BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,020
Salim Said
Mwananchi
October 2, 2009
Mkuu anayeshughulikia Sera na Bunge Philip Marmo, amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano inakwamisha utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati teule ya Bunge kuhusu uchunguzi wa mkataba tata katika kampuni ya Richmond.
Kamati teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe ilifanya uchunguzi kuhusu zabuni ya kufua umeme wa dharura na kugundua kuwepo kwa ukiukwaji wa sheria na taratibu za manunuzi.
Baada ya kamati hiyo, kubaini kuwepo kwa kasoro hizo, mawaziri watatu wa serikali, akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, walijiuzulu.
Kamati hiyo, ilipendekeza mambo mbalimbali ya msingi yatekelezwe ili kukomesha ukiukwaji wa manunuzi.
Moja ya mambo yaliopendekezwa ni kuwaajibisha baadhi ya watendaji wakuu wa taasisi za Serikali.
Akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji (TBC1) Mjini Arusha jana Marmo aliweka hadharani kwamba katiba inakwamisha utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Dk Mwakyembe.
"Kama serikali tunaona tuna mapungufu katika katiba, ndio maana hata utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati teule ya bunge kuhusu uchunguzi wa Richmond yanachelewa.
"Hii ni kwa sababu mapendekezo yale ni nguvu kutoka bungeni na yameletwa serikalini, ambayo nayo ina taratibu na sheria zake na watendaji wa umma nao wana taratibu zao za kushughulikiwa, tofauti na bunge ambavyo imetaka iwe,"alisema Waziri Marmo.
Marmo alisema kwamba matatizo hayo, mwanzo wake ni katiba ya mwaka 1961 ambayo alidai ni katiba chotara, iliyokopa sehemu kubwa kutoka Marekani, Ufaransa na Uingereza.
"Kwa upande wa utendaji wa vyombo vya serikali tumekopa kutoka Uingereza, katika utendaji wa bunge, tumekopa kutoka Ufaransa na Uingereza kidogo, kwa hiyo haya yote yanafanya utendaji wa kila siku wa serikali yetu kuwa mgumu, moja wapo ni hili la utekelezaji wa mapendekezo ya kamati teule ya Bunge kuhusu Richmond," alisema Marmo.
Alisema, kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri, hata kama bunge litapendekeza jambo, lakini mapendekezo hayo, lazima yatekelezwe na serikali, jambo ambalo ni gumu wakati mwingine.
"Katiba hii imegawa madaraka katika misingi ambayo inakuwa ni vigumu kwa serikali kutekeleza kwa haraka mapendekezo ya bunge hata kama yanahusu mambo mazito ya nchi.
"Hivyo basi unaweza kusema kwamba nguvu na uwezo mkubwa wa bunge uanakumbana na vikwazo, vizingiti na masharti magumu kutoka serikalini," alisema Marmo.
Alifafanua kwamba, mgongano wa kimaamuzi kati ya serikali na bunge ni ya kwaida na mara nyingi huwa yanajenga na kutoa changamoto kwa pande zote mbili za serikali na bunge. "Hii ndiyo maana vyombo hivi vimepewa majukumu tofauti, lakini kwa upande wa serikali yetu haya ni mambo mazuri, yanayojenga na kuleta afya ya serikali katika nchi, ili serikali isionekane kwamba muda wote imelala,"alisema.
Mwananchi
October 2, 2009
Mkuu anayeshughulikia Sera na Bunge Philip Marmo, amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano inakwamisha utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati teule ya Bunge kuhusu uchunguzi wa mkataba tata katika kampuni ya Richmond.
Kamati teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe ilifanya uchunguzi kuhusu zabuni ya kufua umeme wa dharura na kugundua kuwepo kwa ukiukwaji wa sheria na taratibu za manunuzi.
Baada ya kamati hiyo, kubaini kuwepo kwa kasoro hizo, mawaziri watatu wa serikali, akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, walijiuzulu.
Kamati hiyo, ilipendekeza mambo mbalimbali ya msingi yatekelezwe ili kukomesha ukiukwaji wa manunuzi.
Moja ya mambo yaliopendekezwa ni kuwaajibisha baadhi ya watendaji wakuu wa taasisi za Serikali.
Akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji (TBC1) Mjini Arusha jana Marmo aliweka hadharani kwamba katiba inakwamisha utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Dk Mwakyembe.
"Kama serikali tunaona tuna mapungufu katika katiba, ndio maana hata utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati teule ya bunge kuhusu uchunguzi wa Richmond yanachelewa.
"Hii ni kwa sababu mapendekezo yale ni nguvu kutoka bungeni na yameletwa serikalini, ambayo nayo ina taratibu na sheria zake na watendaji wa umma nao wana taratibu zao za kushughulikiwa, tofauti na bunge ambavyo imetaka iwe,"alisema Waziri Marmo.
Marmo alisema kwamba matatizo hayo, mwanzo wake ni katiba ya mwaka 1961 ambayo alidai ni katiba chotara, iliyokopa sehemu kubwa kutoka Marekani, Ufaransa na Uingereza.
"Kwa upande wa utendaji wa vyombo vya serikali tumekopa kutoka Uingereza, katika utendaji wa bunge, tumekopa kutoka Ufaransa na Uingereza kidogo, kwa hiyo haya yote yanafanya utendaji wa kila siku wa serikali yetu kuwa mgumu, moja wapo ni hili la utekelezaji wa mapendekezo ya kamati teule ya Bunge kuhusu Richmond," alisema Marmo.
Alisema, kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri, hata kama bunge litapendekeza jambo, lakini mapendekezo hayo, lazima yatekelezwe na serikali, jambo ambalo ni gumu wakati mwingine.
"Katiba hii imegawa madaraka katika misingi ambayo inakuwa ni vigumu kwa serikali kutekeleza kwa haraka mapendekezo ya bunge hata kama yanahusu mambo mazito ya nchi.
"Hivyo basi unaweza kusema kwamba nguvu na uwezo mkubwa wa bunge uanakumbana na vikwazo, vizingiti na masharti magumu kutoka serikalini," alisema Marmo.
Alifafanua kwamba, mgongano wa kimaamuzi kati ya serikali na bunge ni ya kwaida na mara nyingi huwa yanajenga na kutoa changamoto kwa pande zote mbili za serikali na bunge. "Hii ndiyo maana vyombo hivi vimepewa majukumu tofauti, lakini kwa upande wa serikali yetu haya ni mambo mazuri, yanayojenga na kuleta afya ya serikali katika nchi, ili serikali isionekane kwamba muda wote imelala,"alisema.