DOKEZO Mashine ya CT-SCAN katika Hospitali ya Mloganzila ni Mbovu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Habarini, naleta taarifa hii kwa masikitiko makubwa sana...

Mashine ya CT SCAN katika hospitali ya Mloganzila ni mbovu takribani mwezi mmoja na nusu na hali ni mbaya, wagonjwa wengine inawapasa wapange foleni katika kupata huduma hii.

Ni aibu kwa Hospitali yenye hadhi ya TAIFA kama Mloganzila kukosa huduma hii muhimu, pamoja na jitihada za Mh Rais kukuza sekta ya afya lakini kuna baadhi ya watendaji wanamuangusha.

Wagonjwa wanahamishwa kutokea Muhimbili Mloganzila kwenda Muhimbili Upanga jambo ambalo ni usumbufu kwa wagonjwa na vilevile gari wanalotumia (Ambulance) sio salama kwa matumizi ya wagonjwa yaani limechakaa halifai ni basi tu wanaforce ili mambo yaende (NINGEWEKA PICHA YAKE MUONE ILA NAWASITIRI KWA MUDA)

Tunapaza sauti suala hili lifanyiwe kazi haraka na mashine irudi kwenye hali yake ya kawaida.

ASANTE
 
Priority ya serikali ni kununua magari tu, vifaa tiba na vifaa vingine sio vipaumbele vyao.

Wao wakiumwa watakimbizwa nje kwa kodi zenu.

Mnakumbushwa kuchukua risiti za EFD kila siku ila wao hawataki kukumbushwa majukumu yao.
 
Wana billioni 600 wameweka kibindoni wanagonganisha cheers.

Wenyewe wanakuambia serikali imewakopea benki wabomoe muhimbili waijenge upya..
 
JITIHADA ZA RAIS GANI LABDA...? JITIHADA GANI ALIZO NAZO...?
HIZO JITIHADA ANGEKUWA NAZO USINGEKUJA KULETA LALAMIKO HAPA.
 
Mnh-Mloganzila sijui wanakwama wapi?

Walikuwa na uwezo wa kupata mashine mbili za CT scan na MRI kipindi cha mgao wa mashine za covid 19,

wenzao upanga walichangamkia fursa hivi sasa wana mashine mbili za CT scan na MRI 2,

zile changamoto za wagonjwa kukosa huduma pindi mashine inapoharibika hakuna tena,

Nadhani imefika kipindi serikali iziwezeshe hizi hospitali zetu kubwa MLOGANZILA, MOI, BUGANDO, JKCI, na BENJAMIN MKAPA ziwe na backup ya vifaa ambavyo vikiharibika vinachukua muda mrefu kurudi katika hali ya utendaji kazi

Hoja nyingine, kuna hawa biomedical engineers wa hapa kwetu Tanzania, nadhani imefika kipindi nao wajengewe uwezo wa kutengeneza hizi mashine,

Ni aibu kama nchi mashine inaharibika, mtu kutoka India, Kenya, au South Afrika, ndio aje atengeneze mashine na sisi tuna wataalam wetu,

Kingine kuna hawa wataalamu wanazo run hizi mashine, nasikia wengi wao pia ni diploma holders, nao pia wanatakiwa warudi shule wajiendeleze, isije kuwa nao wanachangia mashine kuharibika kutokana na kuwa na ufinyu wa maarifa,

Nawasi wasi pia na vyuo vinavyo zalisha hawa watu, biomedical engineers na hawa wataalamu wanao endesha hizi mashine kama wana walimu, wenye maarifa yanayo endana na mabadiliko ya teknolojia, na vifaa vya kisasa,

Nadhani wizara ya Afya inaweza kwenda uko vyuoni wanapozalishwa hawa wataalamu wetu kujionea,
 
Back
Top Bottom