rmashauri
JF-Expert Member
- Jan 29, 2009
- 3,011
- 454
poa sana
Inaonekana watu wa Fukayosi tumo wengi humu. Nami nina viekari vyangu huko japo vingine vimeshakuwa na mgogoro maana jamaa aliyetuuzia kaviuza tena kwa mtu mwingine.
poa sana
Jamani tuwe makini na Fukayosi, kuna watu walishanunua mapori siku nyingi huko,unaweza uziwa pori la Kigogo, Fukayosi imepata umaarufu ghafla,bei za pale Fukayosi zinabadilika sana kila siku,march nilipima shamba la mtu pale Fukayosi shule ya msingi ng`ambo ya pili kama mita mia nne hivi kuingia ndani, bei ilikuwa laki saba. July 5 nilifika tena kwa kazi hiyo hiyo, naambiwa eti ni milioni moja. Nikapima na kuondoka zangu.
Nilimshauri huyu kigogo asogee kijiji cha Mwavi, mbele ya kidogo kama unakwenda Msata.
Kwa nini Watz tunaumizana na hizi bei za ajabu ajabu?
Malila,
Vipi kwa upande wa kuelekea Mkuranga? Uzoefu wako ukoje huko? Yaani upatikanaji wa mashamba na ubora wa ardhi yenyewe?
Jamani tuwe makini na Fukayosi, kuna watu walishanunua mapori siku nyingi huko,unaweza uziwa pori la Kigogo, Fukayosi imepata umaarufu ghafla,bei za pale Fukayosi zinabadilika sana kila siku,march nilipima shamba la mtu pale Fukayosi shule ya msingi ng`ambo ya pili kama mita mia nne hivi kuingia ndani, bei ilikuwa laki saba. July 5 nilifika tena kwa kazi hiyo hiyo, naambiwa eti ni milioni moja. Nikapima na kuondoka zangu.
Nilimshauri huyu kigogo asogee kijiji cha Mwavi, mbele ya kidogo kama unakwenda Msata.
Kwa nini Watz tunaumizana na hizi bei za ajabu ajabu?
Natembea nuruni kabisa,
Mkuranga ktk vijiji vya Msorwa ( 60Km from Tazara), Shungubweni (67km from Tazara),Mpafu, kuna ardhi nzuri bado kwa ufugaji kwa sababu kuna maji ya kutosha ya mito au kuchimba visima vifupi. Bei zinacheza kati ya 250 mpaka 450 kwa eka. Na sehemu zenye kichanga unaweza pata kwa 200 kamili kwa eka.
Kando ya mito kuna kilimo cha matikiti,mpunga na mboga kama nyanya, pilipili, matango nk. Kididimo kuna ardhi nzuri sana kunafaa kwa mihogo na mazao mengine. Mbezi/Msufini kuna ardhi yenye rutuba sana,ila vijiji hivi havina maji ila viko ktk barabara kuu ya kisiju.
KimanziChana/Mkiu/Mkamba kuna ardhi bomba sana kwa kilimo cha Mpunga,Mahindi,Choroko, na mvua huko zinanyesha vizuri, kama kawaida zikigoma ni hatari tupu. Vijiji hivi vinakabiliwa na tatizo la maji. Huu upande wa Hoyoyo kuna ardhi kubwa na nzuri ila ukame ukipita unaweza kupata ugonjwa ghafla.
Ila kuanzia Vikindu mpaka Mwalusembe kando ya barabara kuu, bei zimepanda ajabu, sababu ya viwanda vinavyojengwa kwa wingi kando ya barabara hii ya kusini. Eka inafika milioni 30 na kuendelea. Pale Mwanambaya niliuliza eka saba ni sh ngapi,nikaambiwa nitoe milioni 80 hivi, hiyo ni january 2012. Juzi Mchina kachukua kwa 100M.
Shamba la ndanindani sio lenyewe kwa kufichia magendo na zile nyara zangu nilizoiba siku nyingi... Naomba uni pm hiyo no ya mzeee.Nina uzoefu na kijiji cha Mwavi (baadaya ya kupita Fukayosi ukitokea bagamoyo). Utapeli wa ardhi bado. Ukishapata sehemu na kuelewana bei unachukua afisa mtendaji wa kijij,mwenyekiti wa kijiji pamoja na wa Kitongoji ambao kimsingi wanapema hilo eneo na kuandikishana kwenye ofisi ya kijiji. Ni lazima ulipa 10% ya kijiji na unapewa risiti. Kwa Mwavi ni kijiji kipya na wanajenga ofisi na kwa vile unakuwa mwanakijiji mpya watakuomba uchangie ujenzi wa ofisi. Ni watu wazuri sana.
Mwavi kuna mashamaba ila yako ndani kidogo na yanacheza kwenye laki 4- 7. Kama unahitaji huko niambia nikupe no.ya simu ya mzee wa huko wakutafutie fasta.