kwenye bafu la sauna baada ya kutoka kwenye mvuke wa moto nilioga maji ya baridi. Baada ya saa moja baadae nikala matunda na mtindi, wacha nikayaruke majoka maana uchovu wote kwisha.

Poleni kwa maelezo marefuuuu mie nashindwaga kufupisha mnisamehe bure, ila msiwaze kuwa huyu kaka wa kunisinga alifanya uhalifu kwenye mwili wa Kasie, hapana. Wafanyakazi wa hapa wamefunzwa kutii maadili ya kazi hivo pamoja na mie kupandisha mihemko wala hakuonesha dalili yoyote ya kushawishika kunanihii…..

Usiku mwema nyote, atakayeweza kusoma habaro yote awasoimulie watakaoona uvivu kusoma habaro yote, maana najua wako watakaosema habari ni ndefu na hawawezi kusoma yote….
Kasie.






Hii massage parlour nimeipenda itabidi niitafute… mwalimu yuko makini na kazi yake, hashawishiki hata kidgo…
 
Mkuu Kasie kwani mengine utasema bs!
im jokin, ucku mwema kwako pias
 
Kasie, i like the flow of your post.

Anyways, learning how to give a massage is a nice skill to have, its pretty easy to learn the basics too. With just a little effort and people will thank you for it. Helps score some brownie points with the ladies, too.

Had a friend whose one of his go to move was that, as he would get the ladies back to his place, he would just offer them a massage/should or foot rub . Talking about how a day can be stressful and it would help them relax and ease the stress. And that would be the start of a slippery slope to pound town. 9/10 it works, even though its a silly move.
 
Dahhhhh.....hivi Mzee Asprin kijana hakuhitimu ile course ya kusinga??? Anamsinga mkenya tuu while kwa Kasie anaachia wengine.

Inabidi kamati ya dharura ikutane kuweka mambo sawa.


Cc Daby
 
Hahaaaaaaaaaahaaa alafu wengine wanalalamika hela hakuna

Hhehehehheeheehee kiukweli hela zipoo sema tuu namna ya kuzitumia na mahitaji ndo husababisha hela zionekane zimepotea.
 
Aisee Kasie usiku huu kuamshana tena maruhani yalikuwa yamelala..daah ila jamaa alifaidi..natamani ingekuwa mimi

Hhahahahahaaaa jamani, npole kwa kuamsha maruhani, hehehehee yaani huwezi hata kuamini yaani wafanyakazi wa hiyo sehemu ya kusinga, wako waaminifu na makini kwenye kazi tuu. Hakuna kilichotokea kabisa labda kama baada ya kunisinga aliingia chooni kulia kwa maumivu hehehee
Pia simtetei sana ila watakuwa washazoea kushika mamshededemengi mengi hivo kuona kawaida tuu.
 
Duuuh . . , Kasie upo vizuriii. . !

Asante nashukuru, ni kuamua tuu kujipa raha maisha yenyewe haya mafupi. Nafanya kzi kwa faida yangu mwenyewe, sina hakika kama ntafika umri wa kustaafu (God knows) na kufaidi kiinua mgongo changu baada ya kustaafu. Hivyo kila nipatapo nafasi najipa raha kama mstaafu.

Wenye lugha yao wanasema its a matter of priority...
 
Hii habari ya kusingwa achana kabisaaaa....niliwahi kubambwa sehemu nikaingia Massage Parlour
Nilikuja kustuka akili zinarudi nipo kwenye gari,naangalia mfukoni sina hata shilingi mia mfukoni
Kumbe wakati ule nasingwa nilikuwa naombwa hela naelekeza tu mtu akatoe kwenye suruali...Achana kabisa na mambo ya "Happy Ending"
 
Mkuu Kasie kwani mengine utasema bs!
im jokin, ucku mwema kwako pias

Wafikiri nimeficha hata kitu kimoja..... waalaaah nimesema yotee kama yalivotokea. Mbona huwa ikitokea nikachubwika huwa nasema.... japo sio vizuri kusema siwadolishii au kuwatia hamu laah, najikuta tuu nasimulia matukio ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…