Mashaka ya uraia na usalama wetu Tanzania, wageni wameingilia mchakato!

busar

JF-Expert Member
Dec 22, 2011
1,068
1,061
Nchi inaporomoka tena kwa kasi, kasi ya ajabu. Imeshaporomoka katika Elimu, Afya,, Kilimo, Ukusanyaji kodi, matumizi ya fedha iliyopo, na mengine mengi.

Hili la uraia ndo litaimaliza nchi yangu Tanzania Tanzania tuipendayo kwa moyo wote. Nimeshuhudia wahindi, waarabu, na weupe kadhaa wakialikana kutoka makwao kuja kujiandikisha kupata vyeti vya uraia. Hata kiswahili hawakijui..

Hii inatufikisha pabaya, tena pabaya.

Nchi Haina mwenyewe...

Napendekeza zoezi hili lifutwe.
 
Nimeshuhudia huku Kiwalani wapakistani na wahindi kibao wakijiandikisha, sijui serikali iko wapi!?
 
Nadhani sio kila kitu cha kulaumu serkali ama usalama wa taifa, katika mahojiano mengi yalofanyika na viongozi mbali mbali juu ya zoezi la kujiandikisha vitambulisho vya taifa walitoa tahadhari kuwa kuna raia watataka kujifanya ni wananchi na wapate hivo vitambulisho. Vigezo na masharti wameweka ni mengi mengine hadi ni kikwazo kwa sie wenyewe wananchi.

Pia tambua kuwa kuna vitambulisho vya wale ambao ni Watanzania na wale ambao sio watanzania na wanaishi hapa Tanzania (ikihusisha wahindi, waarabu, na wengine wengi kutoka nchi za majirani lakini ni wakazi wa Tanzania ambao pia wanapata vitambulisho vya taifa ila vikionesha wazi sio raia bali mgeni).

Sasa sababu wenzetu wana nidhamu sana katika sector ya vitu kama hivo (usalama na kujiandikisha mambo ya msingi) wao ni lazima wameipa kipaumbele kuliko hata sie wenyewe raia. Naamini kabisa kama wana ndugu yupo nje na mara kwa mara huishi hapa nchin hawaoni taabu kugharamia kurudi nchini kujiandikisha.

Na hata hivo umeshauriwa ukiona ukiritimba wowote unafanyika katika uandikishaji iwe reported.
 
Kwanini watu wa muundo huo wapewe vyeti vya uraia jamani?Au wanajiandikisha kama wakimbizi?Hii nchi inakera sana aisee!!
 
Mimi binafsi nashangazwa sana na mchakato mzima wa vitambulisho vya raia wa Tanzania na umuhimu wake, hasa kwa kuwa ni wiki chache tu kabla ya sensa. Ninasikia harufu ya ulaji mkubwa sana ambao unafichwa kupitia zoezi hili.

Sioni kwa nini watu wapange foleni kutwa nzima ili kujaza fomu ambazo baadaye watapatiwa vitambulisho, na huku mwezi huu huu wa nane kutakuwa na zoezi la kuwahesabu watu. Kwa nini kama suala la vitambulisho vya raia wa Tanzania lilikuwa/au ni muhimu, wahusika wa kuandikisha watu wasiwe walewale watakaopita kila nyumba kuhesabu watu? Hapo serikali itakuwa imeua ndege wawili kwa jiwe moja, na kero ya kupanga foleni na hatimaye kuambiwa rudi kalete barua ya mjumbe n.k vitaondoka.

Pili, kwa mtazamo wangu ni rahisi zaidi kujua nani ni raia na nani si raia kwenye kaya zetu. Ninaamini bado wajumbe wa nyumba kumi wapo, hata kama wanaitwa kwa jina lingine, sijui ndiyo wenyeviti wa serikali za mitaa. Hawa watu tunao mitaani mwetu, na ninavyoelewa wao wanawafahamu (au wanatakiwa kuwafahamu) vizuri watu wao. Wangewezeshwa wao kuwa na madaftari ya orodha ya kila mtu anayeishi kwenye mitaa yao.

Kila mtu aende kujiandikisha kwa mjumbe wake, akiwa na taarifa zake kamili. Mjumbe atafahamu mtu huyo anafanya kazi gani (ya kuajiriwa ama ya kujiajiri, ama mkulima n.k.), amezaliwa wapi, kama si mwenyeji wa eneo hilo basi anatokea wapi (mkoa gani au kijiji gani), umri wake, jinsia, ameoa/ameolewa, ana watoto wangapi, elimu yake, na ikibidi hata suala la imani (dini) ambalo limeleta kizungumkuti sana kwenye sensa litapatiwa ufumbuzi. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa anawajua watu wake, hata kama kuna mkimbizi kajichimbia katikati ya watu wa eneo lake atajulikana. Na kama kuna mhamiaji halali au asiye halali atajulikana.

Miaka ya mwanzoni mwa 80 kulikuwa na uhaba wa bidhaa mbalimbali nchini, tukawa na orodha za kaya ili kudhibiti upatikanaji wa bidhaa adimu kama sukari, unga, mchele n.k. Nakumbuka kabisa wenyeviti wa serikali za mitaa enzi hizo tukiwaita wajumbe wa nyumba kumi ndiyo waliopewa jukumu la kuandikisha watu. Zoezi lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuwa mjumbe alikuwa na orodha ya kila mkazi wa nyumba zilizo chini ya eneo lake. Tuliandikisha mpaka wafanyakazi wa majumbani. Nia ilikuwa mtu yeyote asife njaa, na chakula kipatikane kutosheleza idadi ya watu. Ilikuwa ukienda dukani kununua bidhaa unaenda na kitabu chako kinachoonyesha ukubwa wa kaya yako. Na ukipata mgeni ilikuwa lazima utoe taarifa kwa mjumbe ili ijulikane ya kuwa kaya imeongezeka ukubwa na idadi ya mahitaji yako pia imeongezeka. Nakumbuka kuna kaya kubwa zilikuwa zinaweza kupata kilo 3-4 za sukari kwa wiki, lakini kama kaya yako ni ndogo unapewa kilo mbili kwa wiki. Na orodha yote alikuwa nayo mjumbe wa nyumba kumi (mwenyekiti wa serikali ya mtaa)

Nimeurudia mfano huu kuonyesha ya kuwa 'system' ilikuwepo na bado ipo. Kama kweli nia ni kupata vitambulisho vya uraia ingeweza kufanyiwa kazi ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha na kuondoa mianya inayoweza kutumiwa na wajanja kupata vitambulisho ambavyo hawastahili. Vilevile hii ingepunguza kero na usumbufu uliojitokeza wa watu kupanga foleni kutwa nzima, kwa kuwa mjumbe angeweza kwenda majumbani mwa watu wake kwa nafasi zao na kupata taarifa zote.

Kwa huu utaratibu unaotumika sasa hivi zoezi zima ni mchezo wa kitoto.
 
Vitambulisho viingekuwa kwa Watanzania pekee, nahisi kuna ulaji ushaingia hapo.
 
Umewaza vizuri sana kwa hyo wakija kutuhesabu tunajaza na fomu na pia inasaidia kututambua kweli sisi ni Raia wa Tz ina maana wataongozana na afisa mmoja wa uhamiaji hii ingekuwa safi sana na kupunguxa gharama ... sasa changamoto ni kubeba mashine ya kupigia picha kila nyumba
 
Ni wazi kuwa kuna raia wengi wa nchi jirani hapa nchini. Kipindi cha uchaguzi nilikuwa maeneo ya Kimara DSM kuna mama alitiliwa mashaka uraia wake. Alipoulizwa mkoa atokapo akasema Kigoma. Shule ya msingi akasema amesahau. Kuhusu kujua wimbo wa Taifa akasema hajui. Hapo watu wakaanza kumzonga. Majirani wenzke akina mama na mjumbe wake wa nyumba 10 akaja na kusema kuwa yule mama ameolewa na mwanajeshi aliyetoka Kigoma kikazi.
Nilivyompima yule mama si raia kabisa lakini kwa ushahidi wa mjumbe na majirani aliruhusiwa kupiga kura huyu hakuwa na nia mbaya( labda) ya kuwa ndani ya Tanzania.
Hii inanipa picha kuwa je ni wangapi wapo hapa Tz na ni ngumu kujua motives zao kwa haraka.
( sleeper agents)
 
Nchi inaporomoka tena kwa kasi, kasi ya ajabu. Imeshaporomoka katika Elimu, Afya,, Kilimo, Ukusanyaji kodi, matumizi ya fedha iliyopo, na mengine mengi.

Hili la uraia ndo litaimaliza nchi yangu Tanzania Tanzania tuipendayo kwa moyo wote. Nimeshuhudia wahindi, waarabu, na weupe kadhaa wakialikana kutoka makwao kuja kujiandikisha kupata vyeti vya uraia. Hata kiswahili hawakijui..

Hii inatufikisha pabaya, tena pabaya.

Nchi Haina mwenyewe...

Napendekeza zoezi hili lifutwe.

Maoni yako yaheshimiwe. Nadhani pia uwekwe utaratibu wa kuwapa mafunzo wageni hawa juu ya utaifa wa Kitanzania, wa Kiafrika na yanayohusika. Kujua Kiswahili iwe ni moja ya masharti. Wageni wafundishwe utamaduni wa Kitanzania na mila na desturi zinazohusika. Wapewe "semina elekezi" ya kutosha kwa kipindi kirefu ndipo wapewe uraia. Wafundishwe historia yetu. Waelimishwe juu ya "Ujamaa" ama "ubuntu" yaani "utu" katika falsafa na uelewa wa kiafrika. Nchi nyingine wanafanya hivyo kulingana na mazingira yao. Kwa mfano nani anaweza kusema yule Bwana maarufu sana katika uandishi - alifundisha Milambo, Mzumbe, Changombe na Chuo Kikuu DSM - kuwa si mzungu wa Ulaya kwa asili. Yule Bwana ameukubali Uafrika ingawa yeye si Mwafrika kwa kuzaliwa na utaifa. Kuna siku rafiki yangu mmoja alikuwa katika mji fulani hapa Afrika alipoishi kikazi huyu Bwana ninayemsema; waliomfahamu wakamwambia kuna Mtanzania hapa. Maana pote alipoenda alijitambulisha yeye ni Mtanzania. Akapewa simu akaongea naye bila kujua kuwa mgeni huyo alikuwa mwanafunzi wake Milambo Sekondari zamani. Pale pale akamkaribisha kwake mtaani kula chakula. Mtanzania kabisa. Huyo ndiyo raia wa Tanzania anawapenda watanzania, anawakubali, anawaheshimu. Wakaribishwe lakini wapewe utaratibu ili wauthamini uraia ule waliopewa. Wafundishwe kuimba wimbo wa Taifa na mambo mengine.
 
Ni wazi kuwa kuna raia wengi wa nchi jirani hapa nchini. Kipindi cha uchaguzi nilikuwa maeneo ya Kimara DSM kuna mama alitiliwa mashaka uraia wake. Alipoulizwa mkoa atokapo akasema Kigoma. Shule ya msingi akasema amesahau. Kuhusu kujua wimbo wa Taifa akasema hajui. Hapo watu wakaanza kumzonga. Majirani wenzke akina mama na mjumbe wake wa nyumba 10 akaja na kusema kuwa yule mama ameolewa na mwanajeshi aliyetoka Kigoma kikazi.
Nilivyompima yule mama si raia kabisa lakini kwa ushahidi wa mjumbe na majirani aliruhusiwa kupiga kura huyu hakuwa na nia mbaya( labda) ya kuwa ndani ya Tanzania.
Hii inanipa picha kuwa je ni wangapi wapo hapa Tz na ni ngumu kujua motives zao kwa haraka.
( sleeper agents)
Mkuu wapo wengi, hata huyo mwanamke anaweza kuwa ni agent bila kujali ameolewa na nani.
 
Mkuu wapo wengi, hata huyo mwanamke anaweza kuwa ni agent bila kujali ameolewa na nani.
Mkuu nilibishana sana na nafsi yangu kuhusu yule mama tena hilo swali la wimbo wa Taifa nilimuuliza mimi. Alishindwa hata kujua unafananaje lakini umma ulinushinda kuwa pengine nina nia ya kunyima kura upande fulani.
 
Mkuu nilibishana sana na nafsi yangu kuhusu yule mama tena hilo swali la wimbo wa Taifa nilimuuliza mimi. Alishindwa hata kujua unafananaje lakini umma ulinushinda kuwa pengine nina nia ya kunyima kura upande fulani.
Wasiliana na idara ya uhamiaji. Hao watu wa pembezoni mwa nchi sio wa kuwaamini kabisa.
 
Nchi inaporomoka tena kwa kasi, kasi ya ajabu. Imeshaporomoka katika Elimu, Afya,, Kilimo, Ukusanyaji kodi, matumizi ya fedha iliyopo, na mengine mengi.

Hili la uraia ndo litaimaliza nchi yangu Tanzania Tanzania tuipendayo kwa moyo wote. Nimeshuhudia wahindi, waarabu, na weupe kadhaa wakialikana kutoka makwao kuja kujiandikisha kupata vyeti vya uraia. Hata kiswahili hawakijui..

Hii inatufikisha pabaya, tena pabaya.

Nchi Haina mwenyewe...

Napendekeza zoezi hili lifutwe.
Hapa si kama unavyodhan watapata hicho kitambulisho maana kuna process ndefu ya kufanya. I nimebahatika kuandikisha hivi vitambulisho na bado naendelea kuandikisha coz wote wenye asili ya nje watapewa kulingana na sifa zao ie kwa fom kuna aina za uraia hope kwa waliobahatika kwenda nje wanajua, kuna uraia wa kuzaliwa, kurithi na kujiandikisha. Pia kuna aina za vitambulisho so huwedh sema raia wagen watapatiwa kirahisi hivyo kama unavyodhan coz hata baada ya kupiga picha kuna kitu kinaitwa mapingamizi ni stage ya 3 baada ya kupiga picha na kujaza fomu coz picha zote zitawekwa katika kila wilaya na kata ili watu wapate kutoa mapingamizi kwa raia ambaye anamtilia shaka. I.e wenye viti wa vijiji na vitongoji ndio wa kwanza kujua watu wake coz lazma athibitishe. So ww ukidhan wagen watapita kirahc hvyo utafel maana mtu wa asili ya nje lazima achunguzwe kwanza. Hivi si kama vya kupigia kura ndio maana unaambiwa wait mpaka miezi mitatu ndo utapata na si kienyeji hivyo
 
Back
Top Bottom