Masheikh wa Uamsho

Status
Not open for further replies.
Nimesikia rais magufuli katoa msamaha ila kwenye msamaha huo sijasikia kusamehewa masheikh wetu wa uamsho najua kusema ukweli kwao ndo imekuwa tatizo ila naimani ipo siku mungu ataleta neema yake watatoka
1.Kwani Kesi yao imeshaisha?

2.Na kama imeshaisha, walihukumiwa miaka mingapi?

3. Msamaha umetolewa kwa wafungwa waliobakiza muda gani?
 
Miungu watu wabaya sana. Hii kesi hata haifanyiki wamewaweka huko mahabusu sijui mwaka wa ngapi sasa. Utawala bora Tanzanian style. Yaani kwa data za leo mahabusu ni wengi kuliko wafungwa.
 
Kama kuna anayejiita muislam huku akifurahia utawala wa ccm basi huyo ni ibilisi shetani.Masheikh wapo zaidi 2000 katika magereza mbalimbali kwa kesi za ugaidi wengine wamefichwa tuu
FaizaFoxy
Ritz
 
Nimesikia rais magufuli katoa msamaha ila kwenye msamaha huo sijasikia kusamehewa masheikh wetu wa uamsho najua kusema ukweli kwao ndo imekuwa tatizo ila naimani ipo siku mungu ataleta neema yake watatoka
Ametoa msamaha kwa waliohukumiwa tayari. Sheria inamruhusu. Lakini sheria haimruhusu kwa ambao kesi zao zinaendelea. Tofautisha hilo.

Anachoweza kufanya ni kumshauri DPP kama alivyofanya kwa mafisadi. Hawa Ma Sheikh wamekaa sana mahabusu na ni dhahiri serikali haina ushahidi wa kuwatia hatiani. Ni vyema wakaachiwa.
 
Nimesikia rais magufuli katoa msamaha ila kwenye msamaha huo sijasikia kusamehewa masheikh wetu wa uamsho najua kusema ukweli kwao ndo imekuwa tatizo ila naimani ipo siku mungu ataleta neema yake watatoka
Kwani majina ya yalishatoka? Nasubiri jina la Sethi Singh & Co.
 
Hao si wafungwa,hakuna hata sehemu moja alipotaja kwamba amesamehe mahabusu,subiri wafungwe ndio uje na malalamiko hayo.
 
Siwezi kumtetea mtu anayetaka kuhatarisha amani ya nchi hata kama ni muislam au mkristo mwenzangu,kwa hilo suala siyo la kisiasa.
Daah! Hii ndio tz tulikopelekwa kwa sasa kila atakae sema kweli kuhusu muungano ati anataka kuondosha amani ya nchi
 
Miungu watu wabaya sana. Hii kesi hata haifanyiki wamewaweka huko mahabusu sijui mwaka wa ngapi sasa. Utawala bora Tanzanian style. Yaani kwa data za leo mahabusu ni wengi kuliko wafungwa.
KWANI MAREKANI NA NCHI NYINGINE ZIMEWAWEKA GEREZANI WATU WA AINA HII KWA MIAKA MINGAPI? SI NI BADO WAPO KWA AJILI YA USALAMA WA NCHI? FIKIRIA ZAIDI. WEWE UNAWATAKA WA NINI HAUSWALI MPAKA WAWEPO? ENDELEA KUMWOMBA MUNGU WENU ILI AFUNGULIWE NA WENGINE WAOMBE WASIFUNGULIWE TUTAJUA UKWELI NI NANI.
 
Kama kuna anayejiita muislam huku akifurahia utawala wa ccm basi huyo ni ibilisi shetani.Masheikh wapo zaidi 2000 katika magereza mbalimbali kwa kesi za ugaidi wengine wamefichwa tuu
FaizaFoxy
Ritz
Hao sio mashekhe ni wahuni tu waliojivisha ushekhe ndani yake.Mashekhe ni wale wanaowafundisha watu kuacha maovu na kumtafuta Mungu tukiishi kwa kuvumiliana na upendo mkubwa.Ukiona mtu anaeneza chuki,utengano basi huyo ni mhuni Kama wahuni wengine.Kama Kuna Shekhe na hakutendewa haki Basi muda utafika na atatoka.
 
Nimesikia rais magufuli katoa msamaha ila kwenye msamaha huo sijasikia kusamehewa masheikh wetu wa uamsho najua kusema ukweli kwao ndo imekuwa tatizo ila naimani ipo siku mungu ataleta neema yake watatoka
Unataka wauaji wa kibiti wasamehewe?

Wapigana jihadi uchwara
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom