Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,678
- 22,265
Serikali imekuwa ikituaminisha kuwa bima ya afya ni mkombozi kwenye maisha yetu lakini serikali hiyohiyo haikubali kuwapa bima waliopata maradhi yasiyo ya kuambukiza!
Nimekusikia ukisema neno linalotolewa na Watanzania wengi kuwa bima ya afya haitolewi kwa baadhi ya maradhi! Hii inamaanisha kuwa bima ya afya iko kibiashara zaidi kwa wasiopata maradhi ili bima ifaidike! Watanzania ni wakati sasa kutaka mabadiliko ili wazee na wenye maradhi waweze kununua bima badala ya kubaguliwa kwa kosa lisilo lao.
Narudia tena pole kwa mzigo wa gharama za matibabu inayoipata familia yako, Mungu awe nanyi
===
Nimekusikia ukisema neno linalotolewa na Watanzania wengi kuwa bima ya afya haitolewi kwa baadhi ya maradhi! Hii inamaanisha kuwa bima ya afya iko kibiashara zaidi kwa wasiopata maradhi ili bima ifaidike! Watanzania ni wakati sasa kutaka mabadiliko ili wazee na wenye maradhi waweze kununua bima badala ya kubaguliwa kwa kosa lisilo lao.
Narudia tena pole kwa mzigo wa gharama za matibabu inayoipata familia yako, Mungu awe nanyi
===
Pole sana Masoud!
Kidunia ni kawaida sana kwa mashirika ya Bima ya Afya kuzuia matibabu ya magonjwa fulani. Mashirika mengi ya BIMA huzuia baadhi ya magonjwa kuyatibu, mfano magonjwa ya kuzaliwa nayo (Congenital), matibabu ya VVU/UKIMWI, upasuaji wa kutengeneza urembo, kutibu utasa, kutibu magonjwa ya kinywa yasiyosababishwa na ajali, majeraha yako uliyoyasababisha mwenyewe, magonjwa yatokanayo na madhara ya kutumia madawa ya kulevya, kulazwa kwa magonjwa yatokanayo na vita au mionzi n.k.
Watu wengi hususani watanzania hawana elimu ya kutosha kuhusu Bima ya Afya. Hawajui mifuko inavyofanya kazi. Wengi wanadhani hii mifuko ni sawa na Vicoba au SACCOSS. Hawajui kwamba hii mifuko ya Bima ya Afya, inapaswa kuwa endelevu. Mifuko hii inajiendesha. Inalipa mishahara. Hawajui kwamba hakuna pesa ya mjomba inapelekwa Bima ya Afya ili iweze kutoa matibabu kwa wanachama wake. Hawajui kwamba matibabu yote yanatolewa kupitia michango ya wanachama. Hawafahamu kwamba mara nyingi matibabu ya mwanachama au tegemezi hata ya siku moja, yanazidi michango ya mwaka mzima ya mwanachama mkuu (Principal). Nasikia serikali iliwahi kopa pesa huku, hili ni kosa kubwa.
Pindi mfuko wetu mkubwa wa NHIF ukifa, mfumo mzima wa afya wa taifa utaporomoka. Kaziulize hospitali hapa Tanzania jinsi zinavyonufaika kwa kuwepo kwa mfuko wa Bima wa Afya, hata misamaha ya baadhi ya matibabu inategemea mapato yatokayo kwa wagonjwa wa Bima za Afya.
Mimi ni mongoni mwa wanachama wa kawaida wa NHIF, ambaye ninafurahia mfuko ukizidi kukua. Ninakatwa mshahara kila mwezi. Ninafurahia kutokutumia kadi yangu, ninatunza afya yangu, lakini pindi nikiumwa nina kadi nitaitumia.
Ukiacha la Masoud kuna vitu vingine kila mtu anaweza vifikiria na vikampa changamoto ya maamuzi. Hebu fikiria wewe unamiliki kampuni ya bima, halafu mtu analeta gari ambalo limeharibika kabisa anataka umpe insurance kuna vitu gani utaviangalia ili kumpa bima? Kuna mtu mwingine ana duka mtaani amekuja kukata Bima. Baada ya kumtembelea dukani umegundua huyu jana dukani kwake anavamiwa kila wiki, hivi ni vitu gani utaangalia ili kumpa au kutompa bima?
Ningekuwa kiongozi wa Bima ya Afya, labda ningeshauri mtoto wa Masoud apate Bima ila nikazuia baadhi ya benefits.
Kwa kuongeza elimu ya Bima ya Afya, tujue Bima sio vikoba na hivyo usitegemee kesho upate faida ya michango yako bila kuumwa, kwani hiyo sio maana ya Bima zote. Kwa kutokujua hili watu wengi kwa ujinga wao wanalazimisha kupata mafao ya Bima kwa kuchoma mali walizozikatia bima au kulazimisha kwenda hospitali.
Bima ya Afya na Bima nyingine usizifananishe na mifuko ya pensheni. Bima inaweza fanana na mtu mwenye duka, anayeamua kumgharamia mlinzi ili alinde biashara yake. Furaha ya mwenye duka si kuona akiibiwa, bali kuona mali yake ni salama. Lakini mwizi akija, atakutana na mlinzi. Hakuna siku mwenye duka atamwambia mlinzi ampe faida ya mshahara aliomlipa siku zote kwa sababu ya duka lake kutovamiwa na majambazi.