Niliona umegusia sana mpunga ndio maana nikauliza. Na nyanya ni sehem gani zinakubali??
Na mashamba yake lazima ukodi kwenye chama?? Bei shi ngapi?
kutoka dar es salaam hadi Ruvu kwenye hayo mashamba kuna umbali gani ?wanajamviii!
Kwa kilimo cha mpunga, kukodisha mashamba mwisho ni mwezi gani?
kutoka dar es salaam hadi Ruvu kwenye hayo mashamba kuna umbali gani ?wanajamviii!
Mkuu, kuna mashamba ya kulima mbogamboga mm nahitajiHabari zenu.
Nimewahi kuuliza swali kuhusu mashamba ya kulima Ruvu,nikabahatika kupata maelezo,nikaenda na nimeanza.
Lakini,uzi ulioniongoza nimeutafuta sijauona,ila nimetumia muongozo niliopewa.
Ruvu kwa kweli kama una nia ya kulima ni pazuri,maji yapo ya uhakika,mito ni miwili,Ruvu na Msuya.
Pamoja na hayo lakini kuna changamoto kubwa mbili:
1.Usimamizi unahitajika na kama umeamua,hamia au tafuta mtu wako wa karibu.Wajanja huku ni wengi,tena bora niwaite wahuni.Ukituma hela kwamba kazi utafanyiwa utaishia kulia tu.
2.Upatikanaji wa mashamba:
+255 658 899 195.Kuna mtu siku za nyuma alitoa hii number kwamba atafutwe mwenye nayo,atawapa maelezo.Hakika aliyepost hii number wanashilikiana asilimia mia.
Jamani,mtu kama yule unawezaje kuomba watu,walioacha familia zao,wampelekee pesa,awatapeli?
Nawasihi sana,nimeona mengi.
Kama unataka shamba huko,kuna sehemu mbili.Kuna kilimo cha mpunga,kinafanywa na shirika,huyu anawapeleka watu na kuwauzia mashamba ya watu,mwisho wa siku mnaishia kugombana na hela unapoteza.Anauza shamba lililopandwa mpunga kwa laki 5,na lisiti atakupa.Za kughusho,mwisho wa siku unakumbana na mwenye shamba sasa.Kama umeamua kulima huko,nenda ofisini,gharama za ofisi ni 442,000(pesa ya kukodi shamba kwa mwaka,unalimiwa,unapewa maji,mbegu ya mpunga ni ya kwao unauziwa kiasi kidogo si kama madukani nje,mbolea ni za ruzuku,ukihitaji utapewa kwa gharama nafuu)Ukipita pembeni shauri yako.Labda uonane na mwenye shamba mtajuana wenyewe lakini kupitia mtu mwingine utalia.
Mashamba mengine unakodi kwa watu,na kama utakodi la hivo,hakikisha mnaandikishana kwenye uongozi wa kijiji.Tofauti na hapo,utajua mwenyewe.
Ukihitaji maelezo zaidi,nambie,kama kukusindikiza ntakusindikiza,ugharamie usafiri.Ila,kama hujajipanga kulima,usiharibu hela yako.
Mkuu, kuna mashamba ya kulima mbogamboga mm nahitaji
Pia naomba namba Zako
iPhone 6s
Habari mtoa mada.Mie nipo Mapinga bagamoyo nipo interested na kilimo hicho cha umwagiliaji na mara nyingi nimekuwa nikijiuliza namna ya kupata shamba mto Ruvu.Hofu yangu kubwa imekuwa ni utapeli wa watu wa bagamoyo maana vilio vya waliotapeliwa ni vingi.Je naweza kupata shamba la umwagiliaji msimu huu lengo langu ni mahindi niuze mabichi kabla ya Dec.
Mkuu mavuno gunia ngapi wastani kama umefata taratibu vizuri na return inakuaje baada ya kuuza pia kuna gharama zingine zozote nje ya iyo 442,000 adi kuvuna?....100,000 ni malipo ya maji utakayokuwa unawekewa kwenye mpunga mpaka utakapovuna.
342,000; kuna pesa ya kujiunga na uanachama,kuna mshahara wa wanaowaita watermen(wana kazi ya kufungulia maji mashamba yote na kukagua ampapo hayafiki na kurekebisha,kama ni mifereji mikubwa).Kuna pesa ya vibarua wanaofyeka nyasi kwenye mifereji mikubwa ya chama na kuisafisha.
Humo kuna pesa ya kulipa wanaochabanga,na kupiga halow(kusawazisha udongo na kuuweka level ili maji yakiachiwa yawe level moja).
Kwa kule zinaitwa heka,lakini siyo size ya heka unayojua wewe,zinakuwa ni blocks.Kwa hiyo unakuwa na shamba la ukubwa wa 80*50m limekatwa vipande viwili ndo wanavyoviita heka.
Unakodi kwa mwaka mmoja tu.Ila,kama we ni mwanachama,mwaka ujao hutolila hiyo 442,000 tena.
Mashamba kama utachukuwa kama mwanachama,kila jina linapewa tu shamba moja.Kwa hiyo kama unajiweza,majina mengine utatumia ya familia yako,na kila jina utalilipia hiyo 442,000.
Vinginevyo ukimpata mwanachama muaminifu unaweza kulima kwa jina lake.
Kumbuka,ni kilimo cha umwagiliaji.Hivyo,ka eneo kadogo,mavuno mengi.Ukiweza kulihudumia,hilo unaweza kuvuna sawa na aliyelima acre 3 nje. Mhimu dawa,mbolea,usimamizi na maji
Inategemea na ulipo wewe. Ila Ubungo-Ruvu ni kama 69 -70Km +4km kwenda mashambani
Naomba namba yako mkuu.Panda gari za Mbezi(Mbezi ya Kimara),ukifika Mbezi kuna gari za kwenda Mlandizi.Ukifika nipigie
Naomba namba yako mkuu.
Post sent using JamiiForums mobile app
Mkuu mavuno gunia ngapi wastani kama umefata taratibu vizuri na return inakuaje baada ya kuuza pia kuna gharama zingine zozote nje ya iyo 442,000 adi kuvuna?....
Post sent using JamiiForums mobile app
Mkuu hayo maeneo ni CHAURU?
Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
Pia nilisikia kuna maghala ya kijiji sijui ni chama ukivuna unaweza kulipia na kutunza uko mpunga wako adi utakapo taka kuuza...ili limekaaje mkuu??Ni matunzo yako mkuu,ndo maana nikasema kama una hela ya kuungaunga boro ujipange.Ukihudumia shamba lako vizuri,unaweza pata hadi 80.Nasikia aliwahi kupata mtu 92.Ukihudumia vibaya,hukosi 20.Gharama nyingine zipo.Kuvuna,wanatumia machine,na siku hiyo hiyo unasafirisha mpunga wako. Kuvuna ni laki 3.Kutumia vibarua wa kawaida,itachukuwa mda na gharama zinatofautiana kama 50 elfu tu.Ila hawa itachukuwa hadi siku 3
Dunia imebadilika kila kona, hakuna uaminifu sasa lakini baadhi ya watu wa mkoa wa Pwani wengi sana hasa Maeneo ya Wilaya za Kibaha na Bagamoyo ni watapeli na hawaogopi kudhulumu mtu. Wanauza mashamba mara mbilimbili au ambayo sio ya kwao. Hawa watu hawataki kufanya kazi ila wanataka pesa ya kuongeza wanawake. Maeneo ya Ruvu kuna utapeli sana huwezi tuma pesa kwa mtu akafanya mlivyo ahidiana bila kupiga panga, hawajali kama huo mradi utakufa. Kama alivyosema mleta mada ukitaka kulima basi uende ukasimamie kuanzia siku unalima kwa trekta, kupanda, hadi unavuna. Ukisema utume pesa umeumia. Kilimo kinahitaji pesa na ufuatiliaji wa karibu sana.
Pia nilisikia kuna maghala ya kijiji sijui ni chama ukivuna unaweza kulipia na kutunza uko mpunga wako adi utakapo taka kuuza...ili limekaaje mkuu??
Post sent using JamiiForums mobile app