DaudiAiko
JF-Expert Member
- Dec 2, 2012
- 302
- 274
Wanabodi,
Hivi karibuni, tume shuhudia viongozi mbali mbali wa vyama vya upinzani wakifanya mazungumzo na Rais Samia katika mchakato mzima utakao hakikisha kwamba kuna maridhiano kati ya chama tawala na vyama vya upinzani.
Je maridhiano ya kweli yakoje?. Kwanza kabisa ni vyama vya siasa kuhusishwa zaidi katika maamuzi yanayofanywa na serikali. Hii ina maanisha kwamba tofauti zote kati ya chama tawala na wapinzani ziwekwe pembeni na wote waweze kushiriki pamoja katika shughuli zote za kiserikali kwa manufaa ya wananchi.
Pili, tumejionea wenyewe jinsi ambavyo vyama vya upinzani vina chakarika kudai katiba mpya na tume huru. Picha tu hazitoshi katika kuhakikisha kwamba vyama vyote vinashiriki kikamilifu katika chaguzi zijazo. Nina amini kwamba maridhiano yanaenda sambamba na kuhakikisha kwamba madai hayo yanapatiwa suluhisho.
Hivi karibuni, tume shuhudia viongozi mbali mbali wa vyama vya upinzani wakifanya mazungumzo na Rais Samia katika mchakato mzima utakao hakikisha kwamba kuna maridhiano kati ya chama tawala na vyama vya upinzani.
Je maridhiano ya kweli yakoje?. Kwanza kabisa ni vyama vya siasa kuhusishwa zaidi katika maamuzi yanayofanywa na serikali. Hii ina maanisha kwamba tofauti zote kati ya chama tawala na wapinzani ziwekwe pembeni na wote waweze kushiriki pamoja katika shughuli zote za kiserikali kwa manufaa ya wananchi.
Pili, tumejionea wenyewe jinsi ambavyo vyama vya upinzani vina chakarika kudai katiba mpya na tume huru. Picha tu hazitoshi katika kuhakikisha kwamba vyama vyote vinashiriki kikamilifu katika chaguzi zijazo. Nina amini kwamba maridhiano yanaenda sambamba na kuhakikisha kwamba madai hayo yanapatiwa suluhisho.