Mashairi ya Prof. Jay na hali halisi

Tee Bag

JF-Expert Member
Dec 21, 2013
7,200
5,553
Sijui [HASHTAG]#Professor[/HASHTAG] Jay aliwaza nini wakati anatunga mashairi ya wimbo NANG'ATUKA. Hebu msikilize just kwenye verse one then compare na hali ilivyo kwa sasa.
________________
Verse 1:

Muda sasa umewadia ndugu zangu watanzania,

Mambo niliyoyafanya hayapaswi kusimuliwa,

Tangu nilipoomba kura kwenye Ndio Mzee!

Mkanipa na kusababisha Uchumi Ulegee,

Kura zikawa kula nikaiba kwa milungula,

Taratibu nikaanza kubadili mfumo na sura,

Nasisitiza sana maswala ya ajira,

Kumbe uongo, nikaanza kugawa vyeo kwa ukabila,

Hata washauri wangu niliweka mataahira,

Na kusababisha uongozi wangu kupoteza dira,

Nikaona bora uongozi na si uongozi bora,

Na kila aliyenizidi kwa mali nilimpora,

Mambo yote muhimu niliweka ya mwisho,

Na kuwa muumini mzuri wa Mauaji na Vitisho,

Mtu asiyeshindwa katika jambo lolote,

Daima nitapata chochote katika muda wowote.

Malisa GJ

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom