Mashati ya Batiki kwa bei rahisi.

Mashati ya Batiki kwa bei rahisi.

Kuhoji uhalali wa bei ya kitu si kutokuwa na pesa, bei ya kitu inapaswa kulingana na vitu vya aina yake katika soko, ni ujinga kununua kilo ya unga wa mahindi kwa 5000 kwenye duka la vyakula wakati inaeleweka kuwa unga huo unauzwa kote kwa bei isiyozidi sh. 1500.
Kingine ni kuwa bei ya kitu inapaswa kulingana na ubora wake na si kuuziwa kitu cha ubora wa kawaida au wa chini kwa bei kubwa kisa eti una hela ya kulipa. Hii inaexclude exceptional cases kama pale bidhaa inapokuwa inauzwa katika eneo ambalo muuzaji analipia pango kubwa kupita kiasi kitu kinachomlazimu kufidia gharama kwa kupandisha bei ya bidhaa zake kidogo tofauti na zile zinazouzwa maeneo mengine.
Kingine ni kuwa 700,000 inaweza kuwa hela nyingi sana kwako lakini ni hela ya kawaida sana ila kuitoa kwenda kumwangalia Kansiime ni maamuzi binafsi kwani si wote wanaovutiwa na shoo za mtu kama yeye ambae kwako anaweza kuwa mtu wa ajabu sana. Karibu

U have nailed it ....n'dai like mkuu Swordfisher
 
Last edited by a moderator:
U have nailed it ....n'dai like mkuu Swordfisher

Pamoja Mkuu! Unajua inapaswa ifike mahali watu wawe wanaona aibu kuweka bei zisizoendana na hali halisi kisa tu wanauza humu jukwaani, hili si kundi la watu wanaoshinda tu nyuma ya kompyuta. Wapo mitaani, gengeni, ofisini kwani ni watu.
Hii haina maana kuwa watu hawana pesa.
Juzi hapa nilianzisha thread kuwa nahitaji External Hard Disk ya mtumba ya terabyte 1 na kuoffer 100,000 watu wakawa kimya. Kwa kuwa nilikuwa na haraka nayo, nilienda kuchukua mpya kwa 150,000. Wengine walikuja Ni PM nikiwa tayari nimepata. Nalipa hela yangu kwa kitu kinachoendana na hiyo pesa na hata kungekuwa mpya humu ya bei zaidi ya kile nilicho offer tungeelewana tu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hizo za 18-20 zinapatikana wapi? Nazihitaji

Nipe no yako tufanye biashara.
Nina za watoto pia na za mikono mirefu.
Nauza 17,000-20,000 inategemea na idadi.
Pia nauza na pensi bei ni 35,000-40,000 inategemea idadi pia
 
wizi mtupu,
hizo tshirt ni sh 7000 bei ya jumla,


Sent from my iPhone using JamiiForums

Yes ni 7,000 ikiwa plain
Ila kuitoa kwa muuzaji wa jumla kuja kuiza mtaani bei inaongezeka
.kitenge kimenunuliwa
.fundi kalipwa
.na biashara ni kutafuta faida sio zawadi...
 
Lkn kwa 42,000 sidhani kama upo sahihi kufanya biashara pamoja na kujumlisha hayo mengine yote,kuwa serious fanya biashara,have a reasonable price to impress your business...
 
Ndio maana kuna Samsung Galaxy S5 ya Million 1.4 na CLONE ya S5 kwa laki 2. Ila zote ni S5.
 
Ndio maana kuna Samsung Galaxy S5 ya Million 1.4 na CLONE ya S5 kwa laki 2. Ila zote ni S5.

ulinganifu wako hauna maana, hizo matisheti zote ni ni yaleyale tu wamenunua matisheti kwa mchina wakanunua na mackenzi toka kongo wanashona kwa cherehani, sema mmoja wao yuko greedy! yapo mashati mazuri hata laki nne unalipa, siyo hiyo mitisheti!
 
kama hamna pesa mnyamaze msitukane biashara za watu hii ni biashara huria.Nyie ndio mtaweza kununua ticket ya kumuona Kansiime laki 7 kwa meza!!

mtoa mada/mleta tangazo usikate tamaa wenye pesa watakupm.

hawajakosea kusema, ndiyo maana ya soko huria! muuzaji tu anatakiwa aje hapa awashawishi ni kwa nini wasinunue tishirts hizohizo sehemu nyingine kwa less than 20k wanunue kwake kwa more than 40k! kama yeye alipigwa bei wakati wa kununua hilo ni tatizo lake anatakiwa either atafute soko sehemu nyingine ambako atauza bei juu ili apate faida, au auze afuatilie ni wapi zinakotoka hizo za bei rahisi na yeye anunue huko ili auze bei chini! Kuweza au kutoweza kwenda kumwona kansiime kwa laki saba hain uhusiano wowote na kunuua tshirts zilizo overpriced, labda kama mtu anataka kujitangaza "nimenunua elfu hamsini hii"! show ya kansiime nayo iko overpriced tu, elfu tisini kwa kichwa nadhani ni kwa sababu wamefanyia golden tulip, lakini si kweli kwamba kansiime ndiyo wa bei hiyo!
 
ulinganifu wako hauna maana, hizo matisheti zote ni ni yaleyale tu wamenunua matisheti kwa mchina wakanunua na mackenzi toka kongo wanashona kwa cherehani, sema mmoja wao yuko greedy! yapo mashati mazuri hata laki nne unalipa, siyo hiyo mitisheti!

Ume judge baada ya kuona sample. Una force wawe wamenunua T-shirt kwa mchina, au umeziona LIVE hizo kitu?
 
Inabidi kuwa makini sana yaani tshirt zimeshakuwa shirt aisee
 
Back
Top Bottom