Maskini Mji wa Moshi

Maskini Mji wa Moshi

dm2000inter

Member
Joined
Oct 27, 2010
Posts
29
Reaction score
10
Maskini mji wa Moshi,

Hadhi ya Mji wa Moshi inaporomoka kwa kasi kutokana na barabara zake za lami kukithiri mashimo makubwa bila kufanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Leo barabara ya kwenda KCMC ni hatari kwa wagonjwa wanaokimbizwa kuokoa maisha yao kutokana na mashimo barabarani.

Uzuri ule wa barabara za mji wetu unatoweka mithili ya moto wa kifuu huku menejiment wakiwa wamelala usingizi fofofo hadi wananchi sasa wanamkumbuka Mama Bernadeta Kinabo kwa umahiri wake hadi mji wa Moshi ukashika nafasi ya kwanza kitaifa kwa usafi kwa miaka sita mfululizo. Lakini leo tumeshikwa mashati na Iringa na kuporomoka hadi nafasi ya pili. Unafikiri nini chanzo cha hali hii na suluhisho lake ni nini? Tujadili pamoja
attachment.php


 

Attachments

  • 1780779_778147012248196_6929252381625824356_n[1].jpg
    1780779_778147012248196_6929252381625824356_n[1].jpg
    51.6 KB · Views: 4,429
Moshi unakua vizuri tu nilipita majuzi nyumba za juu (ghorofa) zinachipuka kwa kasi ya kuridhisha. Usafi bado ni mzuri sana kila sehemu. Hizo barabara zenye mashimo zitengewe bajeti mara moja kwa sababu sioni mantiki ya kuweka lami barabara zinazotoka nje ya mji tunaacha za ndani ya mji. Manispaa amkeni!
 
Tutoke kwenye ulevi wa vyama na utumbo wa chama flani kimefanya hivi. Moshi yetu tuipende na kuijenga kwa pamoja. Tuangalie maslahi yetu kwanza km tulivyolelewa na wazee wetu.

Hatua za mwanzo za vyama vingi iliwezekana kuwa na wanachama wengi tu wa upinzani na hata kushinda ubunge. Mfano hai imekua na wabunge wa vyama tofauti hata CCM nao wametoka na wamerudi wamechemsha wametupwa.

Tumelelewa kujua tunalotaka kwa wasiotujua. Msitupandikize michuki yenu.

Ni kweli Moshi hapa nyuma iliporomoka. Zile fine kubwa kubwa kwa kuchafua au kupaki hovyo zilisimama na ndo hali ikidorora. Juzi nimeenda na kushuhudia mabadiliko, wamekaza tena kiusafi naamini itarudi. Mzee eti Ndesa pia bado yupo.

Kuhusu ujenzi siridhiki na maendeleo ninayoyaona. kwa utajiri wa watu wa Moshi ningetarajia majengo mazuri na makubwa zaidi kama la NSSF pale.

Barabara pia zimeporomoka.
Ila Nina hakika wanamoshi watajenga na jitihada zipo.

Moshi ya wanamoshi Mi vyama yenu ya siasa sio agenda yetu kwenye maendeleo kama kwa jamaa flani flani humu.

Tuipende na kuilinda Moshi yetu Wanamoshi.
 
Maskini mji wa Moshi,

Hadhi ya Mji wa Moshi inaporomoka kwa kasi kutokana na barabara zake za lami kukithiri mashimo makubwa bila kufanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Leo barabara ya kwenda KCMC ni hatari kwa wagonjwa wanaokimbizwa kuokoa maisha yao kutokana na mashimo barabarani.

Uzuri ule wa barabara za mji wetu unatoweka mithili ya moto wa kifuu huku menejiment wakiwa wamelala usingizi fofofo hadi wananchi sasa wanamkumbuka Mama Bernadeta Kinabo kwa umahiri wake hadi mji wa Moshi ukashika nafasi ya kwanza kitaifa kwa usafi kwa miaka sita mfululizo. Lakini leo tumeshikwa mashati na Iringa na kuporomoka hadi nafasi ya pili. Unafikiri nini chanzo cha hali hii na suluhisho lake ni nini? Tujadili pamoja
attachment.php



Wanachokijua Ni Mbwembwe Za Kujengea Tu Makaburi Kifahari Na Kuishi Ki Dili Dili Na Kimagumashi Humu Mijini Mwetu.
 
Moshi unakua vizuri tu nilipita majuzi nyumba za juu (ghorofa) zinachipuka kwa kasi ya kuridhisha. Usafi bado ni mzuri sana kila sehemu. Hizo barabara zenye mashimo zitengewe bajeti mara moja kwa sababu sioni mantiki ya kuweka lami barabara zinazotoka nje ya mji tunaacha za ndani ya mji. Manispaa amkeni!

Ushauri wako mzuri kama wahusika watauzingatia na kuufanyia kazi!
 
Wanachokijua Ni Mbwembwe Za Kujengea Tu Makaburi Kifahari Na Kuishi Ki Dili Dili Na Kimagumashi Humu Mijini Mwetu.

Wakijengea wewe inakuwashia nini na wewe kajengee ya kwenu na wewe ishi kimagumashi basi ume comment kichuki kabisa
 
Mimi mkoa wa Kilimanjaro sijaona pa kuishi...labda Boma ya Ng'ombe na Kia tu
 
Back
Top Bottom