Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
MASACHE KASAKA ASHINDA KWA KURA 5,572 JIMBO LA LUPA, CHUNYA
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Lupa, Masache Njelu Kasaka ameibuka kidedea kwenye kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Lupa akipata kura 5,572 huku akiwaacha mbali washindani wake.
Masache amepata ushindi huo dhidi ya washindani wake watatu akiwamo Noel Ntangu aliyepata kura 2,821, Geoffrey Mwankenja (2,115) na Sarah Sampo (143).
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Chunya, Charles Jockel ameeleza kwamba uchaguzi huo umekwenda vizuri katika Kata zote 10 zilizopo katika jimbo hilo.