Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,850
- 155,799
- Thread starter
- #41
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’
Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’
Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.
Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.
Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.
Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.
Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.
Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.
Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.
Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’
Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’
Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.
’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’
Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’
Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’
Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.
Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.
Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’
Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.
Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’
Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’
Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’
Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’
Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.
Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’
Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.
Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.
Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’
Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.
Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.
Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.
Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.
Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.
Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.
Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.
Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’
Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’
Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.
’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’
Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’
Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’
Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.
Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.
Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’
Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.
Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’
Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’
Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’
Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’
Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.
Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’
Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.
Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.
Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’