Masaa 168 ya Anita

Masaa 168 ya Anita

manyanga21

Senior Member
Joined
Aug 15, 2018
Posts
173
Reaction score
211
Dar es salaam ,

Katika jiji la dar es salaam uwezi kuwataja wanawake uwezo kipesa ukamkosa kumtaja veronica butimba kutokana na kujitolea kwake kusaidia jamii hasa watu wasio jiweza utajiri aliokuwa nao wengi walimtabilia baada ya miaka kadhaa atakuwa miungoni mwa mabilionea wanawake wenye umri mdogo Afrika mashariki na uwenda hata Afrika mzima

Hakulizika nasifa pamoja na mafanikio aliyokuwa nayo alizidi kujibidiisha katika biashara akiwa kama mmiliki wa kampuni ijulikanayo Tanzania Pure oil distribution ltd kampuni inayojiusisha na usambazaji wa mafuta

Saa iliyonashiwa kwa madini ya Tanzania iliyomka vyema mkononi ilionyesha ni saa tano na nusu baada ya kuitazama saa alipiga miyayo akainuka kwenye kiti alichokalia akachukuwa mkoba wake kwa mwendo wa madaha japokuwa apakuwa na mtu aliyemuona bado akusita kutembelea ule mwendo ambao ungemvutia kila mtu aliyemwona hadi alipofika maegeshoni alimkuta dereva wake na katibu mukta kwa pamoja wakaingia kwenye gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani kwake masaki akitokea posta maali iliyopo ofisini yake richa ya kuwa na uchomvu kwa shughuli za mchana kutwa akuweza kusinzia alitazama uzuri wa bahari uliopambwa na meli zilizokuwa zimetia nanga kando kando ya bandari kusubilia foleni ya upakuwaji wa mizigo mara nyingi akupenda aendeswe kwa mwendo wa kasi alipenda kuendeswa kwa mwendo wa kawaida wakiwa katika daraja la salenda aliona mtu amesimama katika ukingo wa daraja alionekana alikuwa anataka kujitosa majini bila kujiuliza uwamuzi wake akamlisha dereva

simamamisha gari haraka
Dereva alipunguza mwendo kidogo kisha akasimamisha gari pembezoni mwa barabara veronica akashuka ndani ya gari na kuwanza kukimbilia sehemu aliyokuwa Yule mtu aliyemuona amesimama pembezoni mwa daraja hawakumuacha mbali sana ni mwendo wa hatua 30

Hatuwa zilizopigwa haraka richa ya kuvaa viatu virefu vilivyo julikana kama higheels ule uzoefu wake wa kuvitumia viatu ivyo ulimsaidia kumfikia mtu uyo aliyejilusha punde tu alipofikiwa na veronica aliyekuwa akipigiwa makelele na katibu mukta wake pamoja na dereva wote waliisi bosi wao amechanganyikiwa hivyo walishuka ndani ya gari wakitaka kumsaidia hawakumfikia veronica alivuwa viatu na kujilusha ndani ya maji hakujali mavazi yake ya thamani aliyokuwa amevaa richa ya kuwa mrembo mwenye utajiri pia alikuwa mwogeleaji mzuri sana punde alijitosa alizamia kuanza kumtafuta mtu uyo aliyejitosa eneo hilo dereva na katibu mukta Walipofika hawakuweza kuona chochote zaidi ya mawimbi yaliyokuwa yakigonga katika kingo za dalaja wakiwa bado wanatafakari wafanyaje maji nayo yalizidi kujaa wingi wa maji haukumzuiya veronica ashindwe kumpata mtu aliyejitosa baada ya kutafuta kwa dakika kadhaa hatimaye alimfanikiwa kutokana na ule mwanga wa mbaramwezi ulioweza kupenya vizuri hadi ndani ya maji alimshika mtu aliyejitosa na kutoka naye inje ya maji yalionekana kumzidi nguvu hilo alilitambuwa akazidi kujitaidi jitiada ambazo zilizaa matunda alifikia inchi kavu katika kingo za daraja mtu aliyemwokoa alikuwa kimya

veronica alisiliza mapigo ya moyo akagunduwa bado anapumua ndipo alipoanza kusukuma sehemu za tumbo ili aweze kutupia maji alifanya kwa dakika kadhaa pasipo mafanikio akajalibu tena haikusaidia akamuwa kumpulizia punzi mdomoni kisha akaendelea kupiga tena sehemu za kifua ndipo mtu alianza kukohowa kwa sauti iyo iliyomfanya veronica ajuwe kuwa mtuuyo alikuwa ni mwanaume dereva na secretaly nao waliisikia haraka wote walishuka chini ya daraja ilo wakashuka kumkuta velonica amejilaza pembezoni mwa mvulana aliyekuwa hawamtambui kisula kutokana na giza veronica alipowaona akainuka akamtazama yule kijana aliyekuwa anaendelea kuyatapika maji akamalizia kumtazama dereva wake aliyekuwa ameshika simu iliyo msaidia kwa torch
[ICODE]mbebe mpeleke kwenye gari dereva na katibu wake walikuwa bado wanashanga hamsikii au nimbebe mimwenyewe alisema kwa sauti ya kali uku akiwa anaongoza kutoka sehemu iyo dereva alimbeba kijana uyo hadi kwenye gari wote walipangia Diana mpigie simu DR jackson aje nymbani [/ICODE]`

Diana alipiga simu na kufanya kama alivyoamuliswa safari hii alimwambia dereva aongeze mwendo kidogo walipofika hakutaka kuongea na mtu yoyote akatelemka akiwa bado anachluzika maji na kumfungulia mlango wakambeba mgonjwa akisaidiana na Diana hadi katika moja ya chumba cha wageni akamlaza DR Jackson akuchukuwa mda alifika akamfanyia vipimo na kumkuta yupo salama kabisa isipokuwa alionekana amegubikwa na wimbi la mawazo na kushauli apewe muda wa kupunzika velonica akisaidiana na msaidizi wake wakampeleka kwenye chumba cha wageni maarufu

Asubuhi iliyofata
Sizani kama hii ni namna sahihi ya kusimulia simulizi , ngoja kwanza mimi si mwongeaji sana huwa naongea pale inapobidi tuu ninayowaza ni kumbukumbu ya machache kati ya mengi ninayo yakumbuka nisikuchoshe ipo hivi Jana nilikuwa kwenye moja ya baa sijui night club vyovyote utakavyoita sawa tuu haina maana kama hiki ninachokikumbuka navuma sana maeneo ya sinza sikumbuki jina nilipokuwa apo baa nilikunywa pombe nyingi sana na kula pia sikushuhulika na chochote muda wote niliokuwepo baa Zaidi ya kunywa pombe na kula ilikuwa mala yangu ya kwanza kufywa pombe kwa namna nilivyokuwa nakunywa laiti ungeniona ungezani ni mbobezi haswa

Jana kama nakumbuka vyema na si askili ya pombe nilitoka iringa na kuacha kila kitu changu nikaondoka kilichonisaidia ni kiasi cha pesa nilichokuwa nacho mfukoni shilingi million moja na laki tatu ndio pesa niliotumia kwenye nauli na kununulia pombe na chakula nilipokuwa baa ambayo siijui jina

Hivyo tu ninavyokumbuka toka usiku wa jana hamna kingine nimejitaidi kukumbuka kumbu kumbu zimegoma kabisa lakini hayo yanafaida gani,sidhani kama yanausiano au umuimu wowote

Nilijigeuza upande mwingine wa kitanda na kuendelea kulala sikujali nipo wapi wala saangap nilichoitaji mimi nilale tuu hata ikiwezekana milele kuepuka walimwengu na fujo zao sikujuwa ni kipi kilichonikatisha usingizi wangu mpaka nikawaza yale ya jana nilipuzia na kuludi kwenye jitihada zangu za kuutafuta usingizi punde zikakatiswa kiukatili na sauti ya mwanadada aliyeniamsha
Kabla uyo aliyeniamsha sijamtazama nikawanimesha mjuwa atakuwa ni Rose katibu mukta wangu amefikaje dar es salaam wakati nilimwacha iringa akuna mtu anayeweza kuniamsha kwa pupa Zaidi ya mpuuzi huyu
 
Nimekaa siti ya mbeleeee kabisaaaaaa, lkn siti ya upande wa kuume kwangu haina mtu nasubilia aje tupige soga tukisubili ukurasa wa pili ukuje.
 
Masaa 168 ya Anita
Haki ya mungu nachukia sana ninapolala alafu mtu aniamshe pasipokuwa na swala la muimu kabla sijaendelea nadhani kuna haja ya kujitambulisha nadhani ushanijuwa acha niachane nalo halina umuimu sana Zaidi yaliyonikuta naitwa Edward vicent maguli ndio jina langu rasmi wengi upendelea kuniita mr brain kutokana na umakini wangu wa kumbapanuwa mambo na kutoishiwa na suluhisho kwenye jambo lolote hahahaha mpumbavu mmoja amenizidi akili kizembe na kufanya alichotaka kunifanyia kiwepesi na kupotelea pasipojulikana nina miaka 32 ninamiliki kampuni ya EGC Edward Group company inayojiushisha na uzaaji na usambazaji wa mbao ,mboga mboga inje ya nchi pamoja na iringa television unapo wataja vijana wanao jiweza kipesa utoweza kuliacha jina langu hata kwa makusudi wengi wananitabilia kuwa tajiri mkubwa apo baadae kutokana na ukuwaji wa kasi kwa biashara zangu cha kusikitisha ni kwamba sitoweza tena kufikia ndoto izo za kuwa tajiri mkubwa baadae hapa ninavyozungumza sina hata shilingi mia moja na sijui nipo sehemu gani nahisi walikuwa wanajidanganya tuu kunitabilia mafanikio makuwa wamesahau kuwa ng`ombe wa masikini hazai tuwachane naya walimwengu tuendele na utambulisho
Mimi ni mkazi wa iringa mjini maneo ya gangilonga sina mke isipokuwa mchumba ambaye sasa sipo nae tena na sijui ameenda wapi kwani mala ya mwisho nikuwasiliana nae nilipokuwa south Africa si kwamba sijampigia hapana nilimpigia Zaidi ya mala kumi akupatikana niliporudi Tanzania nikamtafuta kila sehemu sikumpata
Sisiti kusema kilichonikuta uwenda yakawa malipo ya kutofata busala za wazazi waliponichagulia mchumba wa kuowa nilikata kata kata kumwowa msichana walie nichagulia ni maswala ya kizamani na kuwapa sababu tela zilizokuwa na mashiko na zile ambazo hazikuwa na mashiko si kwamba umri haujafika hapana nina miaka 32 pengine nilifikilia Anita ndiye mwanamke sahihi kwangu au basi niseme nilipenda kujichelewesha kuowa ili niweze kufanya maamuzi sahihi juu ya kumwowa Anita ila hiyo sababu ya kwanza ndiyo yenye mantiki Zaidi
Kwa upande wa kazi mimi ndiye mmiliki wa kampuni ya EGC kiufupi kifedha najiweza sina haja ya kukwambia ninakiasi gani cha pesa bank account zangu zote tatu balance zinasoma sh o roho inuma sana kutoka kumiliki mamilioni ya pesa hadi shilingi sifuri nimebakiwa na madeni tuu kutoka sehemu mbalimbali si hivyo kwa sasa similiki chochote mali zangu zote zimeuzwa katika mazingira ya kutatanisha, ni kazi iliyofanyika ndani ya masaa 168 sawa na wiki moja tuu kutoka kumiliki mamilioni ya pesa hadi kufirisika kutomiliki chochote Zaidi ya nguo nilizovaa tuu yule mpuuzi haswa ameuza hadi nguo zangu jamani
Nadhani utambulisho huo unatosha mengine utayajua kadri nikusimulipo mkasa ulionikuta na kunifanya niamini kuna muda mwanamke anaweza kuwa mfalme kitu ambacho nilikikata maisha yangu yote
Tukiwa tumetoka Tanzania uwanja wa Ndege wa J K NYERERE INTERNATIONAL AIR PORT siku ya juma nne mchana kuelekea Berlin ujerumani safari iliyochukuwa masaa kumi nanne na dakika ishirini na saba sekunde arobaini kwa ajiri ya maajabu ya kijographia tulifika Berlini asubuhi siku iyo iyo ya jumanne na ndio juma nne iyoiyo mchana tulitoka Tanzania
Usishangae tusipotezane hapa maana kuna mengi ya kuchanganya na kushangaza huko mbele nitakueleza kiufupi ,dunia huzunguka toka magharibi kwenda mashariki hivyo basi upande wa mashriki uwai kuliona jua na upande wa magharibi wanachelewa kuliona jua hivyo ukiwa Tanzania unatangulia kuliona jua kabla ya berlini na tunapishana masaa kumi na tisa sisi tupo mbele kimasa na unakuta Tanzania ni juma tatu wenzetu ujerumani jumapili ,hadhani apo tupo pamoja ngoja nielendelee
Ziala yangu ya kibiashara ilienda vizuri kabisa na muda wote nilikuwa nikiwasiliana na mpenzi wangu Anita pamoja na familia yangu pasipo kusahau marafiki haito kuwa vizuri kuanza kusimulia yaliyonisibu pasipo kueleza wasifu wa huyu mpuuzi Anita alikuwa msichana mremo mno alivutia alikuwa na asili ya Zanzibar mweupe macho ya goroli na kila alipokuwa akicheka ama kutabasamu ilikuwa ni rahisi sana kuviona vishimo vidogo mashavuni mwake
Akuhishia apo sura ya kitoto mrefukiasi nyuma amejazia wastani ile shape ya kuvalia kanga na watu wakamtazama Anita alikuwa ananywele nyeusi ndefu zilizofika kiunoni kwake matiti yaliyosimama mfanano na mchongoma kiuno chake chembamba kama kinu kilihitimisha mwonekano halisi wa mwanamke mrembo kila aliyemuona Anita akusita kumpa sifa zake mwanahalamu huyu
Nilimpenda kupita kitu chochote hapa duniani sitaji hata kuendelea ila mengi nayakumbuka
``maumivu ya kichwa pamoja na sauti ya mwanamke aliyomwamsha ilinifanya niamke na kukaa kitandani nikapokelewa na sura nzuri yenye tabasamu velonica alikuwa ameniamsha na kumpa kifunguwa kinywa
`jana ulilewa sana nimekuwandalia supu kunywa ukate makali ya pombe `sauti yake tuu iliweza kunishawishi kuinywa supu uku nikimtazama kiwizi wizi mrembo huyu naye akusita kunitazama kwa nikubia sujui tulikuwa tunaogopana kwa lipi
nilipomaliza kunywa supu akanielekeza nguo alizonindalia za kuvaa na kuniambia nipige namba Fulani nitakapo maliza kujianda nilifanya kama alivyonielekeza baada ya kuoga na kuvaa nikapiga namba alizonitajia haikupita muda mrembo akanifata tuliongozana wote hadi kwenye meza iliyojaa vyakula anikalibisha muda wote sikuweza kumjuwa wala yeye akunijuwa baada ya kuanza kula ndipo tulipoelekea kwenye bustani nzuri iliyokuwa na kila aina ya mauwa harufu nzuri iliyowavutia vipepeo mbalimbali kuwepo bustanini apo upepo mwanana wa bahari ulitupuliza ipasavyo
Na kunifanya niweze kukumbuka kila kitu hadi wasiwasi ukaningia nikamtazama mrembo aliyepo pembeni yangu
`naitwa Edward vicent maguli`nilijitambulisha pasipo hata kuulizwa sijui mwenzangu unaitwa nani
naitwa velonica butimba
Edward kimekusibu nini hadi jana ukataka kujiuwa
Swali la velonica likanifanya nikumbuke siku ambayo sitaji hata ibakie kwenye kumbukumbu yangu ya kichwa kama ningepata nafasi basi hii siku ningeiluka au ninge ifuta kwenye kichwa changu
Nakumbuka tulifika dar es salaam kutoka berlini ujerumani nikapanda ndege iliyonipeleka iringa kitu cha kwanza ni kuwaza namna gani naweza kulekebisha simu yangu iliyokuwa inasumbuwa mtandao ikawa bahati nafika mtandao ukaka sawa ndipo nilipo kodi tax iliyonipeleka hadi nyumbani sikuwamini nyumba ilikuwa imeuzwa kiasi chake nikachanganyikiwa kwa kuwaoji walionunuwa wakasema wameuziwa na mmiliki wa nyumba ile kila nilipopiga simu ya anita haikupatikana tangu nilipokuwa south Africa simu ya anita haipatikani nikaona isiwe shida niende kazini kwake
Nilifika na nilichoambulia bora nisinge enda tuu wafanyakazi wenzake walishangaa kuonekana wakati wote wanafahamu mimi na Anita tupo marekani tukiyanza maisha mapya nikapata ukakasi kidogo nilimvuta pembeni mmoja wa wafanyakazi wa ofisi iliyokuwa inamilikiwa na anita wangu
`shemeji mbona unashangaa ivyo si juzi tuu wewe na anita mlikuja kutuwaga mkasema mnaama inchi mnaenda kuishi marekani mlikuja pamoja na mtu wa kuununuwa huu mgahawa mkafanya makabidhiano mbele yetu
Unawesa mimi kabisa nilikuwa na anita tumeuza mgahawa
ndio shemeji
Sikutegemea kama anita angeweza kunifanyia jambo la ajabu kama hili ``nilisema pasipokujali kama nazungumza peke yangu ninachoshanga ni kwamba toka nimekuwa nae katika mhusiano hajawai kuonyesha dalili zozote za kuwa na tamaa ya pesa kila anachokifanya amekuwa ananieleza nashangaa katika hili sijui akili amezipata wapi
Sikuwamini kilichotokea kimenifanya nichanganyikiwe natamani nife ndani ya wiki tatu tuu nimepoteza mamilioni ya pesa nimekuwa maskini nitakuwa mgeni wa nani mimi machozi yalimtoka akajifuta na kuchukuwa glass ya mvinyo nikanywa funda moja na kujiweka sawa
Nilihisi kama tamthilia nikaendelea kupiga simu ya anita haipatikani akili ikataka niende kwao sikutaka kutumia gari pikipiki ilinitosha kunifikisha mapema sana nyumbani kwa kina anita napo nikakuta majabu ya mwaka nyumba haikuwa na watu ilifungwa kabisa kama kwamba akuishi watu nilipoulizia majilani wakanipa jibu familia iyo iliondoka siku tatu zilizopita na kuwaag wanaenda Canada ambapo mzee joshuwa ameamiswa kikazi
velonica alichukuwa simu yake na kubonyeza namba furani kisha akasikiliza muito wa simu upande wa pili naomba uniwakilishe kwenye vikao vyangu vyote nimepata safari ya dharula nasafiri ndani ya wiki nitareje``
Nisubili nakuja`` velonica akaondoko bustanini haikupita muda aliludi akiwa ameshika begi na mkoba twende mjini tukafanye shopping ndogo kuna sehemu nataka unisindikize
tukaongozana hadi kwenye megesho na kuchukuwa gari iliyotupeleka uwanja wa ndege na kuchukuwa ndege iliyotusafirisha hadi Zanzibar taratibu za kuweka oda ya hotel ilishafanyika wakati tupo njiani
Saa nane mchana wakapata chakula cha mchana kwa pamoja kisha kila mtu akaelekea kwenye chumba chake kupunzika....itaendelea
 
velonica naomba nipe kazi yoyote nina degree ya ugavi pia nina uzoefu wa kuendesha biashara pia nina dipoloma ya negotiation ``kisha nikampa vyeti vyangu
inamana kampuni uliyanzisha mwenyewe
ndio nilinzisha mwenyewe hadi kufika pale ni juhudi zangu binafsi
Basi sawa nitalifanyia kazi swala lako siku mbili hizi utaanza kazi leo unaonje twende wote kazini na mizinguko mengine haikuwa kazi ngumu kwangu nilikubaliana nae na
tukaongozana hadi kazini ofisini kitendo cha velonica kuongozana na Edwin wengi kiliwashangaza kwakuwa bossi wao akuwai kuonekana yupo karibu sana na mwanume yoyote ni mara chache sana aliambatana na kaka yake Tom au baba yake anapokuwa anaudhulia mialiko ya shuhuli mbalimbali ucheshi niliokuwa nao ulipelekea wafanyakazi wengi wanipende kwa muda mfupi niliotambuliswa kila mtu alivutiwa name baada ya matembezi ya kiofisi na kuka kikao vya bodi tulipomaliza tukamuwa tuelekea ufukweni
tukiwa ufukweni ndipo nilipoanza kumsimulia maisha niliyopitia na mpenzi wangu Anita
Moyoni nilisha apa nitakufa na siri yangu kutowambia mtu yoyote juu yanayonisibu kama ukituona inje mimi na Anita utatuona tunapendana sana ni kweli mimi nilimpenda sana Anita upendo wangu kwake ndio ikawa siraha ya kunifanya atakavyo mambo aliyokuwa ananifanyia Anita yalikuwa ya kuniumiza
Mara ya kwanza nilikutana na Anita kanisahani kutokana kuwa muumini mzuri kanisahani nikamini ndio mke mwema nikatokea kumpenda sana nikaanza taratibu za kumwowa akaomba anijuwe vizuri kabla ajaamuwa rasmi kufunga ndowa nikaona jambo jema basi akaja kuishi nami nyumbani
Ulipita mwaka kila nikimuliza tufunge ndoa akawa anasema nimpe muda nami siku na halaka nae kadri siku zilivyokuwa zinaenda ndipo akaanza kubadilika
akaanza tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani kila mara atokapo kazini ukimuliza akunipa sababu ya msingi ilo nikalivumili labla nikazani nafanya kazi kwa juhudi sana nilimsifu sikusita kumpongeza kwa kumpa zawadi
Baadhi ya marafiki zangu waliambia kuusu tabia ya mchumba wangu kuonekana na mwanaume mwenye asili ya kiarabu akuna aliyemfahamu Zaidi wanamausiano gani kwa muda uwo niliyachaguwa mapenzi na nilivyomuwanimi Anita sikuweza hata kumwihisi vibaya
Hadi siku aliporudi nyumbani na gari ambalo hakuwa analitumia nilipomuliza amelipata wapi akaniambia ni la rafiki yake janet sikutilia maanani
Msiku yakazidi kukata mbuga na maisha yangu ya mausiano hayakuwa na afueni akaniomba ruksa ya kwenda kuwatembelea wazizi wake uko atakaa wiki mzima kuna siku alipitiliza pasipokuwa na mawasiliano yoyote ndipo nilipoenda kwa wazazi wake sikumkuta na hata wao walilalamika Anita apatikaniki kwenye simu
Nikiwa narudi nyumbani nikapoke simu kutoka kwa rafiki yangu amemwona Anita Mombasa akiwa na mwanaume na picha kanitumia sikuwamini nikaona ishiwe kesi nikasafaili usiku uwo uwo hadi Mombasa nakumbuka nilifika jioni rafiki yangu alinipokea uwanja wa ndege kisha akanipeleka hotel aliyopo Anita na mpenzi wake
Tulikaa mgahawani wa pembeni kusubilia yakapita kama masaa mwili nikanza kumlumu kaitani kwa kunipotezea muda `umemfananisha Anita wangu awezi kufanya ivyo`nilimlaumu sana
Mungu si asumani mara Anita na mvulana mwarabu walitoka kwenye hotel gari mbili zilisimama wakapanda welinzi walipanda kwenye gari nyingine sikwambi niliumiaje tuliwafatailia tukakuta wanaelekea uwanja wa ndege palikuwa na ndege binafsi waliopanda na kuondoka Mombasa sikutaka kulala Mombasa nami nilipanda ndege kurudi dar es salaam usiku uwo uwo nikachukuwa ndege hadi iringa
Nilipofika nyumbani nikamkuta Anita wangu amesharudi na kuwandaa chakura nikipendacho kama kwaida yake sura yake ilikuwa na tabasamu kemkem tulikula na kwenda kulala sijui mwanamke linipa nini sikuweza hata kumuliza nikaacha nayo na kuendelea na maisha
Siku zilizidi kwenda mipango ya harusi ikanza baada ya kumaliza taratibu zote za utowaji mahari hata kamati ya sherehe ilipangwa
Kuna siku gari yangu ilipata itilafu nikalazimika kuipaki sehemu na kuchukuwa boda boda nirudi nyumbani ili nikachukuwe gari linguine baada ya kumpigia simu sana anita simu hakuwa inapokelewa nilipofika nyumbani kwangu
Nilistuka kulikuta gari ambalo anita aliwai kuja nalo nyumbani kwakuwa aliniambia ni la rafiki yake zikuzingatia nikaingia ndani nilimkuta mwanaume wa kiarabu akiwa anavaliswa tai na anita jamaa alikuwa amemshika kiuno mke wangu na kumbusu mara kwa mara
Anita alistuka kuniona hadi akacha kumfunga tai mwanaume yule akarudi nyuma uku akisema
mume wangu
ndio kipenzi changu jamaa akamvuta na kumbusu tena busu zito
`Abdul nenda mume wangu`apo ndipo nikagunduwa kuwa jamaa anaitwa Abdul nikiwa siamini nilichokiona
Jamaa akajibu mumeo amefanyaje tena
Uyo apo nyuma
Abbul alikurupuka na kuponyeza kitu wakaingia walinzi wanne waliojazia vilivyo abdul kaondoka kwa pozi na madaha nikatamani ningekuwa na bastora yangu ningeitowa na kummaliza palepale
Nilipomuliza anita akanijibu alikuwa ni rafiki yake nilipadwa na hasila nikaanza kumsema kilio cha anita ndio kikachukuwa nafasi akisema namwona yeye maraya simuwamini bora ndoa usiwepo kitendo cha kulia kikaniumiza sana ikabidi niwe mpole nimwombe msamaha ikawa kama nimemwongeza apo akachukuwa nguo na kuondoka nyumbani
Nilimkimbilia hadi getini anita alishapanda kwenye gari na kuondoka haraka nami nikachukuwa gari kwenda kwao nilipotalajia nitamkuta haikuwa ivyo simu nayo hakupatikana kabisa nilijipa moyo atarudi labla hasira tuu sikutaka tena hata kwenda kazini nilirudi nyumbani
Nilimsubilia hadi subuhi akuwa amerudi wala simuni apatikaniki nilipowauliza wazazi wakaniambia ajarudi
Nikaanza kupata wasiwi wa kumpoteza mpenzi wangu sikuweza hata kwenda kazini kila mala linijalibu kumpigia simuni hapatikani niliendela kuwasiliana na wazazi jibu likawa lile lile zikapita siku tatu ndipo aliporudi nilijiapiza kuto muuzi tena mpenzi wangu nikamsamehe na kuwanza maisha mapya
Nikamwachia kadi zangu za bank na mwila zangu zote aweze kutowa kiasi cha pesa akitakacho kwenye account zangu za bank sikutaka apate shidayoyote siku choka nikamfungulia duka kubwa la mavazi mapenzi yakanoga Zaidi hata mtu anaponiambia kuwa yule yula jamaa bado anakujaga kwangu kila ninapokuwa safari sikuwamini kila siku anita alinisi nisiwasikilize maneno ya watu
Akuwa anarudi nyumbani amchelewa hata pesa akitowa lazima anitalifu siku iyo nipo nyumbani siku ya juma pili akanipa habari iliyostuwa moyo wangu sana kwa furaha
mume wangu leo nimetoka hospital kupima nimekutwa nina mimba
`nilifurai kwa kusikia ivyo na kumshukuru mungu jambo la ajabu Anita akuonyesha furaha hata kidogo na kudai anafikilia kuitowa mimba
Kiukweli swala la kutowa mimba siku liafiki kabisa nilipiga magoti na kumwomba asitowe mimba kwani mtoto ni Baraka kutoka kwa mwenyezimungu sio vyema kutowa
hapana sipo tayari kuzaa inje ya ndoa watu watanifikiliaje na kwetu ni watu wa dini sitotumia pesa yako nitatumia pesa yangu
``mwisho niliafiki kishingo upande nilimwacha anajianda kwenda hospital nami nikaelekea kazini usiku niliporudi ndipo akaniambia kuwa amefanikiwa kuitowa mimba nikampa pole uku moyo ukiniuma sana sikuweza hata kula siku ile
Zilipita kama wiki mbili nakumbuka siku iyo ilikuwa siku ya birthday yake nilimaliza kazi mapema sana nikaitaji kumsapraizi mpenzi wangu kwa zawadi pamoja na out kama kawaida nilifika inje ya geti nikazikuta gari mbili nilipotazama kwa umakini mlangoni palikuwepo wanaume wawili waliojazia walikuwa amevalia suti wote walisimama pembezoni ya mlango apo moyo ukaanza kupata wasiwasi taratibu nikasimamisha gari langu mbali kidogo na kutelemka nikatembea hadi nyuma ya fensi nikaruka ukuta nikitumia mti uliopo karibu na ukuta nashukuru wire za umeme mchana huwa zinazimwa
Kupitia mlango wa uwani nikaingia ndani moja kwa moja hadi chumbani kwangu mlango wa chumba ulikuwa upo wazi kadri niliposogea ndio miguno ya pamezi ilizidi kusikika sikutaka kuwamini nilihisi uwenda mke wangu anatazama video za ngono nikatazama sikuwamini nilichokiona nusura mapigo ya moyo yanisimame kitandani kwangu ,chumba changu,mpenzi wangu alikuwa abdul akihema juu ya kifuwa cha Anita wangu nilibaki nikitazama mtanange ule wa bure ambao ulizaminiwa na mimi mwenyewe pasipo kupenda hadi walipomaliza
 
Nilihisi miguu haina nguvu taratibu nilirudi chini bila kupenda nikaa pembezoni mwa mlango najuta kukaa pembezoni pale laiti ningejuwa bora ningeondoka zilipita dakika chache wakanza kuongea
mpenzi unajuwa sana kunifikisha yani unanipa ile kitu roho inapenda kila siku nakuona mpya kweli jama anafaidi
Anita alicheka kicheko cha sauti ya chini chini na kujibu` asante yule bwege simpi kama ninavyokupa wewe yani nakupa vyote `
sasa kwa nini uliamuwa kuitowa ile mimba wakati tulishakubaliana utoitowa sauti ya kiume ilisema
Anita alijibu ni kweli lakini damu yako ni kali sana ningeiyacha angeniletea matatizo katika mausiano yetu
matatizo gani
unafikilia mtoto akitoka shombe shombe itakuwaje wakati bwege wangu ni mweusi kama mkaa
Kwa pamoja walicheka kicheko kikubwa na kuendelea na maongezi ambayo sikutaka kuyasikia nikajiinuwa na kutoka inje kitendo cha walinzi kuniona natoka pasipokujuwa nilipoingia haraka wakanipita kwa kunipiga kikumbo wakakimbilia ndani sikutaka kufatilia nilienda kwenye gari langu na kuwasha sikujuwa naenda wapi
Nikiwa katika mwendo kasi nikajikuta nimetoka barabarani na kuingia mtaloni apo sikujuwa kilichoendelea mpaka nilipostuliwa na sauti ya mpenzi wangu Anita aliyekuwa pembeni yangu akilia harufu ya madawa yaliniaminisha niamini kuwa nipo hospital mama na baba pia walikuwa wakimbembeleza Anita kitendo cha kufumbuwa macho Anita alinikumbatia na kunimwagia mabusu akimshukulu mungu
Nilikaa hospital siku mbili muda wote alikuwa yupo nami akutaka hata kuondoka kuniacha peke yangu hata siku niliyoruhusiwa ni yeye aliyenifata na kunirudisha nyumbani maisha yakeendelea pasipokumwambia chochote
Kila nilivyokuwa nakumbuka yaliyotokea nikajikuta nalia peke yangu niwapo ofisini au kwenye gari nilipatwa na fikra za kuachana nae lakini moyo ulikataa katakata kwa kuwamini sitapata mwanamke mzuri kama yeye
Nikaamuwa kufa na tai shingoni nilificha siri ile moyoni mwangu kwa kuamini kama ningeisema basi ninge achana naye kila nikiwa mbali na nyumbani nilipata wakati mgumu sana kwani niwapo kazini mwanaume mwenzangu anakuja nyumbani kwangu
Kama angeamuwa kuniacha kwangu lingelikuwa pigo kubwa sana kutengana na Anita lilikuwa ni jambo ambalo ambalo siliwezi kulivumilia kwa namna yoyote pamoja na matatizo yote bado alikuwa mtu muimusana kwangu sisiti kusema nilimpenda kila siku iyendayo kwa mungu hata yeye alijuwa kama nampenda
Kutokana na kuwa na mawazo mengi juu ya Anita utendaji wangu wa kazi ulipunguwa hata hali yangu ilianza kubadilika Anita alikuwa wa kwanza kulibaini ilo tukiwa tunajianda kulala aliniuliza
`mume wangu mbona umepunguwa sana unatatizo gani`aliniuliza
nipo sawa
sio kweli mume wangu kama kuna kitu kinakusumbuwa kama bado unaumwa twende hospital
tangu umetoka hospital umekuwa mtu wa kukaa kimya sana kana kwamba unatatizo
hapana nipo sawa mawazo tuu ya kiofisi
Niliendelea kumdanganya Anita
Ukweli ukabakia palepale kuwa nilipunguwa sana hata rafiki yangu karim akaligunduwa ilo aliponiuliza sana kwa msisitizo ndipo nilipomfungukia yote
heeee Edwin huyo sio mwanamke ni shetani atakuuwa mwache haraka
yani karim bado uwaze kuyajenga mausiano yetu wewe unanishauli niyabomowe kama huna njia nyingine ya kunisaidia Zaidi ya kuniambia nimwache basi nitasolve mwenyewe
hapana Edwin simanishi ivyo ila uyo mwanamke sio mzuri kwako atakuwa
`hapana karimu Anita ananipenda ndio maana ameamuwa kuitowa mimba ya abdul ili tuishi kwa Amani`mapenzi ni upofu kweli kwa anita nilipofuka haswaa sikuzikia la muwazini wala la mnadi swala
kama kuna mganga naomba nipeleka nikamtulize
Edwin umefikia hatuwa iyo hapana mimi simo uyo mganga mtafute mwenyewe ila kuna njia moja itakusaidia kurudisha eshima kwa mpenzi wako `
Nilikaa kimya kumsikiliza karim anavyonielezea njia zake`kwanza siku ukimkuta uyo abdul anzisha valangati mshushie kipigo hata ngumi moja iyo atoweza kuja tena kwako ataogopa kisha mkeo mwambie mambo yake yote anayokufanyia na mkanye kuwa atakapo rudia tena wewe naye basi na mpe beat asisubutu kumwingiza abdul kwako na kila anachokifanya akwambie`
`niliona ushauli wa karim mzuri`nikaupokea kwa mikono miwili nikisubilia iyo siku nimkute abdul kwangu nimwonyeshe baraha mungu si athumani zilipita wiki mbili abdul akaja tena kwangu nakumbuka nilimwambia mfanyakazi aniambie kama jamaa akija araka nilirudi nyumbani na kupita njia ya kuruka ukuta nikaingia ndani nikakutana ndio wapo kwenye mandalizi ya kufanya mapenzi wote wapo uchi sikutaka kusikiliza nikafunga mlango na kuwanza kumshushia kipigo abdul nilimzibiti vilivyo kelele za anita aliyetoka inje zikawafikia walinzi nililigunduwa ilo haraka nikapiga simu police kuwa nimevamiwa na majambazi nikajibanza sehemu kuwasubilia walinzi haikupita muda walinzi wanne wenye bastora kononi walikuwa wakija kwa kasi na kuwanza kupandisha ngazi nami nikatowa bastora yangu na kuwaanza kuwashambulia sebre ikawa uwanja wa vita majibizano ya risasi nashukuru akuna aliye jeruhiwa sio mimi wala wale walinzi hadi police walipofika na kuwakamata wote na bosi wao
Nikaamia kwa Anita niliyemwambia kila kitu alichofanya akabaki kimya uku nikimmwonya kwa ukali akuna siku niliobadilika kama ile hata Anita akutegemea kama ningeweza kufanya vile
Kwa ustarabu aliniomba msamaha akiwa na wazazi wake yakaisha uku akiniahidi kuwa hatorudia tena nikaona kweli ushauli umefanya kazi nyumbani eshima ikawa imerudi na sikuwa nasikia tena habari za abdul japo kuwa kesi alishinda kutokana kuwa ni mtoto wa tajiri anayeishi uwalabuni mausianao ya baba yake na vigogo wa selikali kesi iliishia kiajabu ajabu
 
Afya ilirudi nikawa mwenye furaha kabisa nikaona sasa ndio muda wa kuowa kweli mandalizi ya ndoa yakafanyika zilibaki mwezi mmoja tufunge ndowa ya kawaida akutaka ndowa yetu iwe ya kifahari kwakuwa tutapoteza pesa pasipo sababu ya msingi Anita akapata ujauzito wote tulifurai Zaidi nikaona hakuna haja ya kumweka mbali mali zote na kampuni nikampa share nusu kwa nusu wazazi nikiwachia share zao na mali zingine zote apo ndipo nilipojitusi mwenyewe pasipo kujuwa
Mambo yakazidi kuwa mazuri nilipopata tenda ya kupeleka mbogamboga hostel saba zilizopo inchi tofauti tofauti hivyo nikawa na safari za kwenda kibishara ujerumani,saouth Africa na inchi nyingine nilikaa yapata wiki tatu nikiwasiliana na mke wangu kila muda hadi nilipofika south frica ndipo mawasiliano yakakatika nilipofika iringa nikakutana na baraha ilo kuwa akuna mali ten azote zimeuzwa na muda si mrefu nikapokea ujumbe kwa abdul kuwa mke wangu akuwa na mimba bali alikuwa ananiigizia akanitumia video hata daktari na vipimo vyote feki nikaonda hakuna namna ya kuishi nilipanda ndege hadi dar es salaama kisha nikachukuwa gari hadi sinza kwenye baa nilikunywa pombe japo sikuwa mtumiaji wa kilevi chochote nilipolizika nikachukuwa gari hadi serender brige na kuimaliza safari yangu ya maisha nashukuru ulinisaidia lasiivyo sasa ningekuwa marehemu``alimaliza kusimulia Edwin
duuu pole sana Edwin mungu yupo pamoja nawe atakusaidia
asante nishapowa
Tutaenda kumwona mwanasheria tumsikilize atatushaulini nini ili tupate mali zako
hata nikipata nusu nitashukuru naimani nitazirudisha zote kwa kufanya kazi kwa bidii na juhudi
Siku iliyofatia kama ilivyo kawaida ya velonica kila amkapo lazima afanye mazoezi kisha anaendelea na taratibu zingine baada ya kufanya mazoezi kwa pamoja wakapata kifunguwa kinywa na kuiyanza safari kwenda kunana na mwanasheria
Mwendo wa dakakika arobaini na tano tulifika kwenye jengo la ghorofa mbili mbele ya jengo palikuwa na mandishi makubwa aliyandikwa kwa joice advocate campany tulishuka kwenye gari na kuingia ndani ya jengo ilo mapokezi tukapokelewa na secretary aliyetukaribisha kwa bashasha nasi tukarudisha tabasamu lililotengeneza urafiki kati yetu
karibu dada velonica za masiku
nzuri tuu pole na kazi mdogo wangu
asante piteni tuu alishaniachia magizo
Ilikuwa ofisi kubwa yenye kupagwa na fenicha za kisasa za kifahari joice akatukalibisha
joice huyu anaitwa Edwin rafiki yangu
Edwin nafurai kukufahamu velonica ukuwai kunidokezea kuwa unaurafiki na handsame man kama wewe jamani
Kwa pamoja tukajikuta tunacheka
Ndio leo nimekuletea ujione mwenyewe
`Edwin huyu rafiki yangu anaitwa wakili msomi joice hawa wezetu ndio wanaojiona wamesoma sisiwengine tuliwasindikiza tuu chuoni
``velonica alinieleza kuusu wewe kiufupi pole sana Edwin
asante
nieleze ilikuwaje hadi ukafilisiwa kila kitu chako
Edwin akaanza kumsimulia kuwanzi mwanzo hadi alipokutana na velonica
``kesi yako sio ngumu sana ila inaitaji umakini mkubwa kwakuwa imefika kwangu utapata mali zako baada ya maongezi tuliagana na joice alitusindikiza hadi kwenye maegesho tukapanda gari na kuondoka tukiwa njiani ukimya ulitawala nikiwa makini kwenye usukuni
velonica akauvunja ukimya kwa kuniuliza swali la uchokizi Edwin unajuwa tunaelekea wapi
Edwin akatabasamu `hapana bosi lady nadhani nakurudisha kwako`nilimjibu
kuna sehemu nataka twende tukapate chakura cha mchana
sawa haina shinda bosi
Mbezi beach ndipo ilipoishia safari yetu gari likasimama mbele ya geti lililokuwa linalindwa na askari police geti likafunguliwa taratibu tukaingia ilikuwa nyumba kubwa iliyojngeka vizuri pamoja na mathali yenye kuvutia baada ya velonica kusalimiana na wafanya kazi tuliowakuta inje tukaingia ndani kwenye sebre tuliwakuta wazee wawili tukaalimiana nao salamu ya velonica kwa wazee wale ndio iliyonifumbuwa tupo nyumbani kwao bila kugoja velonica akanitambulisha kw wazazi wake baada ya utambulisho uliofatia na kukalibiswa bi Anna alinyanyuka akiongozana na velonica nikabaki na mzee herman niliyekuwa namwona mara kadhaa kwenye television akiwa katika ziara mbalimbali za kikazi leo hii nipo naye tena nazungumza nae alianzisha mazungumzo
Edwin unajishulisha na nini mwanangu
kwa sasa sijishulishi na chochote Zaidi ya kumsaidia velonica majukumu madogomadogo mweshimiwa waziri mkuu
Mzee herman alitabasamu akiwa ananitazama
hapa tunaongea kama mtu na mwanae sitopendezewa kuniita mweshimiwa nitafurai ukiniita baba tuu basi
`sawa mweshimiwa waziri mkuu oooh sawa baba`nililudia kosa ila haraka nikalilekebisha nadhani hata mzee herman alitambuwa wasiwasi wangu akatabasamu na kuendelea na mazungumzo
Kwanini``
nilimweleza kiufupi yaliyonikuta kwa sasa naitaji muda wa kujipanga upya ili maisha yaendele
pole sana kijana nimependa ulivyo jasili wengine wangejiuwa kama wakikutana na mtiahani kama wako
`ni kweli namshukuru velonica kunisaidia kushinda wazo la kutaka kujiuwa kwa kiasi kikubwa amenisaidia `tuliendelea kuzungumza mambo mengi hadi chakula kilipokuwa tayari mara zote bi Anna wanapokuja wageni au mmewe akiwa nyumbani anapendelea aingie jikoni mwenyewe
Tulipata chakula cha mchana kwa pamoja nikili familia yam zee herman ni familia yenye upendo mkubwa nilipenda hata wanavyo ishi na wafanyakazi wa ndani ambao tulikula nao pamoja mezani tofauti na familia zingine baada ya chakula tuliendelea kuzungumza hadi ilipofika jioni mimi na velonica tukaaga na kuondoka
 
Dah!! Una muandiko mbaya... Hujui kuandika kabisa...
 
"nimewapenda sana wazazi wako ni wachangamfu sikuwaza kama mweshimiwa waziri mkuu ni mchangamfu kiasi kile nilivyokuwa mbele yake nikajihisi kama nina kosa nasubiliwa kupewa hadhabu``niliongea nikiwa makini kuendesha gari mara kadhaa nilimtazama velonica
Aliyekuwa anacheka kwa kile nilichomweleza kiukweli mungu amejuwa kumuumba mrembo kila ninapomtazama velonica Napata kumshukuru mungu kunikutanisha nae
Siku iliyofata joice alifanya mazungumzo na mpelelezi wake wa kujitegemea kuhusu mkasa ulionikuta
` kesi si tata sana nipe muda naitaji kuwanza kumfatilia kwanza Abdul ni nani tukishapata jibu basi itatupa mwangaza`alijibu mpelelezi
sawa malipo ya hawali ni bei gani
dola elfu moja tuu dada
nitakuingizia punde nikikata simu uwe na kazi njema
nawe pia
Baada ya mazungumzo hayo joice akachukuwa computer mpakato iliyopo mezani kwake na kubonyeza vitufe kadhaa kisha akaingiza namba furani akamalizia kiasi cha dora elfu moja akabonyenza enter kuruhusu mwamala ufanyike punde akapokea ujumbe wa kukamilika kwa mwamala .
Ni kawaida yetu mara tunapomaliza kupata chakura cha usiku mimi na velonica tulipenda kutazama filamu sisi wote ni wapenzi wa filamu likawa jambo zuri sana kwetu tukiwa tuantazama filamu nikamuwa kuanzisha maongezi
` velo`nilimwita nikikatisha jina lake
abee
nimeka nawe yapata mwezi sasa sijawai kumwona wala kusikia habari za shemeji yangu yupo wapi
`hapana sina`alinijibu baada ya kutabasamu akaendelea kutazama filamu iliyonoga kwa wakati huo upande wangu ile filamu nilisha iyona hivyo nilikuwa namsindikiza velonica japokuwa sikumwambia
`jamani kuna wanaume hawaoni yani binti mzuri ivyo upo single kweli `niliendeleza maongezi kwa maswali ya kichokozi
sio kama siwapati hapana laa sijampata mtu sahihi
`usijali mungu atakujalia `nilimaliza mjadara kwa mtindo huo kiwepesi kabisa
`arafu nimekumbuka nimepata mwaliko na rafiki yangu aliyepo afrika kusini wiki ijayo anaowa naomba twende sote nitakosa kampani nikiwa peke yangu`velonica akanichombeza kwa tarifa mpya kabisa iliyonivutia masikioni mwangu
sawa usijali safari lini
alhamisi
Sawa baada ya kumaliza kutazama filamu tuliagana kila mtu akaenda chumbani kwake kupunzika siku iliyofata baada ya kufanya mazoezi tulipata kifunguwa kinywa velonica akaelekea kazini nami nikaelekea katika wakala wa anga kwa ajiri ya kukata tiketi mbili daraja la kwanza nilipomaliza nikarudi nyumbani hata kabla sijatelemka kwenye gari simu yangu ilita nilipoitazama sikuona jina la mpigaji simu yangu ya sasa inanamba chache tu velonica wafanya kazi wa nyumbani kwa velonica pamoja na za wazazi wangu japo sijawai kuwasiliana nao kwa namba yangu na mara ya mwisho niliwasiliana wiki tatu zilizo pita nikitumia simu ya mlinzi wa getini
Nilipokea nikasubilia mpigaji ajitambulishe
unaongea na mzee herman
shikamoo baba
marahaba hamjambo
atujambo sijui nyie uko
tupo salama haaa mama yako amesafiri nami nimepata karikizo kidogo naitaji niende shambani morogoro kama unanafasi nisindikize
baba usijali nafika muda si mrefu
usijali nitakupitia mwenyewe
sawa
Simu ikakatwa nilikumbuka sikuchukuwa namba za mzee herman wala yeye akuchukuwa zangu baada ya kujiuliza nikapata jibu namba amezipata kwa velonica nilitelemka kwenye gari na kuingia ndani nikajianda haikupita muda gari mbili zenye namba ya serikali zikafika nyumbani kwa velonica sikupoteza muda nikabeba begi langu na kuingia kwenye gari alilikuwepo mzee herman
Tukiwa njiani tulizungumza habari nyingii mazungumzo yetu yalitawaliwa na vicheko kwa mzee herman richa ya kuwa muda mwingi anaendeswa bado ujuzi wake wa kuendesha gari haukupotea niligundua ilo alipokuwa anaendesha mimi nikiwa pembeni yake
unajuwa mwanangu kipindi nipo kijana nilikuwa napenda michezo wa rally mzizima rally ,mkwawa rally hazikuwa zinanikosa huko ndipo nilipopatia mchumba bi Anna kipindi icho mbichi haswa hii stori nitakusimulia baadae sasa nitamaliza uwondo ngoja nikuonyeshe tuwakimbie walinzi tusiandikie mate wakati wino upo
Akakanyaga pedeli ya mafuta mbw x6 ikaitikia kwa mlio wa injini kubadilika na kupelekea mshare wa speed kupanda kutoka kwenye hamsini kuelekea namba za juu kasi ikaongezeka mara dufu akuishia hapo kaanza kuyapanguwa magari yaliyokuwa yametangulia alikuwa anaover take kwa mtindo wa kipekee japo gari la walinzi lilijitaidi kutufukuzia hawakufua dafu ndani ya muda mfupi tuliwapotea kabisa nikili mzee herman alikuwa fundi wa kuendesha gari mfano akuna kuna muda alimaliza speed zote watoto wa mjini wanaita kulamba kisahani chote hadi alipoona uzio wa skari alipopunguza mwendo akasimama baada ya askari wa barabarani kutupunia mkono wote tulijiwa fikra tumevunja sharia
 
askari wa usalama barabarani aliyevalia sale zilizomkaa vyema mkononi alishikilia bunduki aina ya smg alisogelea mlango upande wa dereva akagonga akionyesha ishara dereva ashushe kioo mzee Herman akafanya kama police alivyo amrisha
Kitendo cha police kumwona mzee Herman alikakamaa kwa heshima akapiga salute kwenye kizuizi
`za kazi mweshimiwaaskari alisalimia `
nzuri pole kwa majukumu
asante mweshimiwa karibu sana
Kwenye kizuizi palikuwa na askari saba walipomwona mzee herman aliyetelemka kwenye gari akaelekea sehemu walipokuwa wamekaa askari wote waka mpigia salute kwa ukakamavu wakaanza wakijitambulisha kesi ya kuvunja sharia za barabarani ikaisha kwa mtindo huo.
Msiwe na wasi nimekuja kuwajulia hali vijana wangu fanyeni mawasiliano na walinzi wangu muwatarifu nipo hapa nawasubilia`` askari mmoja aliyekuwa ananyota moja megeni akapiga saluti na kusogea pembeni akaanza kufanya mawasiliano alipokamilisha akaturudia tulipoketi
mweshimiwa baada ya dakika kumi watakuwa hapa
`sawa`mzee Herman akatoa noti za elfu kumi mbili na kumwita muuza madafu aliyefika tulipokuwa tumekaa akatudumia madafu kwa kila aliyeitaji stori zingine ziliendelea hadi gari za walinzi zilipofika tukaagana na maskari nami wakati wangu wa kushika usukani kuakikisha safari inaendelea hadi tulipofika kilombelo
Ilikuwa ni nyumba ya ghorofa moja iliyozungukwa na miti ya vivuli na matunda bwawa dogo la kuogelea lililofanya uzuri wa nyumba iyo uzudi mara dufu upande wa mashariki ilipakana na mto kilombelo mazingira yalikuwa mazuri kuliko nyumba ya dar es salaam tuliwakuta wafanya kazi wameshatuandalia chakura tukaanza kuburudika ugari samaki pamoja na mbogamboga baada ya kuakikisha matumbo yetu yametosheka tukaelekea sehemu ya kupunzika mzee Herman akaanza kunisimulia alivyokutana na mkewe.
nakumbuka ulikuwa mwaka 1972 mwezi December mimi na timu yangu tulikuwa katika mashindano ya magari uruguru rally mzunguko wa mwisho nilikuwa naongoza posch 911ilijuwa kikimbie hakuna gari iliyonikuta wapinzani wangu saigoni kutoka arusha aliyekuwa anatigisha na gari yake Peugeot 504 kwa wakati huo ilikuwa gari latest kabisa iliogopwa haswa inapokuwa barabarani mwegine jayant patel alikuwa ana endesha Datsun 160j huyu jamaa alikuwa mtaramu wa kucheza na kona hakuna mfano kwa posch 911 wote waliachwa mbali mno akanyamaza na kuvuta glasi yake iliyokuwa na mvinyo akapiga mafundo matatu akaituwa glasi mahara pake muda wote nilimtumbulia macho tuu utazani ndio mara yangu ya kwanza kumuona kitendo icho hakikumshulisha akaendelea
Nikiwa kwenye mwendo kasi mia na arobaini niliona Mercedes benzi ikiyumba yumba ikija uwelekeo wangu nilipolikalibia nikawaona msichana na mwanamama nilikuwa na machaguo mawili niwagonge au nipeleka gari pembeni ya barabara kuwapisha nikakumbuka kitendo cha kutoka inje ya barabara basi lazima ningegonga miti mikubwa iliyokuwa kandokando ya barabara sikujiuliza mara mbili nikaipeleka gari inje ya barabara kishindo kizito kikasikika punde nilipogonga mti nashukuru mungu tulitoka salama hakuna aliyeumia Zaidi ya michubuko midogo midogo nilipotoka kwenye gari nilikuwa na hasila nikaisogelea benz nilishakusanya rundo la matusi nilipolikalibia nikagonga dirisha kwa nguvu mlango ukafunguliwa nikajikuta nimenywea hasila zote zimepotea kwa uzuri wa dereva mlango mwengine ukafunguliwa akatoka mwana mama wa makamo walivyofanana zaili walionekana mtu wa mwane walikuwa na wasiwasi nilimsalimia nikawauliza kama wapo salama wakati mimi ndiye niliyepata jari baada ya kujilizisha wapo salama nikalitoa gari lao barabarani ukawa mwisho wa kucheza rally gari langu lilialibika vibaya mno
Kwa kiasi niliuzunika ila kila nilipomtazama mrembo aliyekuwa amesimama na mama yake wakilitazama gari letu nilifalijika uwo ukawa mwanzo wa kujuwana mimi na Anna ambaye baba yake alikuwa ni waziri mkuu kwa kipindi icho morogoro walikuwa wamekuja likizo mama yake akatumia muda huo kumfundisha kuendesha gari mwanae pasipokujuwa njia wanayoitumia ilitumika katika mbio za magari mausiano yetu yalikuwa kwa kasi hadi tukafunga ndoa nilipopata mtoto wa kwanza nikaacha kucheza mbio za magari kwa Anna alikuwa anawasiwasi sana kila ninapoenda kushiliki mchezo kupitia kipenzi mke wangu akisaidiana na baba mkwe wangu wakaningiza kwenye siasa ndio walionifundisha siasa hadi sasa mke wangu Anna mekuwa mshauri wangu mkubwa na namba moja`` akanyamaza kana kwamba anafikilia kitu kabla ya kutaka kukitamka alipojilizisha akaendelea
``velonica anamekupenda sijawai kumwona binti yangu akiwa katika sura ya furaha kama kipindi hiki alipokuwa na wewe namfahamu vizuri sana naona anajizungusha kukwambia kwa sababu tamaduniz zetu aziruhusu mtoto wa kike kumwanza mtoto wa kiume japo hii zana imepitwa na wakati kila mtu anaweza kueleza hisia zake kwa mtu ampendae.
Nimekuelewa baba nitalifanyia kazi nimependa namna mlivyokutana na mama Anna
Tulizungumza mengi na mzee herman hadi ulipofika usiku tukaagana nikiwa chumbani kwangu nikampigia simu velonica simu haikuchukuwa muda ikapokelewa baada ya salamu na stori mbili tatu nikamjuza
nimenunuwa tiketi za ndege usije ukanunuwa tena nitarudi juma tano
sawa naona mmeamuwa kunikimbia haya bwana usiku mwema
nawe pia nakupenda nililopoka
`Umesemaje velonica akaniuliza`kwa mshangao
`haaa usiku mwema nimesema ivyo `nilijitetea pasipo sababu malumu na simu nikazima
 
Back
Top Bottom