Mashamba ya kulima Ruvu

Mashamba ya kulima Ruvu

Ahsante mkuu. Namba ya ofisi?
Ngoja nikuangalizie,kuna uzi sawa na huu niliitoa sasa naona haupo tena.
Kama unahitaji shamba uje nikuuzie la kwangu,ila msimu ukiisha unarudisha huendelei
 
Ngoja nikuangalizie,kuna uzi sawa na huu niliitoa sasa naona haupo tena.
Kama unahitaji shamba uje nikuuzie la kwangu,ila msimu ukiisha unarudisha huendelei
Nina imani ulimaanisha umkodishie na siyo kumuzia... kwani hii sharti ya kurudisha shamba msimu ukisha isha wakati mtu ameshanunua itamkosesha usingizi na kufeli kabla hajaanza..
 
Mkuu CityHunter1 asante kwa taarifa ila naomba ufafanuzi kidogo kwenye hiyo shs 442,000 ni kwa ajili ya kukodi ekari moja au hekta moja? Na ni kwa msimu au kwa mwaka? Na maximum ni ekari/ hekta ngapi kwa mtu mmoja?
 
Nina imani ulimaanisha umkodishie na siyo kumuzia... kwani hii sharti ya kurudisha shamba msimu ukisha isha wakati mtu ameshanunua itamkosesha usingizi na kufeli kabla hajaanza..

Mashamba ya mpunga,ni ya chama,kwa hiyo mi nachompa ni mpunga, na akishavuna,ni msimu wa chama kuchukua mashamba,kuanza kuyalima na kuyagawa upya,kumbuka,inakuwa ni kwa mda wa mwaka.Huu sasa ni msimu wa mwisho
 
Ngoja nikuangalizie,kuna uzi sawa na huu niliitoa sasa naona haupo tena.
Kama unahitaji shamba uje nikuuzie la kwangu,ila msimu ukiisha unarudisha huendelei
sasa mkuu unauza unakodisha? Narudisha tena!!!!
 
Mkuu CityHunter1 asante kwa taarifa ila naomba ufafanuzi kidogo kwenye hiyo shs 442,000 ni kwa ajili ya kukodi ekari moja au hekta moja? Na ni kwa msimu au kwa mwaka? Na maximum ni ekari/ hekta ngapi kwa mtu mmoja?
100,000 ni malipo ya maji utakayokuwa unawekewa kwenye mpunga mpaka utakapovuna.

342,000; kuna pesa ya kujiunga na uanachama,kuna mshahara wa wanaowaita watermen(wana kazi ya kufungulia maji mashamba yote na kukagua ampapo hayafiki na kurekebisha,kama ni mifereji mikubwa).Kuna pesa ya vibarua wanaofyeka nyasi kwenye mifereji mikubwa ya chama na kuisafisha.
Humo kuna pesa ya kulipa wanaochabanga,na kupiga halow(kusawazisha udongo na kuuweka level ili maji yakiachiwa yawe level moja).

Kwa kule zinaitwa heka,lakini siyo size ya heka unayojua wewe,zinakuwa ni blocks.Kwa hiyo unakuwa na shamba la ukubwa wa 80*50m limekatwa vipande viwili ndo wanavyoviita heka.

Unakodi kwa mwaka mmoja tu.Ila,kama we ni mwanachama,mwaka ujao hutolila hiyo 442,000 tena.
Mashamba kama utachukuwa kama mwanachama,kila jina linapewa tu shamba moja.Kwa hiyo kama unajiweza,majina mengine utatumia ya familia yako,na kila jina utalilipia hiyo 442,000.
Vinginevyo ukimpata mwanachama muaminifu unaweza kulima kwa jina lake.

Kumbuka,ni kilimo cha umwagiliaji.Hivyo,ka eneo kadogo,mavuno mengi.Ukiweza kulihudumia,hilo unaweza kuvuna sawa na aliyelima acre 3 nje. Mhimu dawa,mbolea,usimamizi na maji
 
Mkuu CityHunter1 asante kwa taarifa ila naomba ufafanuzi kidogo kwenye hiyo shs 442,000 ni kwa ajili ya kukodi ekari moja au hekta moja? Na ni kwa msimu au kwa mwaka? Na maximum ni ekari/ hekta ngapi kwa mtu mmoja?

Nimetoa number za mwenyekiti pia,ni vyema ukajilidhisha maana gharama nyingine uaelezwa kabisa,kuchabanga kiasi furani,halow kiasi fulani, ila total itakuwa hio
 
Nilitapeliwa shamba huko aiseee yaani....

Ulikosea sana kukaa na hilo jambo kimya,ndo maana niliamua niwashilikishe wanaohitaji wawe makini.

Kuna mtu wangu wa karibu, kafika, ana mihela yake,kaona hili bonge la deal, kaona sijui siwezi mwambia kitu,kalipia mashamba 12,mwisho wa siku yoooote yana wenyewe,amebaki tu na mawili. Cha ajabu katuma hela 140,000 anunuliwe mbolea aina ya Super Gro,kapewa maji ya bombani kwenye chupa ya maji ya Kilimanjaro.

Kama unachukua kwa mtu,uliza kwanza majirani anaelima ni nani.Si anakuwa anafahamika?! Kule wajanja wengi
 
Ulikosea sana kukaa na hilo jambo kimya,ndo maana niliamua niwashilikishe wanaohitaji wawe makini.
Kuna mtu wangu wa karibu,kafika,ana mihela yake,kaona hili bonge la deal,kaona sijui siwezi mwambia kitu,kalipia mashamba 12,mwisho wa siku yoooote yana wenyewe,amebaki tu na mawili.Cha ajabu katuma hela 140,000 anunuliwe mbolea aina ya Super Gro,kapewa maji ya bombani kwenye chupa ya maji ya Kilimanjaro.

Kama unachukua kwa mtu,uliza kwanza majirani anaelima ni nani.Si anakuwa anafahamika?! Kule wajanja wengi
Nilinunua shamba kwa mtu, nikaenda mpaka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa tukaandikishana, kumbe shamba la mjeda kitambo, alipostaafu Kaja kulilima hapo ndipo nilipolia na kusaga meno, namuuliza mwenyekiti kwanini ulikubali kuandikisha lile shamba wakati unajua lina mtu, ooooh nilisahau maana jamaa kitambo hajalilima.

Ilibidi nimsweke ndani aliyeniuzia.
 
Nilinunua shamba kwa mtu, nikaenda mpaka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa tukaandikishana, kumbe shamba la mjeda kitambo, alipostaafu Kaja kulilima hapo ndipo nilipolia na kusaga meno, namuuliza mwenyekiti kwanini ulikubali kuandikisha lile shamba wakati unajua lina mtu, ooooh nilisahau maana jamaa kitambo hajalilima. Ilibidi nimsweke ndani aliyeniuzia.
Pole sana mkuu. Naona ulikua unataka ingia kwenye anga za mjeda hhaha! Vipi ulipata haki yako??
 
Ulikosea sana kukaa na hilo jambo kimya,ndo maana niliamua niwashilikishe wanaohitaji wawe makini.
Kuna mtu wangu wa karibu,kafika,ana mihela yake,kaona hili bonge la deal,kaona sijui siwezi mwambia kitu,kalipia mashamba 12,mwisho wa siku yoooote yana wenyewe,amebaki tu na mawili.Cha ajabu katuma hela 140,000 anunuliwe mbolea aina ya Super Gro,kapewa maji ya bombani kwenye chupa ya maji ya Kilimanjaro.

Kama unachukua kwa mtu,uliza kwanza majirani anaelima ni nani.Si anakuwa anafahamika?! Kule wajanja wengi
Mleta mada huko wanalima nyanya na cabbage??
 
Kwa kilimo cha mpunga, kukodisha mashamba mwisho ni mwezi gani?
 
Back
Top Bottom