maskini zeruzeru huyu;wazazi walitaka kumuua!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
wanandugu habarini za jioni/aubuhi/mchana
kwa masikitiko makubwa;muda si mrefu nimetoka mitaa ya chalinze kwenye shuguli za kikazi;kwa bahati nashugulika na watu wa vijijini;katika pita pita ya nyumba kwa nyumba;nikakuta nyumba wamejaa watu wengi sana,nikauliza jamani kulikoni,ndipo nilipoambiwa yafuatayo

""kwani wewe nani?nikajitambulisha.baada ya hapo nikamweleza shuguli zangu na wenzangu ndipo nikamwambia embu nieleze vizuri kunani hapa?

UNAJUA;KUNA MAMA MMOJA AMEACHIWA NA MAHAKAMA MUDA SI MREFU
HUYU MAMA ANA MTOTO ZERUZERU (ALBINO),ANAITWA JOYCE TENA KALE UNAKAONA,KUNA MTU WIKI ILIOPITA ALIKUJA NA LANDCRUISER,,;NYEKUNDU T678 ATG, ALIPOKUJA AKAMKUTA MTOTO MWINGINE WA YULE MAMA;AKAMUULIZA MAMA YUPO HAYUPO,AKAMWAMBIA NASIKIA MNA MTOTO ZERUZERU;AKAJIBU NDIO;AKASEMA MI NATAKA NIMNUNUE NIMTUNZE;AKAMWAMBIA MAMA AKIJA MWAMBIE NITAKUJA KESHO JION NIONGEE NAE,,AKAANDIKA BARUA AMBAYO ALIONYESHA ANGETOA MILLION 6 ZA KITANZANIA;...NIKAJIBU EEH MAKUBWA.EEEHHH;AKASEMA YULE MAMA AKAJA MTOTO AKAMWAMBIA YOTE BAADAE AKAWAITA WATOTO WALIOBAKI UKIACHA YULE ALBINO ,AKAWAMBIA JAMANI MI MAMAYENU NIMEKAA NINA SHIDA SIKUZOTE NA NYIE MNAONA HATA JINSI YA KUISHI HAPA,KWA HIYO HUYU MTOTO MNAONAJE TUMUUZE HALI ATAENDELEA KUISHI NA akikua LAZIMA ATAULIZA WAZAZI WAKE AMA NDUGU YAKE NKASEMA LOH!!!!
Eeeh;ALIPOMALIZA KUoNGEA KATIKA WATOTO 4 WA YULE MAMA MMOJA AKACHMOKA AKAENDA KUCHEZA NA WENZAKE;WAKATI AKICHEZA NA WENZAKE AKAWAAMBIA MAMA ANATAKA KUMUUZA YULE MDOGO WETU;MZUNGU;WAKAMALIZA,WALIPOONDOKA HAMAD@@KUNA MTOTO AKAMWAMBIA MZAZI WAKE ALICHOELEZWA KUHUUSU KUUZWA WHITE,NDIPO AKAFWATILIA AKAAMBIWA KWELI NA JAMAA ANAKUJA KESHO;AKAENDA KUONGEA NA JAMAA WA USALAMA;WAKASUBIRI JAMAA AKAINGIA NDANI ,AKAONGEA NAO GAFULA JAMAA WA USALAMA WAKAINGIA(POLISI)..
WAKAMWAMBIA YUKO CHINI YA ULINZI!!!WAKAMCHUKUA NA YULE MAMA WAKAPELEKWA POLISI...MARA MAHAKAMANI ,,WALIPOFIKA HUKO MAMA MZAZIAKAOMBA MSAMAHA NI SHIDA ,HAKIM AKAMWAMBIA KWA NINI WASIMFUNGE...YULE MTOTO ZERUZERU AKAANZA KUPIGA KELELE AKASEMA MKIMFUNGA MAMA YETU HATUNA BABA TUTAISHIJE BORA ANIUZE ....UMATI UKASHTUKA....MARA HAKIMU AKAMHUKUMU MWAKA MMOJA KIFUNGO CHA NJE; SASA BASI HAYA NI YA MAHAKAMANI
YULE BWANA ALIECHUKULIWA ALIONDOKA NA POLISI NA MPAKA LEO HII AIJULIKANI ALIISHIA NAO WAPI,ILA YULE MAMA ANADAI WALIINGIZWA KWENYE NYUMBA MOJA WAKIWA NJIANI;THEN JAMAA AKASHUKA AKAENDESHA DREVA MPAKA POLISI;WAKATI AKISHUKA ASKARI MMOJA ALISHUKA NA KUONGEA NAE KWA NYUMA NINI;ALIMPA NINI SIJUI MIMI NA WEWE TUNAITAJI MAOMBI YAKUWAOMBEA SANA HAWA WATU;;;

bado najiuliza hili zoezi la mauaji kwa kweli ni gumu sana;neno la mungu linatufundisha hakuna kukata tamaaa,tunashukuru kama sio hivyo kwa neema tu tungeshakata tamaa,kwanza mwanzoni tunajua ama tulijua linawahusu wanasiasa;wafanyabiashara,na siku zinavyoenda limeamia kwa wazazi na hiyo aikutosha kama mnaona hapo juu na mapolisi wenye kulinda watu nao wanashiriki;

JF tufanyeje??
 
Back
Top Bottom