Mashirika ya Umma tuyaombee sala gani?

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,446
Nia ya Rais ya kufufua haya mashirika ya Umma ilikuwa njema lakini naona shughuli yake inaenda kuwa pevu.

Kwa mara nyingine jana nilikwenda kubadili fedha kwenye duka la Shirika la Posta Masaki. Mara ya mwisho kwenda pale wahudumu waliokuwepo waliniambia anayehusika na kitengo cha kubadili fedha ana msiba!

Jana alikuwepo na alinibadilishia isipokuwa alisema hawatoi risiti! Nikamuuliza kwa nini, akaniambia mashine ni mbovu na amewatumia wakubwa taarifa mara nyingi lakini mafundi hawajaletwa. Pia alinionya kuwa mashine inatengenezwa mara kwa mara lakini huwa haichelewi kufa

Najiuliza, pamoja na upendeleo huu wa kibiashara, mashirika haya yabebewe mbeleko gani ili yaweze kujiendesha kibiashara? Najiuliza, hali ingekuwaje kama duka binafsi lingebainika kubadili fedha bila kutoa risiti? Lingepewa kesi ya namna gani?

Credit: James Gayo
 
Haya mashirika pamoja na kubebwa hayabebeki wafanyakazi wanafanya kazi kama wamelazimishwa we fikiria ttcl wamezindua kifurushi cha bando tamtam tena kwa gharama kubwa halafu wamekitoa kimyakimya maana yake hawakufanya utafiti wa kutosha au hawajui wafanyalo
 
Haya mashirika pamoja na kubebwa hayabebeki wafanyakazi wanafanya kazi kama wamelazimishwa we fikiria ttcl wamezindua kifurushi cha bando tamtam tena kwa gharama kubwa halafu wamekitoa kimyakimya maana yake hawakufanya utafiti wa kutosha au hawajui wafanyalo
 
Muundo wa shughuli za kiserikali hazijakaa kibiashara kabisa.

Mnaweza mkaishiwa kalamu na ikachukua wiki kadhaa kuzipata, mlolongo wake ni usipime.

Utaambiwa jaza form namba 2 ya ppra kisha wapelekee watu wa procurement kisha na wao watafute supplier wapi sijui huko, tena kumbuka hao procurement wana shughulika na manunuzi yote. Mwisho wa siku kazi ya dakika kumi inachukua wiki mbili.

Ingelikua ni duka binafsi la kubadilisha fedha hapo ni simu tu ingepigwa kisha mashine inatengezwa haraka, serikalini hauwezi kufanya hivyo, utaitwa mhujumu uchumi.
 
Back
Top Bottom