Jamani wanaJF nakuja kwenu na bonge la tatizo. Kwa kuwa hapa ni kigoda cha fikara naamini nitapata ushauri mzuri.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 32. Nina mtoto 1 ambaye nilimpata nikiwa napita ktk kipindi cha balehe.Sina mke hadi sasa. Kwa muda wa miezi 12 nimekuwa ktk mahusiano yenye malengo ya ndoa na dada ambaye naye ana mtoto wa miaka 2. Dada huyu alinihakikishia kuwa mzazi mwenzie hayuko naye tena. Dada huyu pia amewahi kutembea na rafiki yangu wa karibu wa sasa kabla ya kuwa na mtoto. Hili limekuwa likinipa shida hata kumtambulisha demu huyu.
Mbali na hilo miezi 6 iliyopita nilipgiwa simu na jamaa aliyezaa naye akinisihi niachane na mkewe. Mimi nilianza kumkwepa yule dada kwa kuwa hakuwa mkweli maana alisema hana mtui. Baada ya wiki 1 yule dada alinifuata akiwa na marafiki zake 2 akadai yule mzazi mwenzie kesha achana naye na hana mpango wowote isipokuwa anamharibia tu. Mimi nikarudiana naye na nikazama vilivyo ndani ya moyo wake. Ikawa tunakula raha za kila aina za kimwili.
Wiki iliopita nilikwenda kwake bila taarifa mida ya saa 2 usiku. Nilipofika niligonga mlango mara tatu sikupata majibu. Kwa kuwa taa za sebuleni zilikuwa zinawaka nilijipa moyo kuwa huenda yupo chumbani kajilaza kitandani na amepitiwa na usingizi. Nilizunguka nyuma ya nyumba ili nimuite chumbani kwa kupitia dirishani. Niliita mara 2 bila majibu. Mara ya 3 nilikaribishwa na mwanaume aliyekuwa nyuma yangu akitokea ndani ya nyumba ninayogonga. Tulipoingia ndani yule mwanaume alimwita mara 3 yule dada kwa jina aje pale sebuleni ampokee mgeni wake ambaye ni mimi. Dada hakutoka. Ndipo yule jamaa akaniuliza `kwani wewe nani na ni nani yake?` Nikamwambia mm ni mpnz wake na nilipotaja jina langu akaniuliza unakumbuka kuna siku nimekupigia simu kukuonya uachane na mke wangu? Nikampa full story. Akaingia chumbani na kuanza kushusha kichapo kwa yule dada bila huruma, nami nikasepa faster. Leo hii ninavyoandika thread hii yule dada kamtuma rafiki yake aje kumuombea msamaha na kuahidi kumuacha kikweli kweli yule jamaa yake kwani hana malengo mazuri na yule dada kama niliyo nayo mm.
Nimkubalie ama nimkatalie? Maana dada nampenda mno. Naombeni msaada wa kimawazo, niko njia panda.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 32. Nina mtoto 1 ambaye nilimpata nikiwa napita ktk kipindi cha balehe.Sina mke hadi sasa. Kwa muda wa miezi 12 nimekuwa ktk mahusiano yenye malengo ya ndoa na dada ambaye naye ana mtoto wa miaka 2. Dada huyu alinihakikishia kuwa mzazi mwenzie hayuko naye tena. Dada huyu pia amewahi kutembea na rafiki yangu wa karibu wa sasa kabla ya kuwa na mtoto. Hili limekuwa likinipa shida hata kumtambulisha demu huyu.
Mbali na hilo miezi 6 iliyopita nilipgiwa simu na jamaa aliyezaa naye akinisihi niachane na mkewe. Mimi nilianza kumkwepa yule dada kwa kuwa hakuwa mkweli maana alisema hana mtui. Baada ya wiki 1 yule dada alinifuata akiwa na marafiki zake 2 akadai yule mzazi mwenzie kesha achana naye na hana mpango wowote isipokuwa anamharibia tu. Mimi nikarudiana naye na nikazama vilivyo ndani ya moyo wake. Ikawa tunakula raha za kila aina za kimwili.
Wiki iliopita nilikwenda kwake bila taarifa mida ya saa 2 usiku. Nilipofika niligonga mlango mara tatu sikupata majibu. Kwa kuwa taa za sebuleni zilikuwa zinawaka nilijipa moyo kuwa huenda yupo chumbani kajilaza kitandani na amepitiwa na usingizi. Nilizunguka nyuma ya nyumba ili nimuite chumbani kwa kupitia dirishani. Niliita mara 2 bila majibu. Mara ya 3 nilikaribishwa na mwanaume aliyekuwa nyuma yangu akitokea ndani ya nyumba ninayogonga. Tulipoingia ndani yule mwanaume alimwita mara 3 yule dada kwa jina aje pale sebuleni ampokee mgeni wake ambaye ni mimi. Dada hakutoka. Ndipo yule jamaa akaniuliza `kwani wewe nani na ni nani yake?` Nikamwambia mm ni mpnz wake na nilipotaja jina langu akaniuliza unakumbuka kuna siku nimekupigia simu kukuonya uachane na mke wangu? Nikampa full story. Akaingia chumbani na kuanza kushusha kichapo kwa yule dada bila huruma, nami nikasepa faster. Leo hii ninavyoandika thread hii yule dada kamtuma rafiki yake aje kumuombea msamaha na kuahidi kumuacha kikweli kweli yule jamaa yake kwani hana malengo mazuri na yule dada kama niliyo nayo mm.
Nimkubalie ama nimkatalie? Maana dada nampenda mno. Naombeni msaada wa kimawazo, niko njia panda.