dm2000inter
Member
- Oct 27, 2010
- 29
- 10
Maskini mji wa Moshi,
Hadhi ya Mji wa Moshi inaporomoka kwa kasi kutokana na barabara zake za lami kukithiri mashimo makubwa bila kufanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Leo barabara ya kwenda KCMC ni hatari kwa wagonjwa wanaokimbizwa kuokoa maisha yao kutokana na mashimo barabarani.
Uzuri ule wa barabara za mji wetu unatoweka mithili ya moto wa kifuu huku menejiment wakiwa wamelala usingizi fofofo hadi wananchi sasa wanamkumbuka Mama Bernadeta Kinabo kwa umahiri wake hadi mji wa Moshi ukashika nafasi ya kwanza kitaifa kwa usafi kwa miaka sita mfululizo. Lakini leo tumeshikwa mashati na Iringa na kuporomoka hadi nafasi ya pili. Unafikiri nini chanzo cha hali hii na suluhisho lake ni nini? Tujadili pamoja
Hadhi ya Mji wa Moshi inaporomoka kwa kasi kutokana na barabara zake za lami kukithiri mashimo makubwa bila kufanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Leo barabara ya kwenda KCMC ni hatari kwa wagonjwa wanaokimbizwa kuokoa maisha yao kutokana na mashimo barabarani.
Uzuri ule wa barabara za mji wetu unatoweka mithili ya moto wa kifuu huku menejiment wakiwa wamelala usingizi fofofo hadi wananchi sasa wanamkumbuka Mama Bernadeta Kinabo kwa umahiri wake hadi mji wa Moshi ukashika nafasi ya kwanza kitaifa kwa usafi kwa miaka sita mfululizo. Lakini leo tumeshikwa mashati na Iringa na kuporomoka hadi nafasi ya pili. Unafikiri nini chanzo cha hali hii na suluhisho lake ni nini? Tujadili pamoja