Mashine ya LUKU imenigomea kuingiza Umeme

Mashine ya LUKU imenigomea kuingiza Umeme

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,267
Nimefungiwa LUKU mpya inayofungwa juu kwenye NGUZO ZA UMEME ambapo mashine zake unaweka kwa ndani ya nyumba na ni lazima muda wote uwe umechomeka kwenye soketi kwani ukichomoa tu kanakata chaji.

Tangu jana nilinunua umeme lakini kila nikijaribu kuingiza ina serch hadi basi nimejaribu kununua umeme mwingine kwa simu wapi, nimetafuta umeme wa karatasi wapi nimebadili kutoka Max malipo hadi kampuni nyingine ya Selcom lakini wapi na nimelala kiza.

Mwenye ushauri wakuu
 
Ikiwa ni malipo ya kwanza inabidi huo umeme ukalipie Tanesco ili iweze kufunguliwa. Baada ya hiyo ndio utaweza kununua kwa njia hizo nyingine. Nami nilipatwa na tatizo hilo ila nikapata suluhisho hilo na ufafanuzi kutoka tanesco.
 
Kama inasearch muda wote kuna kwenye hako kammashine kuna kiantena cheusi ndio antena yake ya kushika mawimbi, angalia kama mmekavunja hamuwezi kuweka umeme, kama kapo hapo jirani ukaunganishe kisha utaonn kinasoma unit zilizobaki.

Kama umeme uliisha kabisa yaani unit 0, nenda kawekee kwa jirani. Hako kamashine sio muda wote uwe umekachomeka kwenye umeme,ukishaweka umeme unakatoa hakana shida maana kana betri kwa ndani za kawaida ndogo ambazo zikichoka unaweza kubadilisha.
 
Chomeka hicho ki metre kwenye soket ya umeme Kisha ingiza umeme bila kuchomeka kwenye soketi ukutani umeme hauwezi ingia
 
Nimefungiwa LUKU Mpya inayofungwa juu kwenye NGUZO ZA UMEME ambapo mashine zake unaweka kwa ndani ya nyumba na ni lazima muda wote uwe umechomeka kwenye sakiti kwani ukichomoa tu kanakata chaji

tangu jana nilinunua umeme lakini kila nikijaribu kuingiza ina serach hadi basi nimejaribu kununua umeme mwingine kwa simu wapi nimetafuta umeme wa karatasi wapi nimebadili kutoka max malipo hadi kampuni nyingine ya selcom lakini wapi na nimelala kiza

mwenye kaushauri wakuu
Zima switch sockets zako zote bakiza moja tu utakayowekea hicho kidude cha Tanesco. Ingiza hizo units zako
 
Nimefungiwa LUKU Mpya inayofungwa juu kwenye NGUZO ZA UMEME ambapo mashine zake unaweka kwa ndani ya nyumba na ni lazima muda wote uwe umechomeka kwenye sakiti kwani ukichomoa tu kanakata chaji

tangu jana nilinunua umeme lakini kila nikijaribu kuingiza ina serach hadi basi nimejaribu kununua umeme mwingine kwa simu wapi nimetafuta umeme wa karatasi wapi nimebadili kutoka max malipo hadi kampuni nyingine ya selcom lakini wapi na nimelala kiza

mwenye kaushauri wakuu

jaribu leo mchana ucku znagoma
 
Ikiwa ni malipo ya kwanza inabidi huo umeme ukalipie Tanesco ili iweze kufunguliwa. Baada ya hiyo ndio utaweza kununua kwa njia hizo nyingine. Nami nilipatwa na tatizo hilo ila nikapata suluhisho hilo na ufafanuzi kutoka tanesco.

ASANTE SIKUJUA kumbe KATAVI KUNA UMEME
 
Kama inasearch muda wote kuna kwenye hako kammashine kuna kiantena cheusi ndio antena yake ya kushika mawimbi, angalia kama mmekavunja hamuwezi kuweka umeme, kama kapo hapo jirani ukaunganishe kisha utaonn kinasoma unit zilizobaki.

Kama umeme uliisha kabisa yaani unit 0, nenda kawekee kwa jirani. Hako kamashine sio muda wote uwe umekachomeka kwenye umeme,ukishaweka umeme unakatoa hakana shida maana kana betri kwa ndani za kawaida ndogo ambazo zikichoka unaweza kubadilisha.
kanakubali kweli kuongezea kwa jirani?
 
Back
Top Bottom