Maslahi duni kwa watumishi wa umma: Taasisi za kifedha na watu binafsi wanaotoa mikopo wanafaidika na hali hii

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Hivi ndivyo unavyoweza kusema na hali hii utaiona mara tu mishahara ikitoka ambapo baadhi ya watumishi humiminika katika taasisi hizi za kifedha(sio mabenki) kupeleka marejesho au kufuata mishahara yao kwani baadhi ya wanaowakopesha hukaa na kadi zao za ATM kama moja ya mashariti ya kupewa mikopo ingawa siku hizi kuna huduma za mobile banking zinazomuwezesha mtu kutoa hela kutoka kwenye akaunti yake bila kwenda benki wala kutumia kadi yake ya ATM.

Ukiacha hizi financial institutions ambazo nazo hutoza riba kubwa,kuna watu binafsi nao ambao hufaidika na matatizo ya watumishi kwa kuwapa mikopo yenye riba kubwa inayofikia hadi asilimia 20 mpaka 30 ya mkopo mtumishi anaokopeshwa.

Mfano, kila shilingi 100,000/=,wanatoza riba ya asilimia 20 hivyo wanaokopa shilingi 100,000/= kwa mwezi,mwisho wa mwezi wanarudisha shilingi 120,000/=, na wanaokopa shilingi 500,000/=, mwisho wa mwezi wanarudisha shilingi 600,000/=.Kwa wale wenye wateja wengi,hakika hii ni biashara nzuri sana ingawa ina changamoto zake tena isiyo na kodi wala leseni ya biashara.

Hii mikopo imepewa jina la mikopo ya dharura ingawa kiuhalisia sio ya dharura bali ni ya kujaribu kupambana na hali ngumu ya maisha inayochangiwa na masilahi duni ya watumishi inayowakabili watumishi na hata wasio watumishi maana baadhi ina makato ya kufikia mpaka miezi 6 na zaidi.

Kumbuka mikopo hii ni mbali na ile ya mabenki ambayo mtumishi hukatwa moja kwa moja kwenye mshahara wake hivyo jiulize mtumishi huyu anabaki na kiasi gani na hapa ndio huwa nakumbuka ule msemo: "mtanzania anaishi kwa mbinu."

Ukweli ni kwamba hata ilie sheria/utaratibu wa kutaka kila mtumishi abaki na angalau moja ya tatu ya mshahara wake baada ya makato yote,sheria/utaratibu huu umebaki nadharia tu kwa baadhi ya watumishi na binafsi sioni hata umuhimu wa hii sheria kuendelea kuwepo bali ni bora tu ikafutwa na mtumishi abaki huru katika kuamua matumizi ya mshahara wake.

Kwa hakika watumishi wa umma,kama ilivyo kwa raia wengine,wanahitaji mkombozi/meteztei vinginevyo huko mbeleni hali inaweza kuja kuwa mbaya sana kwa baadhi ya watumishi.

Ama hakika karibu kila kitu ni fursa yakiwemo na matatizo ya watu wengine.
 
Platinum, Baypot, na kadhalika. Haya yameeendelea kukopesha watumishi kwa riba za ajabu ajabu, lakini kitu kizuri ni kwamba wanafanya machoni mwa serikali inayowajali wanyonge na masikini wa nchi hii. Inasikitisha mtumishi anakopa 2000,000/= anadaiwa mpaka karibu na kustaafu, maana viwango vinaongezwa, halafu hapewi hata nakala ya mkataba wake. Wabunge wote, wanajua, serikali inajua, police wanajua, ila hii ni nchi ya BONGO. Pamoja na kimshahara kisichotosha, watumishi hawa wanaishi maisha ya dhiki kubwa, na nilwahi kuambiwa kuwa ni miradi ya wakubwa serikalini, ndiyo maana imefumbiwa macho. Aibu iliyoje!!
 
Platinum, Baypot, na kadhalika. Haya yameeendelea kukopesha watumishi kwa riba za ajabu ajabu, lakini kitu kizuri ni kwamba wanafanya machoni mwa serikali inayowajali wanyonge na masikini wa nchi hii. Inasikitisha mtumishi anakopa 2000,000/= anadaiwa mpaka karibu na kustaafu, maana viwango vinaongezwa, halafu hapewi hata nakala ya mkataba wake. Wabunge wote, wanajua, serikali inajua, police wanajua, ila hii ni nchi ya BONGO. Pamoja na kimshahara kisichotosha, watumishi hawa wanaishi maisha ya dhiki kubwa, na nilwahi kuambiwa kuwa ni miradi ya wakubwa serikalini, ndiyo maana imefumbiwa macho. Aibu iliyoje!!!
Mkuu siyo kweli kama mkopo unachukuliwa na watumishi wa Umma kwa sababu ya maslahi duni. Siyo kweli! Kawaida ya mshahara huwa hautoshi siku zote kama hautatambua wewe mwenyewe namna ya kuutumia. Ni lazima ugawe mshahara mara 30 ndipo upange namna yako bora ya kuutumia.

Hata ukisema leo mtumishi wa chini umpe mshahara wa Million tatu bado atakopa tuu! Mshahara unajiadjust automatically na matumizi ya mwenye nao. Kama mtoto alisoma Vingunguti Primary School ukiwa unapokea laki 3 basi ukipata M1 utamhamisha mara moja maana utagundua ile shule haina walimu wazuri na hata location yake haikuvutii! Atasoma st. Brian!

TV utataka smart ya 55 inch tena HDD! Unataka kumuona Messy akiwa mkubwa na mwenye mng'aro thabiti. Na rushwa utapokea kubwa zaidi kulingana na mshahara wako, kama una tabia hizo. Asante mkuu.
 
Kuna mstaafu mmoja alikopeshwa 3milion wakati anasubiri pension alikuta 18mil.

Nadhani kuna haja ya kuliangalia hili kwa pande zote
Kwanza serikali kuna haja ya kuanzishwa kwa subsistence allawance kwa watumishi wote si kwa askari pekee kama ilivyo sasa.
Ile itasaidia siku 30 mpaka 35 kusubiri mshahara na kwa modality ya sasa ya kazi tu Watu wanaangukia kwenye hayo maligonga yaaan choggo-, platinum-, na chomchom credit e.t.c

Pili, watumishi nao wajifunze kupunguza mbwembwe vimshahara vyenyewe hivi njiwa. Sasa MTU unakuta anasomesha mtoto English medium ada yake ni mishahara yake mitatu au minne kwa mwaka, kodi ya pango ni mishahara yake minne ya mwaka. Sasa wakati semina warsha na makongamano yametiwa makufuli ya Mkuu unategemea nini?

Watu wa uchumi wameainisha uchumi wao katika simple model wanasema; uchumi ni rahisi sana unachotakiwa kujua ni nini unachokipata mkono wa kulia na nini unachotumia kwa mkono wako wa kushoto mwishowe unapata balance payment ya familia yako.
Asante
 
Mkuu siyo kweli kama mkopo unachukuliwa na watumishi wa Umma kwa sababu ya maslahi duni. Siyo kweli! Kawaida ya mshahara huwa hautoshi siku zote kama hautatambua wewe mwenyewe namna ya kuutumia. Ni lazima ugawe mshahara mara 30 ndipo upange namna yako bora ya kuutumia.

Hata ukisema leo mtumishi wa chini umpe mshahara wa Million tatu bado atakopa tuu! Mshahara unajiadjust automatically na matumizi ya mwenye nao. Kama mtoto alisoma Vingunguti Primary School ukiwa unapokea laki 3 basi ukipata M1 utamhamisha mara moja maana utagundua ile shule haina walimu wazuri na hata location yake haikuvutii! Atasoma st. Brian!

TV utataka smart ya 55 inch tena HDD! Unataka kumuona Messy akiwa mkubwa na mwenye mng'aro thabiti. Na rushwa utapokea kubwa zaidi kulingana na mshahara wako, kama una tabia hizo. Asante mkuu.
Kwa maana hiyo, wakurugenzi, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu, nao ni wadau wa hayo mashirika na watu binafsi? Acha alinacha zako. Siku zote loan sharks wana target watu wenye matatizo, haijalishi ni matatizo gani.

Hivi wewe, baba mwenye familia ya watoto watano, na mke, unaweza kuishi kwa mshahara wa 450,000/= kwa mwezi? Kama.mshahara unajiadjust wenyewe, kwa nini basi serikali isitoe al least take home iwe 1,500,000/= tuone kama hao wakopeshaji watakuwa na wateja waliona nao?
 
Najua kuna watu wanakopa kwasababu ya matatizo ya dharula sawa, lakini kama unakopa ili kununua mahitaji ya kawaida kwasababu mshahara umeisha nikwambie ndugu mtumishi MKOPO HAUONGEZI KIPATO bali unapunguza! yaani kwa kifupi unaweza kuishi bila mkopo kabisa, unachotakiwa kufanya ni kujikaza mwezi mmoja uvunje huo mnyororo wa kukopakopa, jibane usikope kabisa, mwezi unaofuata utakua na mshahara wako wote!

pia tuishi maisha yanayoendana na vipato vyetu (najua ni maisha ya hovyo) lakini ni bora kuliko kuwapa watu hela kizembezembe kwakua umekopa kutoka kwao. Mwisho kabisa akiba ni muhimu sana hata kama ni 10% ya kipato chako itakufaa sana siku ukipata majanga.
 
Najua kuna watu wanakopa kwasababu ya matatizo ya dharula sawa, lakini kama unakopa ili kununua mahitaji ya kawaida kwasababu mshahara umeisha nikwambie ndugu mtumishi MKOPO HAUONGEZI KIPATO bali unapunguza! yaani kwa kifupi unaweza kuishi bila mkopo kabisa, unachotakiwa kufanya ni kujikaza mwezi mmoja uvunje huo mnyororo wa kukopakopa, jibane usikope kabisa, mwezi unaofuata utakua na mshahara wako wote!
pia tuishi maisha yanayoendana na vipato vyetu (najua ni maisha ya hovyo) lakini ni bora kuliko kuwapa watu hela kizembezembe kwakua umekopa kutoka kwao. Mwisho kabisa akiba ni muhimu sana hata kama ni 10% ya kipato chako itakufaa sana siku ukipata majanga.
Ni kweli mkuu ila take home za watumishi wa serikali ni ndogo mno kiasi kwamba wanalazimika kukopa bila kupenda.

Kwa mfano,mtumishi hata mwenye take home ya 500,000(ingawa wengi wako chini ya hii figure) ni vigumu kuweza kusomesha,kujenga,kuanzisha miradi,n.k bila kukopa tena usisahau familia zetu nyingi ni tegemezi.
 
Ni kweli mkuu ila take home za watumishi wa serikali ni ndogo mno kiasi kwamba wanalazimika kukopa bila kupenda.

Kwa mfano,mtumishi hata mwenye take home ya 500,000(ingawa wengi wako chini ya hii figure) ni vigumu kuweza kusomesha,kujenga,kuanzisha miradi,n.k bila kukopa tena usisahau familia zetu nyingi ni tegemezi.
Ni kweli kabisa mkuu, na ukishakua na kazi basi ukoo mzima wanakuangalia, siku mshahara umeingia tu basi na matatizo yanafunguliwa milango. JPM hajawatendea haki watumishi, yaani imefika kipindi zile annual increment (kwenye salary scale) zinangojea tamko la rais! hii ni 'micromanagement' kutoka kwa rais wetu, aziangalie vizuri priorities zake.
 
Kwa maana hiyo, wakurugenzi, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu, nao ni wadau wa hayo mashirika na watu binafsi? Acha alinacha zako. Siku zote loan sharks wana target watu wenye matatizo, haijalishi ni matatizo gani.

Hivi wewe, baba mwenye familia ya watoto watano, na mke, unaweza kuishi kwa mshahara wa 450,000/= kwa mwezi? Kama.mshahara unajiadjust wenyewe, kwa nini basi serikali isitoe al least take home iwe 1,500,000/= tuone kama hao wakopeshaji watakuwa na wateja waliona nao?
Hata wabunge wanaopata malaki ya oesa kwa siku wanamadeni lukuki. Acha kudanganya watu mkuu.
 
Ni kweli mkuu ila take home za watumishi wa serikali ni ndogo mno kiasi kwamba wanalazimika kukopa bila kupenda.

Kwa mfano,mtumishi hata mwenye take home ya 500,000(ingawa wengi wako chini ya hii figure) ni vigumu kuweza kusomesha,kujenga,kuanzisha miradi,n.k bila kukopa tena usisahau familia zetu nyingi ni tegemezi.
Ninavyofahamu mimi kusomesha kwetu siku hizi ni kununua uniform tu basi! Na hii inakwenda mpaka kidato cha 4. Ukiamua luxury basi hapo kakope. Lakini si lazima.
 
Mkuu siyo kweli kama mkopo unachukuliwa na watumishi wa Umma kwa sababu ya maslahi duni. Siyo kweli! Kawaida ya mshahara huwa hautoshi siku zote kama hautatambua wewe mwenyewe namna ya kuutumia. Ni lazima ugawe mshahara mara 30 ndipo upange namna yako bora ya kuutumia.

Hata ukisema leo mtumishi wa chini umpe mshahara wa Million tatu bado atakopa tuu! Mshahara unajiadjust automatically na matumizi ya mwenye nao. Kama mtoto alisoma Vingunguti Primary School ukiwa unapokea laki 3 basi ukipata M1 utamhamisha mara moja maana utagundua ile shule haina walimu wazuri na hata location yake haikuvutii! Atasoma st. Brian!

TV utataka smart ya 55 inch tena HDD! Unataka kumuona Messy akiwa mkubwa na mwenye mng'aro thabiti. Na rushwa utapokea kubwa zaidi kulingana na mshahara wako, kama una tabia hizo. Asante mkuu.
Hivi wewe unafikiri kwa kutumia akili?
 
Ni kweli mkuu ila take home za watumishi wa serikali ni ndogo mno kiasi kwamba wanalazimika kukopa bila kupenda.

Kwa mfano,mtumishi hata mwenye take home ya 500,000(ingawa wengi wako chini ya hii figure) ni vigumu kuweza kusomesha,kujenga,kuanzisha miradi,n.k bila kukopa tena usisahau familia zetu nyingi ni tegemezi.
Mkuu kwa mfano mtumishi wa kima Cha chini utumishi wa mahakama analipwa 260k kabla ya makato, take home nadhani ni 200 to 210k halafu Hana posho yoyote hahahaha hii nchi acha tu....kipindi hicho Kuna mkurugenzi analipwa 12m kwa mwezi Kama mshahra, analipwa 3m Kama housing allowance, 1.2transport allowance, Bado anapewa gari ya serikali na budget ya mafuta...ana Safari nyingi zenye posho nono,...kila mwaka fenicha za nyumba yake zinabadilishwa, walai huyu atapigana kutetea tumbo lake na Wala sio masilahi ya anaowaongoza kwa utofauti huu wa maslahi
 
Mkuu kwa mfano mtumishi wa kima Cha chini utumishi wa mahakama analipwa 260k kabla ya makato, take home nadhani ni 200 to 210k halafu Hana posho yoyote hahahaha hii nchi acha tu....kipindi hicho Kuna mkurugenzi analipwa 12m kwa mwezi Kama mshahra, analipwa 3m Kama housing allowance, 1.2transport allowance, Bado anapewa gari ya serikali na budget ya mafuta...ana Safari nyingi zenye posho nono,...kila mwaka fenicha za nyumba yake zinabadilishwa, walai huyu atapigana kutetea tumbo lake na Wala sio masilahi ya anaowaongoza kwa utofauti huu wa maslahi
Wanajiongelea tu,isitoshe sisi kama watumishi tusharizika na maisha ya kukopakopa ili siku ziende na family ziende msalani.Hakuna aliyewatuma watupigie kelele.

Acheni kiherehere msifanye wenye hizo microfinance waache kutukopesha,kwani tukikwama hakuna mkuu wa mkoa Wala mkurugenzi atakayekuja tukopesha tulishe family zetu.

Mwenye nchi yake kashasema hatuna tija so haoni sababu ya kujali maslah yetu,mimi ni mnufaika wa hii mikopo,tuacheniii hatujawaomba mtupigie kelele,mshahara ni wangu na jinsi navyoutumia na kukopa hayawahusu

Punguzeni mada za kipuuzi huku mitandaoni,kwani hata tukiwaomba mtupige tafu hamtofanya hivyo.
 
Wanajiongelea tu,isitoshe sisi kama watumishi tusharizika na maisha ya kukopakopa ili siku ziende na family ziende msalani.Hakuna aliyewatuma watupigie kelele.Acheni kiherehere msifanye wenye hizo microfinance waache kutukopesha,kwani tukikwama hakuna mkuu wa mkoa Wala mkurugenzi atakayekuja tukopesha tulishe family zetu.Mwenye nchi yake kashasema hatuna tija so haoni sababu ya kujali maslah yetu,mimi ni mnufaika wa hii mikopo,tuacheniii hatujawaomba mtupigie kelele,mshahara ni wangu na jinsi navyoutumia na kukopa hayawahusu.Punguzeni mada za kipuuzi huku mitandaoni,kwani hata tukiwaomba mtupige tafu hamtofanya hivyo.
Kweli kabisa mdada
 
Hii mikopo imepewa jina la mikopo ya dharura ingawa kiuhalisia sio ya dharura bali ni ya kujaribu kupambana na hali ngumu ya maisha inayochangiwa na masilahi duni ya watumishi inayowakabili watumishi na hata wasio watumishi maana baadhi ina makato ya kufikia mpaka miezi 6 na zaidi.
Mikopo siyo kiashiria cha maslahi duni we taahira! Lema ana madeni mpaka matakoni, huwezi sema ana maslahi duni.
Hivi Chadema mna matatizo gani lakini, mbona mavichwa yenu magumu hivi aisee?
 
Usitegemee riba kuwa chini kama za Bank sababu hawa wanakopesha mpaka elfu hamsini, na gharama ya kufuatilia ulipwe elfu hamsini ni ileile ya kufuatilia ulipwe milioni kumi.
cost per unit ya 50k ni sawa na ya 20m.
 
Bora ukope upeleke mtoto shule kuliko kumpeleka ELIMU BURE hapo unatengeneza chain of poverty. Waliotengeneza sera ya Elimu Bure nenda shule za bure kama utakuta watoto wao. Walimu wenyewe ndio nao siku izi wamejifunza siasa documents nyingi lakini nenda darasani watoto zeeee!!!!!! Kupanga ni kuchagua!!!
 
Bora ukope upeleke mtoto shule kuliko kumpeleka ELIMU BURE hapo unatengeneza chain of poverty. Waliotengeneza sera ya Elimu Bure nenda shule za bure kama utakuta watoto wao. Walimu wenyewe ndio nao siku izi wamejifunza siasa documents nyingi lakini nenda darasani watoto zeeee!!!!!! Kupanga ni kuchagua!!!
Kweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom