Spika Tulia Ackson ilikuwa ni haki yake kutoa hisia kama hizo.
Alikuwa naibu spika wakati Job Ndugai alikuwa Spika kamili.
Tulia Ackson huenda,nasema huenda anakumbuka mengi kutoka Kwa mtangulizi wake ambayo hatoyasema wala kuandika popote.ushauri,kiongozi,maamuzi na kuzingatia itifaki Kwa kiongozi mkubwa kama naibu spika au spika kamili
Tulia Ackson pamoja na madhaifu yake (kama yapo) ni binadamu kama binadamu wengine,anaguswa na hafurahii mengi yanayoendelea,lakini bahati mbaya yupo katika nafasi ya juu tena kwenye muhimili mkuu kama bunge.
Sehemu ambapo hupaswi kutoa matamko Kihisia bali lazima ushirikishe timu, cabinet na watu mbalimbali ili kuchuja nini kizungumzwe kwenye umma.
Martin Maranja Masese ni wa kupuuzwa pamoja na kuwa anafahamika Kwa uwazi lakini ni kijana mropokaji,hafai hata kuwa kiongozi,asiwaige kina Lema ambao ni kama wamekata tamaa na hatima Yao ya kisiasa.
Martin hafai kuwa kiongozi mahali popote ni mtu asiyezingatia miiko,Siri na hata kutoa taarifa ambazo hana uhakika nazo na watu kama Martin wapo wengi hata hapa Jamii Africa,wao mtu yeyote akiwa CCM ni adui kwao.haijalishi atasema vibaya au vizuri .
Martin najua hata uliyoahidiwa na Mbowe hatatatimia kwakuwa hampo tena chadema,hamia chauma basi, James, Yeriko wapo huko
Na hata hapa Jamii Africa wapo wengi tu Ni watu wasiojua kuchambua mambo wao kila mtu ambaye ni trash pale CCM kwao ni Shujaa.
Kuna hawa ambao wameonekana ni mashujaa Kwa wiki za hivi karibuni
Josephat Gwajima,..
Huyu baada ya kuona atakosa nafasi na hayupo kwenye chain akaamua kuja na press kuisimanga serikali huku watu wakimuita ni Shujaa
Luhaga Mpina
Mbunge wa kisesa na kipenzi cha Rais Magufuli, hakuwahi kumkubali Rais wa sasa Samia Suluhu na chuki yake ilikuwa ya wazi baada ya kukosa mianya aliyokuwa kaikusudia.
Humphrey Polepole.
Huyu naye ni kipenzi cha Magufuli,
Namuita mshamba kwakuwa kuna mengi amekuwa akiyaropoka huku wengi wakimuonabl Shujaa kumbe ni mtu alijiona hayupo kwenye ile chain ya CCM
Pumzika mahali pema Job Yustino Ndugai.
Kila nafsi itaonja mauti.
Pole Tulia Ackson,
Pole wanafamilia,.
Pole wana CCM
Pole watanzania
Kwa kuondokewa na moja ya watumishi muhimu kwenye nchi hii.