Kipimo cha kumtambua msomi mpumbavu; msomi mpumbavu huwa anasifia mambo yanayotendwa na kiongozi kwa utashi wake binafsi badala ya kusifia au kuboresha mfumo yakinifu.Maana kiongozi hawezi kuwa madarakani milele,hivyo basi atakapoondoka kiongozi ambaye ulimuona ni mzuri halafu akaja mwingine ambaye naye akaamua kuongoza kwa utashi wake kama vile utashi wa kifisadi,kwakweli hali itakuwa mbaya sana.Hivyo basi msomi asiyempumbavu kamwe hawezi kukesha na kusifia utendaji binafsi wa mtu,bali atajadili namna nzuri ya kuendeleza nchi kwakuangalia dira ya taifa ambayo haitavunjwa na kiongozi yeyote.